Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Ndugu Joseph Rutherford na ndugu wengine wakati walienda kutembelea Ulaya

1920—Kumepita Sasa Miaka Mia Moja

1920—Kumepita Sasa Miaka Mia Moja

KU MWANZO tu wa mwaka wa 1920, watu wa Yehova walikuwa na hamu sana ya kufanya kazi yenye ilikuwa inawangojea. Andiko la mwaka lenye walichagua kwa ajili ya mwaka wa 1920 lilikuwa linasema hivi: “BWANA ni nguvu zangu na wimbo wangu.”​—Zb. 118:14, Union Version.

Yehova alitia nguvu wale wahubiri wenye bidii. Mu ile mwaka, hesabu ya wakolportere, ao mapainia, iliongezeka kutoka 225 na kufikia 350. Na kwa mara ya kwanza, zaidi ya wahubiri 8 000 walituma ripoti yao ya mahubiri ku makao makubwa. Na Yehova aliwabariki sana.

WALIKUWA NA BIDII SANA

Tarehe 21 Mwezi wa 3, 1920, Ndugu Joseph Rutherford, mwenye alikuwa anasimamia kazi ya Wanafunzi wa Biblia ile wakati, alizungumuzia habari yenye kusema “Mamilioni Wanaoishi Sasa Hawatakufa Hata Kidogo.” Wanafunzi wa Biblia walifanya yao yote ili kualika watu wenye kupendezwa juu wakuje kufuata ile programu. Walilipia jumba moja kubwa lenye lilikuwa mu muji wa New York City na walipatia watu mialiko 320 000 hivi.

Gazeti lenye lilikuwa na tangazo kuhusu hotuba yenye kichwa “Mamilioni Wanaoishi Sasa Hawatakufa Hata Kidogo”

Wanafunzi wa Biblia hawakuwazia kama watu wengi watakuja, lakini watu wengi sana walikuja. Watu zaidi ya 5 000 walijaza ile jumba na watu 7 000 hivi hawakuweza kuingia. Gazeti Munara wa Mulinzi lilisema kama ile programu ilikuwa “moja kati ya mikutano ya Wanafunzi wa Biblia yenye watu wengi sana walikuja kusikiliza.”

Wanafunzi wa Biblia walifikia kujulikana kuwa watu wenye kutangaza ujumbe wenye kusema kama “mamilioni wanaoishi sasa hawatakufa hata kidogo.” Ile wakati, hawakuelewa kama ujumbe wa Ufalme ulipaswa kuhubiriwa kwa kiasi kikubwa sana. Hata vile, walikuwa na bidii sana. Dada Ida Olmstead, mwenye alianza kukusanyika mu mwaka wa 1902, alikumbuka hivi: “Tulijua kama kuko baraka za mingi sana zenye wanadamu wote watapata, na tulijikaza kutangaza ile habari njema kwa watu wenye tulikutana nao mu kazi ya kuhubiri.”

WALIANZA KUCHAPISHA VICHAPO WAO WENYEWE

Ili kutolea watu chakula cha kiroho, ndugu wenye walikuwa wanatumikia ku Beteli walianza kuchapisha vichapo fulani wao wenyewe. Waliuza mashini na kuitia mu jengo lenye walikuwa wanalipia lenye halikukuwa mbali na Beteli. Lilikuwa kwenye 35 Myrtle Avenue, Brooklyn, New York.

Ndugu Leo Pelle na Walter Kessler walianza kutumikia ku Beteli mu Mwezi wa 1, 1920. Walter alikumbuka hivi: “Wakati tulifika, ndugu mwenye alikuwa anasimamia kazi ya kuchapisha alituangalia na kusema hivi, ‘Muko na saa moja na nusu ya kutumika mbele saa ya kukula ifike.’ Alitupatia kazi ya kuhamisha makarto ya vitabu.”

Ndugu Leo alikumbuka mambo yenye ilifanyika siku yenye ilifuata. Alisema hivi: “Walitupatia kazi ya kusafisha kuta za sehemu ya chini ya lile jengo la gorofa. Ile kazi ilifanyaka nichafuke sana. Nilikuwa sijafanyaka kazi ya kunichafua vile. Lakini ilikuwa kazi ya Bwana na nilifurahia kuifanya.”

