Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 29

“Wakati Niko Muzaifu, Ndio Wakati Ninakuwa na Nguvu”

“Wakati Niko Muzaifu, Ndio Wakati Ninakuwa na Nguvu”

“Ninapendezwa na uzaifu, na matusi, na nyakati za uhitaji, na mateso na magumu, kwa ajili ya Kristo.”​—2 KO. 12:10.

WIMBO 38 Atakupa Nguvu

KIFUPI CHA HABARI *

1. Mutume Paulo alijua nini juu yake mwenyewe?

MUTUME Paulo alikubali waziwazi kama wakati fulani alijisikia kuwa muzaifu. Alijua kama mwili wake ulikuwa ‘unaharibika,’ kama alipaswa kujikaza sana ili kufanya mambo yenye kuwa sawa, na kama Yehova hakujibu sala zake namna alitazamia. (2 Ko. 4:16; 12:7-9; Ro. 7:21-23) Paulo alijua pia kama watu wenye walimupinga walimuona kuwa muzaifu. * Lakini Paulo hakuacha maoni ya mubaya yenye watu walikuwa nayo juu yake ao uzaifu wake vimufanye ajisikie kuwa wa bure.​—2 Ko. 10:10-12, 17, 18.

2. Kulingana na andiko la 2 Wakorinto 12:9, 10, Paulo alijifunza jambo gani la maana?

2 Paulo alijifunza jambo fulani la maana, ni kusema, mutu anaweza kuwa na nguvu hata kama anajisikia kuwa muzaifu. (Soma 2 Wakorinto 12:9, 10.) Yehova alimuambia Paulo kama nguvu Zake “zinakamilishwa katika uzaifu,” ni kusema, Yehova angemupatia Paulo nguvu yenye alikuwa nayo lazima. Kwanza, tuone sababu gani hatupaswe kuhangaika wakati maadui wetu wanatutukana.

‘PENDEZWA . . . NA MATUSI’

3. Sababu gani tunapaswa kupendezwa na matusi?

3 Hakuna mutu mwenye anapendaka kutukanwa. Lakini, wakati maadui wetu wanatutukana na tunahangaishwa sana na mambo yenye wanasema, ile inaweza kutufanya tuvunjike moyo. (Mez. 24:10) Sasa, tunapaswa kuona namna gani matusi ya watu wenye kutupinga? Kama Paulo, tunaweza ‘kupendezwa . . . na matusi.’ (2 Ko. 12:10) Sababu gani? Sababu wakati watu wanatutukana na kutupinga ile inaonyesha kama tuko wanafunzi wa kweli wa Yesu. (1 Pe. 4:14) Yesu alisema kama wafuasi wake wangeteswa. (Yoh. 15:18-20) Ile ilitokea katika karne ya kwanza (1-100). Wakati huo, watu wenye walichochewa na desturi ya Wagiriki waliona Wakristo kuwa watu wenye hawana akili na wazaifu. Na kati ya Wayahudi, Wakristo walionwa kuwa “watu wenye hawana elimu na watu wa kawaida,” kama vile waliona Petro na Yohana. (Mdo. 4:13) Wakristo walionekana kuwa wazaifu; hawakukuwa wanajiingiza mu mambo ya politike ao ya vita, kwa hiyo hawangetazamia serikali ao jeshi iwapiganie ao kuwalinda. Pia, walikataliwa na watu.

4. Wakristo wa karne ya kwanza walitenda namna gani wakati watu walikuwa na maoni yenye haifae kuwahusu?

4 Wale Wakristo hawakuacha maoni ya mubaya ya wapinzani wao iwafanye wasikuwe tena wanafunzi wa Yesu na waache kuhubiri. Kwa mufano, mutume Petro na Yohana, waliona kama ni pendeleo kuteswa kwa sababu ya kumufuata Yesu na kufundisha wengine juu ya Yesu. (Mdo. 4:18-21; 5:27-29, 40-42) Wanafunzi wa Yesu hawakukuwa na sababu yoyote ya kusikia haya. Wakristo hao wanyenyekevu wa karne ya kwanza walifanyia wanadamu mambo mingi ya muzuri kuliko wapinzani wao wote. Kwa mufano, vitabu vyenye viliongozwa na roho ya Mungu vyenye wamoja kati ya wale Wakristo waliandika, vinaendelea kusaidia mamilioni ya watu na kuwapatia tumaini. Na Ufalme wenye walitangaza uko sasa unatawala mbinguni, na tena karibuni utatawala wanadamu wote. (Mt. 24:14) Serikali kubwa ya zamani ya Roma yenye ilitesa Wakristo imepotea kabisa, lakini wale wanafunzi washikamanifu wako wafalme mbinguni. Wapinzani wao wamekwisha kufa; na hata kama walichukia wanafunzi wa Yesu, ikiwa watafufuliwa, watakuwa raia wa Ufalme wenye wale wanafunzi walitangaza.​—Ufu. 5:10.

