Ĩta kĩrĩ birĩa birĩ ndeene

Ĩta kĩrĩ birĩa birĩ ndeene

KĨTHOOMO GĨA KWIRITANA KĨA 5

“Kristo Niwe Kiongo kia Muntu Murume Kinya Uriku”

“Kristo Niwe Kiongo kia Muntu Murume Kinya Uriku”

“Kristo niwe kiongo kia muntu murume kinya uriku.”​—1 AKO. 11:3.

RWĨMBO 12 Mungu Mkuu, Yehova

MUHTASARI *

1. Nĩ mantũ jarĩkũ joomba kũringithia mwonere jwa muntũ mũrũme jwegie kaanya ga kwĩthĩrwa arĩ kĩongo kĩa nja?

NENO “ukichwa” linamaanisha nini kwako? Baadhi ya wanaume wanaruhusu desturi, utamaduni, au malezi yao yawaongoze inapohusu jinsi wanavyowatendea wake na watoto wao. Ona kile anachosema Yanita, dada anayeishi barani Ulaya: “Mahali ninapoishi, kuna maoni yaliyokita mizizi kwamba wanawake ni watu duni kwa kulinganishwa na wanaume na wanapaswa kuonwa kama watumwa.” Na Luke, ndugu anayeishi Marekani anasema: “Baadhi ya akina baba wanawafundisha wana wao kwamba wanawake wanapaswa kukaa kimya, hawapaswi kueleza maoni au mapendezi yao.” Hata hivyo, mitazamo hiyo haipatani na maoni ya Yehova kuhusu jinsi anavyotaka wanaume watumie ukichwa wao. (Linganisha Marko 7:13.) Hivyo basi, mwanamume anaweza kujifunzaje kuwa kichwa kizuri cha familia?

2. Nĩmbi kĩongo kĩa nja abuĩrĩte kũmenya, na nĩkĩ?

2 Ili kuwa kichwa kizuri cha familia, kwanza, ni lazima mwanamume aelewe Yehova anataka afanye nini. Pia, anahitaji kujua kwa nini Yehova alianzisha mpango wa ukichwa, na kihususa jinsi anavyoweza kuiga mfano uliowekwa na Yehova na Yesu. Kwa nini ni muhimu kwa mwanamume kupata ujuzi huo? Kwa sababu Yehova amewapa vichwa vya familia mamlaka ya kadiri na anatarajia waitumie vizuri.—Luka 12:48b.

KWĨTHĨRWA ŨRĨ KĨONGO NĨ KUUGA ATĨA?

3. Nĩmbi tũkwiritana kĩrĩ mũbango jwegie kĩongo kuumania na jarĩa jagweti kĩrĩ 1 Akorintho 11:3?

3 Soma 1 Wakorintho 11:3. Mstari huo unafafanua jinsi ambavyo Yehova ameipanga familia yake ya mbinguni na duniani. Ukichwa unahusisha mambo mawili muhimu—mamlaka na kuwajibika. Yehova ndiye “kichwa,” au mamlaka ya juu kabisa, na watoto wake wote, wa kiroho na wanadamu, wanawajibika kwake. (Rom. 14:10; Efe. 3:14, 15) Yehova amempa Yesu mamlaka juu ya kutaniko, lakini Yesu anatoa hesabu kwa Yehova kwa jinsi anavyotutendea. (1 Kor. 15:27) Pia, Yehova amempa mume mamlaka juu ya mke wake na watoto, lakini mume anawajibika mbele za Yehova na Yesu kwa jinsi anavyoitendea familia yake.—1 Pet. 3:7.

4. Nĩ waathani bũrĩkũ Jehova na Jesũ barĩ nabu?

4 Akiwa Kichwa cha familia yake ya ulimwengu mzima, Yehova ana mamlaka ya kuweka sheria kuhusu jinsi watoto wake wanavyopaswa kujiendesha, naye anaweza kuhakikisha sheria hizo zinatekelezwa. (Isa. 33:22) Pia, Yesu akiwa kichwa cha kutaniko la Kikristo ana haki ya kuweka sheria na kuhakikisha zinatekelezwa.—Gal. 6:2; Kol. 1:18-20.

