Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 33

Ufufuo Unaonyesha Kama Mungu Iko na Upendo, Hekima, na Uvumilivu

Ufufuo Unaonyesha Kama Mungu Iko na Upendo, Hekima, na Uvumilivu

“Kutakuwa ufufuo.”​—MDO. 24:15.

WIMBO 151 Ataita

KIFUPI CHA HABARI *

1. Juu ya nini Yehova aliumba viumbe vyenye uzima?

WAKATI fulani, Yehova alikuwaka peke yake. Lakini ile haikumufanya ajisikie mubaya. Hakukuwa na lazima ya mutu. Upendo ulimuchochea aanze kuumba, juu alipenda wengine wafurahie maisha.​—Zb. 36:9; 1 Yo. 4:19.

2. Yesu na malaika walijisikia namna gani wakati Yehova aliumba vitu vingine?

2 Kwanza, Yehova aliumba Yesu, Mwana wake wa kwanza, ili atumike naye. Kisha, kupitia ule Mwana wake wa kwanza, aliumba “vitu vingine vyote,” kwa mufano, aliumba malaika wengi sana. (Kol. 1:16) Yesu alikuwa Fundi wa kazi wa Baba yake na alifurahia sana kutumika naye. (Mez. 8:30) Wakati Yehova alikuwa anatumika na Yesu ili kuumba mbingu na dunia, malaika walikuwa wanaona na wao pia walifurahi sana. Walionyesha furaha yao namna gani? “Walianza kupandisha sauti za shangwe” wakati Mungu aliumba dunia. Na waliendelea kushangilia wakati Yehova aliumba vitu vingine, zaidi sana wanadamu. (Yob. 38:7; Mez. 8:31, maelezo ya chini) Kila kitu chenye Yehova aliumba kinaonyesha kama iko na upendo na hekima.​—Zb. 104:24; Ro. 1:20.

3. Kulingana na 1 Wakorinto 15:21, 22, zabihu ya ukombozi ya Yesu inatuletea faida gani?

3 Yehova alipenda wanadamu waishi milele ku dunia ya muzuri yenye aliumba. Lakini wakati Adamu na Eva walikosa kumutii Yehova, Baba yao mwenye upendo, zambi na kifo vilienea mu dunia. (Ro. 5:12) Yehova alitenda namna gani? Palepale, alionyesha namna angeokoa wanadamu. (Mwa. 3:15) Yehova alikusudia kutoa Mwana wake, Yesu, akuwe zabihu ya ukombozi, ili watoto wa Adamu na Eva waweze kukombolewa kutoka katika zambi na kifo. Kisha, angepatia uzima wa milele kila mutu mwenye angeamua kumutumikia.​—Yoh. 3:16; Ro. 6:23; soma 1 Wakorinto 15:21, 22.

4. Tutazungumuzia maulizo gani katika habari hii?

4 Kuko maulizo mingi yenye tunaweza kujiuliza juu ya ahadi ya Mungu ya ufufuo. Kwa mufano tunaweza kujiuliza hivi: Ufufuo utafanywa namna gani? Tutatambua wapendwa wetu wakati watafufuka? Namna gani ufufuo utatuletea furaha? Na namna gani kufikiri sana juu ya ufufuo kunatusaidia tuelewe muzuri zaidi upendo, hekima, na uvumilivu wa Yehova? Tuzungumuzie basi ile maulizo.

INAWEZEKANA UFUFUO UTAFANYWA NAMNA GANI?

5. Juu ya nini tunaweza kusema kama watu wote hawatafufuliwa kwa wakati mumoja?

5 Tunaweza kuwazia kama wakati Yehova atamutumia Mwana wake ili kufufua mamilioni ya watu, wote hawatafufuliwa kwa wakati mumoja. Juu ya nini? Juu, kama Yehova anafufua watu mingi kwa wakati mumoja, ile italeta muvurugo. Yehova haiko Mungu wa muvurugo. Anajua kama inaomba kukuwe utaratibu ili watu waishi mu amani. (1 Ko. 14:33) Mbele aumbe wanadamu, Yehova alitumika na Yesu ili kutayarisha dunia kwa ajili yao. Hakutayarisha dunia kwa wakati mumoja, alifanya vile hatua kwa hatua. Alionyesha hekima na uvumilivu. Yesu pia ataonyesha zile sifa wakati wa Utawala wa Miaka Elfu; wakati atatumika na wale wenye wataokoka Armagedoni ili kutayarisha dunia kwa ajili ya wale wenye watafufuliwa, na kuwatayarishia mambo ingine yenye watakuwa nayo lazima.

