Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 19

“Mufalme wa Kaskazini” Katika Wakati wa Mwisho

“Mufalme wa Kaskazini” Katika Wakati wa Mwisho

“Katika wakati wa mwisho mufalme wa kusini atasukumana naye [mufalme wa kaskazini].”​—DA. 11:40.

WIMBO 150 Mtafute Mungu Upate Ukombozi

KIFUPI CHA HABARI *

1. Unabii wa Biblia unatusaidia kujua nini?

NI NINI itapata watu wa Yehova hivi karibuni? Hatuna lazima ya kuwazia-wazia mambo. Unabii wa Biblia unatusaidia kujua mambo ya maana yenye itatupata sisi wote. Kuko unabii fulani wenye unatusaidia kujua mambo yenye serikali fulani za nguvu zaidi ku dunia zitafanya. Unabii huo unapatikana katika Danieli sura ya 11. Unazungumuzia historia ya wafalme wawili wenye kushindana, ni kusema, mufalme wa kaskazini na mufalme wa kusini. Sehemu kubwa ya unabii huo imekwisha kutimia, kwa hiyo, tunaweza kuwa hakika kama sehemu yenye kubakia itatimia pia.

2. Kulingana na Mwanzo 3:15 na Ufunuo 11:7 na 12:17, ni mambo gani ya maana yenye tunapaswa kukumbuka wakati tunajifunza unabii wa Danieli?

2 Ili tuelewe unabii wenye unapatikana katika Danieli sura ya 11, tunapaswa kujua kama unabii huo unazungumuzia tu watawala na serikali zenye zimetawala inchi kwenye watu wa Mungu waliishi, ao zenye zimeshambulia watu wa Mungu. Na hata kama watumishi wa Mungu wako kidogo sana ku dunia, mara mingi serikali za ulimwengu zinawatesa. Juu ya nini? Juu kusudi kubwa la Shetani na ulimwengu wake wote ni kuharibu wale wenye wanamutumikia Yehova na Yesu. (Soma Mwanzo 3:15 na Ufunuo 11:7; 12:17.) Tena, unabii wa Danieli unapaswa kupatana na unabii mwingine wa Biblia. Na tunapaswa kulinganisha unabii wa Danieli na sehemu zingine za Biblia ili tuelewe muzuri unabii huo.

3. Tutazungumuzia nini mu habari hii na mu habari yenye kufuata?

3 Kwa hiyo, tutazungumuzia sasa Danieli 11:25-39. Tutaona mufalme wa kaskazini alikuwa nani na mufalme wa kusini alikuwa nani kuanzia mwaka wa 1870 mupaka mwaka wa 1991, na tutaona juu ya nini ni muzuri tubadilishe namna tulikuwa tunaelewa sehemu moja ya unabii huo. Mu habari yenye kufuata, tutazungumuzia Danieli 11:40–12:1, na tutapata mafasirio ya mupya juu ya mambo yenye sehemu hiyo ya unabii inaonyesha kuhusu kipindi cha wakati kuanzia mwaka wa 1991 mupaka ku vita ya Armagedoni. Wakati unajifunza zile habari mbili, itakuwa muzuri uchunguze pia muchoro “Wafalme Wenye Kushindana Katika Wakati wa Mwisho.” Lakini, inafaa tujue kwanza wafalme hao wawili ni nani.

