Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 43

Yehova Iko Anaongoza Tengenezo Lake

Yehova Iko Anaongoza Tengenezo Lake

“‘Hapana kwa nguvu za jeshi, wala kwa nguvu, lakini kwa roho yangu,’ ni vile Yehova wa majeshi anasema.”​—ZEK. 4:6.

WIMBO 40 Sisi Ni wa Nani?

KIFUPI CHA HABARI *

1. Mukristo mwenye kubatizwa anapaswa kuendelea kufanya nini?

KAMA ulishabatizwa, umeonyesha kuwa unamuamini Yehova na kuwa unapenda kutumika pamoja na tengenezo * lake. Lakini unapaswa kuendelea kutia nguvu imani yako kwa Yehova. Na unapaswa kuendelea kuwa hakika kama Yehova iko anatumia tengenezo lake ili kuongoza watu wake leo.

2-3. Namna Yehova iko anaongoza tengenezo lake leo inatusaidia kujua nini juu yake? Leta mifano.

2 Namna Yehova iko anaongoza tengenezo lake leo inatusaidia kujua yeye ni mutu wa namna gani, inatusaidia kujua kusudi lake, na kanuni zake. Tuzungumuzie basi sifa tatu za Yehova zenye zinaonekana mu tengenezo lake.

3 Kwanza, “Mungu hana ubaguzi.” (Mdo. 10:34) Kwa sababu Yehova ni Mungu mwenye upendo, alimutoa Mwana wake kuwa “bei ya ukombozi kwa ajili ya wote.” (1 Ti. 2:6; Yoh. 3:16) Yehova iko anatumia watu wake ili kuhubiri habari njema kwa wale wote wenye kuwa tayari kusikiliza. Ile inasaidia watu mingi kadiri inawezekana wapate faida ya bei ya ukombozi, ni kusema, waokolewe. Pili, Yehova ni Mungu wa utaratibu na wa amani. (1 Ko. 14:33, 40) Kwa hiyo, tengenezo la watu wake linapaswa kuwa na utaratibu na amani. Tatu, Yehova ni Mufundishaji . . . Mukubwa.” (Isa. 30:20, 21) Njo maana, ikuwe mu kutaniko ao mu mahubiri, tengenezo lake linajikaza kufundisha Neno lake Biblia. Namna gani kutaniko la Kikristo la karne ya kwanza lilionyesha zile sifa za Yehova? Namna gani watu wa Yehova wanaonyesha zile sifa za Yehova leo? Na namna gani roho takatifu ya Yehova inaweza kukusaidia kuonyesha zile sifa wakati uko unatumika na tengenezo lake leo?

MUNGU HANA UBAGUZI

4. Kama vile Matendo 1:8 inaonyesha, Yesu aliambia wanafunzi wake wafanye nini, na wangepata musaada gani?

4 Mu karne ya kwanza. Ujumbe wenye Yesu alihubiri ulitolea watu wote tumaini. (Lu. 4:43) Aliambia wafuasi wake waendeleshe kazi yenye alianza. Alisema kama walipaswa kuhubiri “mupaka kwenye sehemu ya mbali zaidi ya dunia.” (Soma Matendo 1:8.) Lakini, hawangeweza kufanya ile kazi kwa nguvu zao wenyewe. Walikuwa na lazima ya “musaidizi” mwenye Yesu aliahidi, ni kusema, roho takatifu. ​—Yoh. 14:26; Zek. 4:6.

5-6. Namna gani roho takatifu ilisaidia wafuasi wa Yesu?

5 Wafuasi wa Yesu walipokea roho takatifu kwenye Pentekoste ya mwaka wa 33 kisha kuzaliwa kwa Yesu. Kwa musaada wa ile roho, walianza kuhubiri bila kukawia, na kwa wakati kidogo tu, maelfu ya watu walikubali habari njema. (Mdo. 2:41; 4:4) Wanafunzi wa Yesu hawakuogopa wala kuacha kuhubiri wakati watu walianza kuwatesa. Lakini walimuomba Mungu awasaidie. Walisali hivi: “Uwezeshe watumwa wako waendelee kutangaza neno lako bila woga wowote.” Kisha walijazwa roho takatifu na wakaendelea ‘kusema neno la Mungu bila woga.’​—Mdo. 4:18-20, 29, 31.