Wale wenye wataokoka Armagedoni watafundisha wale wenye watafufuliwa, watawafundisha kuhusu Ufalme wa Mungu na kuhusu kanuni zake (Ona fungu la 6) *

6. Kulingana na Matendo 24:15, ni nani watakuwa kati ya wale wenye Yehova atafufua?

6 Kuko kazi ingine ya maana zaidi yenye wale wenye wataokoka Armagedoni watafanya. Watafundisha wale wenye watafufuliwa kuhusu Ufalme wa Mungu na kuhusu kanuni za Yehova. Sababu gani tunasema vile? Sababu wengi kati ya wale wenye watafufuliwa ni “wenye hawako wenye haki.” (Soma Matendo 24:15.) Itaomba wafanye mabadiliko ili wapate baraka za bei ya ukombozi ya Kristo. Fikiria kazi kubwa yenye tutakuwa nayo ya kufundisha mamilioni ya watu wenye hawajue kitu kumuhusu Yehova. Je, kila mutu atakuwa na mwalimu wa kumufundisha Biblia, sawa vile leo? Je, kutakuwa makutaniko sawa vile leo? Na je, wale wenye watafufuliwa kwanza wataombwa wajiunge na makutaniko fulani ili wajifunze namna watafundisha wale wenye watafufuliwa kisha wao? Kwa sasa, hatujue. Lakini, tunajua kama ku mwisho wa Utawala wa Miaka Elfu wa Kristo, “dunia hakika itajaa ujuzi juu ya Yehova.” (Isa. 11:9) Mu ile miaka elfu, tutakuwa na kazi mingi, tena ya kufurahisha!

7. Juu ya nini watumishi wa Yehova watakuwa na lazima ya kujitia pa nafasi ya wengine wakati watakuwa wanafundisha wale wenye watafufuliwa?

7 Wakati wa Utawala wa Miaka Elfu wa Kristo, watumishi wote wa Yehova wataendelea kufanya mabadiliko ili kumufurahisha. Kwa hiyo, wote watakuwa na lazima ya kujitia pa nafasi ya wengine wakati watakuwa wanasaidia wale wenye watafufuliwa waachane na tabia za mubaya na waishi kulingana na kanuni za Yehova. (1 Pe. 3:8) Bila shaka wale wenye watafufuliwa watafurahia kujiunga na watumishi wa Yehova kwa sababu wataona kama ni wanyenyekevu na kama wao pia wako ‘wanafanyia kazi wokovu wao wenyewe.’​—Flp. 2:12.

ITAWEZEKANA KUTAMBUA WAPENDWA WETU WAKATI WATAFUFUKA?

8. Juu ya nini tunaweza kusema kama itawezekana tutambue wapendwa wetu wenye watafufuliwa?

8 Kuko sababu mingi zenye zinaweza kufanya tuseme kama wakati tutakuwa tunakaribisha wapendwa wetu wenye watafufuliwa, itawezekana tuwatambue. Kwa mufano, wakati tunafikiria mifano ya watu wenye walifufuliwaka zamani, tunaona kama Yehova ataumba tena watu, na atawarudishia sura ileile, sauti ileile, na mawazo ileile yenye walikuwaka nayo muda kidogo mbele wakufe. Kumbuka kama Yesu alifananisha kifo na usingizi, na alifananisha ufufuo na kuamusha mutu mu usingizi. (Mt. 9:18, 24; Yoh. 11:11-13) Wakati unaamusha mutu mu usingizi, anaamukaka na sura ileile, sauti ileile, na mawazo ileile yenye alikuwa nayo mbele alale. Fikiria mufano wa Lazaro. Kulipita siku ine tangu akufe, na mwili wake ulikuwa umeanza kuoza. Lakini, wakati Yesu alimufufua, dada zake walimutambua mara moja, na ni wazi kama Lazaro naye aliwatambua.​—Yoh. 11:38-44; 12:1, 2.

