Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 50

“Wafu Watafufuliwa Namna Gani?”

“Wafu Watafufuliwa Namna Gani?”

“Kifo, uko wapi ushindi wako? Kifo, uko wapi uwezo wako wa kuumiza?”​—1 KO. 15:55.

WIMBO 141 Muujiza wa Uhai

KIFUPI CHA HABARI *

1-2. Juu ya nini Wakristo wanapaswa kujifunza kuhusu ufufuo wa mbinguni?

LEO watu wengi wenye wako wanamutumikia Yehova, wako na tumaini la kuishi ku dunia. Lakini Wakristo watiwa-mafuta wenye wangali ku dunia, wako na tumaini la kuishi mbinguni. Wale Wakristo watiwa-mafuta wanapenda sana kujua namna maisha yao itakuwa wakati watakuwa mbinguni. Lakini juu ya nini wale wenye kuwa na tumaini la kuishi ku dunia wanapaswa kujifunza juu ya ufufuo wa mbinguni? Juu, kama vile tutaona, ufufuo wa mbinguni utaletea pia baraka mingi wale wenye kuwa na tumaini la kuishi milele ku dunia. Kwa hiyo, ikuwe tuko na tumaini la kuenda mbinguni ao la kuishi ku dunia, tuko na lazima ya kujifunza juu ya ufufuo wa mbinguni.

2 Mungu aliongoza wanafunzi fulani wa Yesu katika karne ya kwanza waandike kuhusu ufufuo wa mbinguni. Mutume Yohana aliandika hivi: “Sisi ni watoto wa Mungu, lakini bado haijafunuliwa namna tutakuwa. Tunajua kama wakati atafunuliwa tutakuwa kama yeye.” (1 Yo. 3:2) Kwa hiyo, Wakristo watiwa-mafuta hawajue namna mambo itakuwa wakati watafufuliwa ili kuishi mbinguni. Lakini tunajua kama wakati watapokea zawabu yao, watamuona Yehova kabisa. Biblia haiseme kila kitu kuhusu ufufuo wa mbinguni, lakini mutume Paulo aliandika mambo fulani juu ya ule ufufuo. Wakristo watiwa-mafuta watakuwa pamoja na Yesu wakati ‘ataharibu serikali yote na mamlaka yote na nguvu zote,’ na hata wakati ataharibu “adui wa mwisho,” ni kusema “kifo.” Kisha Yesu pamoja na watawala wenzake watajitiisha kwa Yehova na vitu vyote vitatiishwa kwa Yehova. (1 Ko. 15:24-28) Kile kitakuwa kipindi cha muzuri sana! *

3. Kama vile 1 Wakorinto 15:30-32 inaonyesha, kwa sababu Paulo aliamini ufufuo, ile ilimusaidia kufanya nini?

3 Kwa sababu Paulo aliamini ufufuo, ile ilimusaidia avumilie magumu mbalimbali. (Soma 1 Wakorinto 15:30-32.) Aliambia Wakorinto hivi: “Ninapambana na kifo kila siku.” Paulo aliandika pia hivi: “Nimepigana na wanyama wa pori katika Efeso.” Pengine Paulo alikuwa anapenda kusema kama alipigana na wanyama katika kiwanja cha muchezo mu muji wa Efeso. (2 Ko. 1:8; 4:10; 11:23) Ao pengine alikuwa anazungumuzia Wayahudi na watu wengine wenye chuki wenye walikuwa kama “wanyama wa pori.” (Mdo. 19:26-34; 1 Ko. 16:9) Hata ikuwe alikuwa anazungumuzia nini, tunajua kama, mara mingi Paulo alipambana na hatari. Hata vile, aliendelea kuwa na tumaini kama atakuwa na maisha yenye furaha wakati wenye kuja.​—2 Ko. 4:16-18.

Watu wa familia moja wenye wanaishi mahali kwenye kazi yetu imewekewa vizuizi wanaendelea kumuabudu Yehova. Wako na imani kama watapata baraka wakati wenye kuja (Ona fungu la 4)

4. Namna gani tumaini la ufufuo linatia nguvu Wakristo leo? (Ona picha ku jalada la gazeti hili.)

4 Tunaishi mu kipindi chenye kuwa hatari. Ndugu zetu fulani wametendewa mubaya. Wengine wanaishi mu maeneo yenye kuwa na vita na hawako salama. Tena wengine wako wanamutumikia mu maeneo kwenye kazi yetu imewekewa vizuizi ao imekatazwa, hata kama ile inaweza kufanya wafungwe ao wauawe. Hata vile, wale ndugu na dada wote wanaendelea kumutumikia Yehova, na wanatuwekea mufano muzuri. Hawaogope kwa sababu wanajua kama hata ikiwa wanakufa leo, Yehova atawafufua na kuwapatia maisha ya muzuri wakati wenye kuja.

