Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 39

Tutegemeze Dada Zetu Wakristo

Tutegemeze Dada Zetu Wakristo

“Wanamuke wenye kutangaza habari njema ni jeshi kubwa.”​—ZB. 68:11.

WIMBO 137 Wanawake Waaminifu, Dada Wakristo

KIFUPI CHA HABARI *

Dada zetu wako na mambo mingi ya kufanya na pia wako na bidii. Wanatoa maelezo kwenye mikutano, wanahubiri, wanasaidia kutunza Jumba la Ufalme, na wanahangaikia ndugu na dada zao (Ona fungu la 1)

1. Dada zetu wako wanatimiza mambo gani mu tengenezo, lakini wengi wanapataka magumu gani? (Ona picha ku jalada la gazeti hili.)

TUNAFURAHI sana juu mu makutaniko yetu, muko dada wengi wenye wanatumikaka kwa bidii. Kwa mufano, wanatoaka maelezo ku mikutano na wanajitoaka sana mu kazi ya kuhubiri. Wamoja wanasaidiaka kutunza Jumba la Ufalme na wanahangaikiaka ndugu na dada zao. Lakini tusisahau kama wao pia wanapataka magumu. Wamoja wako wanahangaikia wazazi wao wenye kuzeeka. Wengine wanapingwa na watu wa familia yao. Na wengine wenye wako wanakomalisha watoto wao peke yao, wanapaswa kutumika sana ili kutimiza mahitaji ya watoto wao.

2. Juu ya nini tunapaswa kutegemeza dada zetu?

2 Juu ya nini tunapaswa kutegemeza dada zetu? Juu mu dunia watu wengi hawaheshimiake wanamuke. Zaidi ya ile, Biblia inatutia moyo tuwategemeze. Kwa mufano, Paulo aliambia Wakristo wa kutaniko la Roma wakaribishe Foibe na ‘wamupatie musaada wowote wenye angeweza kuwa nao lazima.’ (Ro. 16:1, 2) Zamani Paulo alikuwa Mufarisayo, na Wafarisayo hawakukuwa wanaheshimia wanamuke, na walikuwa wanawazarau. Lakini wakati Paulo alifikia kuwa Mukristo, alifuata mufano wa Yesu na alianza kuheshimia wanamuke na kuwatendea kwa upendo.​—1 Ko. 11:1.

3. Namna gani Yesu alitendea wanamuke, na aliona namna gani wanamuke wenye walikuwa wanafanya mapenzi ya Mungu?

3 Yesu aliheshimia wanamuke wote. (Yoh. 4:27) Hakuwazarau sawa vile viongozi wa dini ya Wayahudi walikuwa wanafanya. Kitabu kimoja chenye kuzungumuzia Biblia kinahakikisha jambo hilo. Kinasema hivi: “Yesu hakusema hata siku moja jambo lenye lingeshushia wanamuke heshima.” Kuliko kufanya vile, Yesu aliona wanamuke wenye walifanya mapenzi ya Baba yake kuwa wa maana sana. Aliwaona kuwa dada zake. Wakati alizungumuzia wale wenye aliona kuwa watu wa familia yake, hakutaja tu wanaume lakini alitaja pia wanamuke.​—Mt. 12:50.

4. Tutazungumuzia nini mu hii habari?

4 Sikuzote Yesu alikuwa tayari kusaidia wanamuke wenye walikuwa wanamutumikia Mungu. Aliwaona kuwa wa maana na alikuwa anawasemea. Tuzungumuzie basi namna tunaweza kufuata mufano wake ili kuonyesha kama tunahangaikia dada zetu Wakristo.

