Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 46

Ukuwe Hodari​—Yehova Ni Musaidizi Wako

Ukuwe Hodari​—Yehova Ni Musaidizi Wako

“Sitakuacha hata kidogo, na sitakutupa hata kidogo.”​—EBR. 13:5.

WIMBO 55 Msiwaogope!

KIFUPI CHA HABARI *

1. Ni nini itatusaidia wakati tunajisikia kama tuko peke yetu na kama hatutaweza kuvumilia magumu yetu? (Zaburi 118:5-7)

ULISHAKAJISIKIA kama uko peke yako, na kama hakuna mutu wa kukusaidia uvumilie magumu? Watu wengi walishakajisikia vile, hata watumishi waaminifu wa Yehova. (1 Fa. 19:14) Kama siku moja unajisikia vile, ukumbuke hii ahadi ya Yehova: “Sitakuacha hata kidogo, na sitakutupa hata kidogo.” Kwa hiyo, tunaweza kusema hivi kwa uhakika: “Yehova ni musaidizi wangu; sitaogopa.” (Ebr. 13:5, 6) Mutume Paulo aliandikia Wakristo wa Yudea ile maneno mu mwaka wa 61 hivi kisha kuzaliwa kwa Yesu. Ile maneno inatukumbusha mambo yenye kuwa mu Zaburi 118:5-7.​—Soma.

2. Tutazungumuzia nini mu hii habari, na juu ya nini?

2 Kama ule muandikaji wa zaburi, Paulo alijionea namna Yehova alikuwa musaidizi wake. Kwa mufano, zaidi ya miaka mbili mbele aandike barua yake kwa Waebrania, Paulo alifanya safari ya hatari mu bahari yenye ilikuwa na zoruba kali. (Mdo. 27:4, 15, 20) Mbele ya ile safari na wakati wa ile safari, Yehova alimusaidia mu njia mingi. Tutazungumuzia njia tatu. Yehova alimutolea musaada kupitia Yesu na malaika, watu wenye mamlaka, na Wakristo wenzake. Kuchunguza tena mambo yenye ilitokea mu maisha ya Paulo, kutatusaidia tukuwe hakika kama Mungu atatusaidia wakati tunamuomba musaada katika sala.

YEHOVA ANATOA MUSAADA KUPITIA YESU NA MALAIKA

3. Pengine Paulo alijiuliza nini, na juu ya nini?

3 Paulo alikuwa na lazima ya musaada. Mu mwaka wa 56 hivi kisha kuzaliwa kwa Yesu, kikundi cha watu walimupeleka inje ya hekalu katika Yerusalemu, na walijaribu kumuua. Siku yenye ilifuata, wakati Paulo alipelekwa mbele ya Sanhedrini, maadui wake walikuwa karibu kumupasua vipande-vipande. (Mdo. 21:30-32; 22:30; 23:6-10) Ile wakati pengine Paulo alijiuliza hivi: ‘Nitaendelea kuteseka hivi mupaka wakati gani?’

4. Namna gani Yehova alitumia Yesu ili kumusaidia Paulo?

4 Paulo alipata musaada gani? Kisha Paulo kufungwa, “Bwana,” ni kusema Yesu, alisimama pembeni yake usiku na kumuambia hivi: “Usiogope! Kwa maana kama vile umekuwa ukitoa ushahidi kamili juu yangu katika Yerusalemu, ni vile unapaswa kutoa ushahidi katika Roma pia.” (Mdo. 23:11) Ile maneno ilimutia moyo kabisa. Yesu alimupongeza juu alikuwa ametoa ushahidi katika Yerusalemu. Na alimuahidi kama atafika Roma akiwa salama na kama atatoa ushahidi kule pia. Bila shaka ile maneno ilimufanya Paulo ajisikie salama kama vile mutoto anajisikiaka wakati iko mu mikono ya baba yake.

