Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 4

Muendelee Kuonyesha Upendo Wenye Upole

Muendelee Kuonyesha Upendo Wenye Upole

“Katika upendo wa kindugu mukuwe na upendo wenye upole.”​—RO. 12:10.

WIMBO 109 Pendaneni Sana Kutoka Moyoni

KIFUPI CHA HABARI *

1. Nini njo inaonyesha kama leo watu wengi hawana upendo wa asili?

BIBLIA ilitabiri kama mu siku za mwisho watu hawangekuwa na “upendo wa asili.” (2 Ti. 3:1, 3) Ule unabii uko unatimia leo. Kwa mufano, familia za mingi zinagawanyika kwa sababu wazazi wameamua kuvunja ndoa na ile inafanya waendelee kukasirikiana, na watoto wao wajisikie kuwa hawapendwe. Hata watu wa familia wenye wanaishi pamoja wanaweza kukosa kuwa na uhusiano wa karibu. Mutu mumoja mwenye kutolea familia mashauri anasema hivi: “Mama, baba, na watoto hawasemeshanake na wanapitishaka wakati mingi mu kutumia ordinatere, tablete, telefone, ao kucheza michezo ya video. Hata kama wanaishi mu nyumba moja, hawajuane muzuri.”

2-3. (a) Kulingana na Waroma 12:10, ni nani tunapaswa kuonyesha upendo wenye upole? (b) Tutazungumuzia nini mu hii habari?

2 Hatupendi kuwa kama watu wengi mu ulimwengu huu wenye hawana upendo. (Ro. 12:2) Lakini tunapaswa kuonyesha watu wa familia yetu na ndugu na dada zetu upendo wenye upole. (Soma Waroma 12:10.) Upendo wenye upole ni nini? Ile maneno inatumiwaka ili kuzungumuzia urafiki ao uhusiano wa karibu sana wenye watu wa familia wanakuwaka nao. Ni ile aina ya upendo njo tunapaswa kuonyesha ndugu na dada zetu. Wakati tunaonyesha upendo wenye upole, tunasaidia kutaniko liendelee kuwa na umoja.​—Mik. 2:12.

3 Ili tujue namna ya kukomalisha na kuonyesha upendo wenye upole, tuone mifano fulani yenye kuzungumuziwa mu Biblia na mambo yenye inaweza kutufundisha.

YEHOVA NI “MWENYE UPENDO MWINGI SANA”

4. Yakobo 5:11 inasema nini juu ya upendo wa Yehova?

4 Biblia inatusaidia kujua sifa za muzuri za Yehova. Kwa mufano, inasema kama “Mungu ni upendo.” (1 Yo. 4:8) Kujua tu ile kunatuchochea tumukaribie. Lakini Biblia inasema pia kama Yehova “ni mwenye upendo mwingi sana.” (Soma Yakobo 5:11.) Kwa kweli, ile maneno inaonyesha ni kwa kadiri gani Yehova anatupenda!

5. Namna gani Yehova anaonyeshaka rehema, na namna gani tunaweza kumuiga?

5 Zaidi ya kusema kama Yehova iko na upendo mwingi sana, Yakobo 5:11 inasema pia kama ni mwenye rehema. (Kut. 34:6) Yehova anaonyeshaka rehema mu njia mingi. Kwa mufano, anatuonyeshaka rehema kwa kutusamehe wakati tunafanya makosa. (Zb. 51:1) Wakati neno rehema linatumiwa katika Biblia, halimaanishe tu kusamehe. Linamaanisha pia kusikilia huruma mutu mwenye iko na magumu, na kufanya jambo fulani ili kumusaidia. Yehova anasema kama huruma yenye anatusikiliaka, inapita huruma yenye mama anasikiliaka mutoto wake. (Isa. 49:15) Wakati tuko na magumu, rehema yake inamuchochea atusaidie. (Zb. 37:39; 1 Ko. 10:13) Sisi pia tunaweza kuonyesha ndugu na dada zetu rehema kwa kuwasamehe, na kuepuka kuendelea kuwakasirikia kama wanatukosea. (Efe. 4:32) Jambo lingine la maana lenye tunaweza kufanya ili kuonyesha ndugu na dada zetu rehema ni kuwasaidia wakati wako na magumu. Wakati upendo unatuchochea kuonyesha wengine rehema, tunamuiga Yehova, mufano muzuri zaidi wa kuonyesha upendo wenye upole.​—Efe. 5:1.

