Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 20

Ni Nani “Mufalme wa Kaskazini” Leo?

Ni Nani “Mufalme wa Kaskazini” Leo?

“Atakuja mupaka kwenye mwisho wake, na hakutakuwa mwenye atamusaidia.”​DA. 11:45.

WIMBO 95 Nuru Inazidi Kuongezeka

KIFUPI CHA HABARI *

1-2. Tutazungumuzia nini katika habari hii?

KULIKO zamani, leo tuko na mambo mingi yenye kuhakikisha kama tunaishi ku mwisho wa siku za mwisho za mupangilio huu wa mambo. Karibuni, Yehova na Yesu Kristo wataharibu serikali zote zenye zinapinga Ufalme wa Mungu. Mbele jambo hilo litokee, mufalme wa kaskazini na mufalme wa kusini wataendelea kupigana kati yao na kushambulia watu wa Mungu.

2 Katika habari hii, tutazungumuzia unabii wenye kupatikana mu Danieli 11:40–12:1. Tutajua mufalme wa kaskazini ni nani leo na tutaona juu ya nini hatupaswe kuogopa magumu yenye iko mbele.

MUFALME MUPYA WA KASKAZINI ANATOKEA

3-4. Ni nani mufalme wa kaskazini leo? Fasiria.

3 Kisha Muungano wa Sovieti kuanguka mu mwaka wa 1991, watu wa Mungu wenye walikuwa wanaishi katika eneo hilo kubwa walipata “musaada kidogo,” ni kusema, walipata uhuru kwa wakati fulani. (Da. 11:34) Kwa hiyo, waliweza kuhubiri kwa uhuru, na kisha wakati kidogo hesabu ya wahubiri iliongezeka sana mu inchi zenye zilikuwa sehemu ya Muungano wa Sovieti. Lakini, kisha miaka fulani, serikali ya Urusi na inchi zenye kuiunga mukono zilifikia kuwa mufalme wa kaskazini. Kama vile tulijifunza mu habari yenye kutangulia, kusudi serikali fulani ikuwe mufalme wa kaskazini ao mufalme wa kusini, inapaswa kufanya mambo tatu: (1) kutawala inchi kwenye watu wa Mungu wanaishi ao kuwashambulia, (2) kuonyesha kupitia matendo yake ao inamuchukia Yehova na watu wake, na (3) vkupigana na mufalme mwingine mushindani.

4 Ona sababu zenye zinatufanya tuseme kama serikali ya Urusi na inchi zenye kuiunga mukono njo mufalme wa kaskazini leo. (1) Zimeshambulia watu wa Mungu kwa kukataza kazi yao ya kuhubiri na kutesa mamia ya maelfu ya ndugu na dada wenye kuishi mu maeneo yenye wanaongoza. (2) Ile matendo yao inaonyesha kama wanamuchukia Yehova na watu wake. (3) Wameendelea kupigana na mufalme wa kusini, ni kusema, Serikali Kubwa ya Ulimwengu ya Uingereza na Amerika. Tuone basi namna serikali ya Urusi na inchi zenye kuiunga mukono zimetimiza daraka la mufalme wa kaskazini.

MUFALME WA KASKAZINI NA MUFALME WA KUSINI WANAENDELEA KUSUKUMANA

5. Danieli 11:40-43 inazungumuzia kipindi gani cha wakati, na ni mambo gani inafanyika wakati huo?

5 Soma Danieli 11:40-43. Sehemu hii ya unabii inazungumuzia wakati wa mwisho. Inaonyesha namna mufalme wa kaskazini na mufalme wa kusini wanaendelea kushindana. Danieli alitabiri kama, katika wakati wa mwisho, mufalme wa kusini “atasukumana” na mufalme wa kaskazini, ao “atapigana mapembe naye.”​—Da. 11:40; maelezo ya chini.

