Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 25

“Mimi Mwenyewe, Nitatafuta Kondoo Wangu”

“Mimi Mwenyewe, Nitatafuta Kondoo Wangu”

“Mimi mwenyewe, nitatafuta kondoo wangu, na nitawatunza.”​—EZE. 34:11.

WIMBO 105 “Mungu Ni Upendo”

KIFUPI CHA HABARI *

1. Juu ya nini Yehova alijilinganisha na mama mwenye kunyonyesha?

“JE, MWANAMUKE anaweza kumusahau mutoto wake mwenye kunyonya?” Yehova aliuliza vile mu siku za nabii Isaya. Mungu aliambia watu wake hivi: “Hata kama wanamuke hawa wanasahau, mimi siwezi kukusahau hata kidogo.” (Isa. 49:15) Mara mingi Yehova hajilinganishe na mama. Lakini, alifanya vile wakati huo. Yehova alitumia uhusiano kati ya mama na mutoto wake ili kuonyesha namna anapenda sana watumishi wake. Mama wengi wanaweza kujisikia kama dada mwenye kuitwa Jasmin, mwenye alisema hivi: “Wakati unanyonyesha mutoto wako, unafanya naye uhusiano wa pekee wenye utaendelea maisha yote.”

2. Yehova anajisikia namna gani wakati mutoto wake mumoja anaacha kumutumikia?

2 Yehova anatambua wakati hata mutoto wake mumoja anaacha kutaniko la Kikristo na anaacha kuhubiri. Kwa hiyo, wazia namna anaumia sana wakati anawaona maelfu ya watumishi wake wanaacha kutenda * kila mwaka.

3. Yehova anapenda nini?

3 Wengi kati ya ndugu na dada zetu hao wapendwa wenye wameacha kutenda wanarudia mu kutaniko, na tunafurahi sana wakati wanafanya vile! Yehova anapenda warudie, na sisi pia. (1 Pe. 2:25) Namna gani tunaweza kuwasaidia? Mbele ya kujibu ulizo hilo, ni muzuri tujue juu ya nini watu fulani wanaachaka kuhuzuria mikutano na kuhubiri.

JUU YA NINI WATU FULANI WANAACHAKA KUMUTUMIKIA YEHOVA?

4. Kazi inaweza kuletea watu fulani matokeo gani?

4 Ndugu na dada fulani wameacha kazi njo ikuwe jambo la maana zaidi mu maisha yao. Hung, * ndugu mumoja mwenye kuishi Asia ya Kusini-Mashariki anasema hivi: “Nilianza kutumia wakati na nguvu mingi ku kazi yangu. Juu sikukuwa na hekima, niliwaza kama nikikuwa na feza mingi, nitamutumikia Yehova muzuri. Kwa hiyo, nilianza kutumika saa mingi. Nilianza kukosa mikutano mara mingi mupaka nikaacha kutaniko. Shetani anatumia ulimwengu ili kufanya watu wakengeushwe na waache polepole kumutumikia Mungu.”

5. Dada mumoja alitenda namna gani kwa sababu ya magumu mbalimbali yenye ilimufikia?

5 Ndugu na dada fulani wako na magumu mingi yenye inawavunja moyo. Anne wa inchi ya Uingereza ni mama wa watoto tano. Anne anasema hivi: “Mutoto wangu mumoja alizaliwa na ulemavu mukubwa. Kisha wakati fulani, mutoto wangu mumoja mwanamuke alitengwa, na mutoto wangu mumoja mwanaume akagonjwa ugonjwa wa akili. Nilishuka moyo sana na nikaacha kuhuzuria mikutano na kuhubiri. Kisha, nikaacha kutenda.” Tunasikilia huruma Anne na familia yake na wengine wenye wako na magumu kama ile!

6. Namna gani kukosa kutumia shauri lenye kuwa katika Wakolosai 3:13 kunaweza kufanya mutu fulani aache kutaniko?

6 Soma Wakolosai 3:13. Watumishi fulani wa Yehova wamekwazwa na Mukristo mwenzao. Mutume Paulo alijua kama wakati fulani tunaweza kuwa na “sababu [ya muzuri] ya kulalamika juu ya” ndugu ao dada. Pengine hata tumetendewa bila haki. Kama hatuko waangalifu, tunaweza kuwa na kinyongo. Kisha, kinyongo kinaweza kufanya mutu aache kutaniko. Fikiria mufano wa Pablo, ndugu mumoja wa Amerika ya Kusini. Alisingiziwa kama alifanya jambo fulani la mubaya, kwa hiyo, akapoteza pendeleo fulani la utumishi mu kutaniko. Alitenda namna gani? Pablo anasema hivi: “Nilikasirika na polepole nikaacha kutaniko.”