NAMNA YA KUTAMBUA MUFALME WA KASKAZINI NA MUFALME WA KUSINI

4. Ni mambo gani tatu yenye inatusaidia kutambua mufalme wa kaskazini na mufalme wa kusini?

4 Zamani, jina “mufalme wa kaskazini” lilizungumuzia mufalme mwenye alikuwa anatawala maeneo yenye ilikuwa kaskazini mwa Israeli na jina “mufalme wa kusini” lilizungumuzia mufalme mwenye alikuwa anatawala maeneo yenye ilikuwa kusini mwa Israeli. Juu ya nini tunasema vile? Juu malaika alimuambia Danieli hivi: “Nimekuja ili kukufanya uelewe mambo yenye yatapata watu wako [watu wa Mungu] katika kipindi cha mwisho cha zile siku.” (Da. 10:14) Kufikia Pentekoste ya 33 K.K.Y., taifa la Israeli la kimwili njo lilikuwa watu wa Mungu. Lakini, kuanzia wakati huo na kuendelea, Yehova alionyesha waziwazi kama wanafunzi waaminifu wa Yesu njo walikuwa sasa watu wake. Kwa hiyo, sehemu kubwa ya unabii wa Danieli sura ya 11 inahusu wanafunzi wa Kristo, hapana taifa la kimwili la Israeli. (Mdo. 2:1-4; Ro. 9:6-8; Gal. 6:15, 16) Na mufalme wa kaskazini na mufalme wa kusini wamebadilika-badilika kwa miaka mingi yenye imepita. Lakini, kuko mambo fulani yenye haikubadilika. Jambo la kwanza, wafalme hao walitawala inchi kwenye watu wa Mungu waliishi ao walishambulia watu wa Mungu. Jambo la pili, namna wametendea watu wa Mungu ilionyesha kama walimuchukia Mungu wa kweli, Yehova. Na jambo la tatu, wafalme hao wawili wamepigania mamlaka.

5. Je, kulikuwa mufalme wa kaskazini na mufalme wa kusini kati ya mwaka wa 100 na mwaka wa 1870? Fasiria.

5 Wakati fulani kisha mwaka wa 100, Wakristo wengi sana wa uongo walianza kuingia mu kutaniko la kweli la Kikristo; walifundisha mafundisho ya wapagani na kufanya kweli za Neno la Mungu zisikuwe wazi. Kuanzia wakati huo mupaka mwaka wa 1870, hapakukuwa kikundi cha watu wa Mungu wenye kupangwa muzuri ku dunia. Magugu, ni kusema, Wakristo wa uongo, waliongezeka sana na kufunika Wakristo wa kweli. (Mt. 13:36-43) Juu ya nini ni muzuri kujua jambo hilo? Juu jambo hilo linaonyesha kama mufalme wa kaskazini na mufalme wa kusini hawangekuwa watawala ao serikali zenye zilitawala kati ya mwaka wa 100 na mwaka wa 1870. Wakati huo hapakukuwa watu wa Mungu wenye kupangwa muzuri wenye wafalme hao wangeweza kushambulia. * Lakini, mufalme wa kaskazini na mufalme wa kusini wangetokea tena wakati kidogo kisha mwaka wa 1870. Juu ya nini tunasema vile?

6. Ni wakati gani watu wa Mungu walianza tena kuwa kikundi chenye kupangwa muzuri? Fasiria.

6 Kuanzia mwaka wa 1870, watu wa Mungu walianza tena kuwa kikundi chenye kupangwa muzuri. Ni katika mwaka huo njo Charles Taze Russell na wenzake walianzisha kikundi cha kujifunza Biblia. Ndugu Russell na wenzake walitimiza daraka la ule mujumbe mwenye alitabiriwa mwenye ‘alifungua njia’ mbele Ufalme wa Kimasiya usimamishwe. (Mal. 3:1) Yehova alikuwa tena sasa na kikundi cha watu wenye kupangwa muzuri! Je, kulikuwa serikali zenye zingeshambulia watumishi wa Mungu wakati huo? Acha tuone.

MUFALME WA KUSINI NI NANI?

7. Ni nani alikuwa mufalme wa kusini wakati wa Vita ya Kwanza ya Ulimwengu?

7 Kufikia mwaka wa 1870, Uingereza ilikuwa imekuwa serikali kubwa zaidi mu dunia, na ilikuwa na jeshi la nguvu zaidi mu dunia yote. Serikali hiyo ilifananishwa na pembe ya kidogo yenye ilishinda pembe zingine tatu, ni kusema, Ufaransa, Uhispania, na Uholanzi (Pays-Bas). (Da. 7:7, 8) Na serikali ya Uingereza ilikuwa mufalme wa kusini wakati wa Vita ya Kwanza ya Ulimwengu. Wakati uleule, Inchi ya Amerika ilikuwa imekuwa inchi tajiri zaidi mu dunia na ilianza kushirikiana sana na Uingereza.