6. Ni nini inaonyesha kama wafalme wawili wameendelea kusukumana?

6 Mufalme wa kaskazini na mufalme wa kusini wanaendelea kushindana kwa sababu kila mumoja wao anapenda yeye njo atawale ulimwengu. Kwa mufano, fikiria mambo yenye ilitokea kisha Vita ya Pili ya Ulimwengu wakati Muungano wa Sovieti na inchi zenye kuunga mukono muungano huo zilianza kutawala sehemu kubwa ya Ulaya. Mufalme wa kusini alifanya mapatano na inchi zingine ili zitie pamoja majeshi yao juu ya kuanzisha shirika la kijeshi la kupiganisha mufalme wa kaskazini. Shirika hilo linaitwa Shirika la Makubaliano ya Atlantiki ya Kaskazini (OTAN). Mufalme wa kaskazini na mufalme wa kusini wanaendelea kushindana kwa kutumia feza mingi ili kutengeneza silaha za nguvu sana. Kila mumoja wao amepigana na mwingine kwa kutegemeza maadui wa mwenzake katika vita mu Afrika, Asia, na Amerika Latini. Mu miaka ya hivi karibuni, serikali ya Urusi na inchi zenye kuiunga mukono zimeeneza mamlaka yao mu dunia yote. Mufalme wa kaskazini na mufalme wa kusini wamepigana pia kwa kutumia ordinatere. Kila mumoja ameendelea kushitaki mwenzake kama iko anatumia programu za mubaya za ordinatere ili kufanya mwenzake apoteze feza na ili kuharibu serikali yake. Na kama vile Danieli alitabiri, mufalme wa kaskazini anaendelea kushambulia watu wa Mungu.​—Da. 11:41.

MUFALME WA KASKAZINI ANAINGIA KATIKA “INCHI YA LILE PAMBO”

7. “Inchi ya lile Pambo” ni nini?

7 Danieli 11:41 inasema kama mufalme wa kaskazini ataingia katika “inchi ya lile Pambo.” Ni inchi gani? Zamani, ilikuwa inchi ya Israeli; inchi ya Israeli ilionwa kuwa “ya muzuri sana kuliko inchi zote.” (Eze. 20:6) Lakini ile inchi ilikuwa ya maana sana, zaidi sana kwa sababu ni pale watu walikuwa wanamuabudia Yehova. Kuanzia Pentekoste ya mwaka wa 33 K.K.Y., ile “inchi” haiko inchi fulani yenye kupatikana mahali fulani ku dunia, na haiwezi kuwa vile, kwa sababu watu wa Yehova wanapatikana mu dunia yote. Lakini, leo “inchi ya lile Pambo” ni eneo la mufano kwenye watu wa Yehova wanafanyia mambo ya kiroho sawa vile kumuabudu Yehova kupitia mikutano na kazi ya kuhubiri.

8. Namna gani mufalme wa kaskazini ameingia katika “inchi ya lile Pambo”?

8 Katika siku za mwisho, mufalme wa kaskazini ameingia mara mingi katika “inchi ya lile Pambo.” Kwa mufano, wakati serikali ya Ujerumani yenye ilikuwa inaongozwa na chama cha Nazi ilikuwa mufalme wa kaskazini, zaidi sana wakati wa Vita ya Pili ya Ulimwengu, mufalme huyo aliingia katika “inchi ya lile Pambo” kwa kutesa na kuua watu wa Mungu. Kisha Vita ya Pili ya Ulimwengu, wakati Muungano wa Sovieti ulikuwa mufalme wa kaskazini, mufalme huyo aliingia katika “inchi ya lile Pambo” kwa kutesa watu wa Mungu na kuwapeleka mbali na makao yao.

9. Mu miaka ya hivi karibuni, namna gani serikali ya Urusi na inchi zenye kuiunga mukono zimeingia katika “inchi ya lile Pambo”?

9 Mu miaka ya hivi karibuni, serikali ya Urusi na inchi zenye kuiunga mukono zimeingia pia katika “inchi ya lile Pambo.” Namna gani? Mu mwaka wa 2017, mufalme huyu wa kaskazini amekataza kazi ya watu wa Yehova na kutia wamoja kati ya ndugu na dada zetu mu gereza. Pia, amekataza vichapo vyetu, na hata Tafsiri ya Ulimwengu Mupya. Tena, amenyanganya majengo ya biro yetu ya tawi katika Urusi na amenyanganya pia Majumba ya Ufalme na Majumba ya Mikusanyiko. Njo maana, mu mwaka wa 2018, Baraza Lenye Kuongoza limesema kama serikali ya Urusi na inchi zenye kuiunga mukono njo mufalme wa kaskazini. Lakini, hata wakati watu wa Yehova wanateswa kwa ukali, wanakataa kuunga mukono matendo yoyote ya kupinga serikali fulani ao kutafuta kuibadilisha. Kuliko kufanya vile, wanatii shauri la Biblia la kusali kwa ajili ya “wale wote wenye kuwa katika vyeo vya juu,” zaidi sana wakati watu hao wanakamata maamuzi yenye inahusu uhuru wa ibada.​—1 Ti. 2:1, 2.

JE, MUFALME WA KASKAZINI ATASHINDA MUFALME WA KUSINI?