5. Kulingana na Yohana 15:19, juu ya nini watumishi wa Yehova wanazarauliwa?

5 Leo, sisi watu wa Yehova, wakati fulani watu wanatucheka ao kutuzarau na wanatuona kuwa wenye hawana akili na wazaifu. Juu ya nini? Juu hatuna tabia za watu wenye kutuzunguka. Tunajikaza kuwa wanyenyekevu, wapole na wenye kutii. Tofauti na ile, ulimwengu unafurahia watu wenye kiburi, majivuno, na waasi. Zaidi ya ile, hatujiingize mu mambo ya politike, na hatuunge mukono jeshi la inchi yoyote. Hatuige tabia za watu wa ulimwengu, kwa hiyo wanatuona kuwa watu wa hali ya chini.​—Soma Yohana 15:19; Ro. 12:2.

6. Yehova iko anasaidia watu wake kutimiza kazi gani?

6 Hata kama watu wa ulimwengu wanatuona kuwa wazaifu, Yehova iko anatutumia ili kutimiza mambo ya ajabu. Iko anatimiza kampanye kubwa sana ya kuhubiri yenye haijafanyikaka mu historia ya wanadamu. Watumishi wake leo, wako wanatoa magazeti yenye iko inatafsiriwa na kugawanywa sana katika dunia, na wanatumia Biblia ili kusaidia mamilioni ya watu wakuwe na maisha ya muzuri. Yehova anastahili kusifiwa kwa ajili ya ile mambo ya maana yenye kutimizwa, kwa sababu ni yeye njo iko anatumia kikundi cha watu wenye kuonekana kuwa wazaifu ili wafanye ile kazi kubwa. Lakini tuseme nini kuhusu kila mumoja wetu kipekee? Je, Yehova anaweza kutusaidia tukuwe na nguvu? Ikiwa ni vile, tunapaswa kufanya nini ili tupate musaada wake? Tuzungumuzie sasa mambo tatu ya maana yenye tunaweza kujifunza kupitia mufano wa mutume Paulo.

USITEGEMEE NGUVU YAKO MWENYEWE

7. Mufano wa Paulo unatufundisha nini?

7 Jambo moja lenye mufano wa Paulo unatufundisha ni hili: Wakati tunamutumikia Yehova, tusitegemee nguvu ao uwezo wetu wenyewe. Kwa mawazo ya wanadamu, Paulo alikuwa na sababu ya kuwa mutu mwenye majivuno na mwenye kujitumainia. Alikomalia katika Tarso, muji mukubwa wa jimbo fulani la Roma. Tarso ilikuwa muji wenye utajiri na ilikuwa na masomo ya juu yenye ilijulikana sana. Paulo alikuwa mutu mwenye elimu sana, alifundishwa na kiongozi Muyahudi mwenye aliheshimiwa sana wa wakati wake, mwenye kuitwa Gamalieli. (Mdo. 5:34; 22:3) Na kwa kiasi fulani, Paulo alikuwa mutu wa maana sana katikati ya Wayahudi. Alisema hivi: “Nilikuwa ninafanya maendeleo makubwa katika dini ya Kiyahudi kuliko watu wengi wa miaka yangu katika taifa langu.” (Gal. 1:13, 14; Mdo. 26:4) Lakini Paulo hakujitegemea.

Paulo aliona mambo yenye ingefanya aonekane kuwa mutu wa maana, kwa maoni ya wanadamu, kuwa “uchafu mwingi” kwa kuilinganisha na pendeleo la kumufuata Kristo (Ona fungu la 8) *

8. Kulingana na Wafilipi 3:8 na maelezo ya chini, namna gani Paulo aliona mambo yenye aliacha, na juu ya nini ‘alipendezwa na uzaifu’?

