Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI JUU YA MAISHA YA WATU

“Sisi Hapa! Mututume!”

“Sisi Hapa! Mututume!”

JE, UNAPENDA kupanua utumishi wako kwa kuhamia mahali kwenye kuko lazima kubwa ya wahubiri, pengine mu inchi ingine? Kama ni vile, mambo yenye Ndugu Bergame na bibi yake walikutana nayo inaweza kukusaidia sana.

Jack na Marie-Line wamefanya pamoja utumishi wa wakati wote tangu mwaka wa 1988. Wanaweza kujipatanisha na hali mbalimbali na wamekubali migao mingi katika inchi ya Guadeloupe na Guiana ya Ufaransa. Inchi hizo zote mbili zinasimamiwa kwa sasa na tawi la Ufaransa. Tuulize Jack na Marie-Line maulizo fulani.

Ni nini iliwachochea muanze utumishi wa wakati wote?

Marie-Line: Kwa sababu nilikomalia Guadeloupe, mara mingi nilikuwa ninahubiri muchana muzima na mama yangu, mwenye alikuwa Shahidi mwenye bidii. Ninapenda watu, njo maana, kisha tu kumaliza masomo mu mwaka wa 1985, nilianza kazi ya upainia.

Jack: Wakati nilikuwa kijana, nilikuwa ninapitisha wakati mingi na watumishi wa wakati wote wenye walipenda mahubiri. Nilizoea kufanya upainia musaidizi wakati wa mapumuziko ya masomo. Ku mwisho wa juma, tulikuwa tunakamata bisi wakati fulani na kuenda kuhubiri na mapainia fulani katika eneo lao. Tulikuwa tunahubiri muchana muzima, na kisha tulikuwa tunaenda kwenye sehemu ya pembeni ya bahari yenye kuwa na muchanga. Ulikuwa wakati muzuri kabisa!

Wakati mufupi tu kisha kumuoa Marie-Line mu mwaka wa 1988, nilijiambia hivi: ‘Tuko huru, juu ya nini tusifanye mambo mingi mu kazi ya kuhubiri?’ Nilijiunga na bibi yangu Marie-Line katika kazi ya upainia. Mwaka moja kisha kusoma masomo ya mapainia, tulipewa mugao wa kuwa mapainia wa pekee. Tulipewa migao mingi yenye kufurahisha katika Guadeloupe mbele ya kuombwa tuhamie katika Guiana ya Ufaransa.

Migao yenu imebadilika kwa miaka mingi. Ni nini imewasaidia muzoee hali za mupya?

Marie-Line: Ndugu wa Beteli ya Guiana ya Ufaransa walijua kama andiko lenye tunapendaka sana ni Isaya 6:8. Kwa hiyo, wakati walikuwa wanatuita, mara mingi walikuwa wanatuuliza hivi kwa njia ya kuchekesha: “Munakumbuka andiko lenye munapendaka sana?” Mara moja tulitambua kama mugao wetu ungebadilika, kwa hiyo, tulikuwa tunasema hivi: “Sisi hapa! Mututume!”

Tunaepuka kulinganisha mugao wetu wa sasa na migao yetu ya zamani kwa sababu kufanya vile kunaweza kutuzuia tusifurahie mugao wetu wa sasa. Pia, tunajikaza kufanya urafiki na ndugu na dada wenye tunakutana nao mu mugao wetu.

Jack: Zamani, marafiki fulani wenye hawakukuwa na nia ya mubaya walijaribu kutuvunja moyo ili tusihame kwa sababu walipenda tubakie karibu nao. Lakini wakati tulitoka Guadeloupe, ndugu mumoja alitukumbusha maneno ya Yesu yenye kuwa mu Matayo 13:38: “Shamba ni ulimwengu.” Kwa hiyo, wakati mugao wetu unabadilika, tunajikumbusha kama tungali tunatumikia katika shamba hilo, hata tukuwe wapi. Jambo la maana zaidi ni eneo kwenye tunaweza kupata watu!