5. Kĩongo kĩa nja ya Gĩkristũ arĩ na waathani bũrĩkũ, na nĩ mĩanka ĩrĩkũ arĩ nayo?

5 Kwa kufuata kielelezo kilichowekwa na Yehova na Yesu, kichwa cha familia ya Kikristo ana mamlaka ya kuiwekea sheria familia yake. (Rom. 7:2; Efe. 6:4) Hata hivyo, mamlaka yake ina mipaka. Kwa mfano, sheria anazoweka zinapaswa kutegemea kanuni zinazopatikana katika Neno la Mungu. (Met. 3:5, 6) Na kichwa cha familia hana mamlaka ya kuwawekea sheria wale ambao si sehemu ya familia yake. (Rom. 14:4) Pia, wana na binti zake wanapokua na kuondoka nyumbani, wanaendelea kumheshimu, lakini hawapo tena chini ya ukichwa wake.—Mt. 19:5.

NĨKĨ JEHOVA EEKĨRE MŨBANGO JŨU?

6. Nĩkĩ Jehova eekĩre mũbango jwegie kĩongo?

6 Yehova alianzisha mpango wa ukichwa kwa sababu anaipenda familia yake. Ni zawadi kutoka kwake. Mpango wa ukichwa unaiwezesha familia ya Yehova iwe na amani na utaratibu mzuri. (1 Kor. 14:33, 40) Bila kuwa na mpango ulio wazi wa ukichwa, familia ya Yehova ingekuwa bila utaratibu na isiyo na furaha. Kwa mfano, isingejulikana ni nani anayepaswa kufanya maamuzi ya mwisho na kuwa mstari wa mbele kutekeleza maamuzi hayo.

7. Kũringana na Aefeso 5:25, 28, rĩ, neka Jehova eendeete antũ arũme baathaga antũ aka?

7 Ikiwa mpango wa Mungu wa ukichwa ni kitu kizuri, kwa nini basi wanawake wengi leo wanahisi wanakandamizwa na kutawaliwa na waume zao? Hiyo ni kwa sababu wanaume wengi wanapuuza viwango vya Yehova kuhusu familia, na badala yake, wanachagua kufuata utamaduni na desturi za eneo wanaloishi. Pia, huenda wakawatendea vibaya wake zao ili kutimiza tamaa zao za kibinafsi. Kwa mfano, huenda mume akataka kumtawala mke wake ili ahisi kuwa yeye ni bora zaidi au awathibitishie wengine kwamba yeye si mwanamume dhaifu. Anaweza kuwa na maoni ya kwamba hawezi kumlazimisha mke wake ampende, lakini anaweza kumfanya amwogope. Na anaweza kutumia woga huo kama njia ya kumdhibiti. * Ni wazi kwamba njia hiyo ya kufikiri na kutenda inamnyima mwanamke heshima na staha anayostahili, na ni kinyume kabisa na matakwa ya Yehova.—Soma Waefeso 5:25, 28.

NĨATĨA MUNTŨ MŨRŨME OOMBA KWIRITANA KWAA KĨONGO GĨKĨEGA KĨA NJA?

8. Nĩatĩa muntũ mũrũme oomba kwiritana kwaa kĩongo gĩkĩega kĩa nja?

8 Mwanamume anaweza kujifunza kuwa kichwa kizuri cha familia kwa kuiga jinsi ambavyo Yehova na Yesu wanatumia ukichwa wao. Acheni tuchunguze sifa mbili zinazoonyeshwa na Yehova na Yesu, na tuone jinsi ambavyo kichwa cha familia anaweza kuonyesha sifa hizo anaposhughulika na mke na watoto wake.

9. Nĩatĩa Jehova onanagia winyiia?

9 Unyenyekevu. Yehova ndiye mwenye hekima kuliko Mtu yeyote; hata hivyo, anasikiliza maoni ya watumishi wake. (Mwa. 18:23, 24, 32) Anawaruhusu wale walio chini ya mamlaka yake kutoa mapendekezo. (1 Fal. 22:19-22) Yehova ni mkamilifu, lakini kwa sasa hatarajii ukamilifu kutoka kwetu. Badala yake, anawasaidia wanadamu wasio wakamilifu wanaomtumikia wafanikiwe. (Zab. 113:6, 7) Isitoshe, Biblia hata inamfafanua Yehova kuwa “msaidizi.” (Zab. 27:9; Ebr. 13:6) Mfalme Daudi alitambua kwamba angeweza kutimiza kazi kubwa aliyokuwa amepewa, kwa sababu tu Yehova alikuwa mnyenyekevu na alimsaidia.—2 Sam. 22:36.

