Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Mezali 24:16 inasema hivi: “Mwenye haki anaweza kuanguka mara saba (7), na atasimama tena.” Ile maneno inahusu mutu mwenye kufanya zambi tena na tena na kisha Mungu anamusamehe?

Haiko vile. Ile maneno inahusu mutu mwenye anaanguka, ni kusema, anapata magumu mingi na kisha anasimama, ni kusema, anavumilia ile magumu.

Fikiria ile andiko na mustari wenye unaitangu- lia na wenye unaifuata: “Usivizie kwa uovu karibu na makao ya mwenye haki; usiharibu mahali pake pa kupumuzikia. Kwa maana mwenye haki anaweza kuanguka mara saba (7), na atasimama tena, lakini musiba utafanya waovu wajikwae. Wakati adui yako anaanguka, usishangilie, na wakati anajikwaa, usiache moyo wako ufurahi.”​—Mez. 24:15-17.

Watu fulani wanawaza kama mustari wa 16 unazungumuzia mutu mwenye anaanguka katika zambi lakini anatubu na anakuwa tena na uhusiano muzuri pamoja na Mungu. Viongozi wawili wa dini katika Uingereza waliandika kama “wahubiri wa zamani na leo wametumia sana ile andiko mu ile maana.” Walisema pia kama ile mafasirio inamaanisha kama mutu muzuri anaweza kuanguka katika zambi nzito na anaendelea kumupenda Mungu na kukubaliwa naye kwa sababu kila mara anatubu. Ile mafasirio inaweza kufurahisha mutu mwenye hajikazake kuepuka zambi. Anaweza kuwaza kama hata ikiwa anafanya zambi mara mingi, Mungu atamusamehe.

Lakini ile andiko haimaanishe vile.

Neno la Kiebrania lenye kutafsiriwa “kuanguka,” katika mustari wa 16, na “anaanguka,” katika mustari wa 17, linaweza kutumiwa mu njia mbalimbali. Linaweza kumaanisha kuanguka ya kawaida. Kwa mufano, ngombe-dume anaanguka katika barabara, mutu anaanguka kutoka kwenye sehemu ya juu ya nyumba, ao jiwe la kidogo linaanguka chini. (Kum. 22:4, 8; Amo. 9:9) Ile neno inaweza pia kutumiwa kwa njia ya mufano kama vile maneno yenye kufuata inaonyesha: “Yehova anaongoza hatua za mutu wakati Yeye anafurahia njia ya mutu huyo. Hata kama anaanguka, hatatupwa chini, kwa maana Yehova anamutegemeza kwa kumushika mukono.”​—Zb. 37:23, 24; Mez. 11:5; 13:17; 17:20.

Fikiria jambo la maana lenye Profesa Edward Plumptre alisema: “Neno la Kiebrania lenye linatafsiriwa [“kuanguka”] halitumiwe hata kidogo ili kumaanisha kuanguka katika zambi.” Njo maana mutu mwingine mwenye elimu ya Biblia anafasiria mustari wa 16 hivi: “Ni bure kutendea mubaya watu wa Mungu kwa sababu sikuzote wanafanikiwa, lakini watu wabaya hawafanikiwe!”

Kwa hiyo, ile mambo yote inaonyesha kama andiko la Mezali 24:16 halizungumuzie mutu mwenye anaanguka katika zambi, lakini linazungumuzia mutu mwenye anapata magumu ao matatizo, pengine hata mara kwa mara. Mu ulimwengu huu muovu, mwenye haki anaweza kupambana na matatizo ya afya ao matatizo ingine. Anaweza hata kuteswa sana na wakubwa wa serikali. Lakini anaweza kuwa hakika kama Mungu atamutegemeza na kumusaidia ili aweze kupambana na ile magumu na kuivumilia. Fikiria mambo yenye umejionea yenye kuonyesha kama kila mara watu wa Mungu wanakuwaka wanafanikiwa. Juu ya nini tunakuwaka tunafanikiwa? Tuko hakika kama “Yehova anategemeza wale wote wenye kuanguka na anasimamisha wale wote wenye kuinama chini.”​—Zb 41:1-3; 145:14-19.

Jambo lenye linakuwaka linafariji “mwenye haki” haiko kujua kama wengine pia wako wanapata magumu, lakini ni kujua kama “mambo yatawaendea muzuri wale wenye kumuogopa Mungu wa kweli, kwa sababu wanamuogopa.”​—Muh. 8:11-13; Yob. 31:3-6; Zb. 27:5, 6.