Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 7

Ukichwa mu Kutaniko

Ukichwa mu Kutaniko

“Kristo ni kichwa cha kutaniko, yeye mwenyewe akiwa mwokozi wa mwili huu.”​—EFE. 5:23.

WIMBO 137 Wanawake Waaminifu, Dada Wakristo

KIFUPI CHA HABARI *

1. Ni sababu gani moja yenye inafanya familia ya Yehova ikuwe na umoja?

TUNAFURAHIA kuwa katika familia ya Yehova. Juu ya nini familia yetu iko na amani na umoja? Sababu moja ni kwamba tunajikaza sana ili kuheshimia mupango wa ukichwa wenye Yehova ameweka. Kadiri tunaelewa muzuri zaidi mupango wa ukichwa, ni vile tunakuwa na umoja zaidi.

2. Hii habari itajibia maulizo gani?

2 Mu hii habari, tutazungumuzia ukichwa mu kutaniko. Tutajibia pia hii maulizo: Namna gani tunapaswa kuona dada zetu? Kila ndugu ni kichwa cha kila dada? Mamlaka yenye wazee wako nayo juu ya ndugu na dada iko sawasawa na mamlaka yenye kichwa cha familia iko nayo juu ya bibi na watoto wake? Tuzungumuzie kwanza namna tunapaswa kuona dada zetu.

NAMNA GANI TUNAPASWA KUONA DADA ZETU?

3. Nini njo itatusaidia tuone dada zetu kuwa wa maana?

3 Tunaona dada zetu kuwa wa maana kwa sababu wanatumika sana ili kuhangaikia familia zao, kuhubiri habari njema, na kusaidia wengine mu kutaniko. Kuchunguza namna Yehova na Yesu wanaona wanamuke, kutatusaidia tuwaone kuwa wa maana. Na kuchunguza namna mutume Paulo alikuwa anatendea wanamuke kutatusaidia pia.

4. Ni mambo gani mu Biblia yenye inaonyesha kama Yehova anaona wanamuke kuwa wa maana sawa vile tu wanaume?

4 Biblia inaonyesha kama Yehova anaona wanamuke kuwa wa maana sawa vile tu wanaume. Kwa mufano, inaonyesha kama mu karne ya kwanza, Yehova alipatia wanaume roho takatifu, lakini alipatia pia wanamuke. Na aliwapatia wote uwezo wa kufanya mambo ya ajabu, sawa vile kuzungumuza mu luga mbalimbali. (Mdo. 2:1-4, 15-18) Yehova ametia mafuta kwa roho yake wanaume na pia wanamuke ili watawale na Kristo. (Gal. 3:26-29) Wanaume na pia wanamuke watapewa zawadi ya uzima wa milele ku dunia. (Ufu. 7:9, 10, 13-15) Tena, wanaume na pia wanamuke wamepewa kazi ya kuhubiri habari njema na kufundisha wengine kweli za Biblia. (Mt. 28:19, 20) Kwa mufano, kitabu cha Matendo kinazungumuzia dada mwenye kuitwa Prisila. Yeye na bwana yake, Akila, walisaidia mwanaume mwenye kuitwa Apolo, mwenye alikuwa na ujuzi sana, aelewe muzuri Maandiko.​—Mdo. 18:24-26.

5. Namna gani Luka 10:38, 39, 42 inaonyesha kama Yesu alikuwa anaheshimia wanamuke?

5 Yesu aliheshimia wanamuke. Hakufuata desturi za Wafarisayo, wenye walikuwa wanazarau wanamuke. Hawakukuwa wanazungumuza nao mbele ya watu, na hawakukuwa hata wanazungumuza nao juu ya Maandiko. Lakini Yesu alizungumuzia mambo ya kiroho pamoja na wanaume na pia wanamuke. * (Soma Luka 10:38, 39, 42.) Tena, aliruhusu wanamuke wamusindikize wakati alikuwa anaenda kuhubiri. (Lu. 8:1-3) Na ni wanamuke njo Yesu alipatia pendeleo la kujulisha mitume wake kama amefufuliwa.​—Yoh. 20:16-18.