5. Ni mawazo gani yenye haifae yenye inaweza kuregeza imani yetu katika ufufuo?

5 Paulo alishauria Wakristo wenzake waepuke mawazo yenye haifae yenye watu fulani walikuwa nayo. Walikuwa wanasema hivi: “Kama wafu hawatafufuliwa, ‘basi tukule na tukunywe, kwa maana kesho tutakufa.’” Kusema kweli, watu fulani walikuwa na ile mawazo hata mbele ya wakati wa Paulo. Pengine Paulo alikuwa anataja maneno yenye kuwa mu Isaya 22:13, yenye inaonyesha mawazo yenye Waisraeli walikuwa nayo. Kuliko kumukaribia Mungu walikuwa tu wanapenda kujifurahisha. Kwa kweli mawazo yenye wale Waisraeli walikuwa nayo iko sawa mawazo yenye watu wengi wako nayo leo. Watu wengi wanasema: “Kula raha wakati ungali muzima, juu haujue ya kesho.” Lakini Biblia inaonyesha matokeo ya mubaya yenye Waisraeli walipata kwa sababu ya ile mawazo yenye haifae.​—2 Ny. 36:15-20.

6. Namna gani tumaini la ufufuo linaweza kutusaidia tuepuke marafiki wabaya?

6 Tunajua kama Yehova atafufua watu wenye wamekufa. Kwa hiyo, ile inapaswa kutuchochea tuepuke marafiki wabaya. Ndugu katika Korinto walipaswa kuepuka kupitisha wakati na watu wenye hawakuamini ufufuo. Ile inaweza kutufundisha nini? Haiko muzuri kuzoea kupitisha wakati na watu wenye hawahangaikie mambo yenye itatokea wakati wenye kuja na wenye wanapenda tu kujifurahisha. Kama tunazoea kupitisha wakati na wale watu, sisi pia tunaweza kuwa na mawazo yenye haifae. Tunaweza hata kufikia kufanya mambo yenye Mungu anachukia. Njo maana Paulo alitushauri hivi: “Muamuke kwa njia yenye haki na musizoee kufanya zambi.”​—1 Ko. 15:33, 34.

WATAFUFULIWA NA MWILI WA NAMNA GANI?

7. Kama vile 1 Wakorinto 15:35-38 inaonyesha, watu fulani wanaweza kuuliza ulizo gani juu ya ufufuo?

7 Soma 1 Wakorinto 15:35-38. Mutu mwenye anapenda kufanya wengine washakie fundisho la ufufuo, anaweza kuuliza hivi: “Wafu watafufuliwa namna gani?” Ni muzuri tufikirie jibu la Paulo juu watu wako na maoni tofauti-tofauti kuhusu watu wenye wamekufa. Biblia inafundisha nini?

Mutume Paulo alitumia mufano wa mbegu na mumea ili kuonyesha kama Mungu anaweza kupatia mutu mwenye anafufuliwa mwili wenye kufaa (Ona fungu la 8)

8. Ni mufano gani wenye unaweza kutusaidia kuelewa ufufuo wa mbinguni?

8 Wakati mutu anakufa, mwili wake unaharibikaka. Lakini ule mwenye aliumba ulimwengu wote anaweza kumufufua na kumupatia mwili wenye kufaa. (Mwa. 1:1; 2:7) Paulo alitumia mufano wa “mbegu” ili kuonyesha kama wakati Mungu anamufufua mutu haiko lazima amurudishie mwili wenye alikuwa nao zamani. Wakati mutu anapanda mbegu, inaotaka na inafikia kuwa mumea ya mupya. Ile mumea ya mupya inakuwaka tofauti na mbegu yenye ilitumiwa ili kuipanda. Paulo alitumia ile mufano ile kuonyesha kama wakati Muumbaji anafufua mutu, anaweza kumupatia “mwili kama vile [inamupendeza].”

9. 1 Wakorinto 15:39-41 inasema nini kuhusu aina mbalimbali ya miili?