6 Wanafunzi wa Yesu walikuwa na magumu ingine. Kwa mufano, hawakuwa na kopi mingi za Maandiko. Na hawakuwa na vichapo vya kusaidia kuelewa Biblia. Pia, walipaswa kuhubiria watu wenye walikuwa wanazungumuza luga mingi mbalimbali. Lakini, hata kama walikuwa na ile magumu, wale wanafunzi wenye bidii walifanya mambo yenye ilionekana kuwa haingewezekana. Mu miaka makumi tatu hivi, walikuwa wamehubiri habari njema “katika uumbaji wote chini ya mbingu.”​—Kol. 1:6, 23.

7. Zaidi ya miaka 100 yenye imepita, namna gani watu wa Yehova walijua mambo yenye alipenda wafanye, na walitenda namna gani?

7 Mu wakati wetu. Yehova anaendelea kuongoza watu wake na kuwapatia nguvu. Ili kuongoza watu wake, anatumia zaidi sana Neno lake Biblia lenye liliongozwa na roho yake takatifu. Mu Biblia muko habari juu ya utumishi wa Yesu, na muko amri yenye alipatia wafuasi wake ya kuendelesha kazi yenye alianza. (Mt. 28:19, 20) Kufikia Mwezi wa 7, 1881, gazeti Munara wa Mulinzi lilisema hivi: “Yehova hakutuchagua ili tujitafutie utukufu, ao ili tukuwe matajiri, lakini juu tutumie mambo yote yenye tuko nayo ili kuhubiri habari njema.” Kijitabu Ni Nani Waliopewa Kazi Hii (katika Kiingereza), chenye kilitolewa mu mwaka wa 1919, kilisema hivi: “Kuko kazi mingi sana ya kufanya, lakini, ni kazi ya bwana na atatupatia nguvu ya kuifanya.” Kama Wakristo wa karne ya kwanza, wale ndugu walikuwa na uhodari na walitumika sana juu walikuwa hakika kama roho takatifu itawasaidia kuhubiria watu wa namna zote. Sisi pia tuko hakika kama roho takatifu itatusaidia.

Tengenezo la Yehova limetumia vyombo mbalimbali ili kutangaza habari njema (Ona fungu la 8-9)

8-9. Tengenezo la Yehova limetumia njia gani mbalimbali ili kutangazia watu wengi zaidi habari njema?

Tengenezo la Yehova limetumia vyombo mbalimbali ili kutangaza habari njema ya Ufalme. Wakati fulani lilitumia vyombo kama vile: “Foto-Drama ya Uumbaji,” fono, motokari zenye kuwa na vikuza sauti, radio, na leo iko inatumia teknolojia ya sasa. Tengenezo la Yehova liko pia linatafsiri mu luga mingi sana. Hakuna mutu ao tengenezo lenye limefanya kazi ya kutafsiri kwa kiasi kikubwa vile! Juu ya nini liko linafanya vile? Juu watu wa namna zote wasikie habari njema mu luga yao. Yehova hana ubaguzi, alitabiri kama habari njema ingehubiriwa “kwa kila taifa na kabila na luga na watu.” (Ufu. 14:6, 7) Anapenda watu wote wasikie habari njema.

