Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Kuko Muongozo Wenye Kutumainika Wenye Unaweza Kutusaidia Kuwa na Maisha ya Muzuri Wakati Wenye Kuja?

Kuko Muongozo Wenye Kutumainika Wenye Unaweza Kutusaidia Kuwa na Maisha ya Muzuri Wakati Wenye Kuja?

Sawa vile tulizungumuzia mu habari zenye zilitangulia, watu wamefanya yao yote juu wakuwe na maisha ya muzuri wakati wenye kuja kwa kuweka tumaini yao katika mambo sawa vile, bahati, masomo, utajiri ao kwa kuwa tu watu wazuri. Lakini kufanya vile iko sawa kutumia karte ya bongo juu ikupeleke fasi fulani. Je, ile inamaanisha kama hakuna muongozo wowote wenye kutumainika kwa ajili ya maisha yetu ya wakati wenye kuja? Hapana!

MUONGOZO KUTOKA KWENYE CHANZO YA JUU SANA

Wakati tunapendaka kukamata maamuzi, mara mingi tunaombaka mawazo kwa mwenye kutupita miaka ao mwenye kuwa na hekima mingi kuliko siye. Vilevile, tunaweza kupata muongozo wenye kutumainika kwa ajili ya maisha yetu ya wakati wenye kuja kutoka kwenye chanzo ya zamani sana na yenye hekima sana kuliko siye. Mashauri kutoka kwake inapatikana katika maandishi fulani matakatifu yenye ilianza kuandikwa kumepita miaka karibu 3500. Ile maandishi yote matakatifu iko mu kitabu yenye inaitwa Biblia.

Juu ya nini unaweza kutumainia Biblia? Ni juu hakuna mutu mwenye kuwa wa zamani sana na mwenye kuwa na hekima sana mu ulimwengu wote sawa ule mwenye aliiandikisha. Ule mutu anaitwa kuwa “Muzee wa Siku” mwenye ni wa “tangu milele mupaka milele.” (Danieli 7:9; Zaburi 90:2) Yeye ni “Muumbaji wa mbingu, Mungu wa kweli, Mwenye alifanya dunia.” (Isaya 45:18) Yeye mwenyewe anajiita kwa jina Yehova.​—Zaburi 83:18.

Juu Biblia inatoka kwa Muumbaji wa wanadamu haipendelee desturi fulani ao rangi fulani ya ngozi kuliko ingine. Mashauri yake iko ya maana kila siku na imeletea faida watu wa inchi zote. Inapatikana mu luga za mingi sana na hakuna kitabu * ingine sawa Biblia yenye imegawanywa sana mu dunia yote. Ni kusema, watu wenye kuwa fasi yote mu dunia wanaweza kuielewa kwa urahisi na inaweza kuwaongoza. Ile mambo yote inaunga mukono hii maneno ya Biblia yenye inasema:

“Mungu hana ubaguzi, lakini katika kila taifa mutu mwenye anamuogopa na kufanya mambo yenye kuwa sawa anakubaliwa naye.”​—MATENDO 10:34, 35.

Sawa tu vile muzazi mwenye kuwa na upendo anaongozaka watoto wake, Yehova Mungu naye ni Baba mwenye kuwa na upendo, mwenye anatusaidia kupitia Neno yake Biblia. (2 Timoteo 3:16) Unaweza kutumainia Neno yake juu Yeye njo alituumba na anajua ni mambo gani iko ya muzuri ili tukuwe na maisha ya muzuri.

Unapaswa kufanya nini juu ukuwe na maisha ya muzuri wakati wenye kuja? Ona habari yenye kufuata.

^ fu. 6 Ili kupata habari zaidi kuhusu kazi ya kutafsiri na kuhusu kazi ya kugawanya Biblia, fungua www.pr418.com na uende ku sehemu MAFUNDISHO YA BIBLIA > HISTORIA NA BIBLIA.

^ fu. 16 Ili kupata habari zaidi ona sura ya 9 ya Kitabu Biblia​—Neno la Mungu ao la Binadamu? yenye ilichapishwa na Mashahidi wa Yehova. Inapatikana ku Enternete ku www.pr418.com fungua sehemu MAKTABA > VITABU NA BROSHUA.