Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Kusali Kunaweza Kukuletea Faida Gani?

Kusali Kunaweza Kukuletea Faida Gani?

Wakati Pamela alikuwa na ugonjwa wa kansere, alienda kuona munganga ili amusaidie. Lakini, alisali pia kwa Mungu ili kumuomba nguvu ya kuvumilia ugonjwa wake. Kusali kulimusaidia?

Pamela anafasiria hivi: “Wakati walikuwa wananitunza ugonjwa wangu wa kansere, mara mingi nilikuwa naogopa sana. Lakini wakati nilisali kwa Yehova Mungu, nilijisikia kuwa mwenye kutulia na niliweza kuvumilia ile ugonjwa bila kuogopa. Ninaendelea kusikia maumivu, lakini sala inanisaidia niendelee kuwa na mawazo yenye kufaa. Wakati watu wananiuliza namna ninajisikia ninasema, ‘sijisikie muzuri, lakini niko na furaha!’”

Hata hivyo, hatupaswe kuchunga wakati tunakuwa na ugonjwa hatari ao tatizo la nguvu njo tusali. Sisi wote tunakuwaka na magumu, ya nguvu ao hapana, na mara mingi tunakuwaka na lazima ya musaada ili tuweze kupambana nayo. Kusali kunaweza kutusaidia?

Biblia inasema hivi: “Umutupie Yehova muzigo wako, naye atakutegemeza. Hataruhusu hata kidogo mwenye haki aanguke.” (Zaburi 55:22) Ile ni maneno yenye kutia moyo sana! Sasa, sala inaweza kukuletea faida gani? Wakati unasali kwa Mungu mu njia yenye kufaa, atakupatia mambo yenye uko nayo lazima ili uweze kuvumilia magumu yako.​—Ona kisanduku “ Faida Mbalimbali za Kusali.”