Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 52

Namna Gani Unaweza Kupambana na Hali ya Kuvunjika Moyo?

Namna Gani Unaweza Kupambana na Hali ya Kuvunjika Moyo?

“Umutupie Yehova muzigo wako, naye atakutegemeza.”​—ZB. 55:22.

WIMBO 33 Mtupie Yehova Mzigo Wako

KIFUPI CHA HABARI *

1. Kuvunjika moyo kunaweza kuwa na matokeo gani?

KILA siku tunapambana na magumu na tunajikaza sana ili kuivumilia. Lakini inaweza kuwa nguvu kuvumilia ile magumu kama tunavunjika moyo. Kwa hiyo hali ya kuvunjika moyo inaweza kutufanya tujisikie kuwa watu wa bure na tukose furaha. Mezali 24:10 inasema hivi: “Kama unavunjika moyo siku ya taabu, nguvu zako zitakuwa kidogo.” Kwa kweli, kuvunjika moyo kunaweza kutufanya tukose nguvu ya kupambana na magumu yetu.

2. Ni nini inaweza kufanya tuvunjike moyo, na tutazungumuzia nini mu hii habari?

2 Kuko mambo mingi yenye inaweza kufanya tuvunjike moyo. Kwa mufano, makosa yenye tunafanya, uzaifu wenye tuko nao, ao ugonjwa wenye tuko nao. Pia, pengine hatupate mugao fulani wenye tungependa kupata mu kazi ya Yehova ao tuko tunahubiri mu eneo kwenye watu hawapendezwe. Mu hii habari, tutazungumuzia mambo fulani yenye tunaweza kufanya ili kupambana na hali ya kuvunjika moyo.

WAKATI TUNAFANYA MAKOSA NA TUNAPAMBANA NA UZAIFU FULANI

3. Nini njo inaweza kutusaidia tukuwe na mawazo yenye kufaa juu ya makosa yetu?

3 Inaweza kuwa mwepesi kujihukumu kupita kiasi wakati tunafanya makosa na kuwa na mawazo yenye haifae juu ya uzaifu wetu. Na ile inaweza kutufanya tuwaze kama hatuwezi kupata uzima wa milele kwa sababu ya makosa yetu. Ni mubaya sana kuwa na mawazo ya vile. Sasa, namna gani tunapaswa kuona makosa yetu? Biblia inasema kama isipokuwa tu Yesu wanadamu “wote wamefanya zambi.” (Ro. 3:23) Lakini Yehova, mwenye aliandikisha Biblia, hakuwake anatafuta-tafuta makosa na hatazamie tukuwe wakamilifu. Tofauti na ile, yeye ni Baba mwenye upendo mwenye anapenda kutusaidia. Pia ni Mungu muvumilivu. Anaona namna tuko tunajikaza kupiganisha uzaifu wetu, na namna tuko tunajikaza sana kuepuka kujihukumu kupita kiasi, na iko tayari kutusaidia.​—Ro. 7:18, 19.

Yehova anajua mambo ya muzuri yenye tulifanya zamani na mambo ya muzuri yenye tuko tunafanya leo (Ona fungu la 5) *

4-5. Namna gani mawazo yenye kuwa mu 1 Yohana 3:19, 20, ilisaidia dada wawili wasiendelee kuvunjika moyo?

4 Fikiria mufano wa Deborah na Maria. * Wakati Deborah alikuwa mutoto, mara mingi watu wa familia yake walimutendea mubaya na kumufanya ajisikie kuwa mutu mwenye kuzaraulika. Na hawakuzoea kumupongeza. Ile ilifanya aanze kujiona kuwa mutu wa bure. Wakati alifanya makosa ya kidogo-kidogo, aliona kuwa hakuna kitu chenye anaweza kufanya muzuri. Maria alikuwa na tatizo kama la Deborah. Watu wa familia yake walikuwa wanamufanya ajisikie kuwa hafae. Hata kisha kubatizwa, aliona kama hastahili kuwa Shahidi wa Yehova!

5 Hata vile, wale dada wawili hawakuacha kumutumikia Yehova. Nini njo iliwasaidia? Walimutupia muzigo wao kwa kusali sana kutoka mu moyo. (Zb. 55:22) Walifikia kuelewa kuwa Baba yetu wa mbinguni anajua kama mambo yenye tulitendewa zamani inaweza kutufanya tujione kuwa watu wa bure. Lakini anaona pia mambo ya muzuri yenye kuwa mu moyo wetu, ni kusema anaona sifa za muzuri zenye tuko nazo zenye pengine sisi wenyewe hatuone.​—Soma 1 Yohana 3:19, 20.