9 Tuseme nini juu ya watu wenye ni nguvu kuingia kwao? Ili kuhubiria wale watu, tengenezo la Yehova lilianza kutumia njia mbalimbali za kuhubiri mahali pa watu wengi. Kwa mufano, mu mwaka wa 2001, Baraza Lenye Kuongoza lilikubali prezantware na vyombo vingine vya kuwekea vichapo vitumiwe katika Ufaransa, na kisha ndugu wa inchi zingine walianza pia kutumia ile njia ya kuhubiri. Ile njia ya kuhubiri ilileta matokeo ya muzuri. Mu mwaka wa 2011, programu mupya ya kuhubiri nafasi zenye kuwa na watu wengi sana ilianzishwa mu muji wa New York City katika Inchi ya Amerika. Mu mwaka wa kwanza, vitabu 102 129 na magazeti 68 911 vilitolewa, na watu 4 701 waliomba funzo la Biblia! Ile ilionyesha kama roho ya Mungu ilikuwa inaongoza ile kazi. Kwa hiyo, Baraza Lenye Kuongoza lilikubali ndugu wa mu dunia yote waanze kutumia prezantware na vyombo vingine vya kuwekea vichapo.

10. Tunaweza kufanya nini ili tukomalishe ufundi wetu wa kuhubiri na kufundisha?

10 Mambo yenye unaweza kufanya. Utumie mazoezi yenye Yehova anatutolea ku mikutano yetu. Uhubiri kwa ukawaida na ndugu na dada wa mu kikundi chenu cha mahubiri. Wanaweza kukusaidia ili ukomalishe ufundi wako wa kuhubiri na kufundisha, na mufano wao unaweza kukutia moyo. Uendelee kuhubiri hata kama unapata magumu. Kama vile andiko la musingi la hii habari linaonyesha, tuko tunafanya mapenzi ya Mungu kwa musaada wa roho yake takatifu, hapana kwa nguvu zetu wenyewe. (Zek. 4:6) Kwa hiyo, tunaweza kuwa hakika kama Yehova atatupatia nguvu yenye tuko nayo lazima juu tuko tunafanya kazi yake.

YEHOVA NI MUNGU WA UTARATIBU NA WA AMANI

11. Namna gani baraza lenye kuongoza la karne ya kwanza, lilitumika kwa umoja ili utaratibu uendelee kati ya watu wa Mungu?

11 Mu karne ya kwanza. Baraza lenye kuongoza katika Yerusalemu lilitumika kwa umoja ili kuendelee kuwa amani na utaratibu kati ya watu wa Mungu. (Mdo. 2:42) Kwa mufano, mu mwaka wa 49 hivi kisha kuzaliwa kwa Yesu, watu walikuwa na mawazo tofauti juu ya kutahiriwa. Kwa hiyo, baraza lenye kuongoza, chini ya uongozi wa roho takatifu, lilizungumuzia ile jambo. Kama kutaniko lingeendelea kugawanyika juu ya ile jambo, kazi ya kuhubiri haingeendelea muzuri. Hata kama mitume na wazee walikuwa Wayahudi, uamuzi wao haukutegemea desturi za Wayahudi, wala hawakuchochewa na wale wenye kuunga mukono zile desturi. Lakini walitafuta muongozo wa Neno la Mungu, na walimuomba roho yake takatifu ili iwasaidie kukamata uamuzi muzuri. (Mdo. 15:1, 2, 5-20, 28) Ile ilileta matokeo gani? Yehova alibariki uamuzi wao, waliendelea kuwa na amani na umoja, na waliendelea kuhubiri.​—Mdo. 15:30, 31; 16:4, 5.

