Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 45

Namna ya Kusaidia Wengine Washike Amri za Kristo

Namna ya Kusaidia Wengine Washike Amri za Kristo

“Kwa hiyo, muende, na mufanye wanafunzi . . . , muwafundishe kushika mambo yote yenye nimewaamuru ninyi.”​—MT. 28:19, 20.

WIMBO 89 Sikiliza, Tii, Upate Baraka

KIFUPI CHA HABARI *

1. Kulingana na Matayo 28:18-20, Yesu alipatia wanafunzi wake amri gani?

KISHA Yesu kufufuliwa, alitokea wanafunzi wake wenye walikuwa wamekusanyika katika Galilaya. Alikuwa na jambo la maana la kuwaambia. Ni jambo gani? Maneno yake inapatikana mu Matayo 28:18-20.​—Soma.

2. Tutazungumuzia maulizo gani?

2 Amri ya Yesu ya kufanya wanafunzi inahusu pia kila mutumishi wa Mungu leo. Kwa hiyo, tuzungumuzie basi maulizo tatu yenye inahusu kazi yenye Yesu alitupatia. Kwanza, zaidi ya kufundisha wanafunzi wa mupya mambo yenye Mungu anapenda wafanye, tunapaswa kufanya nini ingine? Pili, wahubiri wote mu kutaniko wanaweza kufanya nini ili kusaidia wanafunzi wa Biblia wakomae kiroho? Tatu, tunaweza kufanya nini ili kusaidia ndugu na dada wenye hawatende tena warudilie kazi ya kufanya wanafunzi?

TUWAFUNDISHE KUSHIKA AMRI ZA KRISTO

3. Wakati Yesu alipatia wanafunzi wake amri ya kufanya wanafunzi, alisema jambo gani la maana?

3 Maagizo ya Yesu iko wazi. Tunapaswa kufundisha watu mambo yenye aliamuru. Lakini, kuko jambo la maana lenye hatupaswe kusahau. Yesu hakusema, ‘Muwafundishe mambo yote yenye nimewaamuru ninyi.’ Lakini, alisema hivi: Muwafundishe “kushika mambo yote yenye nimewaamuru ninyi.” Ili kutii ile maagizo ya Yesu tunapaswa kufundisha mwanafunzi wa Biblia mambo yenye anapaswa kufanya na tunapaswa kumuonyesha namna ya kufanya ile mambo. (Mdo. 8:31) Tunaweza kufanya vile namna gani?

4. Kushika amri maana yake nini? Leta mufano.

4 “Kushika” amri maana yake kutii ile amri. Ili kuelewa namna tunaweza kufundisha mutu kushika ao kutii mambo yenye Yesu aliamuru, tufikirie mufano wenye kufuata. Mwalimu wa kufundisha kutembeza motokari anafanyaka nini ili kusaidia mwanafunzi wake ashike sheria zenye kuhusu namna ya kutembeza motokari? Ule mwalimu anaweza kwanza kufundisha mwanafunzi wake zile sheria. Lakini ili kumusaidia ajue namna ya kuzishika, anapaswa kufanya jambo lingine. Anapaswa kuwa pembeni ya mwanafunzi ili kumutolea mashauri, wakati mwanafunzi iko anatembeza motokari na kujaribu kutumikisha mambo yenye amejifunza. Ule mufano unaweza kutufundisha nini?

5. (a) Kulingana na Yohana 14:15 na 1 Yohana 2:3, tunapaswa kusaidia wanafunzi wetu wa Biblia wajue kufanya nini? (b) Namna gani tunaweza kusaidia mwanafunzi wetu atumikishe mambo yenye iko anajifunza?