YONATANI NA DAUDI ‘WALIUNGANISHWA KATIKA URAFIKI WA KARIBU SANA’

6. Namna gani Yonatani na Daudi walionyeshana upendo wenye upole?

6 Mu Biblia muko mifano ya watu wenye walionyeshana upendo wenye upole hata kama hawakukuwa wakamilifu. Fikiria mufano wa Yonatani na Daudi. Biblia inasema hivi: “Yonatani na Daudi wakaunganishwa katika urafiki wa karibu sana, na Yonatani akaanza kumupenda kama vile alijipenda mwenyewe.” (1 Sa. 18:1) Yehova alichagua Daudi ili akuwe mufalme kisha Sauli. Ile ilifanya Sauli amusikilie Daudi wivu na ajaribu kumuua. Wakati Sauli alijaribu kumuua Daudi, Yonatani, mwana wake, hakumuunga mukono. Yonatani na Daudi waliahidiana kama wataendelea kuwa marafiki na watategemezana sikuzote.​—1 Sa. 20:42.

Yonatani na Daudi walikuwa marafiki wa sana hata kama Yonatani alikuwa mukubwa sana kuliko Daudi (Ona fungu la 6-9)

7. Ni nini ingezuia Yonatani na Daudi kuwa marafiki?

7 Inashangaza kuona namna Yonatani na Daudi walionyeshana upendo wenye upole, kwa sababu kuko mambo mingi yenye ingewazuia kuwa marafiki. Kwa mufano, Yonatani alikuwa anashinda Daudi miaka 30 hivi. Yonatani angewaza kama hawezi kufanya urafiki na mutu mwenye kuwa mudogo sana kuliko yeye na mwenye hana uzoefu. Lakini hakuwaza vile, na alimuheshimia sana Daudi.

8. Juu ya nini unawaza kama Yonatani alikuwa rafiki muzuri wa Daudi?

8 Yonatani angeweza kumusikilia Daudi wivu. Kwa sababu Yonatani alikuwa mutoto wa Mufalme Sauli, angesema kama ni yeye alistahili kuwa mufalme kisha baba yake. (1 Sa. 20:31) Lakini alikuwa munyenyekevu na alikuwa mushikamanifu kwa Yehova. Kwa hiyo, aliunga mukono Daudi, mufalme mwenye Yehova alikuwa amechagua ili akamate nafasi ya Sauli. Alikuwa pia mushikamanifu kwa Daudi, hata kama ile ilimukasirisha sana Sauli.​—1 Sa. 20:32-34.

9. Je, Yonatani alimusikilia Daudi wivu? Fasiria.

9 Yonatani alimupenda sana Daudi, kwa hiyo hakumusikilia wivu. Yonatani alikuwa mupiga-mishale mwenye ufundi na alikuwa mupiganaji mwenye uhodari. Yeye na baba yake Sauli walijulikana kuwa “wepesi kuliko tai” na “wenye nguvu kuliko simba.” (2 Sa. 1:22, 23) Kwa hiyo, Yonatani angeweza kujisifu kwa sababu ya mambo ya ajabu yenye alikuwa ametimiza. Lakini, Yonatani hakushindana na Daudi, ao kumusikilia wivu. Kuliko kufanya vile, alifurahia uhodari wa Daudi na namna alimutumainia Yehova. Kwa mufano, ni kisha Daudi kumuua Goliati njo Yonatani alianza kumupenda sana, sawa vile alikuwa anajipenda mwenyewe. Namna gani sisi pia tunaweza kuonyesha ndugu na dada zetu upendo wenye upole?

NAMNA GANI TUNAWEZA KUONYESHA UPENDO WENYE UPOLE LEO?

10. ‘Kupendana sana kutoka katika moyo’ maana yake nini?

10 Biblia inatuambia ‘tupendane sana kutoka katika moyo.’ (1 Pe. 1:22) Yehova anatuwekea mufano muzuri. Anatupenda sana kiasi ya kwamba ikiwa tuko waaminifu kwake, hakuna kitu chenye kinaweza kumufanya aache kutupenda. (Ro. 8:38, 39) Neno la Kigiriki lenye linatafsiriwa “sana” linaleta wazo la kujinyoosha ao hata kujikaza sana. Ile inaonyesha kama wakati fulani, inaomba kujikaza sana ili kuonyesha Wakristo wenzetu upendo wenye upole. Wakati wengine wanatukasirisha, tunapaswa kuendelea ‘kuvumiliana katika upendo, kujikaza sana kuendeleza umoja wa roho katika kifungo chenye kuunganisha cha amani.’ (Efe. 4:1-3) Wakati tunajikaza sana ili kuendeleza “kifungo chenye kuunganisha cha amani,” hatutakazia akili makosa ya ndugu zetu. Tutajikaza sana kuona ndugu zetu sawa vile Yehova anawaona. ​—1 Sa. 16:7; Zb. 130:3.

