Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 23

“Jina Lako Litakaswe”

“Jina Lako Litakaswe”

“Ee Yehova, jina lako linadumu milele.”​—ZB. 135:13.

WIMBO 10 Msifuni Yehova Mungu Wetu!

KIFUPI CHA HABARI *

1-2. Ni mambo gani mbili yenye Mashahidi wa Yehova wanaona kuwa ya maana sana?

KUKO mambo mbili ya maana sana yenye inatuhusu leo: mamlaka makubwa zaidi ya Yehova na kutakaswa kwa jina lake. Sisi Mashahidi wa Yehova, tunafurahia kuzungumuzia ile mambo yenye kupendeza. Lakini, hatupaswe kuona mamlaka makubwa zaidi ya Mungu na kutakaswa kwa jina lake kuwa mambo mbili tofauti.

2 Sisi wote tumefikia kuelewa kama jina la Mungu linapaswa kutakaswa. Pia, tumejifunza kama mamlaka makubwa zaidi ya Yehova, ao namna yake ya kutawala, njo inapaswa kuonekana kuwa ya muzuri zaidi. Kwa hiyo, tunapaswa kuona ile mambo mbili kuwa ya maana sana.

3. Jina Yehova linatia ndani nini?

3 Kwa kweli, jina Yehova linatia ndani mambo yote yenye inahusu Mungu wetu, na pia namna yake ya kutawala. Kwa hiyo, kutakasa jina la Mungu kunatia ndani kuonyesha kama namna yake ya kutawala njo ya muzuri zaidi. Jina la Yehova linahusiana sana na namna yake ya kutawala kwa sababu yeye njo mweza-yote Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi katika ulimwengu wote.​—Ona kisanduku “ Lile Jambo la Maana Zaidi Linatia Ndani Nini?

4. Zaburi ya 135:13 inasema nini juu ya jina la Mungu, na tutajibu maulizo gani katika habari hii?

4 Jina Yehova ni la pekee sana. (Soma Zaburi 135:13.) Juu ya nini jina la Mungu ni la maana sana? Namna gani lilichafuliwa kwa mara ya kwanza? Mungu analitakasa namna gani? Na namna gani tunaweza kusaidia kutetea jina la Mungu? Tujibu basi ile maulizo.

JUU YA NINI JINA NI LA MAANA?

5. Watu fulani wanaweza kujiuliza nini wakati wanasikia kama jina la Mungu linapaswa kutakaswa?

5 “Jina lako litakaswe.” (Mt. 6:9) Yesu alionyesha kama kutakaswa kwa jina la Mungu ni kati ya mambo ya maana zaidi yenye tunapaswa kuomba mu sala zetu. Lakini, Yesu alipenda kusema nini? Kutakasa jambo fulani maana yake kulifanya kuwa takatifu ao safi. Lakini watu fulani wanaweza kujiuliza hivi: ‘Kama jina la Yehova ni takatifu na safi, juu ya nini linapaswa kutakaswa?’ Ili kujibu ulizo hilo, tunapaswa kufikiria jina linatia ndani nini.

6. Sababu gani jina ni la maana sana?

6 Jina haiko tu maneno yenye inaweza kuandikwa ku karatasi ao kutamukwa. Ona mambo yenye Biblia inasema: “Inafaa kuchagua jina la muzuri kuliko kuchagua mali nyingi.” (Mez. 22:1; Muh. 7:1) Sababu gani jina ni la maana sana? Kwa sababu linatia ndani sifa ya mutu, ao mambo yenye watu wengine wanawaza juu ya ule mwenye kuwa na jina hilo. Kwa hiyo, namna jina linaandikwa, ao hata namna linatamukwa haiko njo jambo la maana; jambo la maana ni mambo watu wanawaza wakati wanaona ao kusikia jina hilo.

7. Namna gani watu wamechafua jina la Mungu?

7 Wakati watu wanasema mambo ya uongo juu ya Yehova, wanafanya wengine wawaze mambo ya mubaya juu yake. Wakati wanafanya vile, wanachafua jina lake. Ni mu bustani ya Edeni njo jina la Mungu lilichafuliwa kwa mara ya kwanza. Mambo yenye ilifanyika mu bustani ya Edeni inatufundisha nini?

