Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Maandishi kwenye jiwe: “Yahweh Sabaot alaani Hagaf mwana wa Hagav”

Ulijua?

Ulijua?

Namna gani maandishi fulani ya zamani inaunga mukono Biblia?

MU YERUSALEMU, katika Nyumba ya Kuwekea Vitu vya Zamani vya Maeneo ya Biblia, muko jiwe lenye kuwa na maandishi yenye iliandikwa kati ya mwaka wa 700 na mwaka wa 600 mbele ya kuzaliwa kwa Yesu. Lile jiwe lilipatikana katika pango lenye lilitumiwa ili kuzikia watu, lenye kuwa karibu na Hebroni katika Israeli. Ile maandishi inasema hivi: “Yahweh Sabaot alaani Hagaf mwana wa Hagav.” Namna gani ile maandishi inaunga mukono Biblia? Inaonyesha kama jina la Mungu, Yehova, lenye kuandikwa YHWH katika herufi za Kiebrania cha zamani lilijulikana, na watu walizoea kulitumia wakati wa zamani. Mu ile mapango munapatikana pia maandishi ingine yenye watu wenye walikuwa wanakutana ao kujificha mule walikuwa wanaandika. Walizoea kuandika ku ukuta jina la Mungu pamoja na majina ya kipekee yenye kuwa na sehemu fulani ya jina la Mungu.

Kuhusu ile maandishi, Rachel Nabulsi, mutu mwenye elimu ya luga wa Masomo ya Juu ya Georgia alisema hivi: “Ni jambo la maana kuona namna jina YHWH linarudiliwa mara mingi. . . . Maandiko ya Biblia na ile maandishi inaonyesha kama YHWH alikuwa wa maana kwa watu wa Israeli na Yuda.” Ile inaunga mukono Biblia, kwa sababu mu Biblia jina la Mungu, lenye kuandikwa YHWH katika herufi za Kiebrania linapatikana mara mingi sana. Mara mingi majina ya kipekee ya watu ilikuwa na sehemu ya jina la Mungu.

Maneno “Yahweh Sabaot,” yenye kuandikwa kwenye lile jiwe inamaanisha “Yehova wa majeshi.” Kwa hiyo, inaonekana kama watu wa zamani walizoea kutumia jina la Mungu, Yehova, na pia maneno “Yehova wa majeshi.” Pia, ile inaunga mukono namna Biblia inatumia maneno “Yehova wa majeshi.” Ile maneno inapatikana mara 283 katika Maandiko ya Kiebrania. Zaidi sana mu maandishi ya Isaya, Yeremia, na Zekaria.