Euodia na Sintike wako wanaangaliana mubaya. Kila mumoja wao iko anazungumuza na kikundi fulani cha watu mu kutaniko. (Ona fungu la 11)

11. Juu ya nini wakati fulani inaweza kuwa nguvu kuonyesha upendo wenye upole?

11 Haiko mwepesi kila mara kuonyesha ndugu na dada zetu upendo wenye upole, zaidi sana kama tunajua makosa yao. Inaonekana Wakristo fulani wa karne ya kwanza walikuwa na ile tatizo. Kwa mufano, inawezekana haikukuwa nguvu kwa Euodia na Sintike kutumika “bega kwa bega pamoja na [Paulo] kwa ajili ya habari njema.” Lakini juu ya sababu fulani, Euodia na Sintike hawakukuwa wanasikilizana. Njo maana Paulo aliwatia moyo “wakuwe na akili moja katika Bwana.”​—Flp. 4:2, 3.

Wazee wa kutaniko wenye kuwa vijana na wenye kukomaa wanaweza kuwa marafiki wa sana (Ona fungu la 12)

12. Nini njo inaweza kutusaidia kuonyesha ndugu na dada zetu upendo wenye upole?

12 Nini njo inaweza kutusaidia kuonyesha ndugu na dada zetu upendo wenye upole? Wakati tunajikaza kujua ndugu na dada zetu muzuri zaidi, inaweza kuwa mwepesi kuwaelewa na kuwaonyesha upendo wenye upole. Hatupaswe kujizuia kufanya urafiki pamoja nao kwa sababu ya miaka yao ao desturi yao. Ukumbuke kama Yonatani alimushinda Daudi miaka 30 hivi. Hata vile, alifanya naye urafiki wa sana. Kuko mutu fulani mwenye kukushinda miaka ao mwenye unashinda miaka mwenye unaweza kufanya naye urafiki? Kama unafanya vile, utaonyesha kuwa ‘unapenda ushirika muzima wa ndugu.’​—1 Pe. 2:17.

Ona fungu la 12 *

13. Ni mubaya kuwa na urafiki wa sana na watu fulani mu kutaniko kuliko wengine? Fasiria.

13 Je, kuonyesha ndugu na dada zetu upendo wenye upole kunamaanisha kama tunapaswa kuwa na urafiki wa sana pamoja na kila mutu mu kutaniko? Hapana, ile haiwezekane. Ni kawaida kuwa na urafiki wa sana na watu fulani kwa sababu wanafurahiaka mambo yenye sisi pia tunafurahiaka. Ile haiko mubaya. Yesu aliita mitume wake wote “marafiki,” lakini alikuwa anamupenda sana Yohana. (Yoh. 13:23; 15:15; 20:2) Hata vile, Yesu hakumutendea Yohana muzuri zaidi kuliko mitume wengine. Kwa mufano, wakati Yohana na ndugu yake Yakobo walimuomba awapatie cheo cha juu katika Ufalme wa Mungu, Yesu aliwaambia hivi: “Kukaa kwenye mukono wangu wa kuume ao kwenye mukono wangu wa kushoto, haiko haki yangu kutoa.” (Mk. 10:35-40) Ili kumuiga Yesu, sisi pia hatupaswe kutendea marafiki wetu wa sana muzuri zaidi kuliko wengine. (Yak. 2:3, 4) Kama tunafanya vile, tunaweza kuvuruga amani na umoja katika kutaniko.​—Yud. 17-19.