8. Ni nani amekuwa mufalme wa kusini mu kipindi chote cha siku za mwisho?

8 Wakati wa Vita ya Kwanza ya Ulimwengu, serikali ya Amerika na Uingereza ilifanya mapatano ya kijeshi na jeshi lao lilikuwa na nguvu sana. Wakati huo, Uingereza na Amerika ikakuwa marafiki sana na ikakuwa Serikali Kubwa ya Ulimwengu ya Uingereza na Amerika. Kama vile Danieli alitabiri, mufalme huyo alijifanyia “jeshi kubwa sana na lenye nguvu.” (Da. 11:25) Mu siku za mwisho, serikali ya muungano ya Uingereza na Amerika imekuwa mufalme wa kusini. * Lakini sasa, ni nani amekuwa mufalme wa kaskazini?

MUFALME WA KASKAZINI ANATOKEA TENA

9. Ni wakati gani mufalme wa kaskazini alitokea tena, na namna gani Danieli 11:25 ilitimia?

9 Mu mwaka wa 1871, mwaka moja kisha Russell na wenzake kuanzisha kikundi chao cha kujifunza Biblia, mufalme wa kaskazini alitokea tena. Mwaka huo, Otto von Bismarck aliunganisha maeneo mingi na kuanzisha Utawala wa Ujerumani. Wilhelm wa Kwanza, mufalme wa eneo la Prussia, alikuwa mutawala wa kwanza wa utawala wa Ujerumani, na alimuweka Bismarck kuwa kiongozi wa serikali ya Ujerumani. * Mu miaka mingi yenye ilifuata, Ujerumani ilitawala inchi fulani katika Afrika na maeneo ya Bahari ya Pasifiki, na ilianza kushindana na Uingereza. (Soma Danieli 11:25.) Utawala wa Ujerumani ulifanya jeshi la nguvu na ulifikia kuwa na jeshi la pili mu dunia la maaskari wenye kupigana kwenye maji. Wakati wa Vita ya Kwanza ya Ulimwengu, Ujerumani ilitumia jeshi lake ili kupigana na maadui wake.

10. Namna gani Danieli 11:25b, 26 ilitimia?

10 Danieli alitabiri pia mambo yenye ingepata Utawala wa Ujerumani na jeshi lake. Unabii unasema kama mufalme wa kaskazini “hatasimama.” Sababu gani? “Kwa sababu watafanya mipango mibaya juu yake. Na wale wenye wanakula vyakula vyake vitamu watatokeza kuanguka kwake.” (Da. 11:25b, 26a) Wakati wa Danieli, wale wenye wanakula “vyakula vitamu vya mufalme” walitia ndani maofisa wakubwa wa mufalme wenye walikuwa ‘wanamutumikia mufalme.’ (Da. 1:5) Unabii huo unazungumuzia nani hapa? Unazungumuzia maofisa wa cheo cha juu katika Utawala wa Ujerumani, kutia ndani majenerali wa mutawala wa Ujerumani na washauri wa kijeshi, wenye walifikia kuangusha utawala huo. * Unabii haukusema tu kama utawala huo ungeanguka lakini ulionyesha pia matokeo ya vita yenye utawala huo ungepigana na mufalme wa kusini. Kuhusu mufalme wa kaskazini, unabii unasema hivi: “Lakini jeshi lake, litaharibiwa, na wengi watauawa.” (Da. 11:26b) Mu Vita ya Kwanza ya Ulimwengu, sawa vile tu unabii ulisema, jeshi la Ujerumani ‘liliharibiwa’ ao kushindwa, na watu wengi ‘waliuawa.’ Watu wengi walikufa katika ile vita kuliko vita ingine yoyote ya mbele ya pale.

11. Mufalme wa kaskazini na mufalme wa kusini walifanya nini?

11 Andiko la Danieli 11:27, 28 linazungumuzia mambo yenye ingetokea mbele ya Vita ya Kwanza ya Ulimwengu. Linasema kama mufalme wa kaskazini na mufalme wa kusini ‘wangekaa kwenye meza moja wakiambiana uongo.’ Linasema pia kama mufalme wa kaskazini angejikusanyia “mali nyingi.” Ni vile mambo ilikuwa kabisa. Ujerumani na Uingereza waliambiana kama walitaka amani, lakini maneno yao ilionekana kuwa uongo wakati vita ilitokea mu mwaka 1914. Na mu miaka ya mbele ya mwaka wa 1914, Ujerumani ilifikia kuwa inchi ya pili yenye kuwa tajiri zaidi mu dunia. Kisha, ili kutimiza Danieli 11:29 na sehemu ya kwanza ya mustari wa 30, Ujerumani ilipigana na mufalme wa kusini lakini ilishindwa.

