Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 11

Namna Maandiko Inatupatia Nguvu ya Kuvumilia Magumu

Namna Maandiko Inatupatia Nguvu ya Kuvumilia Magumu

“Mungu . . . anatoa uvumilivu.”​—RO. 15:5.

WIMBO 94 Aksanti Yehova kwa Kutupatia Neno Yako

KIFUPI CHA HABARI *

1. Watu wa Yehova wako wanapata magumu gani?

KUKO jaribu fulani lenye liko nakuhangaisha? Pengine mutu fulani mu kutaniko alikukwaza. (Yak. 3:2) Ao pengine mutu mwenye unatumikaka naye ao mwanafunzi mwenzako alikuzarau juu unamutumikia Yehova. (1 Pe. 4:3, 4) Ao watu wa familia yako wako wanajaribu kukuzuia kukusanyika ao kuhubiri. (Mt. 10:35, 36) Wakati fulani, kama jaribu iko nguvu sana, unaweza kusikia sawa vile uache tu kumutumikia Yehova. Lakini ukuwe hakika kama hata kama uko na magumu ya namna gani, Yehova atakupatia hekima na nguvu ya kuivumilia.

2. Kulingana na Waroma 15:4, ni mambo gani tutapata wakati tunasoma Neno la Mungu?

2 Yehova alihakikisha kama, mu Biblia, muko mifano yenye kuonyesha namna watu wenye hawakamilike walivumilia magumu. Juu ya nini? Juu tuweze kujifunza kupitia mifano yao. Njo maana Yehova alimuchochea mutume Paulo aandike maneno yenye kuwa mu Waroma 15:4 (Soma). Kusoma zile habari kunaweza kututia moyo na kutupatia tumaini. Lakini, haiko kusoma tu Biblia njo kutatuletea faida. Tunapaswa kuacha maandiko ibadilishe namna yetu ya kufikiri na iguse mioyo yetu. Kwa mufano, kama uko na magumu, na uko na lazima ya mashauri fulani, unaweza kufanya nini? Unaweza kufanya hii mambo ine: (1Usali, (2Uwazie mambo mu akili, (3Ufikiri sana, na (4Utumikishe. Tutaona namna ya kutumikisha ile mambo ine. * Kisha, tutatumikisha ile mambo ine ili kujifunza mambo fulani mu habari ya mufalme Daudi na mutume Paulo.

1. USALI

Mbele uanze kusoma Biblia, umuombe Yehova akusaidie uone wazi faida yenye utapata mu mambo yenye utasoma (Ona fungu la 3)

3. Ni nini unaweza kufanya mbele uanze kusoma Biblia, na juu ya nini?

3 (1Usali. Mbele uanze kusoma Biblia, umuombe kwanza Yehova akusaidie uone wazi faida yenye utapata mu mambo yenye utasoma. Kwa mufano, kama uko na lazima ya mashauri ya kukusaidia kushinda magumu yenye uko nayo, umuombe Yehova akusaidie upate kanuni za Biblia zenye zitakuongoza.​—Flp. 4:6, 7; Yak. 1:5.

2. UWAZIE MAMBO MU AKILI

Pima kufanya sawa vile weye njo ule mutu mwenye kuzungumuziwa mu ile habari (Ona fungu la 4)

4. Ni nini inaweza kukusaidia uone habari ya Biblia yenye uko unajifunza kuwa ya kweli kabisa?

4 (2Uwazie mambo mu akili. Yehova alitupatia uwezo wa ajabu sana wa kuwazia mambo mu akili yetu. Juu ya kufanya habari yenye uko unajifunza ikuwe ya kweli kabisa, pima kuwaza mu akili yako namna mambo ilikuwa, na fanya sawa vile weye njo ule mutu mwenye kuzungumuziwa mu ile habari. Pima kuona mu akili yako mambo yenye ule mutu aliona na pima kujiwazia namna ule mutu alijisikia mu ile hali.