10. Nĩatĩa Jesũ oonanĩrie winyiia?

10 Fikiria mfano wa Yesu. Ingawa alikuwa Bwana na Mwalimu wa wanafunzi wake, aliwaosha miguu yao. Ni sababu gani moja iliyomfanya Yehova aongoze simulizi hilo liandikwe kwenye Biblia? Bila shaka, ili kuwapatia vichwa vya familia, pamoja na wengine, kielelezo kilicho wazi cha kufuata. Yesu mwenyewe alisema hivi: “Nimewawekea kielelezo, ili mfanye kama nilivyowafanyia.” (Yoh. 13:12-17) Ingawa alikuwa na mamlaka kubwa, Yesu hakutarajia atumikiwe. Badala yake, aliwatumikia wengine.—Mt. 20:28.

Kichwa cha familia anaonyesha unyenyekevu na upendo kwa kufanya kazi za nyumbani na kwa kuiandalia familia yake mahitaji ya kiroho (Tazama fungu la 11 na 13)

11. Nĩatĩa kĩongo kĩa nja oomba kwiritana bwegie winyiia kuumania na ngerekano ĩrĩa Jehova na Jesũ bekĩte?

11 Somo kwetu. Kichwa cha familia anaweza kuonyesha unyenyekevu kwa njia mbalimbali. Kwa mfano, hatarajii ukamilifu kutoka kwa mke na watoto wake. Anasikiliza maoni ya washiriki wa familia yake, hata ikiwa yanapingana na maoni yake. Marley, dada anayeishi nchini Marekani anasema hivi: “Nyakati nyingine mimi na mume wangu tunakuwa na maoni yanayotofautiana. Lakini ninahisi ananithamini na kuniheshimu kwa sababu yeye huniuliza maoni yangu na kuyafikiria kwa makini kabla ya kufanya maamuzi.” Isitoshe, mume mnyenyekevu yuko tayari kufanya kazi za nyumbani, hata ikiwa katika jamii yake kazi hizo huonwa kuwa za wanawake. Hilo linaweza kuwa changamoto. Kwa nini? Dada anayeitwa Rachel anasema hivi: “Mahali ninakotoka ikiwa mume anamsaidia mke wake kuosha vyombo au kusafisha nyumba, majirani na watu wa ukoo watatilia shaka ikiwa yeye ni ‘mwanamume halisi.’ Watafikiri kwamba hawezi kumdhibiti mke wake.” Ikiwa mtazamo huo ni wa kawaida mahali unapoishi, kumbuka kwamba Yesu aliosha miguu ya wanafunzi wake, hata ingawa kazi hiyo ilionwa kuwa ya watumwa. Kichwa kizuri cha familia hahangaikii kuonekana na wengine kuwa yeye ni mtu mwenye mamlaka au muhimu, badala yake anahangaikia furaha ya mke na watoto wake. Zaidi ya kuwa mnyenyekevu, ni sifa gani nyingine iliyo muhimu kwa kichwa kizuri cha familia?

12. Nĩatĩa wendo bũtũmaga Jehova na Jesũ bathithia?

12 Upendo. Kila kitu ambacho Yehova anafanya kinachochewa na upendo. (1 Yoh. 4:7, 8) Kwa upendo, anatuandalia mahitaji yetu ya kiroho kupitia Neno lake Biblia na tengenezo lake. Anatuandalia mahitaji yetu ya kihisia kwa kutuhakikishia kwamba tunapendwa. Na vipi kuhusu mahitaji yetu ya kimwili? Yehova “hutupatia kwa wingi vitu vyote tunavyofurahia.” (1 Tim. 6:17) Tunapokosea anaturekebisha, lakini haachi kutupenda. Kwa upendo, Yehova aliandaa fidia kwa ajili yetu. Naye Yesu anatupenda sana hivi kwamba alitoa uhai wake kwa ajili yetu. (Yoh. 3:16; 15:13) Hakuna kinachoweza kuvunja kifungo cha upendo ambacho Yehova na Yesu wanacho kuelekea wale walio washikamanifu kwao.—Yoh. 13:1; Rom. 8:35, 38, 39.

13. Nĩkĩ bũrĩ ũntũ bwa gĩtũmi kĩongo kĩa nja kwonia nja yaawe wendo? (Tega kathandũkũ “Nĩatĩa Muntũ Mũrũme Ũrĩa Ũgũrene Rua Oomba Gũcionera Gĩtĩo Kuuma Kĩrĩ Mwekũrũ Wawe?”)

