Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Utimize Mugao Wako kwa Moyo Wako Wote!

Utimize Mugao Wako kwa Moyo Wako Wote!

UNAJISIKIAKA namna gani wakati unapokea barua kutoka kwa rafiki yako mupendwa? Timoteo, mwanafunzi Mukristo alipokea barua ya vile kutoka kwa mutume Paulo. Leo, ile barua inajulikana kuwa kitabu cha Biblia cha 2 Timoteo. Bila shaka, Timoteo alipenda kupata fasi ya kimya kwenye angekaa ili kusoma mambo yenye rafiki yake mupendwa alimuandikia. Pengine Timoteo alikuwa anajiuliza hivi: ‘Paulo iko namna gani? Amenitolea mashauri fulani yenye inaweza kunisaidia ili nitimize migao yangu? Hii barua inaweza kunisaidia nipate matokeo ya muzuri mu kazi yangu ya kuhubiri na kufundisha, na nisaidie wengine?’ Kama vile tutaona, Timoteo alipata majibu ya ile maulizo na mambo ingine mu ile barua yenye kutia moyo. Lakini mu hii habari, tutazungumuzia mambo fulani tu yenye ilikuwa mu ile barua, yenye inaweza kutusaidia.

“NINAENDELEA KUVUMILIA MAMBO YOTE”

Wakati Timoteo alianza kusoma maneno ya kwanza-kwanza ya ile barua, bila shaka mara moja aliona namna Paulo alikuwa anamupenda sana. Kwa uchangamufu, Paulo alimuita “mutoto mupendwa.” (2 Ti. 1:2) Timoteo alipokea ile barua mu mwaka wa 65 hivi kisha kuzaliwa kwa Yesu. Alikuwa na zaidi ya miaka 30 na tayari alikuwa muzee Mukristo mwenye uzoefu. Alikuwa ametumika na Paulo kwa zaidi ya miaka kumi na alikuwa amejifunza mambo mengi.

Bila shaka Timoteo alitiwa moyo sana, wakati alijua kama Paulo alikuwa anavumilia majaribu kwa uaminifu. Paulo alikuwa amefungwa katika Roma, na alikuwa karibu kuuawa. (2 Ti. 1:15, 16; 4:6-8) Timoteo angeweza kuona kama Paulo alikuwa hodari, kwa sababu Paulo alisema hivi: “Ninaendelea kuvumilia mambo yote.” (2 Ti. 2:8-13) Kama Timoteo, uvumilivu wa Paulo unaweza pia kututia nguvu.

“UCHOCHEE KAMA MOTO ZAWADI”

Paulo alishauria Timoteo aone mugao wake mu kazi ya Mungu kuwa jambo la maana sana. Paulo alipenda Timoteo ‘achochee kama moto zawadi ya Mungu’ yenye ilikuwa ndani yake. (2 Ti. 1:6) Khaʹri·sma njo neno la Kigiriki lenye Paulo alitumia ili kuzungumuzia “zawadi.” Mara mingi ile neno ya Kigiriki inatumiwa ili kuzungumuzia zawadi ya bure ao yenye mutu hakustahili. Timoteo alipokea ile zawadi wakati alichaguliwa ili kutumikia kutaniko mu njia ya pekee.​—1 Ti. 4:14.

Timoteo angetumia ile zawadi namna gani? Wakati alikuwa anasoma maneno ‘kuchochea kama moto,’ pengine alifikiria moto wenye watu wanazoea kuwasha ku nyumba, wenye wakati fulani unaweza kufifia. Ile moto inapaswa kuchochewa ili iwake tena na kuleta kifukutu zaidi. Kamusi moja inasema kama neno la Kigiriki (a·na·zo·py·reʹo) lenye Paulo alitumia linamaanisha “kuwasha tena, kuchochea, kupuliza moto ili iwake tena.” Kwa hiyo, maneno ya Paulo ilimaanisha “kufanya kazi kwa bidii.” Ni kama vile Paulo alikuwa anashauria Timoteo hivi: ‘Timiza mugao wako kwa moyo wako wote!’ Sisi pia tunapaswa kufanya vile, ni kusema, tunapaswa kuwa na bidii mu kazi yetu.

