Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 3

Kundi Kubwa la Watu Linamusifu Mungu na Kristo

Kundi Kubwa la Watu Linamusifu Mungu na Kristo

“Wokovu wetu unatoka kwa Mungu wetu, mwenye kukaa kwenye kiti cha ufalme, na kwa Mwana-Kondoo.”​—UFU. 7:10.

WIMBO 14 Kumsifu Mfalme Mpya wa Dunia

KIFUPI CHA HABARI *

1. Hotuba yenye ilitolewa ku mukusanyiko mu mwaka wa 1935, ilikuwa na matokeo gani juu ya kijana fulani?

KIJANA fulani mwanaume alikuwa na miaka 18 wakati alibatizwa mu mwaka wa 1926. Wazazi wake walikuwa wanafunzi wa Biblia. Ni vile Mashahidi wa Yehova walikuwa wanaitwa ile wakati. Wazazi wake walikuwa na watoto tatu wanaume, na watoto wawili wanamuke. Walisaidia watoto wao wote wamutumikie Yehova Mungu na wamuige Yesu Kristo. Ule kijana alikuwa anakula mukate na kunywa divai kila mwaka ku Ukumbusho. Ni vile Wanafunzi wote wa Biblia walikuwa wanafanya ile wakati. Lakini mawazo yake ilibadilika kabisa wakati alisikia hotuba yenye haiwezi kusahauliwa yenye kichwa “Kundi Kubwa la Watu.” Ile hotuba ilitolewa na Ndugu Joseph Rutherford mu mwaka wa 1935 ku mukusanyiko wenye ulifanywa Washington, mu Inchi ya Amerika. Wanafunzi wa Biblia walijifunza nini ku ule mukusanyiko?

2. Ni mwangaza gani mupya wenye Ndugu Rutherford alizungumuzia mu hotuba yake?

2 Mu ile hotuba, Ndugu Rutherford alifasiria ni nani wenye wangefanyiza “kundi kubwa la watu” lenye kuzungumuziwa mu Ufunuo 7:9. Ile wakati, Wanafunzi wa Biblia walikuwa wanawaza kama watu wa kundi kubwa walikuwa wanadamu wenye wangeenda pia mbinguni, lakini wenye hawakukuwa waaminifu sana sawa vile watiwa-mafuta. Ndugu Rutherford alitumia Maandiko ili kufasiria kama watu wa kundi kubwa hawachaguliwe ili kuishi mbinguni. Lakini ni kondoo wengine * wa Kristo wenye wataokoka “taabu kubwa” na kuishi milele ku dunia. (Ufu. 7:14) Yesu alisema hivi: “Niko na kondoo wengine, wenye hawako wa zizi hili; hao pia lazima niwalete, na watasikiliza sauti yangu, na watakuwa kundi moja, muchungaji mumoja.” (Yoh. 10:16) Wale kondoo wengine ni Mashahidi waaminifu wa Yehova wenye wako na tumaini la kuishi milele mu Paradiso ku dunia. (Mt. 25:31-33, 46) Tuone basi namna ule mwangaza mupya ulibadilisha maisha ya watumishi wengi wa Yehova, kutia ndani ule ndugu wa miaka 18 mwenye tulizungumuzia.​—Zb. 97:11; Mez. 4:18.

MWANGAZA MUPYA WENYE ULIBADILISHA MAISHA YA WATU WENGI

3-4. Ku mukusanyiko wenye ulifanywa mu mwaka wa 1935, watu wengi walitambua nini kuhusu tumaini lao, na juu ya nini?

3 Ku ule mukusanyiko, ilifurahisha sana wakati musemaji aliambia hivi wasikilizaji: “Wale wote wenye kuwa na tumaini la kuishi milele ku dunia, wanaweza kusimama tafazali?” Ndugu mumoja mwenye alikuwa ku ule mukusanyiko alisema kama zaidi ya nusu ya watu 20 000 hivi wenye walikuwa ku ule mukusanyiko walisimama. Kisha Ndugu Rutherford alisema hivi: “Muone! Kundi kubwa la watu!” Na kisha watu walipiga vigelegele kwa furaha. Wale wenye walisimama walitambua kama Mungu hakuwachagua ili waishi mbinguni. Walielewa kama Mungu hakukuwa amewatia mafuta kupitia roho yake. Siku yenye ilifuata ya mukusanyiko, watu 840 walibatizwa, na wengi kati yao walikuwa wa kondoo wengine.