7. Ni nini inaweza kufikia mutu mwenye zamiri inaendelea kumusumbua?

7 Kama mutu alitenda zambi zamani, zamiri inaweza kumusumbua kwa wakati murefu na kwa hiyo, anaweza kujisikia kama Mungu hawezi kumupenda. Hata kama alitubu na alionyeshwa rehema, anaweza kujisikia kuwa hastahili tena kuwa mutumishi wa Mungu. Ndugu mumoja mwenye kuitwa Francisco alijisikia vile. Anasema hivi: “Nilikaripiwa kwa sababu nilifanya uasherati. Hata kama niliendelea kwanza kuhuzuria mikutano, nilishuka moyo na nilijisikia kama sistahili kuwa kati ya watumishi wa Yehova. Zamiri yangu ilikuwa inanisumbua, na nilikuwa hakika kama Yehova hakunisamehe. Kisha wakati fulani, nikaacha kutaniko.” Unajisikia namna gani juu ya ndugu na dada wenye kuwa na magumu kama ile yenye tumezungumuzia? Unawasikilia huruma? Na jambo la maana zaidi, Yehova anajisikia namna gani juu yao?

YEHOVA ANAPENDA KONDOO WAKE

Muchungaji Mwisraeli alihangaikia sana kondoo mwenye alipotea (Ona fungu la 8-9) *

8. Je, Yehova anasahau watumishi wake wenye wameacha kumutumikia kwa wakati fulani? Fasiria.

8 Yehova hasahau watumishi wake wenye waliacha kumutumikia kwa wakati fulani; wala hasahau kazi yenye walifanya katika utumishi wake. (Ebr. 6:10) Nabii Isaya aliandika mufano muzuri sana ili kuonyesha namna Yehova anahangaikia watu wake. Isaya aliandika hivi: “Atatunza kundi lake kama muchungaji. Atakusanya wana-kondoo kwa mukono wake, na atawabeba kwenye kifua chake.” (Isa. 40:11) Muchungaji mukubwa anajisikia namna gani wakati kondoo wake mumoja anaacha kutaniko? Yesu alionyesha namna Yehova anajisikia wakati aliuliza wanafunzi wake hivi: “Munawaza nini? Kama mutu iko na kondoo mia moja (100), na mumoja anapotea, je, hataacha wale makumi kenda na kenda (99) kwenye milima na kuenda kutafuta ule mwenye alipotea? Na akimupata, hakika ninawaambia ninyi, anamufurahia zaidi kuliko wale makumi kenda na kenda (99) wenye hawakupotea.”​—Mt. 18:12, 13.

9. Namna gani wachungaji wazuri wa wakati wa zamani walikuwa wanatendea kondoo wao? (Ona picha ku jalada la gazeti hili.)

9 Juu ya nini ni jambo lenye kufaa kumulinganisha Yehova na muchungaji? Juu muchungaji muzuri wa wakati wa zamani alikuwa anahangaikia sana kondoo wake. Kwa mufano, Daudi alipigana na simba na dubu ili kulinda kundi lake. (1 Sa. 17:34, 35) Kwa kweli, muchungaji muzuri alikuwa anatambua wakati hata kondoo mumoja alikosekana. (Yoh. 10:3, 14) Muchungaji wa namna hiyo alikuwa anaacha kondoo wake 99 katika zizi (lupango ya kuchungia wanyama) kwenye walikuwa salama ao alikuwa anawaachia wachungaji wenzake ili kuenda kutafuta kondoo mumoja mwenye alikosekana. Yesu alitumia mufano huo ili kutufundisha kweli hii ya maana: “Baba yangu mwenye kuwa mbinguni hapendi hata mumoja wa hawa wadogo aangamie.”​—Mt. 18:14.

