Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Kila Mtu Anatamani Kuwa na Maisha Bora ya Wakati Ujao

Kila Mtu Anatamani Kuwa na Maisha Bora ya Wakati Ujao

Unatamani wakati wako ujao uweje? Watu wengi wanatamani wao na familia zao wawe na maisha mazuri ya wakati ujao. Bila shaka wewe pia unatamani hilo​—uwe na furaha, afya nzuri, amani, na ufanisi.

Hata hivyo, watu wengi wanatilia shaka ikiwa watakuwa na maisha mazuri wakati ujao. Wamejionea matukio makubwa na yasiyotarajiwa, kama vile janga la ugonjwa wa corona (COVID-19), yakitikisa jamii, yakivuruga uchumi, na kutishia uhai wao. Hivyo, wanahisi maisha yao ya wakati ujao hayatakuwa salama.

Kwa sababu watu hawajui mambo yatakayotokea wakati ujao, wanatafuta kitu kitakachowaongoza ili wawe na maisha bora. Baadhi ya watu huamini kwamba maisha yao huongozwa na mambo kama vile majaliwa au bahati njema. Wengi wanajitahidi kupata elimu ya juu zaidi na utajiri, wakifikiri kwamba mambo hayo yatawapatia kila kitu wanachotaka. Wengine wanafikiri wanahitaji tu kuwa watu wema ili wawe na maisha mazuri.

Je, kuna jambo lolote kati ya hayo litakalokusaidia kuwa na maisha bora ya wakati ujao? Ili kupata jibu, unahitaji kufikiria maswali yafuatayo:

  • Ni jambo gani hasa linaloamua jinsi maisha yako yatakavyokuwa?

  • Je, elimu na pesa zinaweza kukuhakikishia kwamba utakuwa na maisha mazuri?

  • Je, kuwa mtu mwema kutakuhakikishia kwamba utakuwa na maisha bora ya wakati ujao?

  • Unaweza kupata wapi mwongozo unaotegemeka wa kuwa na maisha bora ya wakati ujao?

Gazeti hili la Mnara wa Mlinzi litakusaidia kupata majibu ya maswali hayo.