Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 47

Utaendelea Kurekebishwa?

Utaendelea Kurekebishwa?

“Mwishowe, ndugu, muendelee kufurahi, kurekebishwa upya.”​—2 KO. 13:11.

WIMBO 54 “Hii Ndiyo Njia”

KIFUPI CHA HABARI *

1. Kulingana na Matayo 7:13, 14, juu ya nini tunaweza kusema kama tuko mu safari?

SISI wote tuko mu safari, na nia yetu ni kuingia mu ulimwengu mupya wenye utatawaliwa na Yehova, Mungu wetu mwenye upendo. Kila siku tunajikaza kutembea mu barabara yenye kuongoza kwenye uzima. Lakini kama vile Yesu alisema, ile barabara ni ya kidogo na wakati fulani inaweza kuwa nguvu kuendelea kutembea mu ile barabara. (Soma Matayo 7:13, 14.) Kwa sababu hatukamilike, ni mwepesi kwetu kutoka mu ile barabara.​—Gal. 6:1.

2. Tutazungumuzia nini mu hii habari? (Ona pia kisanduku “ Unyenyekevu Unatusaidia Tufanye Mabadiliko.”)

2 Ili tuendelee kutembea mu barabara yenye kuongoza kwenye uzima, tunapaswa kuwa tayari kubadilisha namna yetu ya kufikiri, namna yetu ya kuona mambo, na matendo yetu. Mutume Paulo alitia moyo Wakristo wenye walikuwa wanaishi mu muji wa Korinto waendelee “kurekebishwa upya.” (2 Ko. 13:11) Ile shauri inatuhusu sisi pia. Mu hii habari tutazungumuzia namna Biblia inaweza kutusaidia tuendelee kufanya mabadiliko, na namna Wakristo wenye kukomaa kiroho wanaweza kutusaidia tuendelee kutembea mu barabara yenye kuongoza kwenye uzima. Tutazungumuzia pia ni wakati gani inaweza kuwa nguvu kufuata muongozo wenye tengenezo la Yehova linatutolea. Tutaona namna unyenyekevu unaweza kutusaidia tuendelee kufanya mabadiliko bila kupoteza furaha yetu ya kumutumikia Yehova.

UACHE NENO LA MUNGU LIKUREKEBISHE

3. Namna gani Neno la Mungu linaweza kutusaidia?

3 Haiko mwepesi kuchunguza mawazo yetu na hisia zetu. Juu ya nini? Kwa sababu moyo wetu ni mudanganyifu na inaweza kuwa nguvu kujua mambo yenye unaweza kutuchochea kufanya. (Yer. 17:9) Ni mwepesi kujidanganya kwa “mawazo ya uongo.” (Yak. 1:22) Kwa hiyo, tunapaswa kutumia Neno la Mungu ili kujichunguza. Neno la Mungu linatusaidia kujua mambo yenye kuwa ndani yetu, ni kusema, “mawazo na makusudio” yenye kuwa ndani kabisa ya moyo wetu. (Ebr. 4:12, 13) Lakini tunapaswa kuwa wanyenyekevu ili tutumikishe mashauri yenye Neno la Mungu linatutolea na yenye wale wenye kuongoza wanatutolea.

4. Nini njo inaonyesha kama Mufalme Sauli alifikia kuwa na kiburi?

4 Mufano wa Mufalme Sauli unatusaidia kujua matokeo ya kukosa unyenyekevu. Kwa sababu Sauli alifikia kuwa na kiburi sana, hakuona kama alikuwa na lazima ya kubadilisha namna yake ya kufikiri na matendo yake. (Zb. 36:1, 2; Hab. 2:4) Ile ilifikia kuonekana wakati Yehova alipatia Sauli maagizo yenye kuwa wazi juu ya mambo yenye alipaswa kufanya kisha kushinda Waamaleki. Lakini Sauli hakumutii Yehova. Na wakati nabii Samweli alizungumuza naye juu ya ile jambo, Sauli hakukubali kama alikuwa na makosa. Alijaribu kutetea matendo yake kwa kuonyesha kama jambo lenye alifanya halikukuwa kosa kubwa, na kwa kusema kama ni wengine njo walimuchochea kufanya vile. (1 Sa. 15:13-24) Mbele ya pale, Sauli alikuwa ameonyesha ile tabia. (1 Sa. 13:10-14) Jambo la kuhuzunisha ni kwamba aliacha moyo wake ukuwe na kiburi. Kwa sababu hakurekebisha namna yake ya kufikiri, Yehova alimukaripia na alimukataa.