TUPITISHE WAKATI PAMOJA NA DADA ZETU WAKRISTO

5. Juu ya nini inaweza kuwa nguvu kwa dada fulani kupitisha wakati pamoja na wengine?

5 Ikuwe tuko ndugu ao dada, sisi wote tuko na lazima ya kupitisha wakati na marafiki wazuri. Lakini wakati fulani, inakuwaka nguvu kwa dada zetu kupata marafiki wazuri wenye watapitisha nao wakati. Juu ya nini? Fikiria mufano wa dada mumoja mwenye kuitwa Jordan. * Anasema hivi: “Juu sijaolewa mara mingi ninaonaka kama siko wa maana mu kutaniko.” Kristen, dada mumoja painia mwenye alihamia mu eneo lenye kuwa na lazima ya wahubiri, anasema hivi: “Wakati uko wa mupya mu kutaniko unaweza kujisikia kuwa peke yako.” Ndugu fulani wanaweza kujisikia pia vile. Wale wenye watu wa familia yao hawako Mashahidi wanaweza kuona kama watu wa familia yao wamewaacha, na wakati uleule wanaweza kuona kama hawako karibu na ndugu na dada zao Wakristo. Pia, wale wenye hawawezi kutoka ku nyumba kwa sababu ya matatizo fulani, ao wale wenye kuhangaikia watu wa familia yao wenye kuwa wagonjwa wanaweza pia kujisikia kuwa peke yao. Dada mwenye kuitwa Annette anasema hivi, “Wakati ndugu na dada walikuwa wananialika ili nipitishe wakati pamoja nao, sikuweza kukubali kwa sababu mimi njo nilikuwa ninahangaikia mama yangu.”

Tunapaswa kuonyesha dada zetu Wakristo kama tunawapenda, na kama tunawahangaikia kama vile Yesu alikuwa anafanya (Ona fungu la 6-9) *

6. Kulingana na Luka 10:38-42, namna gani Yesu alisaidia Marta na Maria?

6 Yesu alikuwa napitisha wakati na wanamuke wenye walikuwa namutumikia Mungu. Na alikuwa kabisa rafiki yao. Kwa mufano, alikuwa rafiki ya Maria na Marta, wenye inawezekana walikuwa hawajaolewa. (Soma Luka 10:38-42.) Maneno ya Yesu na namna alikuwa anawatendea, ilifanya wajisikie huru kumukaribia. Maria alijisikia huru kukaa kwenye miguu ya Yesu, * na wakati Marta aliona kama Maria hakukuwa anamusaidia, alijisikia huru kuambia Yesu mawazo yake. Yesu alitumia ile wakati ili kuwafundisha mambo fulani ya maana. Na alionyesha kama alihangaikia Maria, Marta, na Lazaro kwa kuendelea kuwatembelea. (Yoh. 12:1-3) Na njo maana wakati Lazaro aligonjwa, Maria na Marta walijua kama wangeweza kumuomba Yesu awasaidie.​—Yoh. 11:3, 5.

7. Tunapaswa kufanya nini ili kutia moyo dada zetu?

7 Mara mingi ku mikutano njo dada fulani wanapataka nafasi ya kuwa pamoja na Wakristo wenzao. Kwa hiyo, tunapaswa kuwakaribisha, kuzungumuza nao, na kuwaonyesha kama tunawahangaikia. Dada Jordan, mwenye tulishazungumuzia, anasema hivi: “Ninasikiaka muzuri sana wakati wengine wananiambia kama walifurahia maelezo yangu, wakati wanapanga kuhubiri na mimi, ao wakati wananionyesha kama wananihangaikia mu njia ingine.” Tunapaswa kuonyesha dada zetu kama tunawaona kuwa wa maana. Dada mwenye kuitwa Kia anasema hivi: “Kama sifike ku mukutano, ninajua kama ndugu na dada fulani wataniandikia ujumbe ili kujua kama sina tatizo. Ile inafanya nione kama ndugu na dada zangu wananihangaikia.”