3. UFIKIRI SANA

Waza sana juu ya habari yenye uko unasoma na ona namna inakuhusu (Ona fungu la 5)

5. Kufikiri sana njo nini, na namna gani unaweza kufanya vile?

5 (3Ufikiri sana. Kufikiri sana ni kuwaza sana juu ya habari yenye uko unasoma na kuona namna ile habari inakuhusu. Tena kunakusaidia uone namna mawazo mbalimbali ya ile habari inapatana, na kunakusaidia uelewe muzuri zaidi habari yenye uko unasoma. Kusoma Biblia bila kufikiri sana ni sawa vile kuwa na vyombo vya kinga vyenye viko mu carton bila kuviunganisha. Lakini, kufikiri sana ni sawa vile kuunganisha vile vyombo vyote juu vikuwe kinga. Juu ya kukusaidia ufikiri sana unaweza kujiuliza na kutafuta majibu ya hii maulizo: ‘Ni nini ilisaidia huyu mutu mwenye kuzungumuziwa mu hii habari ashinde magumu yake? Namna gani Yehova alimusaidia? Namna gani habari yenye nimejifunza inaweza kunisaidia nivumilie magumu yangu?’

4. UTUMIKISHE

Utumikishe mambo yenye uko unajifunza, ile itafanya ukamate maamuzi ya muzuri, ukuwe na amani zaidi na ukuwe na imani ya nguvu zaidi (Ona fungu la 6)

6. Juu ya nini tunapaswa kutumikisha mambo yenye tuko tunajifunza?

6 (4Utumikishe. Yesu alisema kama ikiwa hatutumikishe mambo yenye tuko tunajifunza, tutakuwa sawa mutu mwenye anajenga nyumba yake juu ya muchanga. Anatumika sana, lakini anapoteza wakati yake bure. Juu ya nini tunasema vile? Juu, wakati upepo na mafuriko vitapiga nyumba yake, itaharibika kabisa. (Mt. 7:24-27) Ni vile pia kama tunasali, tunajiwazia mu akili mambo yenye tuko tunasoma, na tunafikiri sana juu ya ile mambo yenye tuko tunasoma, lakini hatuitumikishe, ile ni kupoteza tu wakati bure. Na wakati imani yetu itajaribiwa ao wakati tutapata mateso, hatutakuwa na nguvu ya kuivumilia. Lakini, kama tunajifunza, na kutumikisha mambo yenye tuko tunajifunza, tutakamata maamuzi ya muzuri, tutakuwa na amani zaidi na pia imani ya nguvu zaidi. (Isa. 48:17, 18) Tutumikishe sasa ile mambo ine yenye tumetoka tu kuzungumuzia wakati tuko tunachunguza mambo fulani yenye ilimupata Mufalme Daudi.

MUFANO WA MUFALME DAUDI UNAWEZA KUTUFUNDISHA NINI?

7. Ni habari gani ya Biblia yenye tutazungumuzia sasa?

7 Kuko rafiki ao mutu wa familia mwenye amekukwaza? Kama ni vile, habari yenye inazungumuzia Absalomu, mwana wa Mufalme Daudi, inaweza kukusaidia. Absalomu alimusaliti baba yake na alijaribu kuwa mufalme.​—2 Sa. 15:5-14, 31; 18:6-14.

8. Unaweza kufanya nini juu upate musaada wa Yehova?

8 (1Usali. Ukiwa na ile habari mu akili, umuambie Yehova vile walikutendea mubaya na namna unajisikia. (Zb. 6:6-9) Umuambie Yehova waziwazi namna uko unajisikia. Kisha umuombe Yehova akuonyeshe kanuni za Biblia zenye zinaweza kukusaidia ujue namna ya kupambana na ile hali.