9. Juu ya nini watu hawatafufuliwa na akili yenye kukamilika na miili yenye kukamilika?

9 Yehova anaahidi kama wakati wa utawala wa Kristo, hakuna mwenye atasema: “Niko mugonjwa.” (Isa. 33:24; Ro. 6:7) Kwa hiyo, wale wenye watafufuliwa watakuwa na miili yenye iko na afya ya muzuri. Lakini, hawatakuwa wakamilifu kisha tu wao kufufuliwa. Ikikuwa vile, watu wa familia yao na marafiki wao wanaweza kushindwa kuwatambua. Inaonekana kama wakati wa Utawala wa Miaka Elfu wa Kristo, wanadamu watafanywa kuwa wakamilifu hatua kwa hatua. Ni ku mwisho wa miaka elfu njo Yesu atamurudishia Baba yake Ufalme. Ile wakati, Ufalme utakuwa umemaliza kabisa kazi yake, yenye inatia ndani kufanya wanadamu wakuwe wakamilifu.​—1 Ko. 15:24-28; Ufu. 20:1-3.

NAMNA GANI UFUFUO UTATULETEA FURAHA?

10. Utajisikia na kutenda namna gani wakati wapendwa wako watafufuliwa?

10 Wazia furaha yenye utakuwa nayo wakati utakutana tena na wapendwa wako. Je, ile furaha itakufanya ucheke ao ulie? Ao utafurahi sana na kuanza kumuimbia Yehova? Tuko hakika kama zawadi ya muzuri ya ufufuo itafanya umupende zaidi Baba yetu mwenye kutuhangaikia na pia Mwana wake mwenye anatupenda.

11. Kulingana na maneno ya Yesu yenye kuwa mu Yohana 5:28, 29, wale wenye watapatanisha maisha yao na kanuni za Mungu watapata faida gani?

11 Wazia furaha yenye wale wenye watafufuliwa watakuwa nayo wakati watakuwa wanaachana na tabia zao za zamani na kupatanisha maisha yao na kanuni za Mungu za haki. Wale wenye watafanya ile mabadiliko wataishi milele, na ile itaonyesha kama ufufuo wao ulikuwa ufufuo wa uzima. Lakini, wale wenye watakosa kumutii, Mungu hatawaacha wavuruge amani mu Paradiso.​—Isa. 65:20; soma Yohana 5:28, 29.

12. Namna gani Yehova atabariki wale wenye wataishi ku dunia?

12 Mezali 10:22 inasema: “Baraka ya Yehova ndiyo inamufanya mutu kuwa tajiri, naye haongeze maumivu yoyote pamoja nayo.” Wakati Ufalme wa Mungu utatawala, watu wote wa Mungu watajionea kama ile maneno ni ya kweli. Roho ya Yehova itasaidia watu wa Mungu wakuwe matajiri kiroho, ni kusema, itawasaidia wafikie kabisa kuwa na sifa kama za Yesu na wakuwe wakamilifu. (Yoh. 13:15-17; Efe. 4:23, 24) Kila siku, watakuwa na afya ya muzuri zaidi, na watakuwa watu wazuri sana. Maisha itakuwa ya muzuri sana! (Yob. 33:25) Lakini, kufikiri sana juu ya ufufuo kunaweza kukuletea faida gani leo?

UFUFUO UNAONYESHA KAMA YEHOVA IKO NA UPENDO

13. Namna gani Zaburi 139:1-4 inaonyesha kama Yehova anatujua muzuri sana, na namna gani ufufuo utaonyesha vile?

13 Vile tuliona, wakati Yehova atafufua wafu, atawarudishia mawazo ileile na tabia zilezile zenye walikuwa nazo. Nini njo itamuwezesha kufanya vile? Ni upendo. Juu Yehova anakupenda sana, anajua na hawezi kusahau mawazo yako yote, namna unajisikia, mambo yenye unasemaka, na kufanya. Kwa hiyo, kama itaomba akufufue, hatashindwa kukurudishia mawazo, namna yako ya kuona mambo, na tabia zako. Mufalme Daudi alijua kama Yehova anajua kila mumoja wetu muzuri sana. (Soma Zaburi 139:1-4.) Kujua kama Yehova anatujua muzuri sana, kunatuleta faida gani?