6. Mutu anaweza kujisikia namna gani wakati anarudilia tabia fulani yenye alikuwa nayo zamani?

6 Mutu anaweza kuwa iko anajikaza kuachana na tabia fulani ya mubaya. Hata vile, wakati fulani anaweza kurudilia ile tabia yenye iko anajikaza sana kuacha. Na ile inaweza kumufanya avunjike moyo. Kwa kweli, ni jambo la kawaida kujihukumu kwa kiasi fulani wakati tunafanya zambi. (2 Ko. 7:10) Lakini, hatupaswe kujihukumu kupita kiasi na kuwaza kama tuko watu wa bure na kama Yehova hawezi kutusamehe. Ile haiko kweli na inaweza kufanya tuache kumutumikia Yehova. Kumbuka mambo yenye tulisoma mu Mezali 24:10. Ile andiko ilionyesha kama nguvu yetu inakuwa kidogo wakati tunavunjika moyo. Kwa hiyo, kuliko kuvunjika moyo, ‘unyooshe mambo’ pamoja na Yehova kwa kusali kwake na kumuomba akusamehe. (Isa. 1:18) Wakati Yehova ataona kama unahuzunika juu ya mambo yenye ulifanya na uko unajikaza sana ili kubadilika, atakusamehe. Zaidi ya ile, uzungumuze na wazee, watakusaidia kwa uvumilivu ili ukuwe tena na hali ya kiroho ya muzuri.​—Yak. 5:14, 15.

7. Juu ya nini hatupaswi kuvunjika moyo ikiwa tuko tunapambana na uzaifu fulani?

7 Jean-Luc, muzee wa kutaniko mwenye kuishi mu inchi ya Ufaransa, anaambiaka hivi watu wenye wako wanapambana na uzaifu fulani: “Mutu mwenye Yehova anaona kuwa mwenye haki, haiko mutu mwenye hafanyake makosa, lakini ni mutu mwenye anahuzunikaka juu ya makosa yenye alifanya na anajikazaka kubadilika.” (Ro. 7:21-25) Kwa hiyo, usijione kuwa mutu wa bure ikiwa uko unapambana na uzaifu fulani. Ukumbuke kama sisi wote tunafanyaka makosa, njo maana tuko na lazima ya fazili zenye hazistahiliwe za Mungu, zenye tunapata kupitia bei ya ukombozi.​—Efe. 1:7; 1 Yo. 4:10.

8. Wakati tunavunjika moyo, nani njo anaweza kutusaidia?

8 Ndugu na dada zetu wanaweza kututia moyo! Wanaweza kutusikiliza wakati tuko na lazima ya mutu wa kuzungumuza naye na wanaweza kutuambia maneno yenye kutia moyo. (Mez. 12:25; 1 Te. 5:14) Joy, dada mumoja wa mu inchi ya Nigeria mwenye amepambana na hali ya kuvunjika moyo anasema hivi: “Singeweza kuvumilia bila ndugu na dada. Kupitia ndugu na dada zangu, nimeona kuwa Yehova anajibia sala zangu. Nimejifunza hata namna ya kutia moyo watu wengine wenye kuvunjika moyo.” Lakini, tunapaswa kukumbuka kama wakati fulani, ndugu na dada zetu hawatajua ikiwa tuko na lazima ya kutiwa moyo. Kwa hiyo, sisi njo tunapaswa kukamata hatua ya kuzungumuza na ndugu ao dada mwenye kukomaa kiroho na kumuelezea kama tuko na lazima ya musaada.

WAKATI TUKO TUNAPAMBANA NA UGONJWA FULANI

9. Namna gani Zaburi 41:3 na 94:19 inatutia moyo?

9 Utegemee musaada wa Yehova. Wakati hatujisikie muzuri, na zaidi sana ikiwa tuko tunapambana na ugonjwa fulani wa muda murefu, inaweza kuwa mwepesi kuvunjika moyo. Lakini hata kama Yehova hatuponyeshe kwa njia ya muujiza leo, anatufariji na anaweza kutupatia nguvu yenye tuko nayo lazima ili tuendelee kuvumilia. (Soma Zaburi 41:3; 94:19.) Kwa mufano, anaweza kuchochea Wakristo wenzetu ili watusaidie kufanya kazi fulani ku nyumba ao watusaidie kuuza vitu fulani vyenye tuko navyo lazima. Pia, anaweza kuchochea ndugu zetu wasali pamoja na sisi. Ao anaweza kutukumbusha mawazo fulani yenye kufariji yenye kuwa mu Neno lake, sawa vile tumaini la kuwa wakamilifu na kuishi mu ulimwengu mupya bila magonjwa na maumivu.​—Ro. 15:4.