4 Kisha ile hotuba, ule kijana mwanaume mwenye tulizungumuzia na wengine wengi, wenye kuwa na moyo muzuri waliacha kula mukate na kunywa divai ku Ukumbusho. Maneno yenye ndugu mumoja alisema inaonyesha namna wengi walijisikia. Alisema hivi kwa unyenyekevu: “Ni ku Ukumbusho wa mwaka wa 1935 njo nilikula mukate na kunywa divai kwa mara ya mwisho. Nilitambua kama Yehova hakukuwa ametumia roho yake takatifu ili kunipatia tumaini la kuishi mbinguni. Lakini nilikuwa na tumaini la kuishi ku dunia na kusaidia kuifanya kuwa paradiso.” (Ro. 8:16, 17; 2 Ko. 1:21, 22) Tangu ile wakati, wale wenye kufanyiza kundi kubwa la watu, wameendelea kuongezeka. Na wako wanatumika pamoja na watiwa-mafuta wenye wangali ku dunia.

5. Yehova iko na mawazo gani juu ya wale wenye wameacha kula mukate na kunywa divai ku Ukumbusho?

5 Yehova iko na mawazo gani juu ya wale wenye waliacha kula mukate na kunywa divai ku Ukumbusho kisha mwaka wa 1935? Na tuseme nini ikiwa leo, bila kuwa na nia ya mubaya, Shahidi mwenye kubatizwa anakula mukate na kunywa divai ku Ukumbusho, lakini kisha wakati fulani anatambua kama haiko mutiwa-mafuta? (1 Ko. 11:28) Ndugu na dada fulani walikuwa wanakula mukate na kunywa divai ku Ukumbusho juu walikuwa wanawaza kama wako na tumaini la kuenda mbinguni. Lakini ikiwa wanakubali kama walijidanganya, wanaacha kula mukate na kunywa divai, na wanaendelea kumutumikia Yehova kwa uaminifu, Yehova atawaona kuwa washiriki wa kondoo wengine. Hata kama hawakule tena mukate na kunywa divai, wanaendelea kuhuzuria Ukumbusho kwa sababu wako wenye shukrani sana kwa ajili ya mambo yenye Yehova na Yesu wamewafanyia.

TUMAINI LA MUZURI SANA

6. Yesu anaamuru malaika wafanye nini?

6 Kwa sababu taabu kubwa inakaribia sana, itakuwa muzuri tuchunguze tena mambo yenye Ufunuo sura ya 7 inasema juu ya Wakristo watiwa-mafuta na kundi kubwa la watu wa kondoo wengine. Mu mistari ya kwanza-kwanza ya ile sura, Yesu anaamuru malaika waendelee kuzuia pepo ine za uharibifu. Hawapaswe kuziachilia juu ya dunia mupaka Wakristo wote watiwa-mafuta wakuwe wametiwa muhuri, ni kusema, mupaka Yehova akuwe ameamua kama ni waaminifu. (Ufu. 7:1-4) Kwa sababu ya uaminifu wao, ndugu watiwa-mafuta wa Kristo wanapewa zawabu ya kuwa wafalme na makuhani pamoja naye mbinguni. (Ufu. 20:6) Wale wote wenye kuwa katika familia ya Mungu ya mbinguni, watafurahi sana kuona wale watiwa-mafuta 144 000 wanapewa zawabu yao.

Kundi kubwa la watu wenye kuvaa kanzu nyeupe na wenye kuwa na matawi ya mitende mu mikono yao, wanasimama mbele ya kiti cha ufalme chenye utukufu cha Mungu na mbele ya Mwana-Kondoo. (Ona fungu la 7)

7. Kama vile Ufunuo 7:9, 10 inaonyesha, Yohana aliona nani katika maono, na wako wanafanya nini? (Ona picha ku jalada la gazeti hili.)