9. Fasiria kwa kifupi mambo yenye ilitokea kati ya Daudi na Absalomu.

9 (2Uwazie mambo mu akili. Fikiria namna mambo ilikuwa na upime kuwaza mu akili yako namna Mufalme Daudi alijisikia. Absalomu, mwana wa Daudi, alitumika miaka mingi juu ya kufanya watu wamupende. (2 Sa. 15:7) Saa aliona kama wakati unafaa, Absalomu alituma wapelelezi katika Israeli yote, ili watayarishe watu wamukubali kuwa mufalme wao. Na hata alimusadikisha Ahitofeli, mwenye alikuwa kati ya marafiki na washauri wa karibu sana wa Mufalme Daudi, ili amuunge mukono katika uasi wake. Absalomu alijitangaza kuwa mufalme, na kisha, akajaribu kumukamata na kumuua Daudi. Na inawezekana ile wakati Daudi alikuwa mugonjwa sana. (Zb. 41:1-9) Daudi alifikia kujua mambo yenye Absalomu alikuwa anapanga kufanya, na kisha akatoka Yerusalemu na kukimbia. Kisha maaskari wa Absalomu walipigana na maaskari wenye walibakia ngambo ya Daudi. Lakini maaskari wa Absalomu wakashindwa na kisha, Absalomu mwana wa Daudi akauawa.

10. Ni mambo gani yenye pengine Daudi angefanya?

10 Sasa, pima kuwaza mu akili yako namna Daudi alijisikia kisha ile mambo yote kumufikia. Alimupenda sana Absalomu na alimutumainia sana Ahitofeli. Lakini, wote wawili walimusaliti. Walimulumisha roho sana, na walijaribu hata kumuua. Ile ingefanya Daudi aache kutumainia marafiki wake wengine, na kuanza kuwaza kama wao pia walimuunga mukono Absalomu. Pengine angeanza kujitumainia tu yeye peke na kujaribu kukimbia yeye peke bila watu wengine. Ao pengine angevunjika moyo sana. Daudi hakufanya ile mambo yote. Lakini, alishinda ile jaribu. Nini njo ilimusaidia aweze?

11. Daudi alifanya nini wakati alikuwa mu magumu?

11 (3Ufikiri sana. Ni kanuni gani unapata mu hii habari? Jibia hii ulizo, “Daudi alifanya nini?” Hakukuwa na wasiwasi na hakufanya mambo haraka-haraka bila kufikiri. Tena hakuogopa sana mupaka ashindwe kujua jambo la kufanya. Lakini, alimuomba Yehova amusaidie. Aliomba pia marafiki wake wamusaidie. Lakini bila kuchelewa alifanya mambo yenye aliamua kufanya. Hata kama Daudi alikuwa na huzuni sana, hakuacha kutumainia wengine na aliepuka kuwa na chuki. Aliendelea kumutumainia Yehova na kutumainia marafiki wake.

12. Namna gani Yehova alimusaidia Daudi?

12 Namna gani Yehova alimusaidia Daudi? Kama unachunguza maandiko, utaona kama Yehova alimupatia Daudi nguvu yenye alikuwa nayo lazima juu ya kuvumilia jaribu lake. (Zb. 3:1-8; utangulizi) Yehova alibariki maamuzi yenye Daudi alikamata. Na alitegemeza pia marafiki waaminifu wenye walibakia na Daudi wakati walikuwa wanapigana vita juu ya kumulinda mufalme wao.

13. Mufano wa Daudi unaweza kukusaidia namna gani wakati mutu fulani anakukwaza sana? (Matayo 18:15-17)

13 (4Utumikishe. Ujiulize hivi, ‘Namna gani naweza kufuata mufano wa Daudi?’ Ni muzuri utende haraka juu ya kumaliza tatizo fulani. Kulingana na hali, unaweza kutumia shauri la Yesu lenye kuwa mu Matayo sura ya 18. Unaweza kufanya tu vile ile shauri ya Yesu inasema ao kutumia kanuni yenye kuwa mu ile shauri. (Soma Matayo 18:15-17.) Lakini, epuka kukamata maamuzi fulani wakati ulishakasirika. Umuombe Yehova akusaidie utulie na akupatie hekima yenye uko nayo lazima juu ujue jambo la kufanya. Usiache kutumainia marafiki wako. Lakini, ukuwe tayari kukubali musaada wao. (Mez. 17:17) Na jambo la maana zaidi, endelea kufuata mashauri ya Yehova yenye kuwa mu Neno lake.​—Mez. 3:5, 6.