“LINDA JAMBO HILI LA MUZURI LENYE LILIWEKWA KWAKO”

Wakati Timoteo aliendelea kusoma ile barua yenye rafiki yake alimuandikia, aliona maneno ingine yenye ingemusaidia atimize muzuri utumishi wake. Paulo alimuandikia hivi: “Linda jambo hili la muzuri lenye liliwekwa kwako kupitia roho takatifu, yenye inakaa ndani yetu.” (2 Ti. 1:14) Ni jambo gani la muzuri lenye liliwekwa kwake? Mu mustari wa 13, Paulo alizungumuzia “maneno yenye faida,” ni kusema, kweli yenye inapatikana mu Maandiko. (2 Ti. 1:13) Kwa sababu Timoteo alikuwa mutumishi katika kutaniko la Kikristo, alipaswa kufundisha kweli ndani na inje ya kutaniko. (2 Ti. 4:1-5) Pia, kwa sababu Timoteo alikuwa muzee, alikuwa na daraka la kuchunga kundi la Mungu. (1 Pe. 5:2) Kwa hiyo, alipaswa kulinda jambo lenye liliwekwa kwake, ni kusema, kweli yenye alipaswa kufundisha. Angefanya vile kwa kutegemea roho takatifu ya Yehova na Neno lake.​—2 Ti. 3:14-17.

Leo, sisi pia tumepewa kweli yenye tunafundisha wengine. (Mt. 28:19, 20) Tunaweza kufanya nini ili kuonyesha kama tunaendelea kuiona kuwa ya maana? Tunapaswa kudumu katika sala na kujifunza Neno la Mungu kwa ukawaida. (Ro. 12:11, 12; 1 Ti. 4:13, 15, 16) Zaidi ya ile, pengine tuko na migao ingine. Kwa mufano, pengine uko muzee ao uko mu utumishi wa wakati wote. Migao ya vile inapaswa kutusaidia tukuwe wanyenyekevu, na kutusaidia kuelewa kama tuko na lazima ya musaada wa Mungu. Kwa hiyo, tunaweza kulinda migao yenye tulipewa kwa kuiona kuwa ya maana na kumuomba Yehova atusaidie ili tuweze kuitimiza.

“MAMBO HAYO UYAPATIE WANAUME WAAMINIFU”

Mugao wa Timoteo ungemuomba pia azoeze wengine ili waweze kufanya muzuri kazi yenye alikuwa anafanya. Njo maana Paulo alimushauria hivi: “Mambo yenye ulisikia kutoka kwangu . . . , uyapatie wanaume waaminifu, wenye nao watastahili kabisa kufundisha wengine.” (2 Ti. 2:2) Kwa kweli, Paulo alimukumbusha Timoteo kama alipaswa kufundisha ndugu wengine mambo yenye alikuwa amejifunza. Ni jambo la maana kila mwangalizi mu kutaniko la Kikristo ajikaze pia kufanya vile. Mwangalizi muzuri hafichake wengine mambo yenye anajua kuhusu mugao fulani. Lakini, anafundishaka wengine ili wao pia waweze kutimiza ile mugao. Haogopake kama watajua mambo mingi kuliko yeye ao watakuwa na uwezo mukubwa zaidi kuliko yeye. Kwa hiyo, mwangalizi hapaswe kufundisha tu mambo ya musingi kuhusu mugao fulani. Anapaswa kusaidia wale wenye iko anazoeza wakuwe na uwezo wa kukamata maamuzi ya muzuri na wakuwe na uelewaji, ni kusema, wakuwe Wakristo wenye uzoefu. Kama anafanya vile, wale “wanaume waaminifu” wenye alizoeza watasaidia sana kutaniko.

Bila shaka Timoteo alifurahia sana ile barua yenye kutia moyo yenye Paulo alimuandikia. Inawezekana alikuwa anaisoma tena na tena ili kuchunguza ile mashauri na kufikiri namna angeweza kuitumia ili kutimiza muzuri migao yake.

Sisi pia tunapaswa kutumia ile mashauri. Tunaweza kufanya vile namna gani? Tunaweza kujikaza kuchochea kama moto zawadi yenye tuko nayo, kulinda jambo la muzuri lenye tulipewa, na kufundisha wengine mambo yote yenye tunajua. Ikiwa tunafanya vile, ‘tutatimiza kwa ukamili utumishi [wetu],’ kama vile Paulo alimuambia Timoteo.​—2 Ti. 4:5.