14. Kufikiri sana kuhusu namna Yehova anatujua muzuri, kunatusaidia namna gani?

14 Kufikiri sana kuhusu namna Yehova anatujua muzuri, kunatusaidia tusiogope. Juu ya nini tunasema vile? Kumbuka kama Yehova anatupenda sana. Anaona kila mumoja wetu kuwa wa pekee. Anajua kila kitu chenye kimetufikia mu maisha chenye kinafanyaka tukuwe vile tunakuwaka. Ile inatia moyo sana! Hatupaswe hata kidogo kuwaza kama tuko peke yetu. Kila wakati, Yehova iko pamoja na sisi na anapenda kutusaidia.​—2 Ny. 16:9.

UFUFUO UNAONYESHA KAMA YEHOVA IKO NA HEKIMA

15. Namna gani ufufuo unaonyesha hekima ya Yehova?

15 Kwa sababu woga wa kufa ni silaha ya nguvu sana yenye Shetani anatumia, wale wenye kuongozwa naye wanatumia ile silaha juu ya kufanya watu wasaliti ao watoe marafiki wao na wafikie kukana imani yao. Lakini sisi hatuogope kufa. Tunajua kama Yehova atatufufua hata maadui wetu wakituua. (Ufu. 2:10) Tuko hakika kama hakuna kitu wanaweza kufanya chenye kinaweza kufanya tuache kumutumikia Yehova. (Ro. 8:35-39) Yehova ameonyesha kama iko na hekima sana kwa kutupatia tumaini la ufufuo! Tumaini hilo linatusaidia tusiogope wakati watu wa Shetani wanataka kutuua, na linatusaidia tuendelee kuwa washikamanifu kwa Yehova.

Je, maamuzi yetu inaonyesha kama tunatumainia ahadi ya Yehova ya kututimizia mahitaji yetu? (Ona fungu la 16) *

16. Unaweza kujiuliza maulizo gani, na majibu yako ku ile maulizo itakusaidia namna gani?

16 Kama maadui wa Yehova wanakuambia kama watakuua, utamutumainia Yehova na kuwa hakika kama atakufufua? Maulizo yenye kufuata itakusaidia ujue kama utamutumainia Yehova ile wakati. Ujiulize hivi: ‘Ninamutumainiaka Yehova kila siku wakati ninakamata maamuzi ya kidogo-kidogo?’ (Lu. 16:10) Unaweza tena kujiuliza: ‘Maisha yangu inaonyesha kama ninatumainia ahadi ya Yehova ya kunitimizia mahitaji yangu kama ninatafuta kwanza Ufalme?’ (Mt. 6:31-33) Kama unajibu ndiyo ku ile maulizo, ile inaonyesha kama unamutumainia Yehova, na uko tayari kupambana na magumu yoyote yenye inaweza kukufikia.​—Mez. 3:5, 6.

UFUFUO UNAONYESHA KAMA YEHOVA IKO NA UVUMILIVU

17. (a) Namna gani ufufuo unaonyesha kama Yehova iko na uvumilivu? (b) Tunaweza kufanya nini ili kuonyesha kama tunaona uvumilivu wa Yehova kuwa wa maana?

17 Yehova amekwisha kupanga siku na saa yenye ataharibu ulimwengu huu muovu. (Mt. 24:36) Ataendelea kuvumilia na atangojea mupaka ile siku ifike. Kwa kweli, anatamani sana kufufua wafu, lakini anaendelea kuvumilia. (Yob. 14:14, 15) Iko anangojea wakati wenye amepanga ili kufufua wafu. (Yoh. 5:28) Tuko na sababu za kumushukuru Yehova juu ya uvumilivu wake. Waza kidogo: Uvumilivu wa Yehova umesaidia watu mingi ‘wafikie kutubu,’ umetusaidia sisi pia. (2 Pe. 3:9) Yehova anapenda watu mingi, kwa kadiri inawezekana, wafikie kupata uzima wa milele. Tuonyeshe basi kama tunaona uvumilivu wa Yehova kuwa wa maana. Namna gani? Kwa kuendelea kutafuta kwa bidii wale wenye wako na “muelekeo wenye kufaa kwa ajili ya uzima wa milele” na kuwasaidia wamupende Yehova na wamutumikie. (Mdo. 13:48) Tukifanya vile, uvumilivu wa Yehova utawaletea wao pia faida.