5 Wakati tunajifunza Biblia na wengine, tunawafundisha mambo yenye Mungu anapenda wafanye. Lakini, zaidi ya kuwafundisha, tunapaswa kufanya jambo lingine. Tunapaswa kuwasaidia wajue kutumikisha mambo yenye wako wanajifunza. (Soma Yohana 14:15; 1 Yohana 2:3.) Kupitia mufano wetu, tunaweza kuonyesha mwanafunzi wetu wa Biblia namna ya kutumikisha kanuni za Biblia ku masomo, ku kazi, ao wakati iko anajifurahisha. Tunaweza kumuelezea jambo fulani lenye lilitufikia mu maisha yetu, na kumusaidia aone namna kutumikisha kanuni za Biblia kulitulinda na kulitusaidia kukamata uamuzi wenye hekima. Wakati tuko na mwanafunzi wetu, tunaweza kumuomba Yehova amuongoze kupitia roho yake takatifu.​—Yoh. 16:13.

6. Tunapaswa kufanya nini ingine ili kusaidia mwanafunzi wa Biblia ashike amri za Yesu?

6 Tunapaswa kufanya nini ingine ili kusaidia mwanafunzi wa Biblia ashike amri za Yesu? Tunapaswa kumusaidia akuwe na hamu ya kufanya wanafunzi. Wanafunzi fulani wa Biblia wanaweza kuogopa kuhubiri. Kwa hiyo, kama mwanafunzi wetu iko vile, tunapaswa kuwa wavumilivu na kumusaidia aelewe muzuri mafundisho ya Biblia. Ile itamusaidia akuwe na imani yenye nguvu, itagusa moyo wake, na itamuchochea apende kuhubiri.

7. Namna gani unaweza kusaidia mwanafunzi wa Biblia akuwe na hamu ya kutangazia wengine habari njema?

7 Tunaweza kuuliza mwanafunzi wetu wa Biblia maulizo sawa vile: “Kukubali ujumbe wa Ufalme kumekuletea faida gani mu maisha yako? Unawaza kama wengine pia wako na lazima ya kusikia ule ujumbe? Unaweza kufanya nini ili kuwasaidia?” (Mez. 3:27; Mt. 9:37, 38) Uonyeshe mwanafunzi wako trakte zenye kuwa kati ya Vyombo Vyetu vya Kufundishia na umuambie achague trakte zenye zinaweza kufurahisha watu wa familia yake, marafiki wake, ao wafanyakazi wenzake. Kisha, umupatie trakte fulani kati ya zile trakte. Mufanye mazoezi ili ajue namna anaweza kutolea wengine trakte kwa busara. Na tena, wakati atakuwa muhubiri mwenye hajabatizwa, unaweza kuwa unahubiri naye ili kumusaidia.​—Muh. 4:9, 10; Lu. 6:40.

NAMNA KUTANIKO LINAWEZA KUSAIDIA WANAFUNZI WA BIBLIA WAFANYE MAENDELEO

8. Juu ya nini ni jambo la maana mwanafunzi amupende sana Mungu na watu wengine? (Ona pia kisanduku “ Namna ya Kusaidia Mwanafunzi wa Biblia Amupende Mungu Sana.”)

8 Ukumbuke kama Yesu alituambia tufundishe wengine “kushika mambo yote” yenye aliamuru. Kati ya ile mambo, kuko amri mbili kubwa, ni kusema, kumupenda Mungu na kupenda watu wengine. Zile amri zinaweza kutusaidia tuanze kuhubiri na kufanya wanafunzi. (Mt. 22:37-39) Juu ya nini tunasema vile? Juu sababu kubwa yenye inatuchochea kuhubiri ni upendo wenye tuko nao kwa Mungu na kwa watu wengine. Hata vile, wanafunzi fulani wa Biblia wanaweza kuogopa kuhubiri. Lakini, tunaweza kuwahakikishia kama pole kwa pole Yehova atawasaidia wasikuwe wanaogopa wanadamu. (Zb. 18:1-3; Mez. 29:25) Kisanduku chenye kuwa ku ukurasa wa ine kinazungumuzia mambo yenye tunapaswa kufanya ili kusaidia mwanafunzi wa Biblia amupende Mungu sana. Zaidi ya ile, kutaniko linaweza kufanya nini ili kusaidia mwanafunzi mupya akuwe na upendo zaidi?

9. Mutu mwenye iko anajifunza kutembeza motokari, anapaswa kufanya nini ili kujifunza mambo ya maana yenye inaweza kumusaidia?

