Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 22

Onyesha Kama Uko Mwenye Shukrani kwa Ajili ya Zawadi Zenye Hazionekane

Onyesha Kama Uko Mwenye Shukrani kwa Ajili ya Zawadi Zenye Hazionekane

‘Kaza macho [yako] . . . juu ya vitu vyenye havionekane. Kwa maana vitu vyenye vinaonekana ni vya wakati kidogo, lakini vitu vyenye havionekane ni vya milele.’​—2 KO. 4:18.

WIMBO 45 Kutafakari kwa Moyo Wangu

KIFUPI CHA HABARI *

1. Yesu alisema nini juu ya hazina za mbinguni?

KUKO zawadi fulani zenye haziwezi kuonekana. Kwa kweli, zawadi za maana zaidi ni zawadi zenye hatuwezi kuona. Katika Mahubiri yake ya Mulimani, Yesu alizungumuzia hazina za mbinguni zenye kuwa za maana sana kuliko vitu vya kimwili. Kisha aliongeza hivi: “Mahali kwenye kuko hazina yako, ni pale moyo wako pia utakuwa.” (Mt. 6:19-21) Kama tunaona kitu fulani kuwa cha maana sana, tutajikaza sana ili tukipate. Tunajiwekea “hazina mbinguni” kwa kujikaza kuwa na jina la muzuri, ao sifa ya muzuri, mbele ya Mungu. Yesu alisema kama hazina kama hizo haziwezi kuharibiwa ao kuibwa hata siku moja.

2. (a) Kulingana na 2 Wakorinto 4:17, 18, Paulo anatuomba tukaze macho juu ya vitu gani? (b) Tutazungumuzia nini katika habari hii?

2 Mutume Paulo anatuomba ‘tukaze macho yetu . . . juu ya vitu vyenye havionekane.’ (Soma 2 Wakorinto 4:17, 18.) Kati ya vitu hivyo, kuko baraka zenye tutapata mu ulimwengu mupya wa Mungu. Katika habari hii, tutazungumuzia zawadi ine zenye hazionekane zenye tunaweza kupata kuanzia sasa: urafiki pamoja na Mungu, zawadi ya sala, musaada wa roho takatifu, na musaada wenye Mungu na Yesu wanatupatia katika kazi yetu ya kuhubiri. Tutazungumuzia pia namna tunaweza kuonyesha kama tuko wenye shukrani kwa ajili ya zawadi hizo zenye hatuwezi kuona.

URAFIKI PAMOJA NA YEHOVA

3. Zawadi kubwa zaidi yenye haionekane ni gani, na ni nini inatuwezesha kuipata?

3 Zawadi kubwa zaidi yenye haionekane ni urafiki pamoja na Yehova Mungu. (Zb. 25:14) Inawezekana namna gani Mungu afanye urafiki na watu wenye zambi na aendelee kuwa mutakatifu kabisa? Inawezekana kwa sababu zabihu ya bei ya ukombozi ya Yesu ‘inatosha zambi ya ulimwengu.’ (Yoh. 1:29) Yehova alijua mbele ya wakati kama kusudi lake la kutolea wanadamu Mukombozi halingekosa kutimia hata kidogo. Njo maana iliwezekana Mungu afanye urafiki na watu wenye waliishi mbele Kristo akufe.​—Ro. 3:25.

4. Leta mifano ya wanaume fulani wenye waliishi mbele ya kuzaliwa kwa Yesu, wenye walifikia kuwa marafiki wa Mungu.

4 Fikiria wanaume fulani wenye waliishi mbele ya kuzaliwa kwa Yesu, wenye walifikia kuwa marafiki wa Mungu. Abrahamu alikuwa mwanaume mwenye alionyesha imani kubwa. Miaka zaidi ya 1 000 kisha Abrahamu kufa, Yehova alimuita “rafiki yangu.” (Isa. 41:8) Jambo hilo linaonyesha kama, hata wakati watu wanakufa, Yehova anaendelea kuwaona kuwa marafiki wake wa sana. Yehova anaendelea kumukumbuka Abrahamu. (Lu. 20:37, 38) Mufano mwingine ni Yobu. Wakati malaika wote walikusanyika pamoja mbinguni, Yehova alisema kwa uhakika kumuhusu Yobu. Yehova alimuita “mutu munyoofu na muaminifu-mushikamanifu, mwenye kumuogopa Mungu na kuepuka mambo ya mubaya.” (Yob. 1:6-8) Na Yehova alijisikia namna gani juu ya Danieli, mwenye alimutumikia kwa uaminifu kwa miaka karibu 80 katika inchi ya wapagani? Mara tatu, malaika walimuhakikishia mwanaume huyo mwenye kuzeeka kama alikuwa “mwenye samani sana” kwa Mungu. (Da. 9:23; 10:11, 19) Tunaweza kuwa hakika kama Yehova anapenda kabisa kufufua marafiki wake wapendwa wenye wamekufa.​—Yob. 14:15.