13 Somo kwetu. Kila kitu ambacho kichwa cha familia anafanya kinapaswa kuchochewa na upendo. Kwa nini jambo hilo ni muhimu? Mtume Yohana anajibu hivi: “Mtu ambaye hampendi ndugu yake [au mtu wa familia], ambaye amemwona, hawezi kumpenda Mungu ambaye hajamwona.” (1 Yoh. 4:11, 20) Kihususa, mwanamume anayeipenda familia yake na anayetaka kumwiga Yehova na Yesu, ataiandalia familia yake mahitaji ya kiroho, kihisia, na ya kimwili. (1 Tim. 5:8) Atawazoeza na kuwatia nidhamu watoto wake. Pia, ataendelea kujifunza jinsi ya kufanya maamuzi yatakayomletea heshima Yehova na kuinufaisha familia yake. Acheni tuchunguze kila moja ya matakwa hayo na tuone jinsi kichwa cha familia anavyoweza kumwiga Yehova na Yesu.

MANTŨ JARĨA KĨONGO KĨA NJA ABUĨRĨTE KŨTHITHIA

14. Nĩatĩa kĩongo kĩa nja aingagia moobatu ja nja yawe ja gĩkĩrundu?

14 Kuiandalia familia yake mahitaji ya kiroho. Kama tu Baba yake, Yesu pia alihakikisha kwamba wale walio chini ya utunzaji wake wanalishwa vizuri kiroho. (Mt. 5:3, 6; Marko 6:34) Vivyo hivyo, jambo muhimu zaidi kwa kichwa cha familia ni kuiandalia familia yake mahitaji yao ya kiroho. (Kum. 6:6-9) Anafanya hivyo kwa kuhakikisha kwamba yeye na familia yake wanasoma na kujifunza Neno la Mungu, wanahudhuria mikutano, wanahubiri habari njema, na kuimarisha na kudumisha urafiki wao pamoja na Yehova.

15. Nĩ njĩra ĩrĩkũ ĩmwe, kĩongo kĩa nja oomba kwonia nja yawe atĩ nakũmakĩra ũrĩa bakwigua nkorone?

15 Kuiandalia familia yake mahitaji ya kihisia. Yehova alimweleza Yesu waziwazi mbele ya watu kwamba anampenda. (Mt. 3:17) Yesu alionyesha mara kwa mara kwamba anawapenda wafuasi wake kupitia mambo aliyofanya na aliyosema. Wao pia walimwambia kwamba wanampenda. (Yoh. 15:9, 12, 13; 21:16) Kichwa cha familia anaweza kumwonyesha mke na watoto wake kwamba anawapenda kupitia mambo anayofanya, kama vile kujifunza Biblia pamoja nao. Pia, anapaswa kuwaambia kwamba anawapenda na kuwathamini, na inapofaa kuwapongeza mbele ya watu wengine.—Met. 31:28, 29.

Ili kumpendeza Yehova, ni lazima kichwa cha familia aiandalie familia yake mahitaji yao ya kimwili (Tazama fungu la 16)

16. Nĩ ũntũ bũrĩkũ bũngĩ kĩongo kĩa nja abuĩrĩte kũthithia, na nĩatĩa oomba kwonania ũngˈananĩru?

16 Kuiandalia familia yake mahitaji ya kimwili. Yehova aliwaandalia Waisraeli mahitaji ya msingi hata pindi walipokuwa wakiadhibiwa kwa sababu ya kutotii. (Kum. 2:7; 29:5) Pia, anatuandalia mahitaji yetu ya msingi leo. (Mt. 6:31-33; 7:11) Vivyo hivyo, Yesu aliwalisha wale waliomfuata. (Mt. 14:17-20) Pia, aliwaponya wengi waliokuwa wagonjwa. (Mt. 4:24) Ili kumfurahisha Yehova, ni lazima kichwa cha familia aiandalie familia yake mahitaji ya kimwili. Hata hivyo, anahitaji kuwa na usawaziko. Hapaswi kuhangaikia kupita kiasi kazi yake ya kimwili hivi kwamba ashindwe kuiandalia familia yake mahitaji yao ya kiroho na ya kihisia kwa njia nzuri.

17. Nĩ ngerekano ĩrĩkũ Jehova na Jesũ bekĩte, gũkũrũkĩĩra ũrĩa batũritanaga na gũtũkanũkia?

17 Kuwazoeza. Yehova hutuzoeza na kututia nidhamu kwa sababu anataka kutusaidia. (Ebr. 12:7-9) Kama Baba yake, Yesu huwazoeza kwa upendo wale walio chini ya mamlaka yake. (Yoh. 15:14, 15) Yuko thabiti lakini ni mwenye fadhili. (Mt. 20:24-28) Anaelewa kwamba sisi si wakamilifu na tuna mwelekeo wa kukosea.—Mt. 26:41.