8. Ni mu njia gani zingine tunaweza kumuiga Yesu?

8 Tunapaswa kujikaza kupitisha wakati pamoja na dada zetu, kama vile Yesu alikuwa anafanya. Kwa mufano tunaweza kuwaalika ili kula chakula pamoja ao kujifurahisha pamoja. Wakati tunafanya vile, tunapaswa kujikaza ili mazungumuzo yetu ikuwe yenye kutia moyo. (Ro. 1:11, 12) Wazee wanapaswa kujikaza ili kuwa na mawazo kama ya Yesu. Yesu alijua kama inaweza kuwa nguvu kwa Wakristo fulani kubakia bila kuoa ao kuolewa. Lakini alionyesha wazi kama haiko kuoa ao kuolewa wala kuwa na watoto njo kunaletaka furaha ya kweli. (Lu. 11:27, 28) Lakini ili mutu akuwe na furaha ya kweli, anapaswa kutia kazi ya Yehova pa nafasi ya kwanza.​—Mt. 19:12.

9. Wazee wanapaswa kufanya nini ili kusaidia dada Wakristo?

9 Sisi wote tunapaswa kujikaza kutendea wanamuke Wakristo kama dada na mama zetu. Lakini wazee njo wanapaswa kuonyesha mufano katika kufanya vile. (1 Ti. 5:1, 2) Ni muzuri wazee wakuwe na kawaida ya kuzungumuza nao mbele na kisha mikutano. Dada Kristen anasema hivi: “Muzee mumoja aliona kama nilikuwa na mambo mingi ya kufanya, na alipenda kujua namna ninapangaka mambo yenye ninafanyaka. Nilifurahi sana kuona namna alinihangaikia.” Wakati wazee wanajikaza sana ili kuzungumuza na dada zao Wakristo, wanaonyesha kama wanawahangaikia. * Dada Annette mwenye tulishazungumuzia, alionyesha kama ni jambo la maana kuzoea kuzungumuza na wazee. Alisema: “Nafikia kuwajua muzuri, nao pia wanafikia kunijua. Kisha wakati niko na magumu ninajisikia huru kuwaomba musaada.”

TUONYESHE DADA ZETU KAMA TUNAWAONA KUWA WA MAANA

10. Tunaweza kufanya nini ili kusaidia dada zetu wakuwe na furaha?

10 Sisi wote, ikuwe tuko wanaume ao wanamuke, tunafurahiaka sana wakati wengine wanatambua uwezo wetu, na wanatushukuru kwa kazi yenye tuko tunafanya. Lakini wakati wengine hawatambue uwezo wetu, ao kutushukuru, tunavunjikaka moyo. Abigail, dada mumoja painia mwenye hajaolewa, anasema kama wakati fulani anaonaka kuwa watu wanamusahau. Anasema hivi: “Watu hawanijue kipekee, wanajua tu kama niko mutoto wa fulani ao niko dada yake na fulani. Wakati fulani ninaonaka sawa vile hawanitambue.” Fikiria mufano wa dada mwingine mwenye kuitwa Pam. Wakati alikuwa hajaolewa alifanya kwa miaka mingi kazi ya umisionere. Kisha wakati fulani alirudia kwao ili kuhangaikia wazazi wake. Leo angali painia hata kama iko na zaidi ya miaka 70. Anasema hivi: “Jambo lenye linanisaidiaka sana ni kuona vile wengine wako wananishukuru kwa kazi yenye niko nafanya.”

11. Yesu alifanya nini ili kuonyesha kama aliona wanamuke wenye walimutegemeza kuwa wa maana?

11 Yesu alifurahia sana musaada wenye wanamuke wenye walikuwa wanamutegemeza walimutolea “kwa kutumia mali zao.” (Lu. 8:1-3) Zaidi ya kuwapatia pendeleo la kumutegemeza, aliwafundisha pia kweli za maana juu ya mapenzi ya Mungu. Kwa mufano, aliwaambia kama angekufa na kufufuliwa. (Lu. 24:5-8) Pia aliwatayarisha juu ya mateso yenye wangepata, sawa vile tu alikuwa ametayarisha mitume. (Mk. 9:30-32; 10:32-34) Na hata kama mitume walikimbia wakati Yesu alikamatwa, wanamuke fulani walikuwa karibu na Yesu wakati alikuwa ku muti wa mateso.​—Mt. 26:56; Mk. 15:40, 41.