10. Je, mufalme wa kaskazini atashinda mufalme wa kusini? Fasiria.

10 Unabii wenye kupatikana katika Danieli 11:40-45 unazungumuzia zaidi sana mambo yenye mufalme wa kaskazini atafanya. Maana yake atashinda mufalme wa kusini? Hapana. Mufalme wa kusini atakuwa angali ‘muzima’ wakati Yehova na Yesu wataharibu serikali zote ku vita ya Armagedoni. (Ufu. 19:20) Juu ya nini tuko hakika na jambo hilo? Fikiria mambo yenye unabii wa kitabu cha Danieli na Ufunuo unaonyesha.

Wakati wa Armagedoni, Ufalme wa Mungu, wenye kufananishwa na jiwe, utamaliza utawala wa wanadamu, wenye kufananishwa na sanamu kubwa (Ona fungu la 11)

 

11. Unabii wa Danieli 2:43-45 unaonyesha nini? (Ona picha ku jalada la gazeti hili.)

11 Soma Danieli 2:43-45. Nabii Danieli anazungumuzia serikali mbalimbali zenye zilishambulia watu wa Mungu. Zinafananishwa na sehemu mbalimbali za sanamu kubwa ya metali. Serikali ya mwisho kati ya serikali hizo inafananishwa na vikanyangio vya sanamu vyenye kutengenezwa na chuma chenye kuchanganywa na udongo. Vile vikanyangio vinafananisha Serikali Kubwa ya Ulimwengu ya Uingereza na Amerika. Unabii huo unaonyesha kama Serikali Kubwa ya Ulimwengu ya Uingereza na Amerika itakuwa ingali inatawala wakati Ufalme wa Mungu utapiga na kuharibu serikali za wanadamu.

12. Kichwa cha saba cha munyama wa pori kinafananisha nini, na juu ya nini ni jambo la maana kujua vile?

12 Mutume Yohana anazungumuzia pia serikali kubwa za ulimwengu zenye zilitawala watu wa Yehova. Katika unabii wa Yohana, serikali hizo zinafananishwa na munyama wa pori mwenye kuwa na vichwa saba. Kichwa cha saba cha ule munyama kinafananisha Serikali Kubwa ya Ulimwengu ya Uingereza na Amerika. Ni jambo la maana kujua vile kwa sababu hakuna vichwa vingine vyenye vinatokea kisha kichwa cha saba. Kichwa cha saba cha munyama huyu kitakuwa kingali kinatawala wakati Kristo na majeshi yake ya mbinguni watakiharibu pamoja na sehemu yenye kubakia ya ule munyama. *​—Ufu. 13:1, 2; 17:13, 14.

MUFALME WA KASKAZINI ATAFANYA NINI HIVI KARIBUNI?

13-14. “Gogu wa inchi ya Magogu” ni nani, na pengine ni nini itamuchochea ashambulie watu wa Mungu?

13 Unabii fulani wenye uliandikwa na Ezekieli, unatuambia mambo yenye inaweza kutokea katika siku za mwisho za mufalme wa kaskazini na mufalme wa kusini. Kama unabii wenye kupatikana katika Ezekieli 38:10-23; Danieli 2:43-45; 11:44–12:1; na Ufunuo 16:13-16, 21 unazungumuzia wakati na matukio ileile, basi tunaweza kutazamia mambo hii itokee.

14 Wakati fulani kisha taabu kubwa kuanza, “wafalme wa dunia yote yenye kuikaliwa na watu” watajiunga pamoja ili kufanya muungano wa mataifa. (Ufu. 16:13, 14; 19:19) Biblia inaita muungano huo “Gogu wa inchi ya Magogu.” (Eze. 38:2) Muungano huo wa mataifa utashambulia watu wote wa Mungu kwa mara ya mwisho na utajaribu kuwaharibu kabisa. Ni nini itachochea muungano huo ushambulie watu wa Mungu? Katika unabii fulani kuhusu wakati huo, mutume Yohana alisema kama mvua kubwa ya majiwe yenye haiko ya kawaida itapiga maadui wa Mungu. Mvua hiyo ya majiwe ya mufano inaweza kufananisha ujumbe mukali wa hukumu wenye watu wa Yehova watatangaza. Inawezekana ni ujumbe huo njo utachochea Gogu wa Magogu ashambulie watu wa Mungu ili awaharibu kabisa.​—Ufu. 16:21.

15-16. (a) Pengine Danieli 11:44, 45 inazungumuzia matukio gani? (b) Ni nini itapata mufalme wa kaskazini na serikali zingine zenye kufanyiza Gogu wa Magogu?