MUFANO WA MUTUME PAULO UNAWEZA KUTUFUNDISHA NINI?

14. Ni mu hali gani 2 Timoteo 1:12-16; 4:6-11, 17-22 inaweza kukutia moyo?

14 Watu wa familia yako, wako wanakupinga juu uko unamutumikia Yehova? Ao uko unaishi mu inchi yenye kazi yetu ilishatiliwa vizuizi sana ao imefikia hata kukatazwa? Kama ni vile, utatiwa moyo kwa kusoma 2 Timoteo 1:12-16 na 4:6-11, 17-22. * Paulo aliandika hii sehemu ya maandiko wakati alikuwa mu gereza.

15. Unaweza kumuomba Yehova nini?

15 (1Usali. Mbele ya kusoma ile mistari, umuambie Yehova waziwazi magumu yako na namna uko unajisikia. Kisha umuombe akusaidie utambue kanuni zenye kuzungumuziwa mu habari yenye inaonyesha magumu yenye Paulo alipata. Ile itakusaidia na wewe ujue namna ya kutenda wakati unapata magumu.

16. Fasiria kwa kifupi hali yenye ilimufikia mutume Paulo.

16 (2Uwazie mambo mu akili. Pima kujitia mu hali ya Paulo. Iko mu gereza kule Roma na alishafungwa minyororo. Alishakafungwa mu gereza, lakini mara hiyo, iko hakika kama atauawa. Tena, marafiki wake fulani walishamuacha, na yeye alishachoka sana kimwili.​—2 Ti. 1:15.

17. Pengine Paulo angetenda namna gani?

17 Pengine Paulo angekaza akili juu ya mambo ya zamani na kuwaza kama, ikiwa hangekuwa Mukristo mwenye bidii, pengine hangefungwa. Angekasirikia wanaume fulani wa mu jimbo la Asia wenye walimuacha na pengine angeacha kutumainia marafiki wake wengine. Lakini, Paulo hakufanya ile mambo yote. Ni nini ilimuhakikishia Paulo kama marafiki wake hawangemuacha na kama Yehova angemupatia zawabu?

18. Paulo alifanya nini wakati alikuwa na magumu?

18 (3Ufikiri sana. Jibia hii ulizo, “Paulo alifanya nini ili kupiganisha magumu yake?” Hata kama alikuwa anaona kifo mbele yake, Paulo hakusahau kama ni jambo la maana sana kumuletea Yehova utukufu. Na aliendelea kufikiria namna angetia moyo wengine. Alimutegemea Yehova kwa kusali kila mara. (2 Ti. 1:3) Paulo hakuendelea kufikiri sana juu ya ndugu wenye walimuacha, lakini alisema kama alishukuru sana marafiki wake wenye waliendelea kumusaidia na kumutegemeza kwa upendo. Tena, Paulo aliendelea kujifunza Neno la Mungu. (2 Ti. 3:16, 17; 4:13) Na zaidi ya yote, alikuwa hakika kabisa kama Yehova na Yesu wanamupenda. Hawakumuacha, na Paulo alikuwa hakika kama wangemupatia zawabu juu ya utumishi wake wenye alifanya kwa uaminifu.

19. Yehova alimusaidia Paulo namna gani?

19 Yehova alimuambia Paulo mbele ya wakati kama angepata mateso juu alikuwa Mukristo. (Mdo. 21:11-13) Sasa Yehova alimusaidia Paulo namna gani? Yehova alijibia sala za Paulo na alimutia nguvu. (2 Ti. 4:17) Paulo alihakikishiwa kama angepata zawabu yenye alitumikia kwa bidii. Tena, Yehova alimusaidia Paulo kupitia marafiki wake waaminifu.