10. Nini njo ilisaidia Isang asiendelee kuvunjika moyo kisha kupatwa na aksida?

10 Isang, mwenye kuishi mu inchi ya Nigeria alipatwa na aksida yenye ilimufanya apooze. Munganga alimuambia kama hatatembeaka tena. Isang alisema hivi: “Nilivunjika moyo na kupondwa roho.” Lakini Isang alibakia mwenye kuvunjika moyo? Hapana! Nini njo ilimusaidia? Isang anasema hivi: “Mimi na bibi yangu tuliendelea kusali kwa Yehova na kujifunza Neno lake. Pia tulijikaza sana kuwa wenye shukrani kwa ajili ya mambo ya muzuri yenye tuko nayo, sawa vile tumaini letu la kuishi mu ulimwengu mupya.”

Hata wale wenye kuwa na matatizo ya afya wanaweza kupata matokeo ya muzuri mu kazi ya kuhubiri na kuwa na furaha (Ona fungu la 11-13)

11. Cindy alifanya nini ili akuwe na furaha wakati alikuwa mugonjwa?

11 Fikiria pia mufano wa Cindy, mwenye kuishi Meksiko. Munganga alimuambia kama iko na ugonjwa wenye ungeweza kumuua. Cindy alifanya nini ili aweze kuvumilia ile hali? Wakati alikuwa anapata matunzo, alijitilia muradi wa kuhubiri kila siku. Anasema hivi: “Kufanya vile kulinisaidia nisikaze akili juu ya upasuaji wangu, juu ya maumivu yenye nilikuwa nasikia, ao juu ya namna nilikuwa najisikia mubaya. Nilikuwa ninafanya hivi: Wakati nilikuwa ninazungumuza na wanganga, nilikuwa ninawauliza habari ya familia zao. Kisha nilikuwa ninawauliza juu ya nini walichagua ile kazi ya nguvu sana. Majibu yao ilikuwa inanisaidia nijue habari yenye inaweza kuwafurahisha. Wengi kati yao walisema kama mara mingi wagonjwa hawatafutake kujua hali ya wanganga. Na wengi walinishukuru kwa sababu nilikuwa najikaza kujua hali yao. Wamoja kati yao walinipatia hata namba yao ya telefone ao adresi zao. Kwa hiyo, mu ile hali ya nguvu sana mu maisha yangu, Yehova alinisaidia nikuwe na furaha mu moyo, furaha yenye sikuwazia kama ninaweza kuwa nayo!”​—Mez. 15:15.

12-13. Ndugu na dada fulani wenye kuwa wagonjwa ao wenye kuzeeka wamefanya nini ili waweze kuhubiri, na wamepata matokeo gani?

12 Ndugu na dada wenye kuwa wagonjwa ao wenye kuzeeka wanaweza kuvunjika moyo kwa sababu hawawezi kuhubiri sana. Hata vile, wengi kati yao wamepata namna wanaweza kuhubiri. Kwa mufano, dada Laurel wa Inchi ya Amerika alifanya miaka 37 mu mashini ya kumusaidia kupumua. Alikuwa pia na kansere, alifanyiwa upasuaji mara mingi, na alikuwa na magonjwa ya ngozi. Lakini ile magumu yote haikumuzuia kuhubiri. Alihubiria wanganga na watu wengine wenye walikuwa wanakuja kumuona. Alipata matokeo gani? Alisaidia watu karibu 17 wajue kweli ya Biblia! *

13 Richard, muzee wa kutaniko mwenye kuishi Ufaransa, anashauria ndugu na dada wenye hawawezi kutoka ku nyumba ao wenye kuishi mu nyumba ya kutunzia wazee wakuwe wanatia vichapo fasi kwenye watu wanaweza kuviona. Wakati watu wanapita wanaweza kuviona na kuuliza maulizo, na ile inaweza kuwatolea nafasi ya kuanzisha mazungumuzo. Kufanya vile kunaweza kutia moyo ndugu na dada zetu wenye hawawezi tena kuhubiri nyumba kwa nyumba. Wale wenye hawawezi kutoka ku nyumba wanaweza pia kuhubiri kupitia barua ao kupitia telefone.