5. Mufano wa Sauli unaweza kutufundisha nini?

5 Ili kuepuka kufuata mufano wa Sauli, ni muzuri tujiulize maulizo yenye kufuata: ‘Ninajaribu kutetea namna yangu ya kufikiri ili nisitumikishe mashauri yenye ninasoma mu Neno la Mungu? Wakati ninakosa kutii amri za Yehova, ninasema kama mambo yenye ninafanya haiko kosa kubwa? Wakati ninafanya makosa, ninasema kama wengine njo walinichochea kufanya vile na ninajaribu kuonyesha kama wao njo wako na kosa?’ Kama tunajibia ndiyo ku ulizo hata moja kati ya ile maulizo, tunapaswa kurekebisha namna yetu ya kufikiri na namna yetu ya kuona mambo. Juu kama hatufanye vile, moyo wetu unaweza kuwa na kiburi sana na ile itafanya Yehova atukatae na hatutakuwa tena marafiki wake.​—Yak. 4:6.

6. Nini njo inaonyesha kama Mufalme Daudi hakukuwa sawa Mufalme Sauli?

6 Mufalme Daudi njo alikamata nafasi ya Mufalme Sauli. Lakini Mufalme Daudi alipenda “sheria ya Yehova.” Hakukuwa sawa Mufalme Sauli. (Zb. 1:1-3) Daudi alijua kama Yehova anaokoa watu wanyenyekevu, lakini anachukia watu wenye majivuno. (2 Sa. 22:28) Kwa hiyo, Daudi aliacha sheria ya Mungu irekebishe namna yake ya kufikiri. Aliandika hivi: “Nitamusifu Yehova, mwenye amenipa shauri. Hata wakati wa usiku, mawazo yangu ya ndani kabisa yananirekebisha.”​—Zb. 16:7.

NENO LA MUNGU

Neno la Mungu linatuonya wakati tunatoka mu barabara yenye kuongoza kwenye uzima. Kama tuko wanyenyekevu, tutaacha Neno la Mungu liturekebishe wakati tunaanza kufikiri mu njia yenye haipatane na mapenzi yake (Ona fungu la 7)

7. Tutafanya nini kama tuko wanyenyekevu?

7 Kama tuko wanyenyekevu, tutaacha Neno la Mungu liturekebishe wakati tunaanza kufikiri mu njia yenye haipatane na mapenzi yake, mbele mawazo yetu ituchochee kufanya mambo ya mubaya. Neno la Mungu liko sawa vile sauti yenye kutuambia hivi: “Hii ndiyo njia. Mutembee ndani yake.” Litatuonya wakati tunaanza kutoka mu barabara yenye kuongoza kwenye uzima. (Isa. 30:21) Kama tunamusikiliza Yehova, tutapata faida za mingi. (Isa. 48:17) Kwa mufano, tutaepuka haya yenye mutu anasikiaka wakati mutu mwingine anamurekebisha. Na tutamukaribia Yehova kwa sababu tunajua kama anatuhangaikia, sawa vile baba anahangaikiaka mutoto mwenye anapenda sana.​—Ebr. 12:7.

8. Kama vile Yakobo 1:22-25 inaonyesha, namna gani tunaweza kutumia Neno la Mungu kama kioo?

8 Neno la Mungu liko sawa vile kioo. (Soma Yakobo 1:22-25.) Karibu sisi wote tunajiangaliaka mu kioo asubui mbele ya kutoka ku nyumba. Ile inatusaidiaka tujue ikiwa kuko mambo yenye tunapaswa kurekebisha mbele watu wengine watuone. Vilevile, kusoma Neno la Mungu kila siku kunaweza kutusaidia tujue mambo yenye tunapaswa kufanya ili kubadilisha namna yetu ya kufikiri ao namna yetu ya kuona mambo. Watu wengi wanafurahia kusoma andiko la siku kila asubui mbele watoke ku nyumba. Wakati wanafanya vile, wanaacha mambo yenye walisoma ichochee namna yao ya kufikiri. Kisha, muchana yote wanatafuta nafasi za kutumia mambo yenye walisoma. Zaidi ya ile, tunapaswa kuwa na programu ya kusoma Neno la Mungu kila siku na kufikiri juu ya mambo yenye tuko tunasoma. Ile inaweza kuonekana kuwa jambo la kawaida tu. Lakini kusema kweli, kama mutu anapenda kubakia mu barabara ya kidogo yenye kuongoza kwenye uzima, ni jambo la maana akuwe anafanya vile.