7 Kisha kuzungumuzia wale wafalme na makuhani 144 000, Yohana anaona jambo lingine lenye kufurahisha. Anaona, “kundi kubwa la watu” wenye wanaokoka Armagedoni. Tofauti na kile kikundi cha kwanza, kikundi cha pili chenye anaona kiko na watu wengi sana wenye hatujue hesabu yao. (Soma Ufunuo 7:9, 10.) “Wamevaa kanzu za mweupe.” Ile inaonyesha kama wameendelea kujilinda ili kubakia “bila doa,” ni kusema, ili wasichafuliwe na ulimwengu wa Shetani. Na wameendelea kuwa washikamanifu kwa Mungu na Kristo. (Yak. 1:27) Wanasema kwa sauti kubwa kama wameokolewa kwa sababu ya mambo yenye Yehova na Yesu, Mwana-Kondoo wa Mungu, wamefanya. Wako pia na matawi ya mitende mu mikono yao. Ile inaonyesha kama wanakubali kwa furaha kama Yesu njo Mufalme mwenye Yehova ameweka.​—Linganisha na Yohana 12:12, 13.

8. Ufunuo 7:11, 12 inasema nini juu ya familia ya Yehova ya mbinguni?

8 Soma Ufunuo 7:11, 12. Wale wenye kuwa mbinguni walifanya nini wakati waliona kundi kubwa la watu? Yohana anaona familia ya Yehova ya mbinguni inafurahi sana na kumusifu Mungu wakati inaona wale wenye kufanyiza kundi kubwa la watu. Familia ya Yehova ya mbinguni itafurahi sana wakati itaona namna ile maono itatimia wakati kundi kubwa la watu litaokoka taabu kubwa.

9. Kulingana na Ufunuo 7:13-15, kundi kubwa la watu wako wanafanya nini?

9 Soma Ufunuo 7:13-15. Yohana anasema kama kundi kubwa la watu “wamefua kanzu zao na kuzifanya mweupe katika damu ya Mwana-Kondoo.” Ni kusema, wako na zamiri safi na Yehova anawakubali. (Isa. 1:18) Ni Wakristo wenye wamejitoa kwa Yehova na kubatizwa. Wako na imani katika zabihu ya Yesu na wako na uhusiano muzuri pamoja na Yehova. (Yoh. 3:36; 1 Pe. 3:21) Njo maana wanastahili kusimama mbele ya kiti cha ufalme cha Yehova na kumutolea “utumishi mutakatifu muchana na usiku,” katika sehemu ya ku dunia ya hekalu lake la kiroho. Hata leo, wanatanguliza faida za Ufalme kwa kufanya kwa bidii kazi ya kuhubiri na kufanya wanafunzi.​—Mt. 6:33; 24:14; 28:19, 20.

Washiriki wenye furaha wa kundi kubwa la kondoo wengine wanaokoka taabu kubwa (Ona fungu la 10)

10. Kundi kubwa la watu wako hakika na jambo gani, na wataona utimizo wa ahadi gani?

10 Kundi kubwa la watu wenye wataokoka taabu kubwa, wako hakika kama Mungu ataendelea kuwahangaikia, kwa sababu Biblia inasema hivi: “Ule mwenye kukaa kwenye kiti cha ufalme atatandika hema yake juu yao.” Wataona utimizo wa ahadi hii yenye wamengojea sana: “[Mungu] atapanguza kila chozi katika macho yao, na kifo hakitakuwa tena, wala maombolezo wala kilio wala maumivu havitakuwa tena.”​—Ufu. 21:3, 4.

11-12. (a) Kama vile Ufunuo 7:16, 17 inaonyesha, kundi kubwa la watu watapata baraka gani? (b) Kondoo wengine wanaweza kufanya nini ku Ukumbusho, na juu ya nini?

11 Soma Ufunuo 7:16, 17. Leo watumishi fulani wa Yehova wako wanateseka na njaa kwa sababu hawana feza za kuuza chakula, ao kwa sababu ya magumu yenye kuletwa na vita, ao mivurugo katika inchi. Wengine wamefungwa kwa sababu ya imani yao. Lakini kundi kubwa la watu wanafurahi sana kwa sababu wanajua kama kisha kuokoka uharibifu wa ulimwengu huu muovu, watakuwa na chakula mingi ya kimwili na ya kiroho. Wakati ulimwengu wa Shetani utaharibiwa, Yehova atawalinda ili wasichomwe na “joto . . . lenye kuunguza” la kasirani yake yenye atamwanga juu ya mataifa. Kisha taabu kubwa, Yesu atawaongoza kwenye “maji ya uzima [wa milele].” Waza kidogo: Kati ya mamiliare ya watu wenye wameishi ku dunia, kundi kubwa la watu, wako na tumaini la kuendelea kuishi bila kuonja kifo. Ile ni tumaini la muzuri sana!​—Yoh. 11:26.