Mashini yenye ilitumiwa ili kuchapisha Munara wa Mulinzi

Mu majuma kidogo tu, wajitoleaji wenye bidii, walianza kuchapisha gazeti Munara wa Mulinzi. Kopi elfu makumi sita za Munara wa Mulinzi wa tarehe 1 Mwezi wa 2, 1920, zilichapishwa kwenye gorofa ya kwanza. Wakati uleule, ndugu walitia kwenye sehemu ya chini ya nyumba, mashini ya kuchapisha yenye walikuwa wanaita Mashua ya Vita. Kisha, ndugu walianza kuchapisha wao wenyewe gazeti L’Âge d’Or, walianza na gazeti la tarehe 14 Mwezi wa 4, 1920. Bila shaka, Yehova alikuwa anabariki bidii ya wale wajitoleaji.

“Ilikuwa kazi ya Bwana na nilifurahia kuifanya”

“TUISHI KWA AMANI”

Watu wa Yehova waaminifu waliongeza bidii yao kwa ajili ya kazi ya kuhubiri na walifurahia kutumika pamoja kwa umoja. Lakini, Wanafunzi fulani wa Biblia walikuwa wameacha kweli wakati matatizo ilitokea kuanzia mwaka wa 1917 mupaka mwaka wa 1919. Ndugu wangeweza kufanya nini ili kuwasaidia?

Munara wa Mulinzi wa tarehe 1 Mwezi wa 4, 1920, ulikuwa na habari yenye kichwa “Tuishi kwa Amani.” Ile habari ilikuwa na hii maneno yenye kutia moyo: “Tunaamini kama . . . kila mutu mwenye kuwa na roho ya Bwana . . . iko tayari kusahau mambo yenye imepita, . . . na kuishi kwa umoja kama mwili mumoja.”

Ile maneno yenye kutia moyo ilisaidia watu wengi. Bibi na bwana mumoja waliandika hivi: “Tunaelewa kama tulifanya makosa kubakia bila kuhubiri kwa zaidi ya mwaka moja wakati wengine walikuwa wanaendelea kufanya kazi [ya kuhubiri]. . . . Tutajikaza sana ili tusifanyake tena vile.” Wale wahubiri wenye walianza tena kutenda, walikuwa na kazi ya mingi ya kufanya yenye ilikuwa inawangojea.

WALITOLEA WATU KITABU LE MYSTÈRE DE DIEU ACCOMPLI

Tarehe 21 Mwezi wa 6, 1920, Wanafunzi wa Biblia walianza kampanye kubwa ya kutolea watu kitabu Le Mystère de Dieu Accompli, chenye kilichapishwa kama broshua. Kopi za mingi za kile kitabu zilikuwa zimewekwa wakati wenye mamlaka walikataza Wanafunzi wa Biblia kutolea watu kile kitabu mu mwaka wa 1918.

Haiko mapainia tu njo waliombwa wafanye ile kampanye; ni wahubiri wote njo waliombwa kufanya vile. Ndugu Edmund Hooper alikumbuka kama ni wakati wa ile kampanye njo watu wengi walifanya mahubiri ya nyumba kwa nyumba kwa mara ya kwanza. Alisema hivi “Kila muhubiri mwenye kubatizwa mu kila kutaniko, mwenye anaona kama anaweza kufanya ile kazi anapaswa kujitolea ili kuifanya. Kila mutu anapaswa kujiambia hivi, ‘Jambo moja ni hakika,’ nitatolea watu kitabu Le Mystère de Dieu Accompli.” Ndugu Edmund alisema tena hivi: “Tulianza kuelewa kama kazi ya kuhubiri ingefikia kuwa kubwa sana kuliko vile tuliwazia.”

WALIPANGA TENA KAZI YA KUHUBIRI KATIKA ULAYA

Ndugu Rutherford alipenda kutia moyo Wanafunzi wa Biblia wa inchi zingine, na kuwasaidia kupanga tena kazi ya kuhubiri kwa sababu wakati wa Vita ya Kwanza ya Ulimwengu, ilikuwa vigumu kupashana habari nao. Kwa hiyo, tarehe 12 Mwezi wa 8, 1920, yeye pamoja na ndugu wengine ine walienda kutembelea inchi ya Uingereza na inchi zingine za mingi.

Ndugu Rutherford katika Misri

Wakati Ndugu Rutherford alitembelea Uingereza, Wanafunzi wa Biblia walifanya mikusanyiko tatu na mikutano 12 ya watu wote. Hesabu ya watu wenye walihuzuria zile programu zote ilifikia karibu watu 50 000. Gazeti Munara wa Mulinzi lilizungumuzia kwa kifupi matokeo yenye ile safari ilileta. Lilisema hivi: “Ndugu na dada walitiwa moyo na walipata nguvu mupya. Upendo wao na umoja wao viliongezeka na walitumika kwa umoja mu kazi ya kuhubiri. Watu wengi wenye walikuwa na huzuni walifikia kuwa na furaha.” Mu muji wa Paris, Ndugu Rutherford alizungumuzia tena ile habari yenye kichwa “Mamilioni Wanaoishi Sasa Hawatakufa Hata Kidogo.” Jumba lilikuwa limejaa wakati alianza kutoa hotuba. Na watu mia tatu waliomba kupata habari zaidi.