18. Nĩ ũntũ bũrĩkũ mũkũrũ ũmwega arĩ kĩongo kĩa nja abuĩrĩte kũriikana?

18 Kichwa cha familia anayemwiga Yehova na Yesu anakumbuka kwamba mke na watoto wake hawajakamilika. ‘Hamkasirikii kwa uchungu’ mke wake na watoto. (Kol. 3:19) Badala yake, anatumia kanuni ambayo inapatikana katika andiko la Wagalatia 6:1 na kujitahidi kuwarekebisha “kwa roho ya upole,” akikumbuka kwamba yeye pia si mkamilifu. Kama Yesu, anatambua kwamba njia bora ya kuwafundisha ni kupitia kielelezo chake kizuri.—1 Pet. 2:21.

19-20. Rĩrĩa agũtua matua, nĩatĩa kĩongo kĩa nja oomba kwigerekania na Jehova na Jesũ?

19 Kufanya maamuzi yasiyo na ubinafsi. Yehova anafanya maamuzi yanayowanufaisha wengine. Kwa mfano, aliamua kutokeza uhai, si kwa faida yake, bali alitaka kushiriki pamoja nasi shangwe ya kuishi. Hakuna ambaye angeweza kumlazimisha Yehova amtoe Mwana wake ili kufunika dhambi zetu. Kwa hiari, aliamua kutoa dhabihu hiyo kwa faida yetu. Yesu pia alifanya maamuzi ambayo lengo kuu lilikuwa ni kuwanufaisha wengine. (Rom. 15:3) Kwa mfano, aliamua kuahirisha kupumzika ili afundishe umati wa watu.—Marko 6:31-34.

20 Kichwa kizuri cha familia anajua kwamba mojawapo ya mambo magumu zaidi ambayo ni lazima afanye, ni kufanya maamuzi ya hekima kwa ajili ya familia yake, na anachukua wajibu huo kwa uzito. Anajitahidi kuepuka kufanya maamuzi yasiyo na msingi mzuri au yanayotegemea tu hisia. Badala yake, anamruhusu Yehova amzoeze. * (Met. 2:6, 7) Kwa njia hiyo, atafikiria kuwanufaisha wengine, na si kujinufaisha mwenyewe.—Flp. 2:4.

21. Nĩmbi tũkairitana kĩthoomone kĩrĩa kĩthingatĩte?

21 Yehova amewapa vichwa vya familia mgawo usio rahisi, naye atawatoza hesabu kwa jinsi wanavyotimiza mgawo huo. Lakini, ikiwa mume anajitahidi kufuata kielelezo kilichowekwa na Yehova na Yesu, atakuwa kichwa kizuri cha familia. Na ikiwa mke anatimiza wajibu wake, ndoa yao itakuwa yenye furaha. Mke anapaswa kuonaje mpango wa ukichwa, naye anakabili changamoto gani? Makala inayofuata itajibu maswali hayo.

RWĨMBO 16 Msifuni Yah kwa Mwana Wake Mtiwa Mafuta

^ gic. 5 Mwanamume anapooa anakuwa kichwa cha familia yake mpya. Katika makala hii, tutazungumzia maana ya ukichwa, kwa nini Yehova alianzisha mpango huo, na wanaume wanaweza kujifunza nini kutokana na mfano uliowekwa na Yehova na Yesu. Katika makala ya pili kwenye mfululizo huu, tutachunguza mambo ambayo mume na mke wanaweza kujifunza kutoka kwa Yesu na mifano mingine ya Biblia. Na makala ya mwisho kwenye mfululizo huu, itazungumzia mpango wa ukichwa kutanikoni.

^ gic. 7 Maoni ya kwamba ni jambo linalokubalika kwa mwanamume kumtendea vibaya mke wake, na hata kumpiga, ni maoni ambayo nyakati nyingine yameonyeshwa kwenye sinema, maigizo, na hata kwenye vitabu vya katuni. Hivyo, utamaduni huo ulioenea huenda umechangia maoni ya kwamba ni sawa kwa mwanamume kumtawala mke wake.

^ gic. 20 Kwa habari zaidi kuhusu jinsi ya kufanya maamuzi mazuri, tazama makala “Fanya Maamuzi Ambayo Yanamletea Mungu Heshima,” katika gazeti la Mnara wa Mlinzi la Aprili 15, 2011, ukurasa wa 13-17.