Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 40

“Linda Yote Yenye Ulipewa”

“Linda Yote Yenye Ulipewa”

“Timoteo, linda yote yenye ulipewa.”​—1 TI. 6:20.

WIMBO 29 Kuishi Kulingana na Jina Letu

KIFUPI CHA HABARI *

1-2. Kulingana na 1 Timoteo 6:20, Yehova alipatia Timoteo nini?

WAKATI tuko na vitu fulani vya maana tunapatiaka mutu mwingine vile vitu ili avilinde. Kwa mufano, tunaweza kuweka feza zetu ku banke. Wakati tunafanya vile, tunatumainiaka kama watazilinda muzuri, hazitapotea, na hakuna mutu mwenye ataziiba. Ile mufano inatusaidia kuelewa kama wakati tunapatia mutu atuwekee vitu vyetu vya maana, ile inaonyesha kama tunamutumainia.

2 Soma 1 Timoteo 6:20. Mutume Paulo alimukumbusha Timoteo kama Yehova alikuwa amemupatia jambo fulani la maana sana, ni kusema, ujuzi wenye hauna makosa juu ya kusudi la Mungu kwa wanadamu. Alikuwa pia amemupatia pendeleo la ‘kuhubiri neno’ na la ‘kufanya kazi ya mweneza-injili.’ (2 Ti. 4:2, 5) Paulo alishauria Timoteo alinde mambo yenye Yehova alikuwa amemupatia. Kama Timoteo, na sisi Yehova ametupatia mambo ya maana sana. Ni mambo gani? Na juu ya nini tunapaswa kulinda ile mambo?

YEHOVA AMETUPATIA MAFUNDISHO YA KWELI YENYE KUWA MU BIBLIA

3-4. Sababu gani mafundisho ya Biblia ni ya maana sana?

3 Yehova ametusaidia kuelewa mafundisho ya kweli yenye kuwa mu Neno lake Biblia. Ile mafundisho ni ya maana sana sababu inatusaidia tujue mambo yenye tunapaswa kufanya juu tukuwe na urafiki muzuri pamoja na Yehova na juu tupate furaha mu maisha yetu. Kama tunaamini ile mafundisho, na tunaitumikisha mu maisha yetu, ile itatusaidia tusiamini mafundisho ya uongo na tuepuke tabia zenye hazimupendeze Mungu.​—1 Ko. 6:9-11.

Tena mafundisho yenye kuwa mu Biblia ni ya maana sababu Yehova haifunuliake watu wote, lakini anaifunuliaka tu watu wanyenyekevu wenye wako na “mwelekeo wenye kufaa.” (Mdo. 13:48) Wale watu wanyenyekevu wanakubali kama, leo Yehova iko anatumikisha mutumwa muaminifu na mwenye busara ili kutusaidia kuelewa mafundisho ya Biblia. (Mt. 11:25; 24:45) Kusema kweli, tuko na lazima ya musaada ili kuelewa mafundisho ya Biblia. Na kuelewa ile mafundisho, njo jambo la maana zaidi.​—Mez. 3:13, 15.

5. Yehova ametupatia nini ingine?

5 Yehova ametupatia pendeleo la kufundisha wengine mambo yenye Biblia inasema juu yake na pia kusudi lake. (Mt. 24:14) Habari njema yenye tunahubiri ni ya maana sana juu inasaidia watu wamutumikie Yehova na wakuwe na tumaini la uzima wa milele. (1 Ti. 4:16) Ikuwe tuko tunahubiri sana ao tuko tunahubiri kidogo kulingana na uwezo wetu, tujue kama tuko tunasaidia ile kazi ya maana sana iendelee. (1 Ti. 2:3, 4) Kwa kweli, ni pendeleo kubwa sana kutumika pamoja na Mungu!​—1 Ko. 3:9.

LINDA MAMBO YENYE YEHOVA ALIKUPATIA!