12. Ni nini inaonyesha kama kuko utaratibu na amani kati ya watu wa Yehova leo?

12 Mu wakati wetu. Tengenezo la Yehova limejikaza sana ili kuendelee kuwa amani na utaratibu kati ya watu wa Yehova. Kufikia mwaka wa 1895, gazeti Le Phare de la Tour de Sion la tarehe 15 Mwezi wa 11, lilikuwa na habari yenye kichwa “Kwa Adabu na kwa Utaratibu,” yenye ilitegemea 1 Wakorinto 14:40. Ile habari ilisema hivi: “Mitume waliandika mambo mingi sana kwa kutaniko la karne ya kwanza juu ya utaratibu . . . Ni muzuri tuendelee kufuata kwa uangalifu ‘mambo yenye yaliandikwa zamani ili kutufundisha.’” (Ro. 15:4) Ile inaonyesha kama tengenezo la Yehova leo, linatumika sana ili amani na utaratibu viendelee kuwa kati ya watu wa Mungu kama vile Wakristo wa karne ya kwanza walifanya. Kwa mufano, kama unahuzuria funzo la Munara wa Mulinzi mu kutaniko lingine, ao hata mu inchi ingine, hautajiuliza ikiwa funzo litafanyika namna gani, ao ni habari gani mutajifunza. Juu ya nini? Juu unajua namna funzo linafanyikaka na unajua habari yenye mutajifunza. Bila musaada wa roho takatifu haiwezekane kuwa na umoja wa namna ile.​—Sef. 3:9, maelezo ya chini.

13. Yakobo 3:17 inaweza kutuchochea tujiulize maulizo gani?

13 Mambo yenye unaweza kufanya. Yehova anapenda watu wake ‘waendeleze umoja wa roho katika kifungo chenye kuunganisha cha amani.’ (Efe. 4:1-3) Kwa hiyo, ujiulize hivi: ‘Ninaendelezaka umoja na amani mu kutaniko. Ninajikazaka kutii wale wenye kuongoza? Wengine wanajisikia huru kunikaribia ili kuniomba musaada, zaidi sana kama niko na madaraka mu kutaniko? Ninajikazaka kuheshimia wakati, kusaidia wengine, na kuwatumikia?’ (Soma Yakobo 3:17.) Kati ya ile mambo, kama unaona jambo fulani lenye unapaswa kufanyia maendeleo, umuombe Yehova akusaidie na roho yake takatifu. Kadiri unaacha roho takatifu ikusaidie kubadilika na iongoze matendo yako, ni vile ndugu na dada watakupenda na watakuona kuwa wa maana.

YEHOVA ANATUFUNDISHA NA ANATUPATIA ROHO YAKE TAKATIFU

14. (Wakolosai 1:9, 10) Namna gani Yehova alisaidia watu wake mu karne ya kwanza wakuwe na ujuzi wenye hauna makosa?

14 Mu karne ya kwanza. Yehova anapendaka kufundisha watu wake. (Zb. 32:8) Anapenda wamujue, wamupende, na waishi milele. Bila kufundishwa na Yehova, ile mambo yote haiwezekane. (Yoh. 17:3) Yehova alitumia kutaniko la Kikristo la karne ya kwanza ili kufundisha watu wake. (Soma Wakolosai 1:9, 10.) “Musaidizi” mwenye Yesu aliahidi, ni kusema, roho takatifu ilisaidia sana. (Yoh. 14:16) Ilisaidia wanafunzi kuelewa Neno la Mungu, iliwakumbusha mambo mingi yenye Yesu alisema na kufanya. Mambo fulani kati ya ile, ilifikia kuandikwa mu Injili. Kuelewa Neno la Mungu, na kukumbuka mambo yenye Yesu alisema na kufanya, kulitia nguvu imani ya Wakristo wa karne ya kwanza. Na pia, kuliwasaidia wamupende sana Mungu, wapende sana Mwana wake, na wapendane kati yao wenyewe.

15. Ni katika njia gani Yehova iko anatimiza unabii wenye kuwa mu Isaya 2:2, 3?

15 Mu wakati wetu. Yehova alitabiri kama “katika kipindi cha mwisho,” watu wa mataifa yote watakuja kwenye mulima wake, ni kusema, watajiunga na waabudu wake ili kufundishwa njia zake. (Soma Isaya 2:2, 3.) Ule unabii uko unatimia leo. Ibada ya kweli imeinuliwa juu sana kuliko ibada zingine zote za uongo. Na Yehova iko anasaidia watu wake kuelewa mafundisho mingi ya Biblia! (Isa. 25:6) Kupitia “mutumwa muaminifu na mwenye busara,” Yehova iko anatutolea chakula mingi ya kiroho, na iko anafanya vile mu njia mbalimbali. Kwa mufano, anatutolea habari mbalimbali zenye tunaweza kusoma, hotuba, na video mbalimbali. (Mt. 24:45) Tunajisikia kama Elihu, rafiki ya Yobu, mwenye alisema hivi: “Ni mufundishaji gani iko kama [Mungu]?”​—Yob. 36:22.