6. Namna gani mutume Paulo alionyesha kama aliheshimia wanamuke?

6 Mutume Paulo alimukumbusha Timoteo aheshimie wanamuke. Paulo alimuambia atendee “wanamuke wenye kukomaa kama mama” na aone “vijana wanamuke kama dada.” (1 Ti. 5:1, 2) Paulo alimusaidia sana Timoteo akuwe Mukristo mwenye kukomaa kiroho. Lakini, Paulo alitambua kama ni mama ya Timoteo na tate yake njo walikuwa wa kwanza kumufundisha “maandishi matakatifu.” (2 Ti. 1:5; 3:14, 15) Katika barua yenye aliandikia Waroma, Paulo alisalimia dada mbalimbali, na alitaja kila dada kwa jina. Aliona kazi yenye wale dada walikuwa wamefanya kuwa ya maana, na pia aliwapongeza juu ya kazi yao.​—Ro. 16:1-4, 6, 12; Flp. 4:3.

7. Tuko na lazima ya kupata majibu ya maulizo gani?

7 Vile tuliona mu mafungu yenye ilitangulia, Biblia haiseme kama ndugu ni wa maana zaidi kuliko dada. Dada zetu wenye upendo na wakarimu, wanasaidiaka sana kutaniko, na wazee wanafurahi kuona namna wanasaidia ili kuendeleza amani na umoja mu kutaniko. Lakini, tuko na lazima ya kupata majibu ya maulizo fulani. Kwa mufano: Juu ya nini Yehova anaomba dada afunike kichwa wakati fulani? Juu ndugu tu njo wanawekwa kuwa wazee na watumishi wa huduma, je, ile inamaanisha kama kila ndugu ni kichwa cha kila dada mu kutaniko?

KILA NDUGU NI KICHWA CHA KILA DADA?

8. Kulingana na Waefeso 5:23, kila ndugu ni kichwa cha kila dada? Fasiria.

8 Bila kuenda mbali, jibu ni hapana! Ndugu haiko kichwa cha kila dada mu kutaniko. Yesu njo kichwa cha kila dada. (Soma Waefeso 5:23.) Mu familia, bwana iko na mamlaka juu ya bibi yake. Lakini, mutoto mwanaume mwenye kubatizwa haiko kichwa cha mama yake. (Efe. 6:1, 2) Na mamlaka yenye wazee wako nayo juu ya ndugu na dada mu kutaniko iko na mipaka. (1 Te. 5:12; Ebr. 13:17) Dada wenye hawajaolewa wenye hawaishi tena na wazazi wao wanaendelea kuheshimia wazazi wao na kuheshimia pia wazee. Lakini, sawa vile tu Yesu njo kichwa cha ndugu mu kutaniko, wao pia Yesu tu njo kichwa chao.

Vijana wenye hawajaoa ao kuolewa wenye hawaishi tena na wazazi wao, wako chini ya mamlaka ya Kristo (Ona fungu la 8)

9. Juu ya nini dada wanapaswa kufunika kichwa wakati fulani?

9 Ni kweli kwamba, Yehova amepatia wanaume daraka la kufundisha na kusimamia mambo ingine ya kiroho mu kutaniko. Lakini, hakupatia wanamuke ile daraka. (1 Ti. 2:12) Juu ya nini? Sababu ni ileile yenye ilimufanya aweke Yesu kuwa kichwa cha mwanaume, ni kusema, ili mu familia yake mukuwe utaratibu. Ikiwa kwa sababu fulani dada anapaswa kutimiza daraka lenye kwa kawaida ni la ndugu, Yehova anamuomba afunike kichwa. * (1 Ko. 11:4-7) Yehova anaomba dada wafanye vile, haiko ili kuwashushia heshima, lakini ni juu anapenda waonyeshe kama wanaheshimia kanuni ya ukichwa yenye ameweka. Juu tumeelewa ile mambo yote, tujibie sasa hii ulizo: Mamlaka yenye wazee wako nayo iko sawasawa na mamlaka ya vichwa vya familia?