USIKILIZE NDUGU NA DADA WENYE KUKOMAA KIROHO

NDUGU NA DADA WENYE KUKOMAA KIROHO

Wakati ndugu ao dada anakutolea mashauri, unafurahi kuona alijikaza kufanya vile? (Ona fungu la 9)

9. Nini njo inaweza kufanya ndugu ao dada fulani akushaurie?

9 Kuko wakati ulikuwaka ulishaanza kufanya jambo fulani lenye lilikuwa linaharibisha urafiki wako pamoja na Yehova? (Zb. 73:2, 3) Kama kuko ndugu ao dada fulani mwenye alijikazaka kukutolea mashauri, ulisikilizaka ile mashauri? Kama ulisikilizaka, ulifanyaka jambo la muzuri. Na bila shaka unafurahi sana juu ule ndugu ao ule dada alikushauriaka.​—Mez. 1:5.

10. Unapaswa kufanya nini wakati ndugu ao dada fulani anakushauria?

10 Neno la Mungu linatukumbusha hivi: “Vidonda vyenye kutokezwa na rafiki ni vya uaminifu.” (Mez. 27:6) Ile maneno inamaanisha nini? Fikiria hii mufano: Unataka kuvuka barabara yenye kuwa na magari mingi, lakini telefone yako inafanya usikuwe muangalifu. Unaingia mu barabara bila kuangalia kama kuko gari yenye iko inakuja. Kisha mara moja rafiki yako anakukamata nguvu sana ku mukono na kukukokota pembeni. Anakukamata nguvu sana mupaka mukono wako unauma. Lakini juu alifanya vile anaokoa uzima wako. Hata kama mukono utaendelea kukuuma kwa siku fulani, utakasirika juu rafiki yako alikukamata nguvu sana? Hapana! Utafurahi juu alikusaidia. Vilevile ikiwa ndugu ao dada fulani anakuambia kama maneno yako ao matendo yako haipatane na kanuni za Mungu za haki, ku mwanzo unaweza kuhuzunika. Lakini, usimukasirikie kwa sababu alikushauria. Kufanya vile ni upumbavu. (Muh. 7:9) Ufurahi kwa sababu alijikaza ili kukushauria.

11. Ni nini inaweza kufanya mutu asisikilize mashauri ya muzuri yenye ndugu ao dada anamutolea?

11 Nini njo inaweza kufanya mutu asisikilize mashauri ya muzuri yenye ndugu ao dada mwenye upendo anamutolea? Ni majivuno. Watu wenye majivuno wanapendaka “masikio yao yafurahishwe.” ‘Wanageuka na kuacha kusikiliza ile kweli.’ (2 Ti. 4:3, 4) Wanafikiri kama hawana lazima ya mashauri, juu wanawaza kama wako wa maana kuliko watu wengine. Lakini, mutume Paulo aliandika hivi: “Kama mutu yeyote anawaza yeye ni kitu wakati yeye haiko kitu, anajidanganya yeye mwenyewe.” (Gal. 6:3) Mufalme Sulemani pia aliandika hivi: “Mutoto maskini lakini mwenye hekima ni muzuri zaidi kuliko mufalme muzee lakini mujinga, mwenye haone tena ulazima wa kutii maonyo.”​—Muh. 4:13.

12. Kama vile Wagalatia 2:11-14 inaonyesha, mufano wa mutume Petro unaweza kutufundisha nini?

12 Fikiria namna Petro alitenda wakati mutume Paulo alimurekebisha mbele ya watu wengine. (Soma Wagalatia 2:11-14.) Petro angependa angekasirika juu ya namna Paulo alimurekebisha na juu Paulo alifanya vile mbele ya watu wengine. Lakini kwa sababu Petro alikuwa na hekima, hakukasirika na hakuendelea kufikiria ile mambo. Kisha wakati fulani, alifikia hata kumuita Paulo kuwa ‘ndugu yake mupendwa.’​—2 Pe. 3:15.