9 Tufikirie tena mufano wa mutu mwenye iko anajifunza kutembeza motokari. Wakati iko anatembeza motokari, na mwalimu wake iko pembeni yake, anapaswa kufanya nini ili kujifunza mambo ya maana yenye inaweza kumusaidia? Anapaswa kumusikiliza mwalimu wake na kuangalia shofere wengine wenye wako wanatembeza motokari kwa uangalifu. Kwa mufano, mwalimu wake anaweza kumuonyesha shofere mwenye anaachia shofere mwingine njia ili apite mbele yake. Ao anaweza kumuonyesha shofere mwenye anapunguza mwangaza wa taa za motokari yake ili aepuke kuzuia shofere wengine wenye kuja mbele yake kuona muzuri. Mifano ya wale shofere wengine inaweza kumusaidia ajifunze mambo ya maana yenye atatumikisha wakati iko anatembeza motokari.

10. Ni nini itasaidia mwanafunzi wa Biblia afanye maendeleo?

10 Vilevile, mwanafunzi wa Biblia mwenye anaingia katika barabara yenye kuongoza kwenye uzima wa milele anajifunzaka mambo mingi kupitia mwalimu wake, na kupitia watumishi wengine wa Yehova wenye kuwa mufano muzuri. Kwa hiyo, nini njo itasaidia sana mwanafunzi wa Biblia ili afanye maendeleo ya kiroho? Ni kuhuzuria mikutano yetu. Juu ya nini? Juu mafundisho ya Biblia yenye kutolewa ku mikutano itamusaidia ajue mambo mingi juu ya Biblia, akuwe na imani yenye nguvu na amupende zaidi Yehova. (Mdo. 15:30-32) Zaidi ya ile, ku mikutano mwalimu anaweza kusaidia mwanafunzi wake ajuane na ndugu na dada wenye hali yao inafanana na hali ya mwanafunzi katika njia fulani. Mwanafunzi atajionea mifano ya ndugu na dada wenye kuonyeshana upendo mu kutaniko. Fikiria mifano yenye kufuata.

11. Mwanafunzi anaweza kuona mifano gani mu kutaniko, na ile inaweza kuwa na matokeo gani juu yake?

11 Kwa mufano, mwanafunzi wa Biblia mwenye iko anakomalisha watoto wake yeye peke, anaona dada Mukristo mwenye iko mu hali sawa yake. Anafurahi sana kuona namna ule dada iko anajikaza sana kukuja ku mikutano pamoja na watoto wake wadogo. Mwanafunzi mwingine wa Biblia mwenye iko anajikaza sana kuacha kuvuta tumbako, anakutana na ndugu mwenye mbele akuwe Shahidi wa Yehova alikuwaka anavuta tumbako lakini akafikia kuacha ile tabia. Ule ndugu anaambia ule mwanafunzi kama kumupenda sana Yehova njo kulimuchocheaka atii amri zake. (2 Ko. 7:1; Flp. 4:13) Kisha ule ndugu kuelezea ule mwanafunzi namna aliacha kuvuta tumbako, anamuambia hivi: “Na wewe pia unaweza kuacha kuvuta.” Ile inatia moyo sana mwanafunzi na anaamini kama yeye pia anaweza kuacha kuvuta tumbako. Na kijana mwanamuke mwenye iko anajifunza Biblia anaona dada kijana mwenye anafurahia kumutumikia Yehova. Wakati anaona vile, ile inamuchochea apende kujua juu ya nini ule dada iko na furaha.

12. Juu ya nini tunaweza kusema kama kila mutu mu kutaniko anaweza kufanya jambo fulani ili kusaidia mwanafunzi wa Biblia?

