Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Unaweza Kuamua Maisha Yako ya Wakati Ujao Yatakuwaje

Unaweza Kuamua Maisha Yako ya Wakati Ujao Yatakuwaje

Miaka 3,500 hivi iliyopita, Yehova Mungu aliwaambia waabudu wake mambo waliyopaswa kufanya ili wawe na maisha bora ya wakati ujao. Alisema hivi: “Nimeweka uzima na kifo mbele yenu, baraka na laana; nanyi lazima mchague uzima ili mwendelee kuishi, ninyi na wazao wenu.”​—Kumbukumbu la Torati 30:19.

Ili wawe na maisha bora ya wakati ujao, watu hao walihitaji kufanya uamuzi sahihi. Leo, sisi pia, tuna nafasi ya kufanya uamuzi unaofaa. Biblia inafafanua jinsi tunavyoweza kuchagua kuwa na maisha bora ya wakati ujao: “Kwa kumpenda Yehova Mungu wenu, kwa kuisikiliza sauti yake.”​—Kumbukumbu la Torati 30:20.

TUNAWEZAJE KUMPENDA YEHOVA NA KUISIKILIZA SAUTI YAKE?

JIFUNZE BIBLIA: Ili umpende Yehova, kwanza, unahitaji kujifunza kumhusu kutoka kwenye Biblia. Utakapofanya hivyo, utatambua kwamba yeye ni Mungu mwenye upendo na anayekutakia mema. Anakualika usali kwake “kwa sababu yeye [anakujali].” (1 Petro 5:7) Biblia inaahidi kwamba ikiwa utajitahidi kumkaribia, ‘naye atakukaribia.’—​Yakobo 4:8.

TUMIA MAMBO UNAYOJIFUNZA: Kumsikiliza Mungu kunamaanisha kufuata mwongozo wake wenye hekima unaopatikana kwenye Biblia. Ukifanya hivyo, “ndipo utakapofanikisha njia yako na kutenda kwa hekima.”—Yoshua 1:8.