12 Kondoo wengine wako na tumaini la muzuri sana. Wako wenye shukrani kwa Yehova na Yesu kwa ajili ya tumaini hilo. Na hata kama hawakuchaguliwa ili kuenda mbinguni, Yehova anawaona kuwa wa maana kama vile tu watiwa-mafuta. Kondoo wengine na watiwa-mafuta, wote wanaweza kumusifu Mungu na Kristo. Njia moja ya kufanya vile, ni kuhuzuria Ukumbusho.

UMUSIFU SANA YEHOVA NA KRISTO KU UKUMBUSHO

Mukate na divai vyenye kupitishwa ku Ukumbusho vinatukumbusha kama Yesu alikufa kwa ajili yetu ili tuweze kupata uzima (Ona fungu la 13-15)

13-14. Juu ya nini watu wote wanapaswa kuhuzuria Ukumbusho wa kifo cha Kristo?

13 Mu miaka ya hivi karibuni, kati ya watu 1 000 wenye wanahuzuria Ukumbusho, kunaweza kuwa mutu mumoja hivi mwenye anakula mukate na kunywa divai. Mu makutaniko mingi hamuna hata mutu mumoja mwenye anakulaka mukate ao kunywa divai ku Ukumbusho. Watu wengi wenye wanahuzuriaka Ukumbusho wako na tumaini la kuishi ku dunia. Sasa juu ya nini wanahuzuriaka Ukumbusho? Juu tuelewe tufikirie sababu yenye inafanya watu waende ku ndoa ya rafiki yao. Wanaendaka kwa sababu wanapenda wale wenye wanafunga ndoa na wanapenda kuwategemeza. Vilevile wale wa kondoo wengine wanahuzuria Ukumbusho kwa sababu wanapenda Kristo na watiwa mafuta, na wanapenda kuwategemeza. Pia wanahuzuria Ukumbusho kwa sababu wanapenda kuonyesha shukrani yao kwa ajili ya zabihu ya Yesu. Ile zabihu njo inawasaidia wakuwe na tumaini la kuishi milele ku dunia.

14 Sababu ingine yenye inafanya kondoo wengine wahuzurie Ukumbusho ni ili kutii amri ya Yesu. Wakati Yesu alianzisha Chakula cha Mangaribi cha Bwana pamoja na mitume wake waaminifu, aliwaambia hivi: “Muendelee kufanya hivi kwa kunikumbuka mimi.” (1 Ko. 11:23-26) Kwa hiyo, kondoo wengine wataendelea kuhuzuria Ukumbusho mupaka wakati hakutakuwa tena watiwa-mafuta ku dunia. Pia wanaalika watu wengine ili wakuje ku Ukumbusho.

15. Namna gani tunaweza kumusifu Mungu na Kristo ku Ukumbusho?

15 Ku Ukumbusho tuko na nafasi ya kumusifu Mungu na Kristo kupitia nyimbo na sala. Hotuba yenye itatolewa ku Ukumbusho hii mwaka iko na kichwa, “Tuonyeshe Shukrani kwa Ajili ya Mambo Yenye Mungu na Kristo Walitufanyia!” Itatusaidia tukuwe wenye shukrani zaidi kwa Yehova na Kristo. Wakati mukate na divai vitakuwa vinapitishwa, vitatukumbusha mambo yenye vinafananisha, ni kusema mwili wa Yesu na damu yake. Tutakumbuka kama Yehova alitoa Mwana wake akufe kwa ajili yetu ili tuweze kupata uzima. (Mt. 20:28) Kila mutu mwenye anamupenda Baba yetu wa mbinguni na Mwana wake atapenda kuhuzuria Ukumbusho.

UMUSHUKURU YEHOVA KWA AJILI YA TUMAINI LENYE AMEKUPATIA

16. Je, watiwa-mafuta ni wa maana kuliko kondoo wengine? Fasiria.

16 Tusiwaze kama Yehova anaona watiwa-mafuta kuwa wa maana kuliko kondoo wengine. Wote anawaona kuwa wa maana. Tunajua vile juu alilipa bei ileile, ni kusema uzima wa Mwana wake Mupendwa ili kununua watiwa-mafuta na kondoo wengine. Tofauti tu ni kuwa wako na tumaini tofauti. Lakini wote wanapaswa kuendelea kuwa washikamanifu kwa Yehova na kristo. (Zb. 31:23) Na ukumbuke kama roho ya Yehova inaweza kutusaidia sisi wote kwa namna ileile, ikuwe tuko watiwa-mafuta ao kondoo wengine.