Timoteo aliendelea kumutumikia Yehova hata kama wengine waliacha kufanya vile (Ona fungu 6)

6. Ni nini ilipata watu fulani wenye hawakuendelea kulinda mambo yenye Yehova aliwapatia?

6 Wakati wa Timoteo, Wakristo fulani walizarau pendeleo lenye walikuwa nalo la kutumika pamoja na Mungu. Kwa sababu Dema alipenda sana ulimwengu, aliacha pendeleo lenye alikuwa nalo la kutumika pamoja na Paulo. (2 Ti. 4:10) Inaonekana kama Figelo na Hermogene waliacha kuhubiri kwa sababu waliogopa kama mateso yenye ilimupata Paulo ingewapata wao pia. (2 Ti. 1:15) Himenayo, Aleksanda, na Fileto walifikia kuwa waasi-imani na wakaacha kweli. (1 Ti. 1:19, 20; 2 Ti. 2:16-18) Inaonekana kama ku mwanzo, wale watu wote walikuwa wanamupenda Yehova, lakini hawakuendelea kuona pendeleo lenye aliwapatia kuwa la maana.

7. Shetani anatumia njia gani ili kutufanya tupoteze mambo yenye Yehova ametupatia?

7 Shetani anatumia mambo mbalimbali ili kutufanya tupoteze mambo yenye Yehova ametupatia. Kwa mufano, anatumia televizyo, filme na Enternete ili kubadilisha namna yetu ya kufikiri na ya kutenda na kutufanya pole kwa pole tuache kumupenda Yehova na tuache kutii amri zake. Anajaribu kutuogopesha na kutufanya tuache kuhubiri. Anafanya vile kwa kuchochea watu waseme mambo ya mubaya juu yetu ao watutese. Na ili kutufanya tuache kweli, anajaribu kutuchochea tusikilize mafundisho ya waasi imani yenye inaitwa kwa uongo “ujuzi.”​—1 Ti. 6:20, 21.

8. Mufano wa ndugu mwenye kuitwa Daniel unakufundisha nini?

8 Kama hatuko waangalifu, tunaweza kufikia kuacha kweli. Fikiria mufano wa ndugu Daniel, * mwenye alikuwa anapenda michezo ya video. Anasema hivi: “Nilianza kucheza michezo ya video wakati nilikuwa na miaka kumi hivi. Ku mwanzo, michezo yenye nilikuwa ninacheza haikuwa kabisa ya mubaya. Lakini polepole, nilianza kucheza michezo yenye ilikuwa na mambo ya jeuri, na mambo ya mashetani.” Kisha, Daniel alianza kupitisha saa 15 kila siku na iko anacheza michezo ya video. Daniel anasema tena hivi: “Kusema kweli, nilikuwa ninajua kama michezo yenye nilikuwa ninacheza, na wakati wenye nilitumia ili kujifurahisha, viliharibu pole kwa pole urafiki wangu pamoja na Yehova. Lakini, nilijisadikisha kama haiko lazima nifuate mambo yenye Biblia inasema.” Kwa hiyo, kama hatuko waangalifu, mambo ya kujifurahisha inaweza kutufanya tuache kweli na tupoteze mambo ya maana yenye Yehova ametupatia.

MAMBO YENYE TUNAPASWA KUFANYA ILI TUSIACHE KWELI

9. Kulingana na 1 Timoteo 1:18, 19, Paulo alimulinganisha Timoteo na nani?

9 Soma 1 Timoteo 1:18, 19. Paulo alimulinganisha Timoteo na askari, na alimuambia ‘aendelee kupigana vita ya muzuri.’ Vita yenye Paulo alikuwa anazungumuzia, ilikuwa vita ya kiroho, hapana ya kimwili. Ni mu njia gani sisi Wakristo tuko kama maaskari wenye kupigana vita? Sisi maaskari wa Kristo, tunapaswa kuwa na sifa gani? Tuzungumuzie mambo tano yenye tunaweza kujifunza kupitia maneno yenye Paulo alimuambia Timoteo. Ile mambo tano, inaweza kutusaidia tusiache kweli.

10. Juu ya nini tunapaswa kuwa washikamanifu kwa Mungu?

10 Ukuwe mushikamanifu kwa Mungu. Askari muzuri anakuwaka mushikamanifu. Anaweza kupigana sana ili kulinda mutu fulani mwenye anapendaka ao kitu fulani chenye anaona kuwa cha maana. Paulo alimutia moyo Timoteo akuwe mushikamanifu kwa Mungu. (1 Ti. 4:7) Kama tunamupenda Mungu sana na kushikamana naye, tutajikaza sana ili tusiache kweli. ​—1 Ti. 4:8-10; 6:6.