MAMLAKA YA VICHWA VYA FAMILIA NA YA WAZEE

10. Juu ya nini muzee anaweza kupenda kuwekea ndugu na dada sheria?

10 Wazee wanamupenda Kristo, na wanapenda “kondoo” wenye Yehova na Kristo wamewaomba wachunge. (Yoh. 21:15-17) Bila kuwa na nia ya mubaya, muzee anaweza kujiona kama baba mu kutaniko. Anaweza kuwaza hivi: Vile kichwa cha familia iko na haki ya kuweka sheria ili kulinda familia yake, muzee pia anaweza kuwekea watu wa Mungu sheria zenye anawaza kama zinaweza kuwalinda. Na ndugu na dada fulani wanaweza kuchochea wazee watende vile kwa kuwaomba wawakamatie maamuzi. Lakini, je, mamlaka yenye wazee wako nayo iko sawasawa na mamlaka ya vichwa vya familia?

Wazee wanahangaikia mahitaji ya kiroho ya ndugu na dada na wanafanya wajisikie kuwa wanapendwa. Yehova amewapatia daraka la kuondoa mu kutaniko mutenda-zambi mwenye hatubu (Ona fungu la 11-12)

11. Ni mu njia gani mamlaka ya vichwa vya familia inafanana na mamlaka ya wazee?

11 Mutume Paulo alionyesha kama mu njia fulani mamlaka ya vichwa vya familia inafanana na mamlaka ya wazee. (1 Ti. 3:4, 5) Kwa mufano, Yehova anapenda watu wa familia watii kichwa cha familia. (Kol. 3:20) Na anapenda ndugu na dada mu kutaniko watii wazee. Yehova anaomba vichwa vya familia wahangaikie mahitaji ya kiroho ya watu wa familia zao, na anaomba wazee wahangaikie mahitaji ya kiroho ya ndugu na dada. Wote wanapaswa kufanya wale wenye kuwa chini ya mamlaka yao wajisikie kuwa wanapendwa. Na kama vile kichwa muzuri wa familia, wazee wanapaswa kukamata mipango ili kusaidia ndugu na dada wenye kuwa na magumu. (Yak. 2:15-17) Zaidi ya ile, Yehova anaomba wazee na vichwa vya familia wasaidie wale wenye kuwa chini ya mamlaka yao, kusudi watii kanuni zake na ‘wasipite mambo yenye yaliandikwa’ mu Biblia.​—1 Ko. 4:6.

Vichwa vya familia wamepewa mamlaka na Yehova ili kusimamia mambo mu familia zao. Mbele ya kukamata maamuzi, kichwa cha familia mwenye upendo anatafuta kujua mawazo ya bibi yake (Ona fungu la 13)

12-13. Kama vile Waroma 7:2 inaonyesha, ni katika njia gani mamlaka ya vichwa vya familia iko tofauti na mamlaka ya wazee?

12 Hata vile, mu njia fulani mamlaka ya wazee iko tofauti na mamlaka ya vichwa vya familia. Kwa mufano, Yehova amepatia wazee daraka la kuhukumu na kuondoa mu kutaniko mutenda-zambi mwenye hatubu.​—1 Ko. 5:11-13.

13 Lakini, Yehova amepatia vichwa vya familia mamlaka fulani yenye hakupatia wazee. Kwa mufano, amepatia kichwa cha familia mamlaka ya kuwekea watu wa familia yake sheria na kuhakikisha kama wanafuata zile sheria. (Soma Waroma 7:2.) Kwa mufano, kichwa cha familia iko na haki ya kuamua ni wakati gani watoto wake wanapaswa kurudia ku nyumba mangaribi. Iko pia na mamlaka ya kupatia watoto wake nizamu kama hawatii ile sheria. (Efe. 6:1) Lakini, kichwa cha familia mwenye upendo anatafutaka kujua mawazo ya bibi yake mbele ya kuwekea familia yake sheria; kwa sababu yeye na bibi yake ni “mwili mumoja.” *​—Mt. 19:6.

HESHIMIA KRISTO, KICHWA CHA KUTANIKO

Yesu anaongoza kutaniko la Kikristo chini ya mamlaka ya Yehova (Ona fungu la 14)

14. (a) Kulingana na Marko 10:45, juu ya nini Yehova alikuwa na sababu ya muzuri ya kumufanya Yesu kuwa kichwa cha kutaniko? (b) Baraza Lenye Kuongoza liko na daraka gani? (Ona kisanduku “ Daraka la Baraza Lenye Kuongoza.”)