Muchungaji mumoja katika Israeli ya zamani anahangaikia kondoo mwenye alipotea (Ona fungu la 9)

YEHOVA ANATAFUTAKA KONDOO WAKE

10. Kulingana na Ezekieli 34:11-16, Yehova alitoa ahadi kama atafanyia nini kondoo wake wenye kupotea?

10 Yehova anapenda kila mumoja wetu, hata wale “wadogo” wenye wameacha kundi lake. Kupitia nabii Ezekieli, Mungu alitoa ahadi kama atatafuta kondoo wake wenye wamepotea na kuwasaidia wakuwe tena na urafiki muzuri pamoja naye. Na alionyesha mambo fulani yenye angefanya ili kuwakomboa, na ile mambo njo muchungaji wa kawaida katika Israeli alikuwa anafanya kama kondoo anapotea. (Soma Ezekieli 34:11-16.) Kwanza, muchungaji alikuwa anatafuta kondoo, na kufanya vile kungemuomba wakati na nguvu mingi. Kisha, wakati alipata kondoo mwenye alipotea, alikuwa anamurudisha kwenye kundi. Tena, kama kondoo aliumia ao alikuwa na njaa, muchungaji alikuwa anasaidia kwa upendo kondoo huyo mwenye kuwa zaifu, alikuwa anafunga vidonda vyake, alikuwa anamubeba, na kumupatia chakula. Wazee, wachungaji wa “kundi la Mungu,” wanapaswa kufanya mambo ileile ili kusaidia wale wote wenye wameacha kutaniko. (1 Pe. 5:2, 3) Wazee wanawatafuta, wanawasaidia kurudia katika kutaniko, na wanawaonyesha upendo kwa kuwatolea musaada wa kiroho wenye wako nao lazima. *

11. Muchungaji muzuri alielewa nini?

11 Muchungaji muzuri alielewa kama kondoo anaweza kupotea. Na kama kondoo anaenda mbali na kundi, muchungaji hakukuwa anamutendea kwa ukali. Fikiria mufano wenye Yehova alionyesha wakati alisaidia watumishi wake fulani wenye walimuacha kwa wakati fulani.

12. Namna gani Yehova alimutendea Yona?

12 Nabii Yona alikimbia mugao wake. Lakini, Yehova hakumuacha mara moja. Kama muchungaji muzuri, Yehova alimukomboa na alimusaidia apate tena nguvu yenye alikuwa nayo lazima ili atimize mugao wake. (Yon. 2:7; 3:1, 2) Kisha wakati fulani, Mungu alitumia mumea wa mutango ili kumusaidia Yona aelewe kama uzima wa kila mwanadamu ni wa maana. (Yon. 4:10, 11) Hilo linatufundisha nini? Wazee hawapaswe mara moja kuacha wale wenye wanaacha kutenda. Kuliko kufanya vile, wazee wanajikaza kuelewa ni nini ilifanya kondoo aache kundi. Na wakati ule kondoo anamurudilia Yehova, wazee wanaendelea kumuhangaikia kwa upendo.

13. Namna Yehova alimutendea muandikaji wa Zaburi ya 73 inatufundisha nini?

13 Muandikaji wa Zaburi ya 73 alivunjika moyo wakati aliangalia namna watu waovu walionekana kuwa walikuwa wanapata matokeo ya muzuri. Alianza kujiuliza ikiwa kufanya mapenzi ya Mungu kunaleta faida kabisa. (Zb. 73:12, 13, 16) Yehova alitenda namna gani? Hakumuhukumu ule mwanaume. Kwa kweli, Mungu aliandikisha maneno ya ule mwanaume mu Biblia. Kisha, ule muandikaji wa zaburi alifikia kutambua kama kuwa na urafiki muzuri pamoja na Yehova njo jambo lenye kuleta faida zaidi mu maisha kuliko mambo ingine yote. (Zb. 73:23, 24, 26, 28) Hilo linatufundisha nini? Wazee hawapaswe kuhukumu haraka-haraka wale wenye wanaanza kujiuliza ikiwa kumutumikia Yehova kunaleta faida. Kuliko kuwahukumu, wazee wanapaswa kutafuta kuelewa juu ya nini wanasema na kutenda kwa njia fulani. Kama tu wazee wanafanya vile njo wataweza kutumia Maandiko ili kuwatia moyo.

14. Juu ya nini Eliya alikuwa na lazima ya musaada, na namna gani Yehova alimutolea musaada wenye alikuwa nao lazima?

14 Nabii Eliya alimukimbia MalkiaYezebeli. (1 Fa. 19:1-3) Eliya aliwaza kama yeye tu njo nabii wa Yehova mwenye alikuwa amebakia, na kama kazi yake ilikuwa ya bure. Eliya alivunjika moyo sana mupaka akaomba akufe. (1 Fa. 19:4, 10) Yehova hakumuhukumu Eliya lakini alimuhakikishia kama hakukuwa peke yake, angeweza kutumainia nguvu za Mungu, na alikuwa angali na kazi mingi ya kufanya. Yehova alisikiliza kwa fazili mahangaiko ya Eliya na alimupatia migao ya mupya. (1 Fa. 19:11-16, 18) Hilo linatufundisha nini? Sisi wote, zaidi sana wazee, tunapaswa kutendea muzuri kondoo wa Yehova. Ikuwe mutu anasema kama iko na kasirani ao anajisikia kuwa Yehova hawezi kumusamehe, wazee watamusikiliza wakati anaonyesha mambo yenye kuwa mu moyo wake. Kisha, watajikaza kumuhakikishia kondoo mwenye amepotea kama Yehova anamuona kuwa wa maana.