Wakati wa zoruba kali mu bahari, malaika anahakikishia Paulo kama watu wote wenye kuwa mu ile mashua wataokoka mu ile safari ya hatari (Ona fungu la 5)

5. Namna gani Yehova alitumia malaika ili kumusaidia Paulo? (Ona picha ku jalada la gazeti hili.)

5 Paulo alipata magumu gani ingine? Miaka mbili hivi kisha mambo yenye ilimufikia Yerusalemu, Paulo alisafiri kuenda Italia. Wakati alikuwa mu mashua, kulitokea zoruba kali yenye ilifanya wafanyakazi wa mu ile mashua na watu wenye walikuwa wanasafiri mu ile mashua wawaze kama watakufa. Lakini Paulo hakuogopa. Juu ya nini? Aliambia watu wenye walikuwa mu mashua hivi: “Usiku huu malaika wa Mungu mwenye mimi ni mali yake na mwenye ninatolea utumishi mutakatifu alisimama karibu yangu na akasema: ‘Usiogope, Paulo. Unapaswa kusimama mbele ya Kaisari, na angalia! Mungu amekupatia wale wote wenye wanasafiri pamoja na wewe.’” Yehova alitumia malaika ili amuhakikishie Paulo mambo yenye Yesu alikuwa amemuambia. Na kwa kweli, Paulo alifika Roma.​—Mdo. 27:20-25; 28:16.

6. Ni ahadi gani ya Yesu yenye inaweza kututia nguvu, na juu ya nini?

6 Tunapata musaada gani? Yesu atatutegemeza kama vile alimutegemeza Paulo. Kwa mufano, Yesu alitolea wafuasi wake wote ahadi hii: “Niko pamoja na ninyi sikuzote mupaka umalizio wa mupangilio wa mambo.” (Mt. 28:20) Maneno ya Yesu inaweza kututia nguvu. Juu ya nini? Juu wakati fulani, tunapataka magumu yenye iko nguvu kuvumilia. Kwa mufano, tunahuzunikaka sana wakati mutu mwenye tulikuwa tunapenda anakufa. Na ile huzuni haikuwake ya siku kidogo tu, inaweza kufanya miaka mingi. Wengine wako wanapata magumu kwa sababu ya uzee, na wengine wako wanapata magumu kwa sababu wakati fulani wanakuwaka wenye kushuka moyo. Hata hali yetu ikuwe namna gani, tunapata nguvu ya kuvumilia kwa sababu tunajua kama Yesu iko pamoja na sisi sikuzote,”  hata wakati tunapata matatizo ya nguvu sana mu maisha yetu.​—Mt. 11:28-30.

Malaika wanatusaidia na kutuongoza wakati tuko tunafanya kazi ya kuhubiri (Ona fungu la 7)

7. Kulingana na Ufunuo 14:6, namna gani Yehova iko anatusaidia leo?

7 Neno la Mungu linatuhakikishia kama, Yehova anatusaidia kupitia malaika wake. (Ebr. 1:7, 14) Kwa mufano, malaika wanatutegemeza na kutuongoza wakati tuko tunahubiri “habari njema ya Ufalme” kwa watu wa “kila taifa na kabila na luga.”​—Mt. 24:13, 14; soma Ufunuo 14:6.

YEHOVA ANATOA MUSAADA KUPITIA WATU WENYE MAMLAKA

8. Namna gani Yehova alitumia kiongozi wa jeshi ili kumusaidia Paulo?

8 Paulo alipata musaada gani? Mu mwaka wa 56, Yesu alikuwa amemuhakikishia Paulo kama atafika Roma. Lakini Wayahudi fulani katika Yerusalemu walipanga kumushambulia na kumuua. Wakati kiongozi wa jeshi Muroma, mwenye kuitwa Klaudio Lisia alisikia ile mupango, alimusaidia Paulo. Bila kukawia alituma maaskari wengi wamulinde Paulo, na wamupeleke Kaisaria, muji wenye ulikuwa ku kilometre 105 hivi kutoka Yerusalemu. Katika Kaisaria, Gavana Feliksi aliagiza Paulo “awekwe chini ya ulinzi katika nyumba ya kifalme ya Herode.” Wayahudi wenye walikuwa wanapenda kumuua Paulo, hawangeweza kuingia mule.​—Mdo. 23:12-35.