WAKATI HATUPATE MUGAO WENYE TULIKUWA TUNAPENDA SANA

14. Mufalme Daudi alituachia mufano gani muzuri sana?

14 Kuko sababu mingi zenye zinaweza kufanya tusipewe mugao fulani mu kutaniko ao mu muzunguko. Pengine tumezeeka, tuko na matatizo ya afya, ao sababu zingine. Kama tuko mu ile hali, mufano wa Mufalme Daudi unaweza kutusaidia. Daudi alikuwa anapenda sana kujenga hekalu la Mungu, lakini Mungu alimuambia kama haiko yeye njo atafanya ile kazi. Hata vile, Daudi alitegemeza kwa moyo wote ule mwenye Mungu alichagua. Na hata alitoa zahabu na feza mingi yenye ingesaidia mu kazi ya kujenga hekalu. Bila shaka, Daudi alituachia mufano muzuri sana!​—2 Sa. 7:12, 13; 1 Ny. 29:1, 3-5.

15. Nini njo ilisaidia ndugu Hugues asiendelee kuvunjika moyo?

15 Ndugu Hugues wa Ufaransa aliacha kuwa muzee kwa sababu ya matatizo ya afya na hakukuwa tena na nguvu ya kufanya hata kazi za kidogo-kidogo ku nyumba. Anasema hivi: “Ku mwanzo, nilijiona kuwa wa bure na nilivunjika moyo sana. Lakini kisha wakati fulani, nilielewa kama ni muzuri nikubali kuwa kuko mambo yenye siwezi tena kufanya. Ile ilinisaidia nifurahie mambo yenye ninaweza kufanya mu kazi ya Yehova. Ninaazimia kabisa kuendelea kumutumikia Yehova. Nitaendelea kupambana kama vile Gideoni na wanaume wake mia tatu walifanya hata kama walikuwa wamechoka!”​—Amu. 8:4.

16. Mufano wa malaika unaweza kutufundisha nini?

16 Mufano wa malaika waaminifu unaweza pia kutusaidia. Wakati wa utawala wa Mufalme Ahabu, Yehova aliomba malaika walete mawazo yao juu ya namna ya kumudanganya mufalme muovu Ahabu. Malaika wengi walisema mawazo yao. Lakini Yehova alichagua mawazo ya malaika mumoja tu na akamuambia kama mawazo yake italeta matokeo ya muzuri. (1 Fa. 22:19-22) Je, malaika wengine walivunjika moyo na kuwaza kama walijisumbua bure kuleta mawazo yao? Hapana. Malaika ni wanyenyekevu na wanapendaka sifa yote imuendee Yehova.​—Amu. 13:16-18; Ufu. 19:10.

17. Unapaswa kukumbuka nini ikiwa unavunjika moyo kwa sababu haupate mapendeleo fulani mu kazi ya Yehova?

17 Ukumbuke kama pendeleo kubwa sana lenye uko nalo ni kuwa Shahidi wa Yehova na kuhubiri kuhusu Ufalme wa Mungu. Mapendeleo ingine inaweza kuja na kupita. Haiko ile mapendeleo njo inafanya Yehova atuone kuwa watu wa maana. Ni wakati tunajikaza kuwa wanyenyekevu na wenye kiasi njo Yehova na ndugu na dada zetu wanatuona kuwa wa maana. Kwa hiyo, umulilie Yehova akusaidie ukuwe munyenyekevu na mwenye kiasi. Fikiria mifano ya watumishi wa Mungu wenye kuzungumuziwa mu Biblia, wenye walionyesha sifa ya unyenyekevu na ya kiasi. Na kila mara ukuwe tayari kutumikia ndugu na dada zako.​—Zb. 138:6; 1 Pe. 5:5.

WAKATI WATU WA MU ENEO LENU HAWAPENDEZWE NA HABARI NJEMA

18-19. Ni nini inaweza kukusaidia ukuwe na furaha hata kama inaonekana kuwa watu wa mu eneo lenu hawapendezwe na habari njema?