Wakati tunafika mu eneo mupya, tunatambua kama wengine wanafurahia kuishi kule. Kwa hiyo, tunajikaza kuishi kama vile wakaaji wa eneo hilo. Chakula kinaweza kuwa tofauti, lakini tunakula kile wao wanakula na kunywa kile wao wanakunywa, hata hivyo tunakamata hatua fulani zenye kufaa ili tusipatwe na magonjwa. Tunajikaza kusema mambo ya muzuri juu ya kila mugao.

Marie-Line: Pia, tunajifunza mambo mingi kupitia ndugu na dada wa eneo. Ninakumbuka jambo lenye lilitokea wakati tu tulifika Guiana ya Ufaransa. Mvua ilikuwa inanyesha sana, kwa hiyo, tuliwaza kama tulipaswa kungojea kipindi cha mvua kiishe mbele tuanze kuhubiri. Lakini, dada mumoja aliniuliza hivi: “Tutaenda mu mahubiri?” Nilishangaa, na nikamujibu hivi: “Tutaenda namna gani?” Alijibu hivi: “Kamata mwavuli, tutaenda na kinga.” Kwa hiyo, nilijifunza kukamata mwavuli na niko ninatembeza kinga. Kama singejifunza kufanya vile, singehubiri hata siku moja wakati wa mvua!

Mumehama mara 15 hivi. Muko na mapendekezo fulani juu ya kuhama yenye munaweza kupatia wengine?

Marie-Line: Kuhama haiko mwepesi. Lakini, ni muzuri kupata nafasi kwenye utajisikia muzuri wakati unatoka mu mahubiri.

Jack: Ninazoea kupakaa rangi ndani ya nyumba yetu. Ndugu wa Beteli, wakijua kama hatutakawia nafasi fulani, wanazoea kuniambia, “Jack, mara hii usijisumbue kwa kupakaa rangi ndani ya nyumba!”

Marie-Line anajua sana kufunga vitu! Anatia kila kitu mu visanduku na kuandika juu ya visanduku hivyo maneno kama vile “chumba cha kunawia,” “chumba cha kulala,” “mafiga,” na maneno ingine. Kwa hiyo, wakati tunafika mu nyumba yetu ya mupya, inakuwa mwepesi zaidi kujua ni katika chumba gani tutaweka kila kisanduku. Marie-Line anafanya liste ya vitu vyenye kuwa mu kila kisanduku kusudi tupate kwa vyepesi vitu vyenye tuko navyo lazima.

Marie-Line: Kwa sababu tumejifunza kupanga mambo yetu muzuri, tunaweza kuanza kazi yetu ya kuhubiri bila kukawia.

Namna gani munapanga wakati wenu ili ‘mutimize kwa ukamili utumishi wenu’?​—2 Ti. 4:5.

Marie-Line: Kila Siku ya Kwanza, tunapumuzika na kutayarisha mikutano. Kuanzia Siku ya Pili na kuendelea, tunaenda mu mahubiri.

Jack: Hata kama tuko na saa zenye tunaombwa kutimiza kila mwezi, hatukaze akili yetu juu ya saa. Kazi ya kuhubiri njo jambo la maana zaidi mu maisha yetu. Kuanzia wakati tunatoka ku nyumba mupaka wakati tunarudia, tunajikaza kuzungumuza na watu wote wenye tunakutana nao.

Marie-Line: Kwa mufano, kila mara wakati tunaenda kufanya matembezi, ninabeba trakte mbalimbali. Watu fulani wanatukaribia na kutuomba vichapo, hata kama hatujawaambia kama tuko Mashahidi wa Yehova. Njo maana, tuko waangalifu juu ya namna tunavaa na kujiendesha. Watu wanaona ile mambo yote.

Jack: Tunatoa pia ushahidi kwa kuwa majirani wazuri. Ninaokota karatasi, ninatupa uchafu wenye kuwa katika chombo cha kuwekea uchafu, na kukata majani inje ya nyumba yetu. Majirani wetu wanaona na wakati fulani wanauliza hivi: “Unaweza kunitafutia Biblia?”