Ni katika njia gani tunaweza kuonyesha shukrani kwa ajili ya zawadi zenye hazionekane? (Ona fungu la 5) *

5. Ni nini inatuwezesha kufanya urafiki wa karibu pamoja na Yehova?

5 Leo, ni watu ngapi wenye hawakamilike wenye wako marafiki wa Yehova? Ni mamilioni ya watu. Tunajua vile kwa sababu wanaume, wanamuke, na watoto wengi mu dunia yote wako wanaonyesha kupitia mwenendo wao kama wanapenda kuwa marafiki wa Mungu. Yehova anafanya “urafiki wa karibu pamoja na watu wanyoofu.” (Mez. 3:32) Imani yao katika zabihu ya bei ya ukombozi ya Yesu njo inawawezesha kufanya urafiki pamoja na Mungu. Kupitia zabihu ya bei ya ukombozi, tunaweza kuwa marafiki wa Yehova na tunaweza kutoa maisha yetu kwake na kubatizwa. Wakati tunafanya ile mambo ya maana, tunajiunga na mamilioni ya Wakristo wenye wamejitoa kwa Yehova na kubatizwa, wenye wako na “urafiki wa karibu” pamoja na Mutu mukubwa zaidi katika ulimwengu wote!

6. Namna gani tunaweza kuonyesha kama tuko wenye shukrani kwa ajili ya urafiki wetu pamoja na Mungu?

6 Namna gani tunaweza kuonyesha kama tuko wenye shukrani kwa ajili ya urafiki wetu pamoja na Mungu? Kama vile Abrahamu na Yobu, wenye waliendelea kuwa waaminifu kwa Mungu kwa miaka zaidi ya mia moja, tunapaswa kubakia waaminifu, hata ikuwe tumemutumikia Yehova kwa muda gani katika mupangilio huu wa mambo. Kama Danieli, tunapaswa kuona urafiki wetu pamoja na Mungu kuwa wa maana sana kupita uzima wetu. (Da. 6:7, 10, 16, 22) Kwa musaada wa Yehova, tunaweza kuvumilia majaribu yote yenye tunapambana nayo na kuendelea kuwa marafiki wake wa karibu.​—Flp. 4:13.

ZAWADI YA SALA

7. (a) Kulingana na Mezali 15:8, namna gani Yehova anajisikiaka juu ya sala zetu? (b) Namna gani Yehova anajibu sala zetu?

7 Sala ni zawadi ingine yenye haionekane. Marafiki wa sana wanafurahiaka kuambiana mawazo yao na namna wanajisikia. Ni vile pia juu ya urafiki wetu pamoja na Yehova. Yehova anasema na sisi kupitia Neno lake, na katika Neno lake anatujulisha mawazo yake na namna anajisikia. Tunazungumuza naye kupitia sala, na tunaweza kumujulisha mawazo yetu ya ndani sana na namna tunajisikia kabisa. Yehova anafurahia kusikiliza sala zetu. (Soma Mezali 15:8.) Kwa sababu Yehova ni Rafiki mwenye upendo, hasikilizake tu sala zetu lakini anazijibu pia. Wakati fulani, anajibu sala zetu bila kukawia. Wakati mwingine, tunaweza kulazimika kuendelea kusali juu ya jambo fulani. Hata hivyo, tunaweza kuwa hakika kama jibu litakuja kwa wakati wenye kufaa na kwa njia yenye kufaa. Kwa kweli, Mungu anaweza kujibu sala yetu kwa njia yenye kuwa tofauti na vile tuliwazia. Kwa mufano, kuliko kutosha jaribu fulani, anaweza kutupatia hekima na nguvu ya “kulivumilia.”​—1 Ko. 10:13.

