Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 17

“Nimewaita Ninyi Marafiki”

“Nimewaita Ninyi Marafiki”

“Nimewaita ninyi marafiki, kwa sababu nimewajulisha mambo yote yenye nilisikia kutoka kwa Baba yangu.”​—YOH. 15:15.

WIMBO 13 Kristo, Kielelezo Chetu

KIFUPI CHA HABARI *

1. Unafanyaka nini ili kuanzisha urafiki na mutu fulani?

KWA KAWAIDA, jambo la kwanza lenye unafanyaka ili kuanzisha urafiki wa sana na mutu fulani mwenye unakutana naye ni kupitisha wakati pamoja na ule mutu. Wakati munaendelea kuzungumuzia mawazo yenu na namna munajisikia, munakuwa marafiki. Lakini wakati fulani haiko mwepesi kufanya urafiki wa nguvu pamoja na Yesu. Sababu gani?

2. Ni sababu gani ya kwanza yenye inafanya ikuwe nguvu kufanya urafiki pamoja na Yesu?

2 Sababu ya kwanza ni kwamba hatujamuonaka Yesu. Wakristo wengi wa wakati wa mitume nao hawakumuonaka Yesu. Lakini mutume Petro alisema hivi: “Hata kama hamujamuona hata siku moja, munamupenda. Hata kama hamumuone sasa, bado munaonyesha imani katika yeye.” (1 Pe. 1:8) Kwa hiyo, inawezekana mutu afanye urafiki wa sana pamoja na Yesu hata kama hajamuonaka.

3. Ni sababu gani ya pili yenye inafanya ikuwe nguvu kufanya urafiki pamoja na Yesu?

3 Sababu ya pili ni kwamba hatuwezi kuzungumuza na Yesu. Wakati tunasali, tunazungumuza moja kwa moja na Yehova. Kwa kweli, tunasali kupitia jina la Yesu, lakini hatuzungumuze moja kwa moja na Yesu. Yesu hapendi tusali kwake. Juu ya nini? Juu sala ni aina ya ibada, na ni Yehova tu njo mwenye tunapaswa kuabudu. (Mt. 4:10) Lakini tunaweza kuonyesha kama tunamupenda Yesu.

4. Sababu ya tatu ni gani, na tutazungumuzia nini katika habari hii?

4 Sababu ya tatu ni kwamba Yesu anaishi mbinguni, kwa hiyo, hatuwezi kupitisha wakati pamoja naye. Lakini tunaweza kujua mambo mingi juu ya Yesu bila kuwa pamoja naye. Tutazungumuzia mambo ine yenye tunaweza kufanya ili kutia nguvu urafiki wetu pamoja naye. Lakini, tuchunguze kwanza juu ya nini ni jambo la maana kufanya urafiki wa sana na Kristo.

JUU YA NINI TUNAPASWA KUWA MARAFIKI WA YESU?

5. Juu ya nini tunapaswa kuwa marafiki wa Yesu? (Ona visanduku  “Kuwa Marafiki wa Yesu Kunatusaidia Kuwa Marafiki wa Yehova” na “ Umutie Yesu pa Nafasi Yake.”)

5 Tunapaswa kuwa marafiki wa Yesu ikiwa tunapenda kuwa na urafiki muzuri pamoja na Yehova. Juu ya nini? Tuchunguze sababu mbili tu. Sababu ya kwanza, Yesu aliambia wanafunzi wake hivi: “Baba mwenyewe anawapenda ninyi, kwa sababu mumenipenda.” (Yoh. 16:27) Alisema pia hivi: “Hakuna mwenye anakuja kwa Baba isipokuwa kupitia mimi.” (Yoh. 14:6) Kujaribu kuwa rafiki ya Yehova bila kufanya urafiki wa sana na Yesu ni kama vile kujaribu kuingia katika nyumba bila kupita mu mulango. Yesu alitumia mufano kama huo wakati alijiita kuwa “mulango wa kondoo.” (Yoh. 10:7) Sababu ya pili ni kwamba Yesu alionyesha kwa ukamilifu sifa za Baba yake. Aliambia wanafunzi wake hivi: “Kila mutu mwenye ameniona mimi amemuona Baba pia.” (Yoh. 14:9) Kwa hiyo, njia kubwa ya kutusaidia tumujue Yehova ni kujifunza maisha ya Yesu. Kadiri tunajifunza juu ya Yesu, ni vile tutamupenda zaidi. Na wakati urafiki wetu pamoja na Yesu unakomaa, tutamupenda Baba yake zaidi.