Mumehubiri mara mingi mu maeneo ya mbali. Kuko jambo fulani la pekee lenye mungali munakumbuka kuhusu safari fulani yenye mulifanya?

Jack: Katika Guiana, ni nguvu kufika mu maeneo fulani. Mara mingi tulipaswa kusafiri kilometre 600 kwa juma moja mu barabara za mubaya. Hatuwezi kusahau safari yetu ya kutembelea kijiji cha St. Élie, katika pori la Amazoni. Tulifanya saa mingi juu tufike kule na tulitumia motokaa yenye kupita nafasi kwenye kuwa nguvu kupita na pia mutumbwi. Watu mingi wenye walikuwa wanaishi kule walikuwa wanafanya kazi ya kuchimbua zahabu. Ili kuonyesha shukrani yao kwa ajili ya vichapo vyetu, wamoja walikuwa wanatupatia muchango wa vipande vidogo-vidogo vya zahabu! Mangaribi, tulikuwa tunaonyesha watu video moja kati ya video za tengenezo. Wakaaji wengi wa eneo hilo walikuwa wanafika kuona video.

Marie-Line: Hivi karibuni, Jack aliombwa atoe hotuba ya Ukumbusho mu kijiji cha Camopi. Ili tufike kule, tulisafiri saa ine kwa kutumia mutumbwi mu Muto Oyapock. Lilikuwa jambo la kufurahisha sana.

Jack: Kwenye maji ya muto ilikuwa mufupi, maporomoko ilikuwa hatari sana (poromoko ni sehemu ya muto kwenye maji inateremuka mbio sana, kwa kawaida juu ya miamba). Ninaweza kuwahakikishia kama inafurahisha sana kuona ile maporomoko kadiri mutu anaikaribia. Mutu mwenye kutembeza mutumbwi anapaswa kujua muzuri kazi yake. Lakini ilikuwa safari ya muzuri sana. Hata kama kulikuwa Mashahidi 6 tu, watu karibu 50 walihuzuria Ukumbusho, kutia ndani Wahindi fulani wa Amerika!

Marie-Line: Vijana wenye wanapenda kufanya mambo mingi mu kazi ya Yehova wanaweza pia kujionea mambo yenye kufurahisha kama ile. Unapaswa kumutegemea Yehova katika hali hizo, na imani yako itatiwa nguvu. Mara mingi tunajionea mukono wa Yehova.

Mumejifunza luga mingi. Muko na zawadi ya kujifunza luga?

Jack: Hapana kabisa. Nilijifunza luga hizo kusudi niweze kuhubiri na kusaidia katika kutaniko. Nilipaswa kuongoza Funzo la Munara wa Mulinzi mu luga ya Sranantongo * mbele hata nifanye usomaji wa Biblia mu ile luga! Niliuliza ndugu mumoja kama niliongoza muzuri. Alijibu hivi: “Wakati fulani, hatukuelewa maneno fulani, lakini ilikuwa muzuri sana.” Watoto walinisaidia sana. Wakati nilikosea, walikuwa wananiambia, lakini watu wazima hawakukuwa wanafanya vile. Watoto walinifundisha mambo mingi.

Marie-Line: Mu eneo moja, nilikuwa na mafunzo ya Biblia ya Kifaransa, Kireno, na Sranantongo. Dada mumoja alinishauria nianze kuongoza mafunzo mu luga yenye sikukuwa ninajua muzuri na kisha niongoze mafunzo mu luga yenye nilikuwa ninajua muzuri kabisa. Sikukawia kuelewa kama mashauri yake ilikuwa ya hekima.

Siku moja, nilipaswa kuongoza funzo moja la Biblia mu luga ya Sranantongo na funzo lingine mu luga ya Kireno. Wakati nilianza kuongoza funzo la pili, dada mwenye alinisindikiza aliniambia hivi: “Marie-Line, ninawaza kama kuko jambo fulani lenye haliendeke!” Nilitambua kama nilikuwa ninazungumuza na mwanamuke mumoja wa Brazili mu luga ya Sranantongo kuliko kuzungumuza naye mu luga ya Kireno!