12. Yesu alipatia wanamuke waaminifu kazi gani?

12 Yesu alipatia wanamuke kazi ya maana sana. Kwa mufano, wanamuke fulani waaminifu njo walikuwa wa kwanza kujua kama Yesu alishafufuliwa. Na aliambia wale wanamuke waende wajulishe mitume wake kama alishafufuliwa. (Mt. 28:5, 9, 10) Na kwenye Pentekoste ya mwaka wa 33 kisha kuzaliwa kwa Yesu, inawezekana wanamuke walikuwa kati ya wanafunzi wenye walitiwa mafuta kwa roho takatifu. Kama ni vile, wale wanamuke pia walipewa uwezo wa kuzungumuza mu luga zingine na kuambia watu “mambo makubwa ya Mungu.”​—Mdo. 1:14; 2:2-4, 11.

13. Dada Wakristo wako wanafanya nini leo, na tunaweza kufanya nini ili kuonyesha kama tunaona mambo yenye wako wanafanya kuwa ya maana?

13 Tunapaswa kushukuru dada zetu kwa mambo yote yenye wako wanafanya mu tengenezo la Yehova. Kwa mufano, wanasaidia kujenga na kutunza majengo yetu mbalimbali, wanategemeza vikundi vya luga ingine, na wanajitolea mu kazi mbalimbali ku Beteli. Tena wanasaidia mu kazi ya kutoa misaada wakati wa misiba, wanasaidia kutafsiri vichapo vyetu, na wengine ni mapainia na wamisionere. Dada zetu wanasomaka pia masomo mbalimbali sawa vile tu ndugu wanafanyaka. Kwa mufano, wanasomaka masomo ya mapainia, Masomo kwa Ajili ya Waeneza-Injili wa Ufalme, na Masomo ya Gileadi. Zaidi ya ile, bibi Wakristo wanasaidiaka bwana zao ili watimize muzuri madaraka yao mu kutaniko na mu tengenezo la Yehova. Wale ndugu ni “zawadi katika wanadamu” na wanafanya mambo mingi ili kusaidia wengine. Lakini inaweza kuwa nguvu kwao kufanya vile kama bibi zao hawawategemeze. (Efe. 4:8) Unaweza kufanya nini ili kutegemeza dada zetu Wakristo mu kazi yenye wako wanafanya?

14. Maneno yenye kuwa mu Zaburi 68:11, inaweza kuchochea wazee wafanye nini?

14 Wazee wenye wako na hekima wanaelewa kama dada Wakristo ni “jeshi kubwa” la wafanyakazi, na kama mara mingi wanafanyaka muzuri kazi ya kuhubiri. (Soma Zaburi 68:11.) Kwa hiyo, wazee wanajikaza ili kujifunza mambo fulani kupitia mufano wao. Dada Abigail mwenye tulishazungumuzia, anafurahiaka wakati ndugu wanamuuliza ufundi wenye anatumikishaka ili kuanzisha mazungumuzo na watu mu eneo. Anasema hivi: “Ile inanisaidia nione kama niko wa maana mu tengenezo la Yehova.” Zaidi ya ile, wazee wanaelewa kama dada waaminifu wenye kukomaa wanajuaka muzuri namna ya kusaidia dada vijana wenye wako na matatizo. (Tit. 2:3-5) Kwa kweli tunapaswa kupenda dada zetu na kuwaona kuwa wa maana!

TUSEMEE DADA ZETU WAKRISTO

15. Ni wakati gani dada zetu wanaweza kuwa na lazima ya mutu wa kuwasemea?

15 Wakati fulani dada zetu wanaweza kuwa na lazima ya mutu wa kuwasemea wakati wako na magumu fulani. (Isa. 1:17) Kwa mufano, dada mwenye alishafisha bwana ao mwenye ndoa yake ilishavunjika anaweza kuwa na lazima ya mutu wa kumusemea ao wa kumusaidia kufanya kazi fulani zenye bwana yake alikuwaka anafanya. Dada mwenye kuzeeka anaweza kuwa na lazima ya mutu wa kumusaidia kuzungumuza na wanganga. Ao dada painia mwenye iko anafanya kazi zingine mu tengenezo la Yehova, anaweza kuwa na lazima ya mutu wa kumusemea wakati wengine wanasema kama yeye hahubiriake sana sawa vile mapainia wengine. Tunaweza kufanya nini ingine ili kusaidia dada zetu? Tuone tena mufano wa Yesu.