Ubao wenye kuwa na tangazo kuhusu hotuba yenye ilitolewa mu jumba la Royal Albert Hall katika muji wa Londres

Mu majuma yenye ilifuata, ndugu walitembelea muji wa Atene, muji wa Cairo, na wa Yerusalemu. Ili kusaidia watu wenye walipendezwa mu ile miji, Ndugu Rutherford alipanga kukuwe depo ya vichapo mu muji wa Ramallah, karibu na Yerusalemu. Kisha alirudia Ulaya na kuanzisha Biro ya Tawi ya Ulaya ya Kati na akapanga vichapo vikuwe vinachapishwa pale.

WALIONYESHA WAZI NAMNA WALITENDEWA BILA HAKI

Mu Mwezi wa 9, 1920, Wanafunzi wa Biblia walitoa gazeti L’Âge d’Or namba 27. Ile gazeti ilikuwa ya pekee kwa sababu ilionyesha wazi namna Wanafunzi wa Biblia waliteswa mu mwaka wa 1918. Ile mashini ya kuchapisha yenye kuitwa Mashua ya Vita, yenye tulishataja, ilitumika usiku na muchana ili kuchapisha kopi zaidi ya milioni ine za ile gazeti.

Picha yenye polisi walikamata dada Emma Martin

Watu wenye walisoma ile gazeti, walipata habari kuhusu mambo yenye dada Emma Martin alishitakiwa. Dada Emma alikuwa kolportere katika muji wa San Bernardino, California. Tarehe 17 Mwezi wa 3, 1918 yeye pamoja na ndugu wengine watatu, ni kusema, Hamm, Sonnenburg, na Stevens, walienda kuhuzuria mukutano.

Mwanaume mumoja mwenye alikuwa ku ule mukutano hakukuja kusikiliza mafundisho ya Biblia. Alifikia kusema hivi: “Nilienda ku ule mukutano . . . juu mwendesha-mashtaka njo aliniambia nifanye vile. Nilienda kutafuta ushuhuda.” Ule mwanaume alipata kopi ya kitabu Le Mystère de Dieu Accompli, na njo “ushuhuda” wenye alikuwa anatafuta. Siku fulani kisha pale, dada Emma na wale ndugu wengine watatu walifungwa. Walishitakiwa kuwa walivunja sheria kwa kutolea watu kitabu chenye wenye mamlaka walikuwa wamekataza.

Tribinali iliamua kama Emma na wale ndugu watatu walikuwa na makosa na ikawahukumu kifungo cha miaka tatu mu gereza. Waliomba mara mingi wasikilizwe tena, lakini tarehe 17 Mwezi wa 5, 1920, tribinali ilikataa ombi lao na walianza kutumikia kifungo chao. Hata vile, bila kukawia mambo ilibadilika.

Tarehe 20 Mwezi wa 6, 1920, Ndugu Rutherford alizungumuzia habari juu ya wale Wanafunzi wa Biblia kwenye mukusanyiko wenye ulifanyika mu muji wa San Francisco. Wenye walikuwa ku ule mukusanyiko walihuzunika sana kusikia namna wale Wakristo walitendewa mubaya na wakatumia raisi wa Inchi ya Amerika barua. Mu ile barua walionyesha kama dada Emma alihukumiwa bila haki, kwa sababu wenye mamlaka walitumia mubaya mamlaka yao ili kumutega juu tu wapate sababu ya kumutia mu gereza.

Siku yenye ilifuata, Raisi Woodrow Wilson alibadilisha mara moja hukumu ya dada Emma, ndugu Hamm, Sonnenburg, na Stevens na wakatoka mu gereza.

Ku mwisho wa mwaka wa 1920, ndugu walifurahia sana mambo yenye walifanya ile mwaka. Kazi iliendelea kuongezeka ku makao makubwa, na kuliko wakati mwingine wowote Wakristo wa kweli walitangaza kwa bidii kama Ufalme wa Mungu tu njo utamaliza matatizo yote ya wanadamu. (Mt. 24:14) Mwaka wenye kufuata, ni kusema, mwaka wa 1921, kungekuwa kazi kubwa hata zaidi ya kutangaza kweli za Ufalme.