8 Paulo alifurahia kuacha mambo yenye ingefanya aonekane kuwa mutu wa maana kwa maoni ya wanadamu. Kwa kweli, alifikia kuona ile mambo kuwa “uchafu mwingi.” (Soma Wafilipi 3:8 na maelezo ya chini.) Paulo alipata magumu mingi kwa sababu alikubali kuwa mufuasi wa Kristo. Alichukiwa na watu wa taifa lake mwenyewe. (Mdo. 23:12-14) Raia wenzake, Waroma, walimupiga na kumufunga mu gereza. (Mdo. 16:19-24, 37) Zaidi ya ile, Paulo alikubali kama hakukuwa mukamilifu na kama ilikuwa nguvu kwake kufanya mambo yenye kuwa sawa. (Ro. 7:21-25) Lakini kuliko kuacha maadui wake ao uzaifu wake umufanye aache kumufuata Kristo, ‘alipendezwa na uzaifu.’ Juu ya nini? Juu wakati alikuwa muzaifu njo aliona nguvu za Mungu zinafanya kazi katika maisha yake.​—2 Ko. 4:7; 12:10.

9. Utafanya nini kama unakosa mambo fulani?

9 Ikiwa tunapenda kupata nguvu kutoka kwa Yehova hatupaswe kuwaza kama ni nguvu zetu za kimwili, elimu, desturi ao utajiri wetu wa kimwili njo vinafanya tukuwe watu wa maana sana. Ile mambo haiko njo yenye inafanya Yehova atutumie. Kwa kweli, kati ya watu wa Mungu hakuna wengi “wenye hekima katika njia ya kimwili, . . . hakuna wengi wenye nguvu, hakuna wengi wenye kuwa wa kizazi chenye cheo.” Lakini, Yehova alichagua kutumikisha “vitu zaifu vya ulimwengu.” (1 Ko. 1:26, 27) Kwa hiyo, kama unakosa mambo yenye kutajwa ku mwanzo wa fungu hili, usiwaze kama hauwezi kumutumikia Yehova. Tofauti na ile, uone hali yako kuwa nafasi ya kujionea namna Yehova anakupatia nguvu. Kwa mufano, kama unajisikia kuwa unaogopa watu wenye wanajaribu kukufanya ukuwe na mashaka juu ya imani yako, umuombe Yehova akupatie uhodari wakati uko unatetea imani yako. (Efe. 6:19, 20) Kama uko unapambana na ugonjwa fulani wa muda murefu, umuombe Yehova akupatie nguvu yenye uko nayo lazima ili uendelee kuwa na mambo mingi ya kufanya katika kazi yake, kulingana na uwezo wako. Kila mara, wakati unaona Yehova anakusaidia, imani yako itaongezeka na utakuwa na nguvu zaidi.

UJIFUNZE KUPITIA MIFANO YA WATU WENYE KUZUNGUMUZIWA KATIKA BIBLIA

10. Juu ya nini tunapaswa kujifunza mifano ya watu waaminifu wenye kuzungumuziwa katika Biblia, kama vile wale wenye kutajwa katika andiko la Waebrania 11:32-34?

10 Paulo alikuwa anajifunza Maandiko kwa bidii, na alijifunza pia mambo mingi kupitia mifano ya watu waaminifu wenye kuzungumuziwa katika Neno la Mungu. Wakati aliandikia Wakristo Waebrania, Paulo aliwaomba wafikirie mifano ya watumishi wengi waaminifu wa Yehova. (Soma Waebrania 11:32-34.) Fikiria Mufalme Daudi, mumoja wa wale watumishi wa Yehova. Alipaswa kupambana na upinzani wa maadui wake, lakini pia wa watu wenye kwa wakati fulani walikuwa marafiki wake. Wakati tunafikiria mufano wa Daudi, tutaona kama Paulo alipata nguvu kwa sababu alifikiri sana juu ya mufano wa Daudi, na tutaona namna tunaweza kufuata mufano wa Paulo.

Daudi hakuogopa kupigana na Goliati hata kama alikuwa kijana na alionekana kuwa hana nguvu. Alimutegemea Yehova, sababu alijua kama Yehova angemupatia nguvu ya kumushinda Goliati, na ni vile alifanya (Ona fungu la 11)

11. Juu ya nini Daudi alionekana kuwa muzaifu? (Ona picha ku jalada la gazeti hili.)

11 Goliati, askari mwenye alikuwa na nguvu mingi za kimwili, alimuona Daudi kuwa muzaifu. Wakati Goliati alimuona Daudi, “akamuchekelea kwa zarau.” Kusema kweli, Goliati alikuwa murefu na munene, alikuwa na silaha mingi za vita, na alikuwa amezoezwa muzuri kwa ajili ya vita. Kwa upande wake, Daudi alikuwa tu kijana mwenye hana uzoefu, mwenye alionekana kuwa hana vifaa vyenye kufaa kwa ajili ya vita. Lakini Daudi alifanya jambo lenye lilionekana kuwa uzaifu ligeuke kuwa nguvu. Alimutumainia Yehova ili apate nguvu, na akapata ushindi juu ya adui yake.​—1 Sa. 17:41-45, 50.