6. Ni sababu gani ingine yenye inapaswa kutuchochea tukuwe na urafiki na Yesu? Fasiria.

6 Tunapaswa kuwa na urafiki na Yesu ili Mungu ajibu sala zetu. Hilo linaomba mambo mingi zaidi ya kusema tu “katika jina la Yesu” ku mwisho wa sala yetu. Tunapaswa kuelewa namna Yehova anamutumia Yesu ili kujibu sala zetu. Yesu aliambia mitume wake hivi: “Kila jambo lenye munaomba katika jina langu, nitalifanya.” (Yoh. 14:13) Hata kama ni Yehova njo mwenye anasikilizaka sala zetu na kuzijibu, amemupatia Yesu mamlaka ya kutimiza maamuzi yake. (Mt. 28:18) Kwa hiyo, mbele Mungu ajibu sala zetu, anaangalia kama tumetii mashauri yenye Yesu alitupatia. Kwa mufano, Yesu alisema hivi: “Kama munasamehe watu makosa yao, Baba yenu wa mbinguni atawasamehe ninyi pia; lakini kama hamusamehe watu makosa yao, Baba yenu pia hatawasamehe ninyi makosa yenu.” (Mt. 6:14, 15) Kwa hiyo, ni jambo la maana tutendee wengine muzuri kama vile Yehova na Yesu wanatutendea!

7. Ni nani watapata faida za zabihu ya bei ya ukombozi ya Yesu?

7 Ni wale tu wenye kuwa na urafiki pamoja na Yesu njo watapata faida za zabihu yake ya bei ya ukombozi. Ni nini inaonyesha vile? Yesu alisema kama ‘angetoa uzima wake kwa ajili ya marafiki wake.’ (Yoh. 15:13) Watu waaminifu wenye waliishi mbele Yesu akuje ku dunia watakuwa na lazima ya kujifunza juu yake na kufikia kumupenda. Wanaume na wanamuke kama vile Abrahamu, Sara, Musa, na Rahabu watafufuliwa, lakini hata watumishi hao waaminifu wa Yehova watakuwa na lazima ya kufanya urafiki na Yesu ili wapate uzima wa milele.​—Yoh. 17:3; Mdo. 24:15; Ebr. 11:8-12, 24-26, 31.

8-9. Kulingana na Yohana 15:4, 5, urafiki wetu na Yesu unatusaidia kufanya nini, na juu ya nini jambo hilo ni la maana?

8 Tunafurahi kutumika pamoja na Yesu katika kazi ya kuhubiri na kufundisha watu habari njema ya Ufalme. Wakati Yesu alikuwa ku dunia, alikuwa mwalimu. Na tangu wakati alirudia mbinguni, Yesu, akiwa kichwa cha kutaniko, anaendelea kuongoza kazi ya kuhubiri na kufundisha. Anaona na anapendezwa na bidii yenye unafanya ili kusaidia watu wengi kadiri inawezekana wamujue yeye na Baba yake. Kwa kweli, ni kupitia musaada wa Yehova na Yesu tu njo tunaweza kutimiza ile kazi.​—Soma Yohana 15:4, 5.

9 Neno la Mungu linafundisha waziwazi kama, ili tumupendeze Yehova, tunapaswa kumupenda Yesu na kuendelea kumupenda. Tuzungumuzie basi mambo ine yenye tunapaswa kufanya ili tukuwe marafiki wa Yesu.