(Ona fungu la 8) *

8. Namna gani tunaweza kuonyesha kama tuko wenye shukrani kwa ajili ya zawadi ya sala?

8 Namna gani tunaweza kuonyesha kama tuko wenye shukrani kwa ajili ya zawadi ya muzuri sana ya sala? Njia moja ni kutii shauri lenye Mungu anatupatia la ‘kusali bila kuacha.’ (1 Te. 5:17) Yehova hatulazimishe tusali kwake. Lakini, anaheshimia uhuru wetu wa kuchagua na anatuomba ‘tudumu katika sala.’ (Ro. 12:12) Kwa hiyo, tunaweza kuonyesha kama tuko wenye shukrani kwa ajili ya zawadi ya sala wakati tunasali mara mingi kila siku. Kwa kweli, hatupaswe kusahau kumushukuru Yehova na kumusifu katika sala zetu.​—Zb. 145:2, 3.

9. Ndugu mumoja anajisikia namna gani juu ya sala, na wewe unajisikia namna gani juu ya zawadi hiyo?

9 Kadiri tunaendelea kumutumikia Yehova na kuona namna anajibu sala zetu, ni vile tunakuwa wenye shukrani zaidi kwa ajili ya zawadi ya sala. Fikiria mufano wa Chris, ndugu mwenye amefanya miaka 47 katika utumishi wa wakati wote. Anasema hivi: “Ninafurahia kuamuka asubui sana kila siku ili nisali kwa Yehova. Inafurahisha sana kuzungumuza na Yehova wakati jua linatokea na kila kitu kinaonekana kuwa chenye kupendeza! Jambo hilo linanichochea nimushukuru kwa ajili ya zawadi zake zote za muzuri, na hata zawadi ya sala. Na kisha kusali mangaribi, ninafurahi kabisa kuenda kulala na niko na zamiri ya muzuri.”

ZAWADI YA ROHO TAKATIFU

10. Juu ya nini tunapaswa kuona roho takatifu kuwa ya maana sana?

10 Roho takatifu ya Mungu ni zawadi ingine yenye haionekane yenye tunapaswa kuona kuwa ya maana sana. Yesu alituomba tuendelee kusali ili kupata roho takatifu. (Lu. 11:9, 13) Kupitia roho yake takatifu, Yehova anatupatia “nguvu zenye kupita zile za kawaida.” (2 Ko. 4:7; Mdo. 1:8) Roho takatifu ya Mungu inaweza kutusaidia kuvumilia majaribu yote yenye pengine tuko tunapambana nayo.

(Ona fungu la 11) *

11. Roho takatifu inaweza kutusaidia katika njia gani?

11 Roho takatifu inaweza kutusaidia kutimiza migao yetu katika utumishi wa Mungu. Roho ya Mungu inaweza kufanya vipawa vyetu na uwezo wetu mbalimbali ukuwe muzuri zaidi. Inatuwezesha kutimiza madaraka yetu ya Kikristo. Tunajua kama matokeo ya muzuri yenye tunapata katika kazi ya Mungu inawezekana tu kupitia musaada wa roho yake takatifu.

12. Kulingana na Zaburi 139:23, 24, tunaweza kumuomba Mungu roho yake takatifu ili itusaidie kufanya nini?

12 Namna gani tunaweza kuonyesha kama tunaona roho takatifu ya Mungu kuwa ya maana sana? Njia moja ni kumuomba Yehova roho yake takatifu ili itusaidie kutambua mawazo yote ya mubaya ao tamaa zote za mubaya zenye kuwa mu moyo wetu. (Soma Zaburi 139:23, 24.) Kama tunasali vile, Yehova anaweza kutumia roho yake takatifu ili kutusaidia kutambua mawazo na tamaa za mubaya zenye tuko nazo. Na kama tunatambua kuwa tuko na wazo ao tamaa fulani ya mubaya, tunapaswa kumuomba Mungu roho yake takatifu ili itupatie nguvu za kuachana kabisa na wazo ao tamaa hiyo. Kama tunafanya vile, Yehova ataona kama hatupendi kufanya jambo lolote lenye linaweza kufanya asitupatie roho yake takatifu.​—Efe. 4:30.

13. Tunaweza kufanya nini ili tukuwe wenye shukrani zaidi kwa ajili ya zawadi ya roho takatifu?

13 Tunaweza kuwa wenye shukrani zaidi kwa ajili ya roho takatifu wakati tunafikiri sana juu ya mambo yenye roho takatifu iko inatimiza leo. Mbele Yesu apande mbinguni, aliambia wanafunzi wake hivi: “Mutapokea nguvu wakati roho takatifu itakuja juu yenu, na mutakuwa mashahidi wangu . . . mupaka kwenye sehemu ya mbali zaidi ya dunia.” (Mdo. 1:8) Ile maneno iko inatimizwa katika njia ya ajabu. Kwa musaada wa roho takatifu, watu milioni munane na nusu hivi kutoka mu dunia yote wamekuwa waabudu wa Yehova. Pia, tunafurahia paradiso ya kiroho kwa sababu roho ya Mungu inatusaidia kukomalisha sifa za muzuri sana, kama vile upendo, furaha, amani, uvumilivu, fazili, wema, imani, upole, na kujizuia. Sifa hizo zinafanyiza “tunda la roho.” (Gal. 5:22, 23) Roho takatifu ni zawadi ya muzuri kabisa!