15 Pengine ujumbe huo mukali na shambulizi hilo la mwisho lenye litafanywa na maadui wa Mungu njo matukio yenye inazungumuziwa mu Danieli 11:44, 45. (Soma.) Katika andiko hilo, Danieli anasema kama “habari kutoka mashariki na kutoka kaskazini” zinasumbua mufalme wa kaskazini, na kwa hiyo, atatoka na iko na “kasirani kali.” Nia ya mufalme wa kaskazini ni “kuangamiza watu wengi.” Inaonekana kama “watu wengi” wenye andiko hilo linataja ni watu wa Yehova. * Pengine katika andiko hilo, Danieli iko anazungumuzia shambulizi la mwisho kabisa juu ya watu wa Mungu.

16 Shambulizi hilo lenye mufalme wa kaskazini atafanya pamoja na serikali zingine za dunia, linamufanya Mweza-Yote akasirike sana na kuleta vita ya Armagedoni. (Ufu. 16:14, 16) Wakati huo, mufalme wa kaskazini ataharibiwa pamoja na mataifa ingine yenye kufanyiza Gogu wa Magogu, na hakuna “mwenye atamusaidia.”​—Da. 11:45.

Ku vita ya Armagedoni, Yesu Kristo na majeshi yake ya mbinguni wataharibu ulimwengu muovu wa Shetani na kuokoa watu wa Mungu(Ona fungu la 17)

 

17. Mikaeli “ule mukubwa” mwenye Danieli 12:1 inazungumuzia ni nani, na anafanya nini?

17 Andiko lenye kufuata katika unabii wa Danieli linatupatia habari zaidi juu ya namna mufalme wa kaskazini na inchi zingine zenye kumuunga mukono zitaharibiwa na namna tutaokolewa. (Soma Danieli 12:1.) Andiko hili maana yake nini? Mikaeli ni jina lingine la Mufalme wetu mwenye kutawala, Kristo Yesu. ‘Amesimama kwa ajili’ ya watu wa Mungu tangu mwaka wa 1914 wakati Ufalme wake ulisimamishwa mbinguni. Hivi karibuni, ‘atasimama,’ ao ataharibu maadui wake, ku vita ya Armagedoni. Ile vita itakuwa tukio la mwisho mu kipindi chenye Danieli anaita “wakati wa taabu” kubwa kabisa katika historia. Unabii wa Yohana katika kitabu cha Ufunuo unaita wakati wenye utatangulia ile vita kuwa “taabu kubwa.”​—Ufu. 6:2; 7:14.

JINA LAKO ‘LITAANDIKWA KATIKA KILE KITABU’?

18. Sababu gani tunaweza kupambana bila woga na matukio ya wakati wenye kuja?

18 Tunaweza kupambana bila woga na matukio ya wakati wenye kuja kwa sababu Danieli na Yohana, wote wawili, wanaonyesha kama wale wenye kumutumikia Yehova na Yesu wataokoka kipindi hicho cha taabu kubwa yenye haijatokeaka. Danieli anasema kama majina ya wale wenye wataokoka itakuwa ‘imeandikwa katika kile kitabu.’ (Da. 12:1) Tunaweza kufanya nini ili majina yetu iandikwe katika kile kitabu? Tunapaswa kuonyesha waziwazi kama tuko na imani katika Yesu, Mwana-kondoo wa Mungu. (Yoh. 1:29) Tunapaswa kujitoa kwa Mungu na kubatizwa. (1 Pe. 3:21) Na tunapaswa kutegemeza Ufalme wa Mungu kwa kufanya yote yenye tunaweza ili kusaidia wengine wajifunze juu ya Yehova.

19. Tunapaswa kufanya nini sasa, na juu ya nini?

19 Sasa njo wakati wa kumutegemea Yehova zaidi na tengenezo lake lenye kufanyizwa na watumishi wake waaminifu. Sasa njo wakati wa kutegemeza Ufalme wa Mungu. Kama tunafanya vile, tutaokolewa wakati Ufalme wa Mungu utaharibu mufalme wa kaskazini na mufalme wa kusini.

WIMBO 149 Wimbo wa Ushindi

^ fu. 5 Ni nani “mufalme wa kaskazini” leo, na namna gani atafikia mwisho wake ao kuharibiwa? Kujua majibu ya ile maulizo kunaweza kutia nguvu imani yetu na kutusaidia tukuwe tayari kupambana na majaribu yenye itatupata hivi karibuni.