12. Daudi alipaswa kupambana na tatizo gani lingine?

12 Daudi alipaswa kupambana na tatizo lingine lenye lingemufanya aonekane kuwa muzaifu na mwenye hana nguvu. Kwa uaminifu, Daudi alimutumikia Sauli, mufalme wa Israeli mwenye Yehova alichagua. Ku mwanzo, Mufalme Sauli alimuheshimia Daudi. Kisha, kiburi kilimufanya Sauli akuwe na wivu kumuelekea Daudi. Sauli alimutendea Daudi mubaya, hata alijaribu kumuua.​—1 Sa. 18:6-9, 29; 19:9-11.

13. Daudi alitenda namna gani wakati Mufalme Sauli alimutendea mubaya?

13 Hata kama Mufalme Sauli alikuwa anamutendea Daudi mubaya, Daudi aliendelea kumuheshimia kwa sababu aliwekwa na Yehova. (1 Sa. 24:6) Hakumulaumu Yehova kwa sababu ya mambo ya mubaya yenye Sauli alikuwa anamutendea. Kuliko kufanya vile, Daudi alimutegemea Yehova ili amupatie nguvu yenye alikuwa nayo lazima juu avumilie ile hali.​—Zb. 18:1, utangulizi.

14. Mutume Paulo alipambana na hali gani yenye inafanana na ile ya Daudi?

14 Mutume Paulo alipambana na hali fulani yenye inafanana na ile ya Daudi. Maadui wa Paulo walikuwa wenye nguvu sana kuliko yeye. Viongozi wengi wa wakati wake wenye walijulikana sana walimuchukia. Mara mingi walimupiga na walimutia mu gereza. Kama Daudi, Paulo pia alitendewa mubaya na watu wenye walipaswa kuwa marafiki wake. Hata wamoja katika kutaniko la Kikristo walimupinga. (2 Ko. 12:11; Flp. 3:18) Lakini, Paulo alipata ushindi juu ya wale wote wenye walimupinga. Juu ya nini tunasema vile? Juu aliendelea kuhubiri hata kama kulikuwa upinzani. Aliendelea kubakia mushikamanifu kwa ndugu na dada zake hata wakati walimuvunja moyo. Na zaidi ya yote, alikuwa muaminifu kwa Mungu mupaka mwisho wa maisha yake. (2 Ti. 4:8) Alipata ushindi juu ya ile matatizo yote, haiko kwa sababu ya nguvu yake ya kimwili, lakini kwa sababu alimutegemea Yehova.

Wakati unajikaza kufikiri na wale wenye kupinga imani yako ya Kikristo, uwaheshimie na uwatendee muzuri (Ona fungu la 15) *

15. Kusudi letu ni gani, na namna gani tunaweza kufikia kusudi hilo?

15 Wanafunzi wenzako, wafanyakazi wenzako, ao watu wa familia yako wenye hawako Mashahidi, wako wanakutukana ao kukutesa? Umekwisha kutendewa mubaya na mutu fulani katika kutaniko? Ikiwa ni vile, kumbuka mufano wa Daudi na wa Paulo. Unaweza kuendelea “kushinda uovu kwa wema.” (Ro. 12:21) Kusudi letu haiko kuingiza jiwe katika paji la uso wa mutu fulani, kama vile Daudi alifanya, lakini ni kuingiza Neno la Mungu katika akili na mioyo ya watu wenye wako tayari kusikiliza. Tunaweza kufanya vile kwa kutumia Biblia ili kujibia maulizo ya watu, kwa kuheshimia na kutendea muzuri watu wenye kututendea mubaya, na kwa kutendea watu wote mema, hata maadui wetu.​—Mt. 5:44; 1 Pe. 3:15-17.

UKUBALI MUSAADA WA WENGINE

16-17. Paulo hakusahau jambo gani?