18. Juu ya nini tunapaswa kuvumilia wengine?

18 Yehova anatazamia kama tutakuwa wakamilifu ku mwisho wa miaka elfu. Kwa hiyo, ataendelea kutuvumilia. Mupaka ile wakati, Yehova ataendelea kusamehe makosa yetu. Kwa hiyo, tunapaswa kufuata mufano wake kwa kukazia sifa za muzuri za wengine na kuendelea kuwavumilia. Fikiria mufano wa dada mumoja mwenye bwana yake alianza kuwa na wasiwasi sana na hata akaacha kufika ku mikutano. Anasema: “Ilikuwa nguvu sana. Maisha yetu ilibadilika bila kutazamia, na mipango yetu yote ilivurugika.” Ijapokuwa ile yote, aliendelea kumupenda bwana yake na kumuvumilia. Alimutegemea Yehova bila kuacha. Alimuiga Yehova kwa kuendelea kuangalia sifa za muzuri za bwana yake, kuliko kuwaza sana juu ya magumu. Anasema: “Bwana yangu iko na sifa za muzuri, na iko anajikaza kupunguza wasiwasi yake.” Ni muzuri tukuwe tunavumilia watu wa familia yetu ao ndugu na dada wenye wako wanapambana na magumu!

19. Unapaswa kujikaza kufanya nini?

19 Yesu na malaika walifurahi sana wakati Yehova aliumba dunia. Wazia namna watafurahi sana wakati wataona dunia inajaa watu wakamilifu, wenye kumupenda Yehova na kumutumikia. Wazia furaha yenye wale wenye wataenda kutawala na Kristo watakuwa nayo wakati wataona namna wanadamu wako wanafaidika na kazi yao. (Ufu. 4:4, 9-11; 5:9, 10) Tena, wazia namna maisha itakuwa wakati hakutakuwa tena machozi, magonjwa, huzuni, na kifo. (Ufu. 21:4) Wakati unangojea ile wakati, ujikaze kufuata mufano wa Yehova, Baba yetu kwa kuendelea kuonyesha upendo, hekima, na uvumilivu. Kufanya vile kutakusaidia uendelee kuwa na furaha, hata upate magumu gani. (Yak. 1:2-4) Tunamushukuru sana Yehova kwa kutuahidi kama “kutakuwa ufufuo”!​—Mdo. 24:15.

WIMBO 141 Muujiza wa Uhai

^ fu. 5 Yehova ni Baba mwenye upendo, hekima, na uvumilivu. Wakati tunachunguza vitu vyenye aliumba na pia ahadi yake ya kufufua wafu, tunaona kama iko na zile sifa. Habari hii itazungumuzia maulizo fulani yenye tunaweza kujiuliza kuhusu ufufuo. Itazungumuzia pia namna ufufuo unaonyesha kama Yehova iko na upendo, hekima na uvumilivu na ile inapaswa kutuchochea kufanya nini.

^ fu. 59 MAFASIRIO YA PICHA: Mutu fulani wa Amerika mwenye alikufaka zamani sana anafufuliwa wakati wa Utawala wa Miaka Elfu wa Kristo. Ndugu mwenye aliokoka Armagedoni anafurahia kumufundisha ili ajue mambo yenye anapaswa kufanya juu afaidike na bei ya ukombozi ya Kristo.

^ fu. 61 MAFASIRIO YA PICHA: Ndugu anaambia mukubwa wake wa kazi kama hatakuwa anatumika siku fulani kisha saa za kazi. Anamufasiria kama mangaribi ya zile siku, amepanga kufanya mambo ya kiroho. Lakini, siku zingine, kama ni lazima kabisa, iko tayari kutumika kisha saa za kazi.