12 Wakati mwanafunzi wa Biblia anajuana na ndugu na dada mbalimbali wenye kuwa waaminifu, anajifunza kupitia mifano yao namna anaweza kutii amri ya Kristo ya kumupenda Mungu na jirani. (Yoh. 13:35; 1 Ti. 4:12) Zaidi ya ile, kama vile tuliona, mwanafunzi wa Biblia anaweza kujifunza kupitia mifano ya ndugu na dada wenye wako wanapambana na magumu sawa yake. Mifano ya wale ndugu na dada inaweza kumusaidia aone kama yeye pia anaweza kufanya mabadiliko ili akuwe mwanafunzi wa Kristo. (Kum. 30:11) Ndugu na dada wote mu kutaniko wanaweza kufanya jambo fulani ili kusaidia mwanafunzi wa Biblia afanye maendeleo ya kiroho. (Mt. 5:16) Na wewe unafanyaka nini ili kutia moyo mwanafunzi wa Biblia mwenye iko anakuja ku mikutano?

TUSAIDIE WALE WENYE HAWATENDE TENA ILI WARUDILIE KAZI YA KUHUBIRI

13-14. Namna gani Yesu alitendea mitume wake wakati walikuwa wenye kuvunjika moyo?

13 Tunapenda kusaidia ndugu na dada zetu wenye hawatende tena ili warudilie kazi ya kuhubiri na kufanya wanafunzi. Namna Yesu alitendea mitume wake wakati walikuwa wenye kuvunjika moyo, inatuonyesha mambo yenye tunaweza kufanya leo.

14 Ku mwisho wa utumishi wa Yesu hapa ku dunia, mbele tu ya kifo chake, mitume “wote walimuacha na kukimbia.” (Mk. 14:50; Yoh. 16:32) Juu walikuwa wenye kuvunjika moyo, Yesu aliwatendea namna gani? Muda mufupi kisha tu kufufuliwa kwake, Yesu aliambia hivi wanafunzi wake fulani: “Musiogope! Muende, mujulishe ndugu zangu [kama nimefufuliwa].” (Mt. 28:10a) Hata kama mitume wake walimuacha, yeye hakuwaacha na aliendelea kuwaita “ndugu zangu.” Kama Yehova, Yesu aliwaonyesha rehema na aliwasamehe.​—2 Fa. 13:23.

15. Tunaona namna gani wale wenye wameacha kuhubiri?

15 Sisi pia tunahangaikia sana wale wenye wameacha kuhubiri. Wao ni ndugu na dada zetu, na tunawapenda! Tungali tunakumbuka namna walikuwa wanamutumikia Yehova kwa bidii sana zamani. Na wamoja kati yao walifanya vile kwa miaka mingi. (Ebr. 6:10) Tunawakumbuka sana! (Lu. 15:4-7) Kama Yesu, tunaweza kufanya nini ili kuonyesha kama tunawahangaikia?

16. Tunaweza kufanya nini ili kuonyesha kama tunahangaikia ndugu na dada zetu wenye hawatende tena?

16 Tuwaalike ku mikutano. Ili kutia moyo mitume wake wenye walikuwa wamevunjika moyo, Yesu aliwaalika ku mukutano. (Mt. 28:10b; 1 Ko. 15:6) Leo pia, ili kutia moyo wale wenye hawatende tena, tunaweza kuwaalika ku mikutano. Lakini tunajua kama pengine inaomba kuwaalika mara mingi ili wakuje. Kwa kweli, Yesu alifurahi sana wakati wanafunzi wake walikuja ku ule mukutano.​—Linganisha na Matayo 28:16, na Luka 15:6.

17. Tunapaswa kufanya nini wakati ndugu ao dada mwenye hatende tena anakuja ku mukutano?

17 Tuwakaribishe kwa furaha. Yesu alifanya wanafunzi wake wajisikie kuwa wenye kukaribishwa wakati walikutana naye; aliwakaribia ili kuzungumuza nao. (Mt. 28:18) Tutafanya nini wakati ndugu ao dada mwenye hatende tena anakuja kwenye Jumba la Ufalme? Tunapaswa kumukaribisha kwa furaha. Ku mwanzo, tunaweza kuwa na wasiwasi juu ya mambo yenye tutamuambia. Lakini bila kumufanya asikie haya, tunaweza tu kumuambia kama tunafurahi sana kumuona.