9 Soma 1 Wakorinto 15:39-41. Paulo alisema kama kuko aina mbalimbali ya miili. Kwa mufano, kuko miili ya nyama, kama vile ya mifugo, ya ndege, na ya samaki. Alisema kama wakati tunaangalia anga tunaona tofauti kati ya jua na mwezi. Na alisema tena kama “nyota moja iko tofauti na nyota ingine kwa utukufu.” Kwa kweli, hata kama hatuwezi kuona ile tofauti na macho yetu, wanasayansi wanasema kama kuko nyota za aina mbalimbali. Kuko nyota kubwa-kubwa, nyota ndogo-ndogo, nyota za rangi mwekundu, nyota za rangi ya mweupe, na nyota za rangi ya manjano, kama vile jua. Paulo alisema kama kuko “miili ya mbinguni na miili ya duniani.” Alimaanisha nini? Alimaanisha kama ku dunia kuko miili ya nyama lakini mbinguni kuko miili ya roho, kama miili yenye malaika wanakuwaka nayo.

10. Watu wenye wanafufuliwa ili kuishi mbinguni wanafufuliwa na mwili gani?

10 Ona mambo ingine yenye Paulo alisema: “Ni vile juu ya ufufuo wa wafu. Mwili unapandwa katika uharibifu; unafufuliwa katika kutokuharibika.” Tunajua kama wakati mutu anakufa, mwili wake unaharibikaka na unageuka kuwa mavumbi. (Mwa. 3:19) Sasa namna gani mwili unaweza kufufuliwa katika kutokuharibika? Paulo hakukuwa anazungumuzia watu wenye wanafufuliwa ili kuishi ku dunia, kama vile watu wenye Eliya, Elisha, na Yesu walifufua. Alikuwa anazungumuzia watu wenye wanafufuliwa na mwili wenye unaweza kuishi mbinguni, ni kusema, “mwili wa roho.”​—1 Ko. 15:42-44.

11-12. Yesu alifufuliwa na mwili wa aina gani, na Wakristo watiwa mafuta wanafufuliwa pia na mwili wa aina gani?

11 Wakati Yesu alikuwa ku dunia, alikuwa na mwili wa nyama. Lakini wakati alifufuliwa, “akakuwa roho yenye inatoa uzima” na akaenda mbinguni. Vilevile, Wakristo watiwa mafuta wangefufuliwa na mwili wa roho. Paulo alisema hivi: “Kama vile tumechukua mufano wa ule mwenye alifanywa kwa mavumbi, tutachukua pia mufano wa ule wa mbinguni.”​—1 Ko. 15:45-49.

12 Wakati Paulo alikuwa karibu kumaliza mazungumuzo yake kuhusu ufufuo alifasiria juu ya nini Yesu hakufufuliwa na mwili wa nyama. Alisema hivi: “Nyama na damu haviwezi kuriti Ufalme wa Mungu” wenye kuwa mbinguni. (1 Ko. 15:50) Mitume na Wakristo wengine watiwa-mafuta hawangefufuliwa na miili yenye inaweza kuharibika, ni kusema miili ya nyama na damu. Sasa wangefufuliwa wakati gani? Paulo alisema kama hawangefufuliwa kisha tu wao kufa. Wangefufuliwa wakati wenye kuja. Wakati Paulo aliandika 1 Wakorinto, wanafunzi fulani, kama vile mutume Yakobo, walikuwa “wamelala usingizi katika kifo.” (Mdo. 12:1, 2) Mitume wengine na Wakristo watiwa-mafuta wengine wangefikia pia kulala “usingizi katika kifo.”​—1 Ko. 15:6.

USHINDI JUU YA KIFO

13. Ni mambo gani ingetokea wakati wa kuwapo kwa Yesu?

13 Yesu na Paulo walizungumuzia wakati wa maana sana wenye ungekuja, ni kusema, wakati wa kuwapo kwa Kristo. Wakati wa kuwapo kwa Kristo kungekuwa vita, matetemeko ya inchi, magonjwa ya kuambukiza, na mambo ingine ya mubaya katika dunia yote. Tumeona namna ule unabii wa Biblia uko unatimia tangu mwaka wa 1914. Lakini kungekuwa jambo lingine la maana lenye lingefanyika ile wakati. Yesu alisema kama habari njema yenye kuonyesha kama Ufalme wa Mungu umeanza kutawala, ingehubiriwa “katika dunia yote yenye kuikaliwa na watu ili kuwa ushahidi kwa mataifa yote, na kisha ule mwisho [ungekuja].” (Mt. 24:3, 7-14) Paulo alisema kama ni wakati wa “kuwapo kwa Bwana” njo Wakristo watiwa-mafuta wenye walikuwa “wamelala usingizi katika kifo” wangefufuliwa.​—1 Te. 4:14-16; 1 Ko. 15:23.