MUSAADA WA YEHOVA, YESU, NA MALAIKA KATIKA KAZI YETU YA KUHUBIRI

14. Wakati tuko katika mahubiri, tunapata musaada gani wenye hatuwezi kuona?

14 Tuko na zawadi ingine yenye haionekane: ‘kufanya kazi pamoja’ na Yehova, Yesu, na malaika. (2 Ko. 6:1) Tunafanya kazi pamoja nao kila wakati tunahubiri. Paulo alisema hivi juu yake mwenyewe na juu ya wale wenye wanasaidia katika kazi hiyo: “Sisi ni wafanyakazi pamoja na Mungu.” (1 Ko. 3:9) Wakati tunahubiri, tuko wafanyakazi pamoja na Yesu pia. Kisha kuamuru wafuasi wake ‘wafanye wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote,’ kumbuka kama Yesu alisema hivi: “Niko pamoja na ninyi.” (Mt. 28:19, 20) Na tuseme nini juu ya malaika? Tuko wenye shukrani sana kwamba malaika wanatuongoza wakati tunatangaza “habari njema ya milele . . . kwa wale wenye wanakaa katika dunia”!​—Ufu. 14:6.

15. Zungumuzia mufano moja wa Biblia wenye kuonyesha sehemu ya maana yenye Yehova anatimiza katika kazi yetu ya kuhubiri.

15 Musaada huo wenye hauonekane unatusaidia kutimiza nini? Wakati tunatangaza ujumbe wa Ufalme, mbegu fulani zinaanguka kwenye mioyo yenye kuwa tayari kukubali ujumbe wetu na zinakomaa. (Mt. 13:18, 23) Ni nani anafanya mbegu hizo za kweli zikomae na kuzaa matunda? Yesu anafasiria kama hakuna mutu mwenye anaweza kuwa mwanafunzi wake isipokuwa “Baba . . . amuvute.” (Yoh. 6:44) Biblia inazungumuzia mufano fulani wenye kuonyesha kama jambo hilo ni la kweli. Kumbuka wakati Paulo alihubiria kikundi cha wanamuke inje ya muji wa Filipi. Fikiria mambo yenye Biblia inasema juu ya mwanamuke mumoja kati yao, mwenye aliitwa Lidia. Biblia inasema kama ‘Yehova alifungua wazi moyo wake asikilize kwa uangalifu mambo yenye Paulo alikuwa anasema.’ (Mdo. 16:13-15) Kama vile Yehova alimuvuta Lidia, amevuta pia mamilioni ingine ya watu.

16. Ni nani mwenye anapaswa kusifiwa kwa ajili ya matokeo yote ya muzuri yenye tunapata katika kazi ya kuhubiri?

16 Ni nani anapaswa kusifiwa kwa ajili ya matokeo ya muzuri yenye tunapata katika mahubiri? Paulo alijibu ulizo hilo wakati aliandika hivi kuhusu kutaniko la Korinto: “Mimi nilipanda, Apolo akatia maji, lakini Mungu akaendelea kuikomalisha, kwa hiyo mwenye anapanda haiko kitu wala mwenye anatia maji, lakini Mungu mwenye anaikomalisha.” (1 Ko. 3:6, 7) Kama Paulo, tunapaswa kumusifu Yehova sikuzote kwa ajili ya matokeo yote ya muzuri yenye tunapata katika kazi ya kuhubiri.

17. Namna gani tunaweza kuonyesha kama tuko wenye shukrani kwa ajili ya pendeleo la ‘kufanya kazi pamoja’ na Mungu, Kristo, na malaika?