Kisha kutumika muchana yote, tunapaswa kujikaza sana ili kuenda ku mukutano. Lakini kama tunafanya vile Yehova atatubariki! (Ona fungu la 11)

11. Juu ya nini tunapaswa kujikaza sana ili tuendelee kuwa na hali ya muzuri ya kiroho?

11 Ujikaze sana kufanya mambo yenye kuwa sawa. Askari anapaswa kujikaza sana ili akuwe tayari kwa ajili ya vita. Timoteo aliweza kuendelea kuwa na hali ya muzuri ya kiroho, juu alifuata mashauri ya mutume Paulo. Paulo alimushauria akimbie tamaa za ujana, akomalishe sifa za muzuri, na apitishe wakati pamoja na Wakristo wenzake. (2 Ti. 2:22) Timoteo alipaswa kujikaza sana ili aweze kufanya ile mambo yote. Sisi pia tunapaswa kujikaza sana ili tuweze kupiganisha tamaa za mubaya. (Ro. 7:21-25) Na tena, tunapaswa kujikaza sana ili tuweze kuachana na tabia za mubaya, na tukomalishe sifa za muzuri. (Efe. 4:22, 24) Na wakati tunachoka sana kisha kutumika muchana yote, tunapaswa kujikaza sana ili tuende ku mukutano.​—Ebr. 10:24, 25.

12. Tunapaswa kufanya nini ili tujue namna ya kutumikisha Biblia muzuri?

12 Askari anapaswa kujizoeza kwa ukawaida ili ajue namna ya kutumikisha muzuri silaha zake. Sisi pia, tunapaswa kujizoeza kwa ukawaida ili tujue namna ya kutumikisha Neno la Mungu. (2 Ti. 2:15) Ku mikutano yetu, tunajifunzaka namna mbalimbali za kufanya vile. Lakini, tunapaswa kujifunza Biblia kwa ukawaida kama tunapenda kusaidia wengine waamini kama mafundisho ya Biblia inaweza kuwaletea faida mu maisha yao. Pia tunapaswa kujifunza Biblia kama tunapenda kuwa na imani yenye nguvu. Lakini tujue kama kujifunza Biblia haiko tu kuisoma, tunapaswa kufikiri sana juu ya mambo yenye tuko tunasoma na kutafuta habari mu vichapo vyetu. Ile itatusaidia tuelewe muzuri mafundisho ya Biblia na tujue namna ya kuitumikisha mu maisha yetu. (1 Ti. 4:13-15) Kama tunafanya vile, tutaweza kutumia muzuri Neno la Mungu ili kufundisha wengine. Tena, tukumbuke kama kufundisha watu haiko tu kuwasomea maandiko. Tunapenda kuwasaidia waelewe mafundisho ya Biblia na wajue namna wanaweza kuitumikisha mu maisha yao. Kwa hiyo, kama tunazoea kujifunza Biblia kwa ukawaida, tutakuwa walimu wazuri.​—2 Ti. 3:16, 17.

13. Kulingana na Waebrania 5:14, juu ya nini tunapaswa kuwa na utambuzi?

13 Ukuwe na utambuzi. Askari anapaswa kufikiria mbele ya wakati hatari yenye inaweza kutokea na namna anaweza kuiepuka. Sisi pia tunapaswa kutambua mambo yenye inaweza kuharibu hali yetu ya kiroho na kisha tunapaswa kuiepuka. (Mez. 22:3; Soma Waebrania 5:14.) Kwa mufano, tunapaswa kuchagua mambo ya kujifurahisha kwa hekima. Mambo yenye inakuwaka ku televizyo na mu filme mbalimbali inachocheaka mwenendo wa uasherati. Ile mambo haimufurahishe Mungu na inaweza kuharibu hali yetu ya kiroho. Njo maana, tunapaswa kuepuka mambo yote ya kujifurahisha yenye inaweza kufanya upendo wetu kwa Mungu uanze kupunguka pole kwa pole.​—Efe. 5:5, 6.

14. Namna gani utambuzi ulimusaidia Daniel?

14 Ndugu Daniel, mwenye tulishazungumuzia, alianza kutambua kama haikuwa muzuri kucheza michezo ya video yenye kuwa na mambo ya jeuri ao mambo ya mashetani. Alitafuta habari mu Watchtower Library, yenye ingemusaidia. Kisha kufanya vile aliacha kucheza michezo ya video yenye haiko ya muzuri. Na alivunja uhusiano na watu wenye alikuwa anacheza nao ile michezo. Daniel anasema hivi: “Kuliko kucheza michezo ya video, nilianza kufanya mambo mbalimbali yenye haingeniomba nibakie mu nyumba, na nilianza kupitisha wakati pamoja na marafiki wa mu kutaniko.” Leo, Daniel ni muzee na ni painia.

