Je, Mungu Husikiliza Sala Zako?
Unaposali, je, unahisi kweli Mungu anakusikiliza?
BIBLIA INASEMA NINI?
Mungu husikiliza. Biblia inatuhakikishia kwamba “Yehova yuko karibu na wote wanaomwitia, wote wanaomwitia yeye katika ukweli. . . . Husikia kilio chao cha kuomba msaada.”—Zaburi 145:18, 19.
Mungu anataka usali kwake. Biblia inatusihi hivi: “Katika kila jambo kwa sala na dua pamoja na kutoa shukrani, mjulisheni Mungu maombi yenu.”—Wafilipi 4:6.
Mungu anakujali wewe binafsi. Mungu anaelewa vizuri kabisa mahangaiko na mikazo uliyo nayo, naye anataka kukusaidia. Biblia inasema: “[Tupeni] mahangaiko yenu yote juu yake, kwa sababu yeye anawajali ninyi.”—1 Petro 5:7.