NAMNA JINA LA MUNGU LILICHAFULIWA KWA MARA YA KWANZA

8. Adamu na Eva walikuwa wanajua nini, na hilo linatokeza maulizo gani?

8 Adamu na Eva walijua jina la Yehova, na walijua pia mambo ya maana juu yake. Walijua kama yeye njo Muumbaji, Ule mwenye aliwapatia uzima, makao yao ya muzuri yenye ilikuwa Paradiso, na ndoa kamilifu. (Mwa. 1:26-28; 2:18) Lakini, je, wangeendelea kufikiri juu ya mambo yote ya muzuri yenye Yehova alikuwa amewafanyia? Je, wangeendelea kukomalisha upendo wao kwa Yehova na kuwa wenye shukrani kwake? Majibu ya ile maulizo ilionekana wazi wakati adui ya Mungu aliwajaribu.

9. Kulingana na Mwanzo 2:16, 17 na 3:1-5, Mungu aliambia nini mwanaume na mwanamuke wa kwanza, na namna gani Shetani alipotosha kweli?

9 Soma Mwanzo 2:16, 17 na 3:1-5. Shetani alizungumuza na Eva kupitia nyoka, na akamuuliza hivi: “Je, ni kweli kwamba Mungu alisema hamupaswe kula matunda ya kila muti wa bustani?” Ulizo hilo lilikuwa na uongo fulani juu ya Mungu, na Eva akaanza kuwa na mawazo ya mubaya juu ya Mungu. Mungu alikuwa ameambia Adamu na Eva wakule matunda ya miti yote, isipokuwa tu muti moja. Wangeweza kula matunda ya aina mingi sana za miti. (Mwa. 2:9) Kwa kweli, Yehova ni mukarimu kabisa. Lakini, alikataza Adamu na Eva kula matunda ya muti moja. Kwa hiyo, ulizo la Shetani lilipotosha kweli. Alifanya ionekane kuwa Mungu hakukuwa mukarimu. Pengine Eva alijiuliza hivi: ‘Mungu ananiima jambo fulani la muzuri?’

10. Namna gani Shetani alichafua waziwazi jina la Mungu, na kufanya vile kulileta matokeo gani?

10 Mupaka pale, Eva alikuwa angali anamuona Yehova kuwa Mutawala wake. Alimuambia Shetani maagizo ya waziwazi yenye Mungu alikuwa amewapatia. Alisema pia kama hawakuruhusiwa hata kugusa ule muti. Alikuwa anajua muzuri kama Mungu aliwaonya kuwa ikiwa wangekosa kumutii, wangekufa. Lakini Shetani akajibu hivi: “Hakika hamutakufa.” (Mwa. 3:2-4) Shetani hakuficha tena uongo wake. Sasa, alichafua waziwazi jina la Mungu, ni kama vile alimuambia Eva kuwa Yehova ni muongo. Kwa kufanya vile, Shetani akakuwa ibilisi, ao muchongezi. Eva alidanganywa kabisa; akamuamini Shetani. (1 Ti. 2:14) Alimutumainia Shetani zaidi kuliko kumutumainia Yehova. Ile ilifanya ikuwe mwepesi kwa Eva kukamata uamuzi mubaya zaidi. Eva aliamua kukosa kumutii Yehova. Akaanza kula tunda lenye Yehova alikuwa amemukataza. Kisha, akamupatia pia Adamu.​—Mwa. 3:6.

11. Wazazi wetu wa kwanza wangeweza kufanya nini, lakini walishindwa kufanya nini?

11 Fikiria kidogo mambo yenye Eva alipaswa kumuambia Shetani. Wazia angemuambia jambo fulani kama vile: “Sikujue wewe, lakini ninamujua Baba yangu, Yehova, ninamupenda na ninamutumainia. Amenipatia mimi na Adamu kila kitu chenye tuko nacho. Sababu gani unaweza kusema mubaya vile juu yake? Toka kabisa mbele yangu!” Yehova angefurahi sana kusikia mutoto wake mupendwa anasema maneno kama ile, yenye kuonyesha ushikamanifu! (Mez. 27:11) Lakini, Eva hakukuwa na upendo mushikamanifu kwa Yehova; na Adamu pia hakukuwa na sifa hiyo. Sababu Adamu na Eva hawakukuwa na upendo mushikamanifu kwa Baba yao, walishindwa kutetea jina lake.

12. Namna gani Shetani alitia mashaka mu akili ya Eva, na Adamu na Eva walishindwa kufanya nini?

12 Kama vile tumeona, Shetani alianza kuchafua jina la Mungu kwa kutia mashaka mu akili ya Eva. Alimufanya akuwe na mashaka ikiwa Yehova alikuwa Baba muzuri. Njo maana Adamu na Eva walishindwa kutetea jina la Yehova, ni kusema, walishindwa kuonyesha kama mambo yenye Shetani alisema ilikuwa ya uongo kabisa. Jambo hilo lilifanya ikuwe mwepesi kwao kumusikiliza Shetani na kumuasi Baba yao. Leo, Shetani anatumia ufundi uleule. Anachafua jina la Mungu kwa kumusemea mambo ya uongo. Watu wenye wanaamini uongo wa Shetani wanakataa kwa vyepesi utawala wa Yehova wenye haki.