16. Kulingana na Marko 14:3-9, namna gani Yesu alimusemea Maria?

16 Yesu alikuwa tayari kusemea wanamuke waaminifu wakati watu waliwaelewa mubaya. Kwa mufano, alisemea Maria wakati Marta alishindwa kumuelewa. (Lu. 10:38-42) Na alimusemea tena wakati wengine walimusema mubaya kwa sababu waliwaza kama jambo lenye alifanya halikukuwa la muzuri. (Soma Marko 14:3-9.) Yesu alielewa kama Maria alikuwa na nia ya muzuri na alimupongeza kwa kusema hivi: “Amenifanyia tendo la muzuri. . . . Amefanya kile ameweza.” Na zaidi ya ile, Yesu alitabiri kama tendo la Maria lingezungumuziwa “kila mahali kwenye habari njema itahubiriwa katika ulimwengu wote.” Na ile maneno ya Yesu iko inatimia hata sasa juu tuko tunazungumuzia habari ya Maria. Kwa kweli, ile maneno ya Yesu ilitia Maria moyo kabisa kwa sababu watu walikuwa wamemuelewa mubaya! Inafurahisha kuona kama ni wakati Yesu alimusifu Maria juu ya tendo lake njo wakati alisema kama habari njema ingehubiriwa mu dunia yote!

17. Ni katika hali gani unaweza kusemea dada fulani Mukristo? Leta mufano.

17 Unakuwaka tayari kusemea dada zako? Fikiria hali yenye kufuata. Wahubiri fulani wanaona kama dada mumoja mwenye bwana yake haiko Shahidi wa Yehova anazoeaka kuchelewa ku mikutano, na anarudiaka ku nyumba wakati tu mikutano inamalizika. Tena wanaona kama mara mingi haletake watoto wake ku mikutano. Kwa hiyo, wanaanza kumusema mubaya. Wanafanya vile juu wanawaza kama anapaswa kulazimisha bwana yake amuruhusu akuwe analeta watoto ku mikutano. Lakini wanasahau kama ule dada iko anafanya yake yote ili akuwe na hali ya muzuri ya kiroho. Na ikiwa anachelewaka ku mikutano na anaendaka kisha tu mikutano kumalizika, ni juu iko chini ya mamlaka ya bwana yake na bwana yake njo anamupangiaka namna atatumia wakati wake. Pia wanasahau kama haiko yeye njo anakamataka uamuzi wa mwisho juu ya mambo yenye watoto wake wanapaswa kufanya. Sasa, unaweza kufanya nini kama unasikia wengine wako wanamusema ule dada vile? Unapaswa kusifu ule dada na kuwaambia mambo ya muzuri yenye iko anafanya. Kama unafanya vile, utawasaidia waache kumusema mubaya.

18. Ni mu njia gani mbalimbali tunaweza kusaidia dada zetu?

18 Tunaweza kuonyesha kama tunahangaikia dada zetu kwa kuwatolea musaada wenye wako nao lazima. (1 Yo. 3:18) Dada Annette mwenye tulishazungumuzia, mwenye alikuwa anahangaikia mama yake mugonjwa, anasema hivi: “Ndugu na dada fulani walikuwa wanakuja kunisaidia kuhangaikia mama yangu ao walikuwa wanaleta chakula. Ile ilifanya nijisikie kuwa wananipenda na niko wa maana mu kutaniko.” Jordan alipata pia musaada. Ndugu mumoja alimusaidia ajue namna ya kutengeneza motokari yake. Anasema hivi: “Wakati ninaona vile ndugu na dada wananihangaikia na wanapenda niendelee kuwa salama, ile inanifurahisha sana.”