NAMNA GANI TUNAPASWA KUONA KONDOO WA MUNGU WENYE WAMEPOTEA?

15. Kulingana na Yohana 6:39, namna gani Yesu aliona kondoo wa Baba yake?

15 Namna gani Yehova anapenda tuone kondoo wake wenye wamepotea? Mufano wa Yesu unatusaidia kupata jibu. Alijua kama Yehova anaona kondoo wake wote kuwa wa maana, njo maana alifanya mambo yote yenye aliweza ili kusaidia “kondoo wenye kupotea wa nyumba ya Israeli” wamurudilie Yehova. (Mt. 15:24; Lu. 19:9, 10) Kwa sababu Yesu ni muchungaji muzuri, alifanya mambo yote yenye aliweza ili hata kondoo mumoja wa Yehova asipotee.​—Soma Yohana 6:39.

16-17. Wazee wanapaswa kujisikia namna gani juu ya kusaidia wale wenye wameacha kutaniko? (Ona kisanduku “ Namna Kondoo Mwenye Amepotea Anaweza Kujisikia.”)

16 Mutume Paulo aliomba wazee wa kutaniko la Efeso waige mufano wa Yesu. Alisema hivi: “Munapaswa kusaidia wale wenye kuwa wazaifu, na munapaswa kuweka katika akili maneno ya Bwana Yesu, wakati yeye mwenyewe alisema: ‘Kuko furaha zaidi katika kutoa kuliko katika kupokea.’” (Mdo. 20:17, 35) Kwa kweli, leo wazee wako na daraka la maana la kuhangaikia watu wa Yehova. Salvador, muzee mumoja mu inchi ya Uhispania anasema hivi: “Wakati ninafikiria namna Yehova anahangaikia sana kondoo wake wenye wamepotea, hilo linanichochea kufanya mambo yote yenye ninaweza ili kuwasaidia. Kwa sababu mimi ni muchungaji wa kiroho, niko hakika kama Yehova anapenda niwahangaikie.”

17 Watu wote wenye tumezungumuzia katika habari hii wenye waliacha kutaniko walipata musaada na wakamurudilia Yehova. Kwa wakati huu, wengine wengi wenye wameacha kumutumikia Yehova wanapenda kumurudilia. Habari yenye kufuata itazungumuzia zaidi mambo yenye tunaweza kufanya ili kuwasaidia wamurudilie Yehova.

WIMBO 139 Wazia Wakati Vitu Vyote Vitakuwa Vipya

^ fu. 5 Juu ya nini watu fulani wenye wamemutumikia Yehova kwa uaminifu kwa miaka mingi wanaachaka kutaniko? Mungu anajisikia namna gani juu yao? Habari hii itajibu ile maulizo. Inazungumuzia pia mambo yenye tunaweza kujifunza kupitia namna Yehova alisaidia watu fulani wa zamani wenye waliacha kumutumikia kwa wakati fulani.

^ fu. 2 MAFASIRIO YA MANENO FULANI: Muhubiri mwenye hatende tena ni muhubiri fulani mwenye hakutoa ripoti ya mahubiri kwa miezi sita ao zaidi. Lakini, hata kama hawatende tena wangali ndugu na dada zetu, na tunawapenda.

^ fu. 4 Majina fulani imebadilishwa.

^ fu. 10 Habari yenye kufuata itaonyesha namna wazee wanafanya ile mambo tatu yenye wachungaji walikuwa wanafanya.

^ fu. 60 MAFASIRIO YA PICHA: Kwa sababu muchungaji Muisraeli alikuwa anahangaikia kondoo mwenye alipotea, alikuwa anamutafuta na kumurudisha katika kundi. Leo pia wachungaji wa kiroho wako wanafanya vile.

^ fu. 64 MAFASIRIO YA PICHA: Wakati dada mumoja mwenye hatende tena iko anangoja bisi iondoke, anaangalia Mashahidi wawili wenye wako wanahubiri kwa furaha mahali pa watu wengi.