9. Namna gani Gavana Festo alimusaidia Paulo?

9 Miaka mbili kisha pale, Paulo alikuwa angali mu kifungo katika Kaisaria. Gavana Festo alikuwa amekamata nafasi ya Gavana Feliksi. Wayahudi walimuomba Festo amutume Paulo Yerusalemu ili ahukumiwe. Lakini Festo alikataa. Pengine alijua kama Wayahudi walikuwa “wanapanga kumuvizia Paulo na kumuua katika barabara.”​—Mdo. 24:27–25:5.

10. Gavana Festo alifanya nini wakati Paulo aliomba kesi yake ipelekwe kwa Kaisari?

10 Kisha, Paulo alihukumiwa katika Kaisaria, lakini kwa sababu Festo alitaka “kukubaliwa na Wayahudi,” alimuuliza Paulo hivi: “Je, ungependa kupanda kuenda Yerusalemu uhukumiwe kule mbele yangu?” Paulo alijua kama pengine Wayahudi watamuua Yerusalemu. Na alijua mambo yenye alipaswa kufanya ili kuokoa uzima wake, kufika Roma, na kuendelea kuhubiri. Alisema hivi: “Ninapeleka kesi yangu ya hukumu kwa Kaisari!” Kisha Festo kuzungumuza na washauri wake, alimuambia Paulo hivi: “Umeomba kesi yako ya hukumu isikilizwe na Kaisari; utaenda kwa Kaisari.” Uamuzi wa Festo ulimuokoa Paulo. Kisha wakati fulani, Paulo angeenda Roma, mbali na Wayahudi wenye walikuwa wanapenda kumuua.​—Mdo. 25:6-12.

11. Inawezekana Paulo alifikiria maneno gani yenye kutia moyo yenye Isaya aliandika?

11 Wakati Paulo alikuwa anangojea safari yake ya kuenda Italia, inawezekana alikuwa anafikiria maneno yenye nabii Isaya aliandika kuhusu wale wenye kumupinga Yehova. Nabii Isaya aliandika hivi: “Mufanye mupango, lakini utavunjwa! Museme kile munataka, lakini hakitafanikiwa, kwa maana Mungu iko pamoja na sisi!” (Isa. 8:10) Paulo alijua kama Mungu atamusaidia. Na ile ilimupatia nguvu ya kuvumilia magumu yenye ingemupata.

Kama vile alifanya zamani, leo pia Yehova anaweza kutumia wenye mamlaka ili kulinda watumishi wake (Ona fungu la 12)

12. Namna gani Yulio alimutendea Paulo, na inawezekana Paulo alielewa nini?

12 Mu mwaka wa 58 kisha kuzaliwa kwa Yesu, Paulo alianza safari yake ya kuenda Italia. Kwa sababu alikuwa mufungwa, aliwekwa chini ya mamlaka ya ofisa wa jeshi Muroma mwenye kuitwa Yulio. Kuanzia ile wakati, Yulio alikuwa na mamlaka ya kumutesa Paulo, ao kumutendea muzuri. Namna gani alitumia mamlaka yake? Siku yenye ilifuata, wakati walifika Sidoni, ‘Yulio alimutendea Paulo kwa fazili na kumuruhusu aende kwa marafiki wake.’ Wakati fulani kisha pale, Yulio alifikia hata kuokoa uzima wa Paulo. Namna gani? Wakati maaskari walipenda kuua wafungwa wote wenye walikuwa mu ile mashua, Yulio aliwakataza. Juu ya nini? Juu “alikuwa anapenda kabisa kumufikisha Paulo salama.” Inawezekana kama Paulo alielewa kuwa Yehova alikuwa anatumia ule ofisa mwenye fazili ili kumusaidia na kumulinda.​—Mdo. 27:1-3, 42-44.