YEHOVA ANATAKASA JINA LAKE

13. Namna gani Ezekieli 36:23 inaonyesha ujumbe mukubwa wa Biblia?

13 Je, Yehova anavumilia tu uongo huo bila kujitetea? Hapana! Biblia yote iko na habari yenye kuonyesha mambo yenye Yehova amefanya ili kutakasa jina lake lenye lilichafuliwa mu bustani ya Edeni. (Mwa. 3:15) Kwa kifupi, ujumbe mukubwa wa Biblia ni huu: Yehova anatumia Ufalme wenye kuongozwa na Mwana wake ili kutakasa jina lake na kurudisha haki na amani ku dunia. Biblia iko na habari yenye inatusaidia kuelewa namna Yehova iko anatakasa jina lake.​—Soma Ezekieli 36:23.

14. Namna Yehova ameshugulikia uasi katika Edeni imetakasa jina lake. Imefanya vile namna gani?

14 Shetani amefanya nguvu yake yote ili kumuzuia Yehova kutimiza kusudi lake. Lakini, Shetani ameshindwa tena na tena. Biblia inaonyesha namna Yehova ametenda, na inaonyesha kama hakuna mwenye iko sawa na Yehova. Kwa kweli, uasi wa Shetani na wale wote wenye kumuunga mukono umemuletea Yehova huzuni mingi. (Zb. 78:40) Lakini, Yehova ameshugulikia uasi huo kwa hekima, uvumilivu, na haki. Pia, ameonyesha nguvu zake kubwa katika njia mingi sana. Zaidi ya yote, upendo wake unaonekana mu mambo yote yenye anafanya. (1 Yo. 4:8) Yehova ameendelea kutumika ili kutakasa jina lake.

Shetani alimuambia Eva mambo ya uongo juu ya Yehova, na kwa miaka mingi, ameendelea kumusingizia Mungu (Ona fungu la 9-10, 15) *

15. Namna gani Shetani iko anachafua jina la Mungu leo, na ile inaleta matokeo gani?

15 Shetani angali anachafua jina la Mungu leo. Anajikaza kufanya watu wakuwe na mashaka kama Mungu ni mwenye nguvu, haki, hekima, na upendo. Kwa mufano, Shetani anajikaza kufanya watu waamini kama Yehova haiko Muumbaji. Na kama watu wanakubali kuwa Mungu iko, Shetani anajikaza kuwafanya waamini kama Mungu haachie watu uhuru na haiko mwenye haki. Hata anafundisha watu kama Yehova hana huruma na anaunguza watu mu moto wa mateso. Wakati watu wanaamini ile mambo ya uongo, inakuwa mwepesi kwao kufanya jambo lingine, ni kusema, kupinga utawala wa Yehova wenye haki. Mupaka wakati ataharibiwa, Shetani ataendelea kumusingizia Yehova. Na atajaribu kukufanya wewe pia umuache Yehova. Ataweza?

DARAKA LAKO KUHUSU LILE JAMBO LA MAANA ZAIDI

16. Unaweza kufanya jambo gani lenye Adamu na Eva walishindwa kufanya?

16 Yehova anapatia wanadamu wenye hawakamilike nafasi ya kutakasa jina lake. Kwa kweli, unaweza kufanya jambo lenye Adamu na Eva walishindwa kufanya. Hata kama tuko katika ulimwengu wenye kujaa watu wenye kuchafua jina la Mungu, uko na nafasi ya kutetea kweli, ni kusema, kuonyesha kama Yehova ni mutakatifu, mwema, na mwenye upendo. (Isa. 29:23) Unaweza kuunga mukono utawala wake. Unaweza kuonyesha kama utawala wa Yehova tu njo wenye haki na njo wenye utaletea viumbe vyote amani na furaha.​—Zb. 37:9, 37; 146:5, 6, 10.