17. Watiwa-mafuta wenye wangali ku dunia wanangojea nini kwa hamu?

17 Wakristo watiwa-mafuta hawazaliwe na tumaini la kuenda mbinguni. Ni Mungu njo anatia tumaini hilo mu moyo wao. Wanakuwaka wanafikiri na kusali juu ya tumaini lao. Wanangojea kwa hamu kupewa zawabu yao mbinguni. Hawawezi hata kuwazia namna miili yao ya kiroho itakuwa. (Flp. 3:20, 21; 1 Yo. 3:2) Hata vile, wanangojea kwa hamu kuonana na Yehova, Yesu, malaika, na watiwa-mafuta wengine. Wanangojea kwa hamu kuwa pamoja nao katika Ufalme wa mbinguni.

18. Kondoo wengine wanangojea nini kwa hamu?

18 Kondoo wengine wanangojea kwa hamu kuishi milele ku dunia. Ile ni tamaa yenye wanadamu wote wanakuwaka nayo. (Muh. 3:11) Wanangojea kwa hamu kugeuza dunia yote kuwa paradiso. Wanangojea kwa hamu siku yenye watajenga nyumba zao, kupanda mabustani, na kukomalisha watoto wakamilifu. (Isa. 65:21-23) Wanangojea kwa hamu kutembelea nafasi mbalimbali mu dunia; kuona milima, mapori, na bahari, na kujifunza vitu vingi vyenye Yehova aliumba. Zaidi ya yote wanafurahi sana kwa sababu urafiki wao pamoja na Yehova utaendelea kuwa nguvu zaidi na zaidi.

19. Ukumbusho unatupatia nafasi ya kufanya nini, na Ukumbusho wa hii mwaka utafanywa wakati gani?

19 Yehova amepatia watumishi wake wote wenye wamejitoa kwake tumaini la muzuri. (Yer. 29:11) Ukumbusho wa kifo cha Kristo unapatia kila mumoja wetu nafasi ya muzuri sana ya kumusifu Mungu na Kristo, kwa sababu ya mambo yenye wametufanyia ili tuweze kuishi milele. Bila shaka Ukumbusho njo mukutano wa maana zaidi wenye Wakristo wanafanyaka kila mwaka. Utafanywa Siku ya Posho, tarehe 27 Mwezi wa 3, 2021, kisha jua kushuka. Hii mwaka watu wengi watahuzuria Ukumbusho bila vizuizi. Wengine watahuzuria ijapokuwa upinzani. Na wengine watahuzuria mu gereza. Hata ikuwe tutahuzuria mu hali gani, tukumbuke kama Yehova na Yesu, na sehemu ya mbinguni ya familia ya Yehova watakuwa wanatuangalia. Basi kila kutaniko, kila kikundi, na kila mumoja wetu afurahie Ukumbusho!

WIMBO 150 Mtafute Mungu Upate Ukombozi

^ fu. 5 Tarehe 27 Mwezi wa 3, 2021, itakuwa siku ya pekee kwa Mashahidi wa Yehova. Mangaribi ya ile siku tutafanya Ukumbusho wa kifo cha Kristo. Wengi kati ya wale wenye watahuzuria ni wa kikundi chenye Yesu aliita “kondoo wengine.” Mu mwaka wa 1935, Mashahidi wa Yehova walijifunza kweli gani ya maana juu ya kile kikundi? Kondoo wengine wanangojea nini kisha taabu kubwa? Na namna gani wanaweza kumusifu Mungu na Kristo ku Ukumbusho?

^ fu. 2 MAFASIRIO YA MANENO FULANI: Kondoo wengine wanatia ndani wale wote wenye wamemutumikia Yehova mu kipindi chote cha siku za mwisho. Wanamufuata Kristo na wako na tumaini la kuishi milele ku dunia. Kundi kubwa la watu ni washiriki wa kondoo wengine wenye watakuwa wangali wazima wakati Kristo atahukumu wanadamu wakati wa taabu kubwa na wenye wataokoka taabu kubwa.