15. Juu ya nini tunapaswa kuepuka kusikiliza habari za uongo?

15 Kama Timoteo, tunapaswa kutambua hatari ya kusikiliza habari za uongo zenye waasi-imani wanaeneza. (1 Ti. 4:1, 7; 2 Ti. 2:16) Kwa mufano, wanaweza kueneza habari za uongo juu ya ndugu zetu ao kujaribu kutufanya tukuwe na mashaka juu ya tengenezo la Yehova. Zile habari za uongo zinaweza kuregeza imani yetu. Hatupaswe kuziamini. Juu ya nini? Juu “watu wenye wameharibika katika akili na [wenye] hawaelewe tena ile kweli” njo wanaenezaka zile habari. Nia yao ni kuanzisha “ubishi na mashindano.” (1 Ti. 6:4, 5) Wanapenda tuamini zile habari za uongo na tusiaminie tena ndugu zetu.

16. Tunapaswa kuepuka mambo gani yenye inaweza kutukengeusha?

16 Epuka mambo yenye inaweza kukukengeusha. Kama “askari wa Kristo Yesu,” Timoteo alipaswa kuendelea kutia kazi ya kuhubiri pa nafasi ya kwanza kuliko kukazia akili vitu vya kimwili ao miradi ingine ya kimwili. (2 Ti. 2:3, 4) Sisi pia tunapaswa kuepuka kupenda vitu vya kimwili, juu “nguvu za udanganyifu wa utajiri” zinaweza kutufanya tuache kumupenda Yehova, tusifurahie tena Neno lake, na tusipende tena kuhubiri. (Mt. 13:22) Tunapaswa kuendelea kuishi maisha ya mwepesi na kutumia wakati wetu na nguvu zetu ili ‘kuendelea kutafuta kwanza Ufalme.’​—Mt. 6:22-25, 33.

17-18. Tunapaswa kuepuka nini ili kulinda urafiki wetu pamoja na Yehova?

17 Ujitayarishe ili uweze kutenda haraka. Askari anapaswa kupanga mbele ya wakati namna atatenda kama hatari inatokea. Kama tunapenda kulinda mambo yenye Yehova ametupatia, tunapaswa kutenda haraka wakati tunaona hatari. Nini njo inaweza kutusaidia kufanya vile? Tunapaswa kupanga mbele ya wakati namna tutatenda kama hatari inatokea.

18 Kwa mufano, mulimaji mwenye hekima, anajengaka kanyumba ka kidogo pembeni ya shamba yake mbele kipindi cha mvua kianze. Juu ya nini? Juu kama mvua inaanza kunyesha bila kutazamia wakati iko mu shamba yake, anaweza kukimbilia mu kale kanyumba ili kujilinda. Sisi pia, tunapaswa kufikiria mbele ya wakati kama tutafanya nini ikiwa bila kutazamia mambo ya uasherati, mambo ya jeuri ao ya waasi imani inajitokeza wakati tuko tunaangalia televizyo, filme ao wakati tuko ku Enternete. Kama tunajitayarisha mbele ya wakati juu ya mambo yenye inaweza kutokea, tutatenda haraka ili kulinda urafiki wetu pamoja na Yehova, na tutaendelea kuwa safi mbele yake.​—Zb. 101:3; 1 Ti. 4:12.

19. Tutapata baraka gani kama tunalinda mambo ya maana yenye Yehova ametupatia?

19 Tunapaswa kulinda mambo ya maana yenye Yehova ametupatia, ni kusema, mafundisho ya kweli yenye kuwa mu Biblia na pendeleo la kuifundisha wengine. Kama tunafanya vile, tutakuwa na zamiri safi, tutakuwa na maisha yenye furaha, na tutafurahia kusaidia wengine wafikie kumujua Yehova. Kwa kweli Yehova anaweza kutusaidia ili tulinde mambo yenye ametupatia.​—1 Ti. 6:12, 19.

WIMBO 127 Napaswa Kuwa Mtu wa Namna Gani?

^ fu. 5 Tuko na pendeleo kubwa la kujua kweli na kuifundisha wengine. Hii habari itatusaidia tulinde ile pendeleo na tusiipoteze hata kidogo.

^ fu. 8 Majina fulani imebadilishwa.