16 Mbele Paulo akuwe mwanafunzi wa Kristo, alikuwa kijana mwenye zarau, mwenye alitesa wafuasi wa Yesu. (Mdo. 7:58; 1 Ti. 1:13) Yesu mwenyewe alimuzuia Paulo, mwenye wakati huo alijulikana kwa jina la Sauli, kuendelea kutesa kutaniko la Kikristo. Yesu akiwa mbinguni, alizungumuza na Paulo na akamufanya akuwe kipofu. Ili aanze kuona tena, Paulo alilazimika kutafuta musaada kwa watu walewale wenye alikuwa anatesa. Kwa unyenyekevu, Paulo alikubali musaada wa Anania, mwenye alimusaidia aanze kuona tena.​—Mdo. 9:3-9, 17, 18.

17 Kisha, Paulo alifikia kuwa mushiriki wa kutaniko la Kikristo mwenye kujulikana sana, lakini hakusahau hata kidogo jambo lenye Yesu alimufundisha wakati alikuwa anaenda Damasko. Paulo aliendelea kubakia munyenyekevu, na alikubali musaada wa ndugu na dada zake kwa kupenda. Alikubali kama walikuwa “musaada wenye kutia nguvu” kwake.​—Kol. 4:10, 11, maelezo ya chini.

18. Ni nini inaweza kufanya tusikuwe tayari kukubali musaada wa wengine?

18 Mufano wa Paulo unaweza kutufundisha nini? Wakati tulianza kushirikiana na watu wa Yehova, pengine tulikuwa tayari kukubali musaada wa wengine, juu tulielewa kama tulikuwa watoto kiroho na kama tulikuwa na mambo mingi ya kujifunza. (1 Ko. 3:1, 2) Lakini hali iko namna gani sasa? Kama tumemutumikia Yehova kwa miaka mingi na tumepata uzoefu mwingi, inaweza kuwa nguvu kukubali musaada, zaidi sana kama unatolewa na mutu mwenye hajafanya miaka mingi katika kweli kama sisi. Lakini, mara mingi Yehova anatumia ndugu na dada ili watutie nguvu. (Ro. 1:11, 12) Tunapaswa kukubali jambo hilo kama tunapenda kupata nguvu kutoka kwa Yehova.

19. Juu ya nini Paulo alitimiza mambo mingi yenye kushangaza?

19 Kisha kuwa Mukristo, Paulo alitimiza mambo fulani yenye kushangaza. Juu ya nini? Juu alijifunza kama mafanikio haitegemee nguvu ya kimwili yenye mutu iko nayo, elimu, utajiri, ao desturi yake, lakini inategemea unyenyekevu wake na namna anamutegemea Yehova. Kila mumoja wetu aazimie basi kufuata mufano wa Paulo (1) kwa kumutegemea Yehova, (2) kwa kujifunza kupitia mifano ya watu wenye kuzungumuziwa katika Biblia, na (3) kwa kukubali musaada wa waamini wenzetu. Kama tunafanya vile, hata tujisikie kuwa wazaifu namna gani, Yehova atatufanya tukuwe na nguvu!

WIMBO 71 Sisi Ni Jeshi la Yehova!

^ fu. 5 Katika habari hii tutazungumuzia mufano wa mutume Paulo. Tutaona kama ikiwa tuko wanyenyekevu, Yehova atatupatia nguvu yenye tuko nayo lazima ili tushinde uzaifu wetu na ili tuvumilie wakati tunazarauliwa.

^ fu. 1 MAFASIRIO YA MANENO FULANI: Kuko mambo mingi yenye inaweza kufanya tujisikie kuwa wazaifu. Tunaweza kujisikia vile kwa sababu hatukamilike, kwa sababu ya magonjwa, umaskini, ao kwa sababu hatukusoma mingi. Zaidi ya ile, maadui wetu wanajaribu kutufanya tujione kuwa wazaifu kwa kutushambulia kupitia maneno ao kwa kututesa kimwili.

^ fu. 57 MAFASIRIO YA PICHA: Wakati Paulo alianza kuhubiri juu ya Kristo, aliacha vitu vyenye alitumia katika maisha yake ya zamani akiwa Mufarisayo. Pengine vile vitu vilitia ndani vitabu fulani vya kukunjwa, na kisanduku chenye kuwa na maandiko ndani.

^ fu. 61 MAFASIRIO YA PICHA: Ndugu mumoja anakazwa na wafanyakazi wenzake ili ajiunge nao katika karamu ya siku ya kuzaliwa ya mufanyakazi mwenzao.