WAFALME HAO WANASHAMBULIA WATU WA MUNGU

12. Wakati wa Vita ya Kwanza ya Ulimwengu, mufalme wa kaskazini na mufalme wa kusini walifanya nini?

12 Kuanzia mwaka wa 1914, wafalme hao wawili wameendelea kupigana kati yao na kushambulia watu wa Mungu tena na tena. Kwa mufano, wakati wa Vita ya Kwanza ya Ulimwengu, serikali ya Ujerumani na serikali ya Uingereza zilitesa watumishi wa Mungu, wenye walikataa kupigana vita. Na serikali ya Amerika ilitia ndani ya gereza ndugu wenye walikuwa wanaongoza kazi ya kuhubiri. Ile mateso ilitimiza unabii wa Ufunuo 11:7-10.

13. Mu miaka ya 1930 na wakati wa Vita ya Pili ya Ulimwengu, mufalme wa kaskazini alifanya nini?

13 Kisha, mu miaka ya 1930 na zaidi sana wakati wa Vita ya Pili ya Ulimwengu, mufalme wa kaskazini alishambulia watu wa Mungu bila huruma. Wakati chama cha Nazi kilianza kutawala Ujerumani, Hitler na wenzake walikataza kazi ya watu wa Mungu. Mufalme wa kaskazini aliua watumishi wengi wa Yehova na alituma maelfu mu kambi za mateso. Ile yote ilitabiriwa na Danieli. Mufalme wa kaskazini aliweza “kuchafua patakatifu” na “kuondoa zabihu ya kuendelea” kwa kuzuia kwa ukali watu wa Mungu wasisifu jina la Yehova waziwazi. (Da. 11:30b, 31a) Hitler, kiongozi wa chama cha Nazi alifikia hata kusema kama atamaliza watumishi wote wa Mungu katika Ujerumani.

MUFALME MUPYA WA KASKAZINI ANATOKEA

14. Ni nani alikuwa mufalme wa kaskazini kisha Vita ya Pili ya Ulimwengu? Fasiria.

14 Kisha Vita ya Pili ya Ulimwengu, serikali ya Kikomunisti ya Muungano wa Sovieti ilianza kutawala maeneo makubwa yenye ilikuwa imenyanganya Ujerumani, na ikakuwa mufalme wa kaskazini. Kama vile serikali ya kidikteta ya Nazi ilifanya, Muungano wa Sovieti ulitesa kila mutu mwenye alimutii Mungu wa kweli kuliko kutii serikali.

15. Mufalme wa kaskazini alifanya nini kisha Vita ya Pili ya Ulimwengu kumalizika?

15 Kisha tu Vita ya Pili ya Ulimwengu kumalizika, mufalme mupya wa kaskazini, ni kusema, Muungano wa Sovieti na inchi zenye kumuunga mukono, alishambulia watu wa Mungu. Kupatana na unabii wa Ufunuo 12:15-17, mufalme huyo alikataza kazi yetu ya kuhubiri na kupeleka maelfu ya watumishi wa Yehova mu uhamisho katika Siberia. Kwa kweli, katika kipindi chote cha siku za mwisho, mufalme wa kaskazini amemwanga “muto” wa mateso juu ya watu wa Mungu ili kujaribu kusimamisha kazi yao, lakini ameshindwa. *