18 Je, wakati fulani unavunjikaka moyo kwa sababu watu wa mu eneo lenu hawapendezwe na habari njema, ao kwa sababu watu wengi hawakuwake ku nyumba wakati unaenda kuhubiri? Kama ni vile, unaweza kufanya nini ili uendelee kuwa na furaha ao ili uongeze furaha yako? Mapendekezo fulani yenye inaweza kukusaidia inapatikana mu kisanduku chenye kichwa “ Mambo ya Kufanya ili Ukuwe na Furaha Zaidi mu Kazi ya Kuhubiri.” Pia, ni jambo la maana ukuwe na mawazo yenye kufaa juu ya kazi ya kuhubiri. Ile inamaanisha nini?

19 Ukumbuke kama kusudi letu ni kutangaza jina la Mungu na Ufalme wake. Yesu alionyesha wazi kama ni watu kidogo tu njo watapata barabara yenye kuongoza kwenye uzima. (Mt. 7:13, 14) Wakati tuko mu mahubiri, tuko na pendeleo la kutumika pamoja na Yehova, Yesu, na malaika. (Mt. 28:19, 20; 1 Ko. 3:9; Ufu. 14:6, 7) Yehova anavuta watu wenye wanapenda kumutumikia. (Yoh. 6:44) Kwa hiyo, hata kama mutu hasikilize ujumbe wetu kwa sasa, pengine anaweza kutusikiliza wakati tutamutembelea tena.

20. Namna gani Yeremia 20:8, 9 inaweza kutusaidia wakati tunavunjika moyo mu kazi ya kuhubiri?

20 Mufano wa Yeremia unaweza kutufundisha mambo mingi. Watu wenye alikuwa anahubiria hawakukuwa wanamusikiliza. Walikuwa wanamutukana na kumuchekelea “muchana wote.” (Soma Yeremia 20:8, 9.) Wakati fulani alivunjika moyo sana na alipenda kuacha kuhubiri. Lakini aliendelea kuhubiri. Nini njo ilimusaidia? “Neno la Yehova” lilikuwa kama moto ndani ya mifupa ya Yeremia, na hakuweza kulizuia! Tunaweza kuwa kama Yeremia ikiwa tunajifunza Neno la Mungu kila siku na kufikiri sana juu ya mambo yenye tuko tunajifunza. Kama tunafanya vile, furaha yetu itaendelea kuongezeka na pengine watu wengi zaidi watatusikiliza.​—Yer. 15:16.

21. Tunaweza kufanya nini ili tuweze kupambana na hali ya kuvunjika moyo?

21 Dada Deborah mwenye tulishazungumuzia anasema hivi: “Kuvunjika moyo ni silaha kubwa yenye Shetani anatumia.” Lakini Yehova Mungu iko na nguvu zaidi kuliko Shetani na silaha zake zote. Kwa hiyo, hata ikuwe nini njo inafanya uvunjike moyo, umulilie Yehova ili akutegemeze. Atakusaidia ili usijihukumu kupita kiasi wakati unafanya makosa, na ili upambane na uzaifu wako. Atakutegemeza wakati uko mugonjwa. Atakusaidia ukuwe na mawazo yenye kufaa juu ya mapendeleo katika kazi yake. Na atakusaidia ukuwe na mawazo yenye kufaa juu ya kazi ya kuhubiri. Zaidi ya yote, umutupie Baba yako wa mbinguni mahangaiko yako yote. Atakusaidia ili uweze kupambana na hali ya kuvunjika moyo.

WIMBO 41 Tafadhali Sikiliza Sala Yangu

^ fu. 5 Sisi wote tunavunjikaka moyo wakati fulani. Mu hii habari tutazungumuzia mambo mbalimbali yenye tunaweza kufanya wakati tunavunjika moyo. Na kama vile tutaona, Yehova anaweza kutusaidia kupambana na hali ya kuvunjika moyo.

^ fu. 4 Majina fulani imebadilishwa.

^ fu. 12 Soma habari juu ya maisha ya Laurel Nisbet mu Amuka! ya tarehe 22 Mwezi wa 1, 1993.

^ fu. 69 MAFASIRIO YA PICHA: Dada mwenye alivunjika moyo wakati fulani, anakumbuka mambo yenye alifanya zamani mu kazi ya Yehova na anasali kwa Yehova. Iko hakika kama Yehova anakumbuka mambo yenye alifanya zamani na yenye iko anafanya leo.