Uendelee kuamini mambo yenye unajifunza na kuitumikisha mu maisha yako (Ona fungu la 16) *

16. Unaweza kufanya nini ili kukomaa kiroho?

16 Mambo yenye unaweza kufanya. Roho ya Mungu itakusaidia ili utumikishe mambo yenye uko unasoma na kujifunza katika Neno la Mungu. Usali kama muandikaji mumoja wa Zaburi, mwenye alisali hivi: “Unifundishe, Ee Yehova, kuhusu njia yako. Nitatembea katika kweli yako. Unganisha moyo wangu ili niogope jina lako.” (Zb. 86:11) Kwa hiyo, uendelee kusoma na kujifunza Biblia na vichapo vingine vyenye Yehova anatutolea kupitia tengenezo lake. Lakini nia yako haipaswe kuwa kujua tu mambo mingi. Unapaswa kuamini kabisa mambo yenye uko unajifunza, na unapaswa kuitumikisha mu maisha yako. Roho ya Yehova inaweza kukusaidia ufanye vile. Unapaswa pia kutia moyo ndugu na dada zako. (Ebr. 10:24, 25) Juu ya nini? Juu wako katika familia yako ya kiroho. Umuombe Mungu akupatie roho yake takatifu ili ikusaidie juu wakati wa mikutano utoe majibu yenye kutoka mu moyo. Na kama uko na mugao, ujikaze ili kuupitisha muzuri. Kama unafanya vile, utaonyesha Yehova na Mwana wake kama unapenda “kondoo” wao wa maana sana.​—Yoh. 21:15-17.

17. Unaweza kufanya nini ili kuonyesha kama unaunga mukono tengenezo la Yehova?

17 Karibuni, ku dunia kutabakia tu tengenezo moja, lenye kuongozwa na roho ya Mungu. Kwa hiyo, uendelee kutumika kwa bidii pamoja na tengenezo la Yehova. Uige Yehova mwenye hana ubaguzi, kwa kuhubiri habari njema kwa watu wa namna zote. Kama Yehova, uonyeshe kama unapenda utaratibu na amani kwa kuendeleza umoja katika kutaniko. Na umusikilize Mufundishaji wako Mukubwa kwa kusoma na kujifunza Biblia na vichapo vyenye anatutolea kupitia tengenezo lake. Kama unafanya vile, hautaogopa wakati ulimwengu wa Shetani utaharibiwa. Utakuwa hodari na utakuwa upande wa watu wenye wako wanatumika pamoja na tengenezo la Yehova kwa ushikamanifu.

WIMBO 3 Tumaini, Nguvu, na Uhakika Wetu

^ fu. 5 Uko hakika kama Yehova iko anaongoza tengenezo lake leo? Mu hii habari, tutaona namna Yehova aliongoza kutaniko la Kikristo la karne ya kwanza na namna anaendelea kuongoza watu wake leo.

^ fu. 1 MAFASIRIO YA MANENO FULANI: Tengenezo la Yehova la ulimwenguni pote liko na sehemu mbili: sehemu ya mbinguni na sehemu ya ku dunia. Mu hii habari neno “tengenezo” linahusu sehemu ya ku dunia ya tengenezo la Yehova.

^ fu. 52 MAFASIRIO YA PICHA: Kisha kuangalia video zenye kuonyesha wengine wenye wako wanatumikia mahali kwenye kuwa lazima kubwa ya wahubiri, dada mumoja painia anaamua kufuata mufano wao. Kisha wakati fulani, anatimiza muradi wake wa kutumikia mahali kwenye kuwa lazima kubwa ya wahubiri.