Ona fungu la 13

13. Namna gani Yehova anaweza kutumia wenye mamlaka ili kusaidia watu wake?

13 Tunapata musaada gani? Wakati inapatana na kusudi lake, Yehova anaweza kutumia roho yake takatifu yenye nguvu, ili kuchochea watu wenye mamlaka wafanye mambo yenye anapenda. Mufalme Sulemani aliandika hivi: “Moyo wa mufalme ni kama mito midogo ya maji katika mukono wa Yehova. Anauongoza mahali popote kwenye anapenda.” (Mez. 21:1) Ile mezali inamaanisha nini? Wanadamu wanaweza kuchimba mufereji ili kufanya maji ya muto mudogo ipite mu njia yenye wanapenda. Vilevile Yehova anaweza kutumia roho yake ili kuchochea wenye mamlaka wafanye mambo yenye inaweza kusaidia kusudi lake litimie. Wakati Yehova anafanya vile, watu wenye mamlaka wanachochewa kukamata maamuzi yenye inasaidia watu wake.​—Linganisha na Ezra 7:21, 25, 26.

14. Kama vile Matendo 12:5 inaonyesha, tunaweza kusali kwa ajili ya nani?

14 Tunaweza kufanya nini? Tunaweza kusali “kwa ajili ya wafalme na wale wote wenye mamlaka” wakati wanapenda kukamata maamuzi yenye inaweza kuwa na matokeo juu ya maisha yetu ya Kikristo na utumishi wetu. (1 Ti. 2:1, 2, maelezo ya chini; Ne. 1:11) Kama vile Wakristo wa karne ya kwanza walifanya, sisi pia tunapaswa kusali sana kwa ajili ya ndugu na dada zetu wenye kuwa mu gereza. (Soma Matendo 12:5; Ebr. 13:3) Zaidi ya ile, tunaweza kusali kwa ajili ya walinzi wa gereza wenye wako wanasimamia ndugu na dada zetu wenye kuwa mu gereza. Tunaweza kumulilia Yehova, awachochee ili watendee wale ndugu na dada zetu kwa “fazili za kibinadamu,” kama vile Yulio alimutendea Paulo​—Mdo. 27:3, maelezo ya chini.

YEHOVA ANATOA MUSAADA KUPITIA WAKRISTO WENZETU

15-16. Namna gani Yehova alitumia Aristarko na Luka ili kumusaidia Paulo?

15 Paulo alipata musaada gani? Wakati Paulo alikuwa anasafiri ili kuenda Roma, mara kwa mara Yehova alitumia Wakristo wenzake ili kumusaidia. Tuzungumuzie mifano fulani.

16 Marafiki wawili wa Paulo wenye walikuwa waaminifu, ni kusema, Aristarko na Luka, waliamua kusafiri pamoja naye ili kuenda Roma. * Biblia haiseme kama Yesu aliahidi Aristarko na Luka kuwa watafika Roma wakiwa salama. Kwa hiyo, tunaweza kusema kama walitia maisha yao mu hatari wakati walikubali kuenda na Paulo mu ile safari. Lakini walifanya vile juu walipenda kumusaidia Paulo. Ni kisha wakati fulani mu ile safari ya mateso njo walifikia kujua kama watafika salama. Kwa hiyo, wakati Aristarko na Luka, waliingia mu mashua katika Kaisaria, inawezekana Paulo alisali kwa Yehova ili kumushukuru kwa sababu alitumia wale ndugu wawili wenye walikuwa hodari ili kumusaidia.​—Mdo. 27:1, 2, 20-25.

17. Namna gani Yehova alitumia Wakristo wengine ili kumusaidia Paulo?

17 Wakristo mbalimbali walimusaidia Paulo mu ile safari. Kwa mufano, mu muji wa Sidoni, Yulio alimuruhusu Paulo “aende kwa marafiki wake ili wamuhangaikie.” Na kisha, mu muji wa Puteoli, Paulo na wenzake ‘walikuta pale ndugu na [wale ndugu] wakawaomba kwa mukazo wakae pamoja nao kwa siku saba (7).’ Wakati wale Wakristo wa ile miji walikuwa wanahangaikia Paulo na wenzake, bila shaka Paulo alikuwa anawafanya wakuwe na furaha kwa kuwaambia mambo yenye kutia moyo yenye alikuwa amejionea. (Linganisha na Matendo 15:2, 3.) Kisha kutiwa moyo, Paulo na wenzake walikuwa wanaendelea na safari.​—Linganisha na Matendo 27:3; 28:13, 14.