14. Ni nini inafikia Wakristo watiwa-mafuta wenye wanakufa mu kipindi cha kuwapo kwa Kristo?

14 Wakristo watiwa-mafuta wenye wanakufa leo, wanafufuliwa mara moja na kuenda mbinguni. Maneno ya Paulo yenye kuwa mu 1 Wakorinto 15:51, 52 inaonyesha jambo hilo. Alisema hivi: “Sisi wote hatutalala usingizi katika kifo, lakini sisi wote tutabadilishwa, kwa wakati kidogo, kufunga na kufungua jicho, wakati wa tarumbeta ya mwisho.” Ile maneno ya Paulo iko inatimia leo! Kisha tu kufufuliwa kwao, ndugu za Kristo wanakuwa na furaha kubwa; ‘watakuwa pamoja na Bwana sikuzote.’​—1 Te. 4:17.

Wale wenye wanabadilishwa “kwa kufunga na kufungua jicho,” watasaidia Yesu kuharibu watu wote wabaya ku dunia (Ona fungu la 15)

15. Wale wenye wanabadilishwa “kwa kufunga na kufungua jicho” watafanya kazi gani?

15 Biblia inatuambia kazi yenye wale wenye wanabadilishwa “kwa kufunga na kufungua jicho” watafanya mbinguni. Yesu aliwaambia hivi: “Ule mwenye atashinda na kushika matendo yangu mupaka mwisho, nitamupatia mamlaka juu ya mataifa, na atachunga watu kwa fimbo ya chuma na hivyo watavunjwa vipande-vipande kama vyombo vya udongo, kama vile nimepokea kutoka kwa Baba yangu.” (Ufu. 2:26, 27) Kama Yesu, Kamanda wao, watachunga mataifa kwa fimbo ya chuma.​—Ufu. 19:11-15.

16. Namna gani wanadamu wengi watapata ushindi juu ya kifo?

16 Ni wazi kuwa Wakristo watiwa-mafuta watapata ushindi juu ya kifo. (1 Ko. 15:54-57) Ufufuo wao utawapatia nafasi ya kusaidia kumaliza mambo yote ya mubaya yenye iko ku dunia wakati wa vita ya Armagedoni. Mamilioni ya Wakristo wengine, wanaume na wanamuke, “watatoka katika ile taabu kubwa” na kuingia mu ulimwengu mupya. (Ufu. 7:14) Wale Wakristo wenye watakuwa ku dunia, watajionea ushindi mwingine juu ya kifo, ni kusema wataona namna mamiliare ya watu wenye walikufa zamani, watafufuliwa. Fikiria furaha yenye itakuwa wakati jambo hilo litafanyika! (Mdo. 24:15) Na wale wenye wataendelea kuwa washikamanifu kwa Yehova watapata ushindi juu ya kifo chenye tuliriti kutoka kwa Adamu, ni kusema, wataishi milele.

17. Kulingana na 1 Wakorinto 15:58, tunapaswa kufanya nini?

17 Kila Mukristo mwenye kuwa muzima leo, anapaswa kufurahia maneno yenye kutia moyo yenye Paulo aliandikia Wakorinto kuhusu ufufuo. Kwa hiyo, tunapaswa kutii shauri la mutume Paulo la kujikaza kufanya mengi “katika kazi ya Bwana.” (Soma 1 Wakorinto 15:58.) Kama tunafanya ile kazi kwa bidii na kwa ushikamanifu, tunaweza kuwa na tumaini la kuwa na maisha ya muzuri wakati wenye kuja. Ile maisha itakuwa ya muzuri sana kuliko vile tunaweza kuwazia. Wakati ile ahadi itatimia tutaona kama kazi yetu haikukuwa ya bure kuhusiana na Bwana.

WIMBO 140 Uzima wa Milele​—Hatimaye!

^ fu. 5 Sehemu ya pili ya 1 Wakorinto sura ya 15 inazungumuzia mambo ingine juu ya ufufuo, zaidi sana ufufuo wa Wakristo watiwa-mafuta. Lakini, mambo yenye Paulo aliandika ni ya maana pia kwa kondoo wengine. Hii habari itaonyesha namna tumaini la ufufuo linaweza kutusaidia leo, na namna linaweza kutusaidia tutazamie kuwa na maisha yeye furaha wakati wenye kuja.

^ fu. 2 Habari yenye kichwa “Maulizo ya Wasomaji Wetu” yenye kuwa mu gazeti hili inazungumuzia mambo yenye Paulo alisema mu 1 Wakorinto 15:29.