Wale wenye mumetumika nao wanawapenda sana. Mumefanya nini ili kuwa na urafiki wa sana na ndugu na dada?

Jack: Mezali 11:25 inasema hivi: “Mutu mukarimu atafanikiwa.” Hatusite kujitoa kwa ajili ya wengine. Wakati wa kufanya kazi ya kutunza Jumba la Ufalme, ndugu fulani wameniambia hivi: “Acha wahubiri wafanye ile kazi.” Lakini ninajibu hivi: “Mimi pia niko muhubiri. Kwa hiyo, kama kuko kazi ya kufanya, ninapenda nisaidie pia.” Hata kama sisi wote tuko na lazima ya kuwa peke yetu wakati fulani, mara mingi tunajikumbusha kama ile haipaswe kutuzuia kutendea wengine mambo ya muzuri.

Marie-Line: Tunajikaza kupendezwa na kila ndugu na dada. Kwa kufanya vile, tunafikia kujua wakati wako na lazima mutu fulani awasaidie kuhangaikia watoto wao ao kuenda kukamata watoto ku masomo. Kwa hiyo, tunaweza kupanga muzuri wakati wetu ili tuweze kuwasaidia. Kuwa tayari kusaidia wengine wakati wako na lazima ya musaada kumefanya urafiki wetu pamoja nao ukuwe nguvu.

Mumepata baraka gani kwa kutumikia mahali kwenye kuwa lazima kubwa ya wahubiri?

Jack: Utumishi wa wakati wote umetuletea baraka mingi. Mara mingi, tumepata nafasi ya kufurahia uumbaji wa Yehova. Hata kama tumepambana na magumu fulani, tuko na amani ya akili kwa sababu tunajua kama watu wa Mungu wanatutegemeza kila mahali kwenye tunapatikana.

Wakati nilikuwa kijana, nilifungwa katika Guiana ya Ufaransa kwa sababu nilikataa kuwa askari. Nilikuwa sijafikiriaka kama siku moja ningeweza kurudia kule na niko misionerena kuruhusiwa kutembelea magereza nikiwa mutumishi wa dini fulani. Kwa kweli, Yehova anatubariki kwa ukarimu kabisa!

Marie-Line: Kujitoa kwa ajili ya wengine kunanileta furaha sana. Tunafurahi kuwa katika utumishi wa Yehova. Kuwa katika utumishi wa Yehova kumefanya ndoa yetu ikuwe nguvu zaidi. Wakati fulani, Jack ananiuliza kama tunaweza kualika bibi na bwana wenye wako na lazima ya kutiwa moyo juu tukule nao chakula. Mara mingi ninajibu hivi: “Na mimi pia nilikuwa na ile mawazo!” Mara mingi inakuwaka vile.

Jack: Hivi karibuni, nilivumbuliwa na kansere ya prostate. Hata kama Marie-Line hapendi kusikia hii maneno, nimemuambia hivi: “Mupendwa, sijazeeka kabisa, lakini hata kama ninakufa leo ao kesho, ninajua kama nilitumia maisha yangu ili kufanya mambo ya maana kabisa, ili kumutumikia Yehova, na ile inaniletea furaha.”​—Mwa. 25:8.

Marie-Line: Yehova ametupatia migao yenye hatukufikiriaka na ameturuhusu kufanya mambo yenye hatukuwaziaka. Tumepata mambo mingi ya muzuri mu maisha yetu. Tutaenda kila mahali kwenye tengenezo lake litatutuma kwa sababu tuko hakika kabisa kama Yehova ataendelea kutusaidia!

^ fu. 32 Sranantongo ni luga yenye watumwa walianzisha kwa kuchanga Kiingereza, Kiholanzi, Kireno, na luga za Afrika.