Sawa vile alisaidia Paulo, Yehova anatumia Wakristo wenzetu ili kutusaidia (Ona fungu la 18)

18. Juu ya nini Paulo alimushukuru Mungu na kujipa uhodari?

18 Wakati Paulo alikuwa anakaribia kufika Roma, inawezekana alikuwa anafikiria maneno yenye alikuwa ameandikia Wakristo wa Roma miaka tatu mbele ya pale. Alikuwa amewaandikia hivi: “Kwa miaka mingi nimetamani kuja kwenu.” (Ro. 15:23) Lakini, Paulo hakuwaziaka kama atafikaka Roma akiwa mufungwa. Bila shaka, Paulo alitiwa moyo sana wakati aliona ndugu wenye wanatokea Roma wako wanamungoja mu njia ili kumukaribisha! “Wakati Paulo aliwaona, akamushukuru Mungu na akajipa uhodari.” (Mdo. 28:15) Juu ya nini Paulo alimushukuru Mungu wakati aliona wale ndugu? Juu kwa mara ingine Paulo alijionea kama Yehova alikuwa anatumia Wakristo wenzake ili kumusaidia.

Ona fungu la 19

19. Kama vile 1 Petro 4:10 inaonyesha, namna gani Yehova anaweza kututumia ili kusaidia wengine?

19 Tunaweza kufanya nini? Mu kutaniko lenu muko ndugu ao dada mwenye iko na magumu juu iko mugonjwa, juu alifiwa na mutu mwenye anapenda, ao juu iko anapambana na matatizo ingine? Ikiwa unajua ndugu ao dada mwenye iko na lazima ya musaada, unaweza kumuomba Yehova akusaidie umuambie jambo fulani lenye kutia moyo, ao umufanyie jambo fulani la muzuri. Pengine mambo yenye utasema ao kufanya njo yenye ule ndugu ao dada alikuwa nayo lazima ili ajisikie muzuri. (Soma 1 Petro 4:10.) * Wale wenye tunasaidia wanaweza tena kuamini hii ahadi ya Yehova: “Sitakuacha hata kidogo, na sitakutupa hata kidogo.” Na ile inaweza kutuletea furaha kabisa.

20. Juu ya nini tunaweza kusema kwa uhakika kama ‘Yehova ni musaidizi wetu’?

20 Kama Paulo na wenzake, sisi pia tunaweza kupata magumu yenye kuwa kama zoruba kali. Lakini tunajua kama tunaweza kuwa hodari kwa sababu Yehova iko pamoja na sisi. Anatumia Yesu na malaika ili kutusaidia. Pia kama inapatana na kusudi lake, anaweza kutumia watu wenye mamlaka ili kutusaidia. Na kama vile wengi kati yetu wamejionea, Yehova anatumia roho yake takatifu ili kuchochea watumishi wake wasaidie Wakristo wenzao wenye kuwa na lazima ya musaada. Kwa hiyo kama Paulo, tunaweza kusema hivi kwa uhakika: “Yehova ni musaidizi wangu; sitaogopa. Mwanadamu anaweza kunifanya nini?”​—Ebr. 13:6.

WIMBO 38 Atakupa Nguvu

^ fu. 5 Mu hii habari tutazungumuzia njia tatu zenye Yehova alitumia ili kumusaidia mutume Paulo avumilie magumu. Kujifunza namna Yehova alisaidia watumishi wake wa zamani, kutatusaidia tukuwe hakika kama Yehova atatusaidia sisi pia leo ili tuweze kuvumilia magumu ya maisha.

^ fu. 16 Mbele ya pale, Aristarko na Luka walikuwa walishasafiri pamoja na Paulo. Wale wanaume washikamanifu walibakia pia pamoja na Paulo wakati alikuwa mufungwa katika Roma.​—Mdo. 16:10-12; 20:4; Kol. 4:10, 14.