NAMNA YA KUFANYA URAFIKI NA YESU

Unaweza kuwa rafiki wa Yesu kwa (1) kufikia kumujua muzuri zaidi, (2) kufikiri na kutenda kama yeye, (3) kutegemeza ndugu za Kristo, na (4) kuunga mukono mipango ya kutaniko (Ona fungu la 10-14) *

10. Ni jambo gani la kwanza lenye tunapaswa kufanya ili tukuwe marafiki wa Yesu?

10 (1) Ufikie kumujua Yesu. Tunaweza kufanya vile kwa kusoma vitabu vya Biblia kama vile Matayo, Marko, Luka, na Yohana. Wakati tunaendelea kufikiri sana juu ya habari za Biblia zenye kuzungumuzia maisha ya Yesu, tunafikia kumupenda Yesu na kumuheshimia kwa sababu alikuwa anatendea watu muzuri. Kwa mufano, hata kama alikuwa Bwana wao, hakutendea wanafunzi wake kama watumwa. Lakini aliwaambia mawazo yake ya ndani na namna alikuwa anajisikia. (Yoh. 15:15) Wakati walikuwa na huzuni, yeye pia alihuzunika, na alilia pamoja nao. (Yoh. 11:32-36) Hata maadui wake walijua kama alikuwa rafiki ya wale wenye walikubali ujumbe wake. (Mt. 11:19) Wakati tunamuiga Yesu katika namna yenye alitendea wanafunzi wake, uhusiano wetu na wengine unakuwa muzuri, tunajisikia kuwa wenye kutosheka na wenye furaha zaidi, na tunamupenda Kristo na kumuheshimia hata zaidi.

11. Ni jambo gani la pili lenye tunapaswa kufanya ili tukuwe marafiki wa Yesu, na juu ya nini jambo hilo ni la lazima?

11 (2) Ufikiri na kutenda kama Yesu. Kadiri tunajua na kuiga namna ya Yesu ya kufikiri, ni vile urafiki wetu pamoja na Yesu utakuwa nguvu. (1 Ko. 2:16) Namna gani tunaweza kumuiga Yesu? Fikiria mufano moja tu. Yesu alifikiria sana namna ya kusaidia wengine kuliko kujipendeza yeye mwenyewe. (Mt. 20:28; Ro. 15:1-3) Kwa sababu alikuwa na ile mawazo, alikuwa mwenye kujitoa kwa ajili ya wengine na mwenye kusamehe. Hakukuwa anakwazika mbio juu ya mambo yenye watu walikuwa wanasema juu yake. (Yoh. 1:46, 47) Na Yesu hakuacha makosa yenye mutu alifanya zamani imuchochee akuwe na mawazo ya mubaya juu ya ule mutu. (1 Ti. 1:12-14) Yesu alisema hivi: “Wote watajua kama ninyi ni wanafunzi wangu​—kama muko na upendo kati yenu.” (Yoh. 13:35) Ni muzuri ujiulize hivi: “Niko nafuata mufano wa Yesu kwa kufanya nguvu yangu yote ili kuendeleza amani pamoja na ndugu na dada zangu?”

12. Ni jambo gani la tatu lenye tunapaswa kufanya ili tukuwe marafiki wa Yesu, na namna gani tunaweza kufanya vile?

12 (3) Utegemeze ndugu za Kristo. Mambo yenye tunafanya kwa ajili ya ndugu zake watiwa-mafuta, Yesu anaona kuwa ni yeye njo tunafanyia ile mambo. (Mt. 25:34-40) Njia kubwa ya kutegemeza watiwa-mafuta ni kufanya kwa uwezo wetu wote kazi ya kuhubiri Ufalme na kufanya wanafunzi, yenye Yesu aliamuru wanafunzi wake wafanye. (Mt. 28:19, 20; Mdo. 10:42) Ni kwa musaada tu wa “kondoo wengine” njo ndugu za Kristo wanaweza kutimiza kazi ya kuhubiri mu dunia yote, yenye iko inafanywa sasa. (Yoh. 10:16) Kama uko kati ya kondoo wengine, kila wakati unafanya ile kazi, unaonyesha kama unapenda ndugu za Yesu na Yesu mwenyewe.

13. Namna gani tunaweza kutumia shauri la Yesu lenye kupatikana katika Luka 16:9?

13 Pia tunafanya urafiki pamoja na Yehova na Yesu kwa kutoa feza zetu ili kutegemeza kazi yenye wanaongoza. (Soma Luka 16:9.) Kwa mufano, tunaweza kutoa michango kwa ajili ya kazi yenye kufanywa mu dunia yote, na michango hiyo inatumiwa ili kutegemeza kazi ya kuhubiri habari njema katika maeneo ya mbali, kujenga na kutunza majengo yenye kutegemeza ibada ya kweli, na kupatia musaada wale wamepatwa na misiba ya asili ao misiba ingine. Tunaweza pia kutegemeza kutaniko letu kwa kutoa michango ya feza na kusaidia wale tunajua kama wako na lazima ya musaada. (Mez. 19:17) Zile ni njia za kutegemeza ndugu za Kristo.