19. Ni mu njia gani ingine wazee wanaweza kutegemeza dada zetu?

19 Wazee wanajikazaka pia kuhangaikia dada zetu Wakristo. Wanajua kama Yehova anapendaka tuwatendee muzuri. (Yak. 1:27) Kwa hiyo wanajikaza kuiga mufano wa Yesu kwa kuonyesha sifa ya usawaziko. Wanatambua kama wakati fulani ni muzuri kuwaelewa kuliko tu kukazia sheria fulani. (Mt. 15:22-28) Wakati wazee wanajikaza kufanya vile, ile inafanya dada waone kama Yehova anawapenda na pia tengenezo lake. Kwa mufano, dada Kia alikuwa anapanga kuhamia mu nyumba ingine. Wakati mwangalizi wa kikundi chao alijua vile, alifanya mipango ili kumusaidia. Dada Kia anasema hivi: “Ile ilinisaidia nisikuwe na mahangaiko mingi. Kwa sababu wazee walinitia moyo na kunisaidia, walinifanya nione kama niko wa maana mu kutaniko, na siko peke yangu wakati wa magumu.”

TUNAPASWA KUTEGEMEZA DADA ZETU WOTE

20-21. Tunaweza kufanya nini illi kuonyesha kama tunapenda dada zetu?

20 Mu makutaniko yetu muko dada wengi wenye kutumika kwa bidii. Kwa hiyo tunapaswa kuwategemeza. Kama vile tumejifunza kupitia mufano wa Yesu, tunaweza kuwasaidia kwa kupitisha wakati pamoja nao na kujikaza kuwajua muzuri. Tunaweza pia kuonyesha kama tunafurahia mambo yenye wako wanafanya mu kazi ya Yehova. Na tunaweza kuwasemea wakati ni lazima kufanya vile.

21 Ku mwisho wa barua yenye Paulo aliandikia Waroma, alitaja majina ya wanamuke Wakristo kenda. (Ro. 16:1, 3, 6, 12, 13, 15) Bila shaka wale wanamuke walifurahi sana wakati walisikia kama aliwasalimia na kuwapongeza. Sisi pia tuendelee basi kutegemeza dada zetu wote mu kutaniko. Wakati tunafanya vile tunaonyesha kama tunawapenda na kama tunawaona kuwa wa maana mu familia yetu ya kiroho.

WIMBO 136 “Malipo Kamili Kutoka kwa Yehova”

^ fu. 5 Dada zetu Wakristo wanapataka magumu mingi. Mu hii habari tutaona namna tunaweza kuwategemeza. Tutazungumuzia namna Yesu alikuwa anapitisha wakati pamoja na wanamuke, namna aliwaonyesha kama anawaona kuwa wa maana, na namna alikuwa anawasemea. Kisha tutaona namna tunaweza kuiga mufano wake.

^ fu. 5 Majina fulani imebadilishwa.

^ fu. 6 Kitabu kimoja chenye kuzungumuzia Biblia kinasema hivi: “Wanafunzi wenye walikuwa wanapenda kukuwa walimu njo walikuwa wanakaa kwenye miguu ya walimu wao. Lakini wanamuke hawakuruhusiwa kuwa walimu. . . . Njo maana wanaume wengi Wayahudi hawangefurahi ikiwa wangeona Maria anakaa kwenye miguu ya Yesu ili kusikiliza mafundisho ya Yesu.”

^ fu. 9 Wazee wanapaswa kuwa waangalifu wakati wanapenda kusaidia dada zao Wakristo. Kwa mufano, kama muzee anapenda kutembelea dada fulani, anapaswa kuepuka kuenda peke yake.

^ fu. 65 MAFASIRIO YA PICHA: Ndugu watatu wanahangaikia wanamuke waaminifu sawa vile Yesu alikuwa anafanya. Mumoja anasaidia dada wawili kubadilisha gurudumu la gari yao, mwingine anaenda kutembelea dada mwenye kuwa na uzaifu fulani wa kimwili, na mwingine anaenda pamoja na bibi yake ku ibada ya familia ya dada fulani na mutoto wake mwanamuke.