13. Tunapaswa kukumbuka nini mbele ya kutolea wengine mashauri?

13 Ikiwa unafikiri kama ni lazima ushaurie ndugu ao dada fulani, unapaswa kukumbuka mambo gani? Mbele uzungumuze naye, ujiulize hivi, ‘Niko “mwenye haki kupita kiasi”?’ (Muh. 7:16) Mutu mwenye haki kupita kiasi anahukumu wengine kulingana na vile yeye anaona mambo, haiko kulingana na kanuni za Yehova. Na inawezekana hakuwake mwenye rehema. Kisha kujichunguza, ikiwa unaona kama ni lazima tu ushaurie ndugu ao dada fulani, umuambie tatizo ni nini na utumie maulizo ili kumusaidia aelewe kama mambo yenye alifanya ilikuwa ya mubaya. Uhakikishe kama mambo yenye unasema inategemea Neno la Mungu, Biblia. Na ukumbuke kama hauna daraka la kuhukumu ndugu ao dada yako. Yehova tu njo iko na ile daraka. (Ro. 14:10) Wakati uko unashauria mutu fulani, utumie hekima yenye kuwa mu Neno la Mungu na umuonyeshe huruma kama vile Yesu alikuwa anafanya. (Mez. 3:5; Mt. 12:20) Juu ya nini tunapaswa kufanya vile? Kwa sababu, vile tunatendeaka wengine njo vile Yehova naye atatutendea.​—Yak. 2:13.

UFUATE MUONGOZO WA TENGENEZO LA YEHOVA

TENGENEZO LA YEHOVA

Tengenezo la Yehova linatutolea vichapo, video, na pia mikutano yenye inatusaidia kujua namna ya kutumikisha mashauri ya Neno la Mungu. Wakati fulani, ndugu wa Baraza Lenye Kuongoza wanafanya mabadiliko kuhusu namna kazi inapaswa kufanywa (Ona fungu la 14)

14. Tengenezo la Yehova linatutolea mambo gani?

14 Yehova anatumia sehemu ya ku dunia ya tengenezo lake ili kutusaidia tubakie mu barabara yenye kuongoza kwenye uzima. Tengenezo lake linatutolea video, vichapo, na pia mikutano yenye inatusaidia tujue namna ya kutumikisha mashauri yenye kuwa mu Neno la Mungu. Mafundisho yenye tunapata inatoka mu Maandiko. Ndugu wa Baraza Lenye Kuongoza wanategemea musaada wa roho takatifu ili kukamata maamuzi juu ya namna kazi ya kuhubiri inaweza kufanywa muzuri. Hata vile, ndugu wa Baraza Lenye Kuongoza wanachunguzaka maamuzi yao mara kwa mara ili kuona kama wanapaswa kufanya mabadiliko. Juu ya nini? Juu “tamasha ya ulimwengu huu inabadilika,” na tengenezo la Mungu linapaswa kujipatanisha na hali za mupya.​—1 Ko. 7:31.

15. Wahubiri fulani wamepambana na hali gani?

15 Wakati tengenezo la Yehova linatutolea mafasirio ya mupya juu ya mafundisho fulani ya Biblia, tunakuwaka tayari kuikubali. Na wakati inatutolea muongozo juu ya kanuni za mwenendo, tunakuwaka tayari kuitumikisha. Lakini tunatendaka namna gani wakati tengenezo la Yehova linafanya mabadiliko ingine yenye inatuhusu mu njia moja ao ingine? Kwa mufano, miaka ya hivi majuzi, garama ya kutunza na kujenga Majumba ya Ufalme imeongezeka sana. Kwa hiyo, Baraza Lenye Kuongoza liliamua kama Jumba la Ufalme linapaswa kutumiwa na makutaniko mingi kadiri inawezekana. Ile imefanya makutaniko fulani ichangwe na Majumba fulani ya Ufalme iuzishwe. Feza zenye zimepatikana ziko zinasaidia kujenga Majumba ya Ufalme mu maeneo yenye iko na lazima kabisa ya Majumba ya Ufalme. Kama unaishi mu eneo lenye Majumba ya Ufalme iko inauzishwa na makutaniko iko inachangwa pamoja, inaweza kuwa nguvu kwako kujipatanisha na ile hali ya mupya. Sasa wahubiri fulani wanapaswa kuenda mbali ili kuhuzuria mikutano. Wengine wenye walitumika sana ili kujenga na kutunza ile majumba wanaweza kujiuliza juu ya nini ile majumba iko inauzishwa. Wanaweza kuona kama walipoteza wakati wao na nguvu yao bure. Lakini wale ndugu na dada wanakubali ile mabadiliko na wanastahili pongezi.

