Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Mungu Anasikiaka Sala Zako?

Mungu Anasikiaka Sala Zako?

Wakati unasali, unakuwaka hakika kama Mungu anakusikiaka?

BIBLIA INASEMA NINI?

  • Mungu anasikilizaka sala. Biblia inatuhakikishia kama “Yehova iko karibu na wale wote wenye kumuitia, wote wenye kumuitia katika ukweli. . . . Anasikia kilio chao cha kuomba musaada.”​—Zaburi 145:18, 19.

  • Mungu anapenda usali kwake. Biblia inatutia moyo hivi: “Katika kila jambo kwa sala na sala ya kumulilia Mungu pamoja na kutoa shukrani, maombi yenu yajulishwe Mungu.”​—Wafilipi 4:6.

  • Mungu anakuhangaikia kabisa. Mungu anajua muzuri mahangaiko yetu na magumu yetu, na anapenda kutusaidia. “Mumutupie mahangaiko yenu yote, kwa sababu yeye anawahangaikia ninyi.”​—1 Petro 5:7.