17. Namna gani Yesu alijulisha jina la Baba yake?

17 Wakati tunatetea jina la Yehova, tunafuata mufano wa Yesu Kristo. (Yoh. 17:26) Yesu alijulisha jina la Baba yake kwa kulitumia na pia kwa kutetea sifa ya Yehova. Kwa mufano, alipinga Wafarisayo, wenye walikuwa wanafanya Yehova aonekane kuwa mukali, mwenye kuwekea watu sheria mingi, mwenye watu hawawezi kukaribia, na mwenye hana huruma. Yesu alisaidia watu wamuone Baba yake kuwa mwenye usawaziko, mwenye upendo, na mwenye kusamehe. Pia, alisaidia watu wamujue Yehova kupitia namna aliiga kwa ukamilifu sifa za Baba yake mu maisha yake ya kila siku.​—Yoh. 14:9.

18. Namna gani tunaweza kusaidia watu wakatae mambo ya uongo yenye wamesikia juu ya Yehova?

18 Kama vile Yesu, tunaweza kusaidia watu wajue kweli juu ya Yehova, kwa kuwaonyesha kama Mungu ni mwenye upendo na mwema. Wakati tunafanya vile, tunasaidia watu wakatae mambo ya uongo yenye wamesikia juu ya Yehova. Tunatakasa jina la Yehova kwa kusaidia watu walione kuwa takatifu. Tunaweza pia kumuiga Yehova. Tunaweza kufanya vile hata kama hatukamilike. (Efe. 5:1, 2) Kupitia maneno na matendo yetu, tunasaidia watu wajue Yehova iko namna gani kabisa; na wakati tunafanya vile, tunasaidia kutakasa jina lake. Tunatetea jina la Yehova kwa kusaidia watu wajue kweli juu yake. * Pia, tunaonyesha kama watu wenye hawakamilike wanaweza kuwa waaminifu-washikamanifu kwa Mungu.​—Yob. 27:5.

Tunapenda kusaidia wanafunzi wetu wa Biblia wafikie kuelewa kama Yehova ni mwema na mwenye upendo (Ona fungu la 18-19) *

19. Namna gani Isaya 63:7 inatusaidia kujua kusudi letu kubwa wakati tunafundisha watu?

19 Ona jambo lingine lenye tunaweza kufanya ili kutakasa jina la Yehova. Wakati tunafundisha wengine kweli za Biblia, mara mingi tunakazia mamlaka makubwa zaidi ya Mungu, ni kusema kama tunakazia kuwa Yehova iko na haki ya kutawala ulimwengu wote, na ile ni kweli kabisa. Lakini, hata kama ni jambo la maana kufundisha watu sheria za Mungu, kusudi letu kubwa ni kusaidia watu wafikie kumujua Yehova, Baba yetu, na kuwa washikamanifu kwake. Kwa hiyo, tunapaswa kukazia sifa za muzuri za Yehova, ni kusema, kuonyesha watu mwenye jina hilo ni Mutu wa namna gani. (Soma Isaya 63:7.) Wakati tunafundisha watu kwa njia hiyo, tutawasaidia wamupende Yehova na kumutii kwa sababu wanapenda kuwa washikamanifu kwake.

20. Tutazungumuzia nini mu habari yenye kufuata?

20 Sasa, tunaweza kufanya nini ili mwenendo wetu na mafundisho yetu vitukuze jina la Yehova na kusaidia wengine wamukaribie? Habari yenye kufuata itajibu ulizo hilo.

WIMBO 2 Jina Lako Ni Yehova

^ fu. 5 Ni jambo gani la maana lenye linahusu wanadamu na malaika? Juu ya nini jambo hilo ni la maana sana, na namna gani linatuhusu? Kuelewa majibu ya ile maulizo na maulizo ingine kutatusaidia kutia nguvu urafiki wetu pamoja na Yehova.

^ fu. 18 Wakati fulani, vichapo vyetu vilionyesha kama jina la Yehova halina lazima ya kutetewa juu hakuna mwenye amesema kama Mungu hana haki ya kuwa na jina hilo. Lakini, mwangaza mupya ulitolewa ku mukutano wa kila mwaka wa 2017. Mwenyekiti alisema hivi: “Kwa kifupi, haiko mubaya kusali jina la Yehova litetewe kwa sababu sifa yake inapaswa kabisa kutetewa.”​—Ona programu ya JW Télédiffusion ya Mwezi wa 1, 2018 ku jw.org®. Fungua sehemu MAKTABA > JW TÉLÉDIFFUSION®.

^ fu. 62 MAFASIRIO YA PICHA: Ibilisi alimusingizia Mungu, alimuambia Eva kama Mungu ni muongo. Kwa miaka mingi, Shetani ameanzisha mawazo ya uongo, kama vile fundisho la kusema kama Mungu hana huruma na kama hakuumba wanadamu.

^ fu. 64 MAFASIRIO YA PICHA: Ndugu anakazia sifa za Mungu wakati anaongoza funzo la Biblia.