16. Namna gani shauri lenye kuwa mu Wakolosai 3:23, 24 linaweza kutusaidia tuendelee kuwa na furaha?

16 Kama tunapenda kuendelea kuwa na furaha, tunapaswa kukumbuka kama kazi yenye tuko tunafanya ni ya Yehova na kama Yehova iko anaongoza tengenezo lake. (Soma Wakolosai 3:23, 24.) Mufalme Daudi alituachia mufano muzuri kwa sababu alitoa michango ili kutegemeza kazi ya kujenga hekalu. Alisema hivi: “Mimi ni nani na watu wangu ni nani hata tuweze kutoa matoleo ya kujipendea kama haya? Kwa maana kila kitu kinatoka kwako, na sisi tumekupatia kile chenye kutoka katika mukono wako mwenyewe.” (1 Ny. 29:14) Wakati tunatoa michango, sisi pia tunapatia Yehova kile chenye kutoka katika mukono wake mwenyewe. Hata vile, Yehova anafurahi kuona tunatumia wakati wetu, nguvu yetu, na vitu vyetu vya kimwili ili kutegemeza kazi yake.​—2 Ko. 9:7.

UBAKIE MU BARABARA YA KIDOGO

17. Juu ya nini haupaswe kuvunjika moyo ikiwa unaona kuwa kuko mabadiliko fulani yenye unapaswa kufanya?

17 Ili tubakie mu barabara ya kidogo yenye kuongoza kwenye uzima, tunapaswa kufuata hatua za Yesu kwa ukaribu. (1 Pe. 2:21) Ikiwa unaona kuwa kuko mabadiliko yenye unapaswa kufanya, usivunjike moyo. Ile ni alama ya muzuri yenye kuonyesha kama unapenda kufuata muongozo wa Yehova. Ukumbuke kama Yehova anajua kuwa hatuko wakamilifu. Kwa hiyo hatazamie tufuate mufano wa Yesu kwa ukamilifu.

18. Tunapaswa kufanya nini ili tuingie mu dunia mupya?

18 Sisi wote tuendelee basi kukaza akili juu ya wakati wenye kuja, na kuwa tayari kurekebisha namna yetu ya kufikiri, namna yetu ya kuona mambo, na matendo yetu. (Mez. 4:25; Lu. 9:62) Tuendelee kuwa wanyenyekevu, na ‘tuendelee kufurahi, kurekebishwa upya.’ (2 Ko. 13:11) Kama tunafanya vile, “Mungu wa upendo na amani atakuwa pamoja na [sisi].” Tutakuwa na furaha leo, na tutaingia mu dunia mupya.

WIMBO 34 Kutembea kwa Utimilifu

^ fu. 5 Wamoja kati yetu wanaweza kuona kama ni nguvu kubadilisha namna yao ya kufikiri, namna yao ya kuona mambo, na matendo yao. Hii habari itatusaidia tujue juu ya nini ni jambo la maana tuendelee kufanya mabadiliko, na tutaona namna tunaweza kuendelea kuwa na furaha wakati tuko tunafanya vile.

^ fu. 76 MAFASIRIO YA PICHA: Wakati ndugu kijana iko anaeleza mambo yenye ilimufikia kisha kukamata uamuzi mubaya, ndugu mwenye kukomaa (mwenye kuwa ku upande wa kuume) iko anamusikiliza kwa uangalifu ili kuona ikiwa ni lazima amutolee mashauri.