14 Kupitia bei ya ukombozi, Yehova aliuza uzima wa kila mutu mu kutaniko, na pia uzima wa kila mutu mwenye anaweza kufikia kumuamini Yesu. (Soma Marko 10:45; Mdo. 20:28; 1 Ko. 15:21, 22) Kwa hiyo, kwa sababu Yesu alitoa uzima wake kuwa bei ya ukombozi, Yehova alikuwa na sababu ya muzuri ya kumufanya kuwa kichwa cha kutaniko. Kwa kuwa Yesu njo kichwa chetu, iko na mamlaka ya kuweka sheria juu ya namna kila mutu, kila familia, na kila kutaniko linapaswa kujiendesha. Na iko pia na mamlaka ya kuhakikisha kama tunafuata zile sheria. (Gal. 6:2) Lakini, kazi ya Yesu haiko tu kutuwekea sheria. Anatupatia pia chakula cha kiroho na kutuhangaikia kwa upendo.​—Efe. 5:29.

15-16. Maneno ya dada mwenye kuitwa Marley na ndugu mwenye kuitwa Benjamin inakufundisha nini?

15 Dada wanaonyesha kama wanamuheshimia Kristo wakati wanafuata muongozo wa wanaume wenye ameweka ili kuwahangaikia. Dada wengi wanakubaliana na Marley, mwenye anaishi mu inchi ya Amerika. Anasema hivi: “Niko bibi katika ndoa na dada mu kutaniko. Ninaona ile mambo kuwa ya maana sana. Kila wakati ninapaswa kujikaza ili kuwa na mawazo yenye kufaa juu ya mupango wa ukichwa wenye Yehova ameweka. Lakini bwana yangu na ndugu mu kutaniko wamefanya ikuwe mwepesi kwangu kufanya vile kwa sababu wananiheshimia, na wananishukuru juu ya mambo yenye ninafanya.”

16 Ndugu wanaonyesha kama wanaelewa mupango wa ukichwa wakati wanaheshimia dada mu kutaniko. Benjamin, ndugu mwenye anaishi Uingereza, anasema hivi: “Nimejifunza mambo mingi kupitia maelezo yenye dada wanatoa ku mikutano, na mapendekezo yao kuhusu namna ya kujifunza na namna ya kuhubiri na kufundisha muzuri zaidi. Ninawaza kama mambo yenye wanafanya ni ya maana sana.”

17. Juu ya nini tunapaswa kuheshimia kanuni ya ukichwa?

17 Wakati kila mutu mu kutaniko, ni kusema, wanaume, wanamuke, vichwa vya familia, na wazee, wanaelewa na kuheshimia kanuni ya ukichwa, mu kutaniko munakuwa amani. Na zaidi ya yote, tunamutukuza Baba yetu wa mbinguni mwenye upendo, Yehova.​—Zb. 150:6.

WIMBO 123 Kutii Utaratibu wa Kitheokrasi kwa Ushikamanifu

^ fu. 5 Namna gani tunapaswa kuona dada zetu mu kutaniko? Kila ndugu ni kichwa cha kila dada? Mamlaka yenye wazee wako nayo iko sawasawa na mamlaka ya vichwa vya familia? Mu hii habari, tutaona namna Biblia inajibia ile maulizo.

^ fu. 5 Ona fungu la 6 la habari yenye kichwa “Tutegemeze Dada Zetu Wakristo,” yenye ilitolewa mu Munara wa Mulinzi wa Mwezi wa 9, 2020.

^ fu. 13 Ili kujua mwenye anapaswa kuamua kama familia itakuwa mu kutaniko gani, ona fungu la 17-19 la habari yenye kichwa “Heshimia Kila Mutu mu Kutaniko la Yehova,” yenye ilitolewa mu Munara wa Mulinzi wa Mwezi wa 8, 2020.

^ fu. 59 Ili kupata habari zaidi juu ya mambo ya kufunika kichwa, ona kitabu Mubaki “Katika Upendo wa Mungu,” uku. 209-212.

^ fu. 64 Ili kupata habari zaidi juu ya daraka la Baraza Lenye Kuongoza, ona Munara wa Mulinzi wa tarehe 15 Mwezi wa 7, 2013, uku. 20-25.