14. Kulingana na Waefeso 4:15, 16, ni jambo gani la ine lenye tunapaswa kufanya ili tukuwe marafiki wa Yesu?

14 (4) Uunge mukono mipango ya kutaniko la Kikristo. Tunatia nguvu urafiki wetu na Yesu akiwa kichwa cha kutaniko wakati tunatii wale wenye ameweka ili kutuhangaikia. (Soma Waefeso 4:15, 16.) Kwa mufano, sasa tuko tunajaribu kuhakikisha kama Majumba yote ya Ufalme inatumiwa kabisa. Njo maana, makutaniko fulani imechangwa pamoja na mipaka ya maeneo imerekebishwa. Mupango huo umesaidia kutumia muzuri feza zenye kutolewa kwa ajili ya tengenezo la Yehova. Lakini, kwa wakati uleule, imeomba wahubiri fulani wajipatanishe na hali za mupya. Pengine wahubiri hao waaminifu wamekuwa katika kutaniko moja kwa miaka mingi na pengine wamefikia kupenda sana ndugu na dada katika kutaniko hilo. Lakini sasa wanaombwa kuhamia katika kutaniko lingine. Yesu anafurahi sana wakati anaona wanafunzi hao waaminifu wanaunga mukono mupango huo!

TUTAKUWA MARAFIKI WA YESU MILELE

15. Namna gani urafiki wetu pamoja na Yesu utakuwa nguvu zaidi wakati wenye kuja?

15 Wale wenye kutiwa mafuta kwa roho takatifu wako na tumaini la kuwa pamoja na Yesu milele. Watatawala pamoja naye katika Ufalme wa Mungu. Kwa kweli, watakuwa na Yesu, watamuona, watazungumuza naye na kupitisha wakati pamoja naye. (Yoh. 14:2, 3) Yesu atahangaikia pia na kuonyesha upendo wale wenye kuwa na tumaini la kuishi ku dunia. Hata kama hawatamuona Yesu, urafiki wao pamoja naye utaendelea kuwa nguvu kadiri watakuwa wanafurahia uzima wenye Yehova na Yesu watakuwa wamewapatia.​—Isa. 9:6, 7.

16. Kuwa marafiki wa Yesu kunatuletea baraka gani?

16 Wakati tunakubali mualiko wa Yesu wa kuwa marafiki wake, tunapata baraka mingi. Kwa mufano, anatuonyesha upendo na kututegemeza hata sasa. Tuko na tumaini la kuishi milele. Na jambo la maana zaidi, urafiki wetu pamoja na Yesu utatusaidia kupata utajiri muzuri zaidi kupita wote, ni kusema, urafiki pamoja na Baba ya Yesu, Yehova. Ni pendeleo kubwa sana kuitwa marafiki wa Yesu!

WIMBO 17 “Nataka”

^ fu. 5 Mitume walipitisha miaka fulani pamoja na Yesu; katika miaka hiyo walikuwa wanazungumuza na Yesu na kutumika pamoja naye. Kwa hiyo, wakakuwa marafiki wa sana. Yesu anapenda na sisi tukuwe marafiki wake, lakini haiko mwepesi kwetu kuwa marafiki wa Yesu kama vile ilikuwa mwepesi kwa mitume wake. Habari hii itazungumuzia mambo fulani yenye inafanya ikuwe nguvu kwetu kuwa marafiki wa Yesu, na itatutolea mapendekezo juu ya namna tunaweza kufanya urafiki wa nguvu na Yesu na kuendelea kuwa na urafiki huo.

^ fu. 55 MAFASIRIO YA PICHA: (1) Wakati wa ibada ya familia, tunaweza kujifunza juu ya maisha ya Yesu na utumishi wake. (2) Katika kutaniko, tunaweza kujikaza sana kuwa na amani pamoja na ndugu na dada zetu. (3) Tunaweza kutegemeza ndugu za Kristo kwa kuhubiri kwa uwezo wetu wote. (4) Wakati makutaniko inachangwa pamoja, tunaweza kuunga mukono maamuzi ya wazee.