14. Kulingana na Wafilipi 2:3, nini njo inaweza kutusaidia tuepuke kushindana na ndugu na dada zetu?

14 Wakati tunaonyeshana upendo wenye upole, tunasaidia kutaniko lisikuwe na roho ya kushindana. Ukumbuke kama Yonatani hakumusikilia Daudi wivu, na hakujaribu kuwa mufalme pa nafasi yake. Sisi wote tunaweza kuiga mufano wa Yonatani. Usisikilie wivu ndugu na dada zako kwa sababu ya uwezo mbalimbali wenye wako nao. ‘Lakini kwa unyenyekevu uone wengine kuwa wazuri zaidi kuliko wewe.’ (Soma Wafilipi 2:3.) Ukumbuke kama kila mutu anaweza kusaidia kutaniko mu njia fulani. Kama tunaendelea kuwa wanyenyekevu, tutaona sifa za muzuri za ndugu na dada zetu, na mufano wao wa uaminifu utatusaidia.​—1 Ko. 12:21-25.

15. Mambo yenye ilifikia Tanya na watoto wake inakufundisha nini?

15 Wakati tunapata magumu, Yehova anaweza kuchochea ndugu na dada zetu ili watuonyeshe upendo wenye upole na wafanye jambo fulani ili kutusaidia. Fikiria mambo yenye ilimupata Tanya na watoto wake watatu. Walihuzuria moja kati ya Mikusanyiko ya Kimataifa ya mwaka wa 2019, yenye kichwa “Upendo Haushindwe Hata Kidogo!” yenye ilifanywa katika Inchi ya Amerika. Kisha kuhuzuria programu ya Siku ya Posho, jambo fulani lilitokea. Tanya anasema hivi: “Wakati tulikuwa tunarudia ku hoteli, gari moja iligonga gari yenye tulikuwa ndani. Hakuna mwenye aliumia, lakini tulishangaa sana, tukatoka inje ya gari, na kusimama mu barabara. Mutu fulani alituita tuende mu gari yake ili tukuwe salama. Alikuwa ndugu yetu mwenye naye alikuwa anatoka ku mukusanyiko. Na haiko yeye tu njo alisimama. Mashahidi wengine tano wenye walitoka Suède ili kuja kuhuzuria mukusanyiko walisimama pia. Dada walitukumbatia sana mimi na mutoto wangu mwanamuke, na ile ilifanya tujisikie muzuri. Niliwaambia kama tuko salama, lakini hawakupenda kutuacha. Walibakia na sisi mupaka wakati wanganga walikuja ili kutusaidia. Na walihakikisha kama tuko na kila kitu chenye tulikuwa nacho lazima. Wakati wa ile magumu, tuliona upendo wa Yehova. Ile mambo yenye ilitufikia ilifanya tupende zaidi ndugu na dada zetu, tumupende zaidi Yehova, na kumuonyesha shukrani zaidi.” Unakumbuka wakati wenye ulikuwa na lazima ya musaada na Mukristo mwenzako akakuonyesha upendo wenye upole?

16. Wakati tunaonyeshana upendo wenye upole, ile inaleta faida gani?

16 Wakati tunaonyeshana upendo wenye upole, ile inaleta faida gani? Tunafariji ndugu na dada zetu wakati wako na magumu. Tunasaidia kutaniko likuwe na umoja zaidi. Tunaonyesha kama tuko wanafunzi wa Yesu, na ile inaweza kusaidia watu wenye kuwa na moyo muzuri wakuwe na nia ya kumutumikia Yehova. Zaidi ya yote, tunamutukuza Yehova, “Baba wa rehema nyingi na Mungu wa faraja yote.” (2 Ko. 1:3) Sisi wote tuazimie basi kuendelea kukomalisha upendo wenye upole na kuuonyesha!

WIMBO 130 Uwe Mwenye Kusamehe

^ fu. 5 Yesu alisema kama upendo wenye wanafunzi wake wangeonyeshana njo ungewatambulisha kuwa Wakristo wa kweli. Sisi wote tunajikazaka kuonyesha ule upendo. Lakini, hatupaswe tu kuonyesha ndugu na dada zetu upendo wa kawaida. Tunapaswa pia kuwaonyesha upendo wenye upole, ni kusema, kuwapenda vile tunapendaka watu wa familia yetu. Hii habari itatusaidia tukomalishe upendo wenye upole na tuendelee kuuonyesha ndugu na dada zetu.

^ fu. 55 MAFASIRIO YA PICHA: Muzee kijana iko anazungumuza kulingana na mambo yenye alijifunza kutoka kwa muzee mwenye kukomaa mwenye kuwa na uzoefu. Ule muzee mwenye kukomaa anakaribisha kwake ule muzee kijana na bibi yake.