Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Mambo Unaweza Kufanya juu Uishi mu Dunia Mupya

Mambo Unaweza Kufanya juu Uishi mu Dunia Mupya

Mu habari zenye zilitangulia, tuliona kama hivi karibuni, Mungu atatosha watu wote wabaya na magumu yote yenye iko mu dunia. Tunaweza kuwa hakika kama ile itatimia. Juu ya nini? Juu Neno ya Mungu, Biblia, ilishaahidi hivi:

“Ulimwengu (ao dunia) unapita.”​—1 YOHANA 2:17.

Tunaweza kuwa hakika kama kutakuwa watu fulani wenye wataokoka juu hii andiko ya Biblia ilishaahidi hivi:

“Ule mwenye anafanya mapenzi ya Mungu anadumu milele.”

Kwa hiyo, siri ya kuokoka ni kufanya mapenzi ya Mungu. Ili tufikie kujua mapenzi ya Mungu, tunapaswa kwanza kumujua Mungu muzuri.

JUU UOKOKE UNAPASWA ‘KUFIKIA KUMUJUAʼ MUNGU

Yesu alisema: “Uzima wa milele ndio huu, wafikie kukujua wewe Mungu wa pekee wa kweli.” (Yohana 17:3) Juu tuokoke na kuishi milele, tunapaswa ‘kufikia kumujua’ Mungu. Ile haimaanishe tu kukubali kama Mungu iko na kujua mambo fulani juu yake. Tunapaswa kuwa marafiki wake. Iko tu sawa vile tunapenda urafiki wetu na mutu fulani ukuwe nguvu, tunapaswa kupitisha wakati pamoja naye. Ni vile pia juu ya kuwa rafiki ya Mungu. Ona kweli fulani za maana zenye ziko mu Biblia, zenye zitakusaidia kukomalisha urafiki wako pamoja na Mungu na kuendelea kuwa rafiki yake.

USOME NENO YA MUNGU, BIBLIA, KILA SIKU

Wakati unamuomba Mungu akusaidie na wakati unafanya mapenzi yake unaweza kuokoka wakati dunia itaharibiwa

Tunakulaka chakula kila siku juu tuishi. Lakini Yesu alisema: “Mwanadamu hapaswe kuishi kwa mukate tu, lakini kwa kila neno lenye linatoka katika kinywa cha Yehova.”​—Matayo 4:4.

Leo, tunapata Neno ya Yehova mu Biblia. Wakati unajifunza ile kitabu takatifu, utajua kweli za musingi juu ya mambo yenye Mungu alifanyaka zamani, mambo yenye iko anafanya sasa, na juu ya mambo yenye atafanya wakati wenye kuja.

UMUOMBE MUNGU AKUSAIDIE

Unaweza kufanya nini kama unapenda kutii maagizo ya Mungu lakini ni nguvu kwako kuacha kufanya mambo yenye haimufurahishe? Mu ile hali, kufikia kumujua Mungu kunaweza kukusaidia umutii.

Fikiria mwanamuke mwenye tutaita Sakura, mwenye alikuwa na mwenendo mubaya sana. Wakati alianza kujifunza Biblia, alifikia kujua amri ya Mungu yenye inasema “mukimbie uasherati.” (1 Wakorinto 6:18) Sakura alimuomba Mungu amupatie nguvu na alifikia kuacha ile tabia ya mubaya. Lakini iko anafanya yake yote juu asiangukie mu ile mutego. Anasema: “Wakati mawazo ya uasherati inakuya mu akili yangu, nasali waziwazi kwa Yehova, nikijua kama siwezi kupiganisha ile hali miye peke. Sala imenisaidia nimukaribie Yehova zaidi.” Sawa vile Sakura, mamilioni ya watu wamefikia kumujua Mungu. Iko anawapatia nguvu yenye wako nayo lazima ili kufanya mabadiliko mu maisha na kuishi mu njia yenye inamufurahisha.​—Wafilipi 4:13.

Kadiri unafikia kumujua Mungu muzuri, ni vile ‘Mungu atakujua’ sawa rafiki wake wa sana. (Wagalatia 4:9; Zaburi 25:14) Njo utaishi milele mu dunia mupya. Lakini ile dunia mupya itakuwa namna gani? Habari yenye kufuata itafasiria ile jambo.

a Yehova njo jina ya Mungu sawa vile inaonyeshwa mu Biblia.