18. Tunaweza kufanya nini ili kutegemeza wahubiri wenye hawatende tena?

18 Tuwahakikishie kama tutawategemeza. Pengine wanafunzi wa Yesu waliona kama hawataweza kuhubiri mu dunia yote. Yesu aliwahakikishia kama atawategemeza. Aliwaambia hivi: “Niko pamoja na ninyi sikuzote.” (Mt. 28:20) Ile maneno ya Yesu iliwasaidia? Ndiyo. Juu ya nini tunasema vile? Juu wakati kidogo kisha pale, walianza “kufundisha na kutangaza habari njema” kwa bidii. (Mdo. 5:42) Sisi pia tunapaswa kuhakikishia wahubiri wenye hawatende tena kuwa tutawategemeza. Juu ya nini? Juu wanaweza kuogopa kuanza kuhubiri tena. Kwa hiyo, tunaweza kuwahakikishia kama hawatakuwa wanahubiri peke yao. Kisha, wakati wataanza kuhubiri tena, tunaweza kuhubiri pamoja nao. Kwa kweli, watafurahi sana kama tunawategemeza. Ni muzuri tuwaone na kuwatendea kama ndugu na dada zetu. Kama tunafanya vile, wanaweza kuanza kutenda tena na kutaniko lote linaweza kuwa na furaha.

TUNAPENDA KUMALIZA KAZI YENYE YESU ALITUPATIA

19. Tuko na nia ya kufanya nini, na juu ya nini?

19 Kazi ya kufanya wanafunzi itaendelea mupaka wakati gani? Itaendelea mupaka ku umalizio wa mupangilio huu wa mambo. (Mt. 28:20; ona Maana ya Maneno ya Biblia, “Umalizio wa mupangilio wa mambo.”) Tutaweza kumaliza kazi yenye Yesu alitupatia? Ndiyo. Tutajikaza sana kufanya vile! Tuko tayari kutumia wakati wetu, nguvu yetu, na vitu vyetu ili kutafuta wale wenye kuwa na “mwelekeo wenye kufaa kwa ajili ya uzima wa milele.” (Mdo. 13:48) Wakati tunafanya vile, tunafuata mufano wa Yesu. Alisema hivi: “Chakula changu ni kufanya mapenzi ya ule mwenye alinituma na kumaliza kazi yake.” (Yoh. 4:34; 17:4) Sisi pia tuko na ile nia. Tunapenda kumaliza kazi yenye Yesu alitupatia. (Yoh. 20:21) Na tunapenda wengine, kutia ndani wale wenye hawatende tena, waendelee kufanya ile kazi pamoja na sisi.​—Mt. 24:13.

20. Kulingana na Wafilipi 4:13, juu ya nini tuko hakika kama tutaweza kufanya kazi yenye Yesu alitupatia?

20 Kwa kweli, haiko mwepesi kufanya kazi yenye Yesu alitupatia. Lakini, hatuko tunafanya ile kazi peke yetu. Yesu alituambia kama atakuwa pamoja na sisi. Mu kazi ya kufanya wanafunzi, tuko “wafanyakazi pamoja na Mungu” na “pamoja na Kristo.” (1 Ko. 3:9; 2 Ko. 2:17) Kwa hiyo, tuko hakika kama tutaweza kufanya ile kazi. Ni pendeleo kabisa kufanya wanafunzi na kusaidia wengine pia wafanye ile kazi. Kufanya vile, kunatuletea furaha!​—Soma Wafilipi 4:13.

WIMBO 79 Wafundishe Kusimama Imara

^ fu. 5 Yesu aliambia wafuasi wake wafanye wanafunzi na wawafundishe kushika mambo yote yenye alikuwa amewaamuru. Hii habari inazungumuzia namna tunaweza kufanya vile. Sehemu fulani ya habari hii inategemea habari yenye ilitolewa mu Munara wa Mulinzi wa tarehe 1 Mwezi wa 7, 2004 ukurasa wa 14-19.

^ fu. 66 MAFASIRIO YA PICHA: Dada mwenye iko anaongoza funzo la Biblia anafasiria mambo yenye mwanafunzi anapaswa kufanya ili amupende Mungu sana. Kisha, ule mwanafunzi anafanya mambo tatu yenye mwalimu wake alimuambia.