17 Namna gani tunaweza kuonyesha kama tuko wenye shukrani kwa ajili ya pendeleo la ‘kufanya kazi pamoja’ na Mungu, Kristo, na malaika? Tunaweza kufanya vile kwa kujikaza sana ili kupata nafasi za kutangazia wengine habari njema. Tunaweza kufanya vile katika njia mingi, kwa mufano, kuhubiri “mbele ya watu wote na nyumba kwa nyumba.” (Mdo. 20:20) Wengi wanafurahia pia mahubiri ya wakati wowote. Wakati wanakutana na mutu mwenye hawajue, wanamusalimia kwa urafiki na wanajaribu kuanzisha naye mazungumuzo. Kama iko tayari kuzungumuza, wanatumia ufundi ili kutafuta nafasi ya kuzungumuza naye juu ya habari njema.

(Ona fungu la 18) *

18-19. (a) Namna gani tunamwangia maji mbegu za kweli? (b) Zungumuzia mufano wenye kuonyesha namna Yehova alisaidia mwanafunzi mumoja wa Biblia.

18 Sisi “wafanyakazi pamoja na Mungu,” hatupaswe tu kupanda mbegu za kweli lakini tunapaswa pia kuzimwangia maji. Wakati mutu anaonyesha kama anapendezwa na kweli, tutafanya nguvu yetu yote ili kumurudilia ao kufanya mupango ili Shahidi mwingine amutembelee na kujaribu kuanzisha naye funzo la Biblia. Wakati funzo linaendelea, tunafurahi kuona namna Yehova anasaidia mwanafunzi abadilishe mawazo yake na namna anajisikia juu ya mambo mbalimbali.

19 Fikiria mufano wa Raphalalani, mufumu mumoja mu inchi ya Afrika ya Kusini. Alifurahia mambo yenye alikuwa anajifunza katika Biblia. Lakini, ilikuwa nguvu sana kwake kukubali mambo yenye Neno la Mungu linasema juu ya kupashana habari na mababu ao wazazi wa zamani wenye wamekufa. (Kum. 18:10-12) Polepole, alimuruhusu Mungu abadilishe mawazo yake. Na kisha wakati fulani, alifikia kuachana na kazi ya ufumu, hata kama hakukuwa na kazi ingine. Raphalalani, mwenye iko sasa na miaka 60, anasema hivi: “Niko mwenye shukrani sana kwa Mashahidi wa Yehova kwa sababu walinisaidia katika njia mingi; kwa mufano, walinisaidia kupata kazi. Zaidi ya yote, niko mwenye shukrani kwa Yehova kwa kunisaidia kufanya mabadiliko katika maisha yangu; leo ninaweza kufanya kazi ya kuhubiri nikiwa Shahidi wake mwenye kubatizwa.”

20. Unaazimia kufanya nini?

20 Katika habari hii, tumezungumuzia zawadi ine zenye hazionekane. Zawadi kubwa zaidi kati ya zote ni pendeleo la kufanya urafiki wa sana pamoja na Yehova. Wakati tunakuwa marafiki wa sana wa Yehova, tunaweza kupata zawadi zingine zenye hazionekane: kumukaribia katika sala, musaada wa roho takatifu ya Yehova, na musaada wa Yehova, Yesu, na malaika katika kazi yetu ya kuhubiri. Tuazimie kuonyesha kama tuko wenye shukrani zaidi kwa ajili ya zawadi hizo zenye hazionekane. Na tuendelee kumushukuru Yehova sikuzote kwa sababu iko Rafiki muzuri sana.

WIMBO 145 Ahadi ya Mungu Kuhusu Paradiso

^ fu. 5 Katika habari yenye ilitangulia, tulizungumuzia zawadi fulani zenye Mungu ametupatia zenye tunaweza kuona. Habari hii itazungumuzia zawadi zenye hatuwezi kuona na namna tunaweza kuonyesha kama tuko wenye shukrani kwa ajili ya zawadi hizo. Itatusaidia pia tukuwe wenye shukrani zaidi kwa Yehova Mungu, mwenye anatupatia zawadi hizo.

^ fu. 58 MAFASIRIO YA PICHA: (1) Wakati dada mumoja anaangalia vitu vyenye Yehova aliumba, anafikiri sana juu ya urafiki wake pamoja naye.

^ fu. 60 MAFASIRIO YA PICHA: (2) Dada uleule anamuomba Yehova nguvu ili aweze kutoa ushahidi.

^ fu. 62 MAFASIRIO YA PICHA: (3) Roho takatifu inamusaidia ule dada akuwe na uhodari ili kuhubiri wakati wowote.

^ fu. 64 MAFASIRIO YA PICHA (4) Ule dada anajifunza Biblia na mutu mwenye alihubiria wakati wowote. Dada yetu anafanya kazi ya kuhubiri na kufanya wanafunzi kwa musaada wa malaika.