16. Namna gani Muungano wa Sovieti ulitimiza unabii wa Danieli 11:37-39?

16 Soma Danieli 11:37-39. Ili kutimiza unabii huo, mufalme wa kaskazini ‘hakumuheshimia Mungu wa baba zake’ hata kidogo. Namna gani? Muungano wa Sovieti ulikuwa na kusudi la kuondoa dini zote, kwa hiyo, ulijaribu kuvunja mamlaka ya dini hizo. Tangu mwaka wa 1918, serikali ya Sovieti ilikuwa imetoa amri yenye ilifikia kufanya masomo ianze kufundisha wanafunzi kama hakuna Mungu. Namna gani mufalme huyo wa kaskazini ‘alimutukuza mungu wa ngome’? Muungano wa Sovieti ulitumia feza mingi ili kufanya jeshi lake likuwe nguvu na kutengeneza silaha mingi za nyuklia ili kutia nguvu mamlaka yake. Wote wawili, mufalme wa kaskazini na mufalme wa kusini, walifikia kujikusanyia silaha za nguvu zenye zinaweza kuua mamilioni ya watu!

MAADUI WAWILI WANATUMIKA PAMOJA

17. “Chukizo lenye linaleta uharibifu” ni nini?

17 Mufalme wa kaskazini ametumika pamoja na mufalme wa kusini katika jambo moja la maana. Walitumika pamoja ili ‘kusimamisha lile chukizo lenye linaleta uharibifu.’ (Da. 11:31) “Chukizo” hilo ni Umoja wa Mataifa.

18. Sababu gani Umoja wa Mataifa unaitwa “chukizo”?

18 Umoja wa Mataifa unaitwa “chukizo” kwa sababu unasema kama unaweza kufanya jambo fulani lenye Ufalme wa Mungu tu njo unaweza kufanya, ni kusema, kuleta amani mu dunia. Na unabii unasema kama chukizo hilo “linaleta uharibifu” kwa sababu Umoja wa Mataifa utashambulia na kuharibu dini zote za uongo.​—Ona muchoro “Wafalme Wenye Kushindana Katika Wakati wa Mwisho.”

JUU YA NINI NI LAZIMA TUJUE HISTORIA HII?

19-20. (a) Juu ya nini ni lazima tujue historia hii? (b) Habari yenye kufuata itajibu ulizo gani?

19 Ni lazima tujue historia hii kwa sababu inaonyesha kama kuanzia mwaka wa 1870 mupaka mwaka wa 1991, unabii wa Danieli kuhusu mufalme wa kaskazini na mufalme wa kusini ulitimia. Njo maana tunaweza kuwa hakika kama sehemu yenye inabakia ya unabii huo itatimia pia.

20 Mu mwaka wa 1991, Muungano wa Sovieti ulianguka. Sasa, nani njo mufalme wa kaskazini leo? Habari yenye kufuata itajibu ulizo hilo.

WIMBO 128 Kuvumilia Mpaka Mwisho

^ fu. 5 Tuko tunajionea mambo yenye kuhakikisha kama unabii wa Danieli juu ya “mufalme wa kaskazini” na “mufalme wa kusini” unaendelea kutimia. Juu ya nini tuko hakika na jambo hilo? Na juu ya nini tuko na lazima ya kuelewa mambo yenye unabii huo unazungumuzia?

^ fu. 5 Juu ya sababu yenye kuonyeshwa hapa, haifae tena kusema kama Mutawala wa Roma Aurélien (270-275 K.K.Y.) alikuwa “mufalme wa kaskazini” ao kama Malkia wa Siria Zenobia (267-272 K.K.Y.) alikuwa “mufalme wa kusini.” Hii mafasirio inabadilisha mambo yenye ilichapishwa mu sura ya 13 na 14 ya kitabu Sikiliza Unabii wa Danieli!

^ fu. 9 Mu mwaka wa 1890, Mufalme Wilhelm wa Pili alimuondoa Bismarck kwenye madaraka.

^ fu. 10 Walifanya mambo mingi yenye ilifanya utawala huo uanguke haraka. Kwa mufano, waliacha kumutegemeza mufalme, walifunua habari za siri kuhusu vita, na walilazimisha mufalme aache madaraka.

^ fu. 15 Kama vile Danieli 11:34 inaonyesha, kwa muda kidogo, mufalme wa kaskazini aliacha kutesa Wakristo wa kweli. Kwa mufano, ilikuwa vile wakati Muungano wa Sovieti ulianguka mu mwaka wa 1991.