20. Kulingana na Waroma 8:38, 39, namna gani tunaweza kuiga imani yenye Paulo alionyesha?

20 (4Utumikishe. Ujiulize hivi: ‘Namna gani naweza kufuata mufano wa Paulo?’ Kama vile Paulo, tunapaswa kujua kama tutateswa juu tuko tunamutumikia Yehova. (Mk. 10:29, 30) Kama tunapenda kubakia waaminifu kwa Yehova wakati wa magumu, tunapaswa kuendelea kusali kwake na kujifunza Neno lake kwa ukawaida. Na tusisahau hata kidogo kama jambo la maana zaidi lenye tunaweza kufanya ni kumuletea Yehova utukufu. Tukuwe hakika kama Yehova hatatuacha hata kidogo na kama hakuna mutu mwenye anaweza kumufanya Yehova aache kutupenda.​—Soma Waroma 8:38, 39; Ebr. 13:5, 6.

UJIFUNZE KUPITIA MIFANO YA WATUMISHI WAAMINIFU WENYE KUTAJWA MU BIBLIA

21. Ni nini ilisaidia Aya na Hector washinde magumu yao?

21 Mifano yenye kuwa mu Biblia inaweza kutusaidia tupate nguvu yenye tuko nayo lazima ili kuvumilia kila hali. Hata tukuwe mu hali gani, mifano ya mu Biblia inaweza kutusaidia tupate nguvu yenye tuko nayo lazima ili kuvumilia. Kwa mufano, Aya, painia mumoja wa Japani, alisema kama hadisi ya Yona ilimusaidia kushinda woga wenye alikuwa nao wa kuhubiri fasi ya watu wengi. Kijana Hector, mwenye anaishi Indonesia na mwenye wazazi wake hawako Mashahidi wa Yehova, anasema kama mufano wa Rutu ulimuchochea ajifunze mengi zaidi juu ya Yehova na amutumikie.

22. Unaweza kufanya nini ili usomaji wa Biblia wenye kuchezwa ao sehemu “Tuige Imani Yao” ikuletee faida?

22 Ni wapi tunaweza kupata mifano ya Biblia yenye inaweza kututia nguvu? Video zetu, usomaji wa Biblia wenye kuchezwa na sehemu “Tuige Imani Yao” vinaweza kutusaidia tuelewe muzuri zaidi habari za Biblia. * Mbele ya kuangalia, kusikiliza, ao kusoma zile habari zenye zilitayarishwa muzuri kabisa, umuombe Yehova akusaidie upate mambo fulani yenye unaweza kutumikisha mu hali yako. Ufanye sawa vile weye njo ule mutu mwenye kuzungumuziwa sana mu ile habari. Ufikiri sana juu ya mambo yenye wale watumishi waaminifu wa Yehova walifanya na namna Yehova aliwasaidia washinde magumu yao. Kisha, utumikishe mambo yenye unajifunza mu hali yako. Umushukuru Yehova kwa musaada wenye tayari iko anakupatia. Na uonyeshe shukrani yako kwa kutafuta njia za kusaidia na kutia moyo wengine.

23. Kulingana na Isaya 41:10, 13, Yehova anatupatia ahadi gani?

23 Haiko mwepesi kuishi mu hii dunia yenye kutawaliwa na Shetani, na wakati fulani tunaweza kukosa hata kujua mambo ya kufanya. (2 Ti. 3:1) Lakini ile haipaswe kutuhangaisha sana ao kutuogopesha. Yehova anajua magumu yenye tuko nayo. Wakati tuko na lazima ya musaada, Yehova anatuahidi kama atatushika kwa mukono wake wa kuume wenye nguvu. (Soma Isaya 41:10, 13.) Kwa hiyo, tuko hakika kama Yehova atatusaidia na pia Maandiko itatupatia nguvu yenye tuko nayo lazima ili kuvumilia magumu, hata ikuwe ya namna gani.

WIMBO 96 Biblia Ni Kitabu ya Maana Sana

^ fu. 5 Habari mingi zenye kuwa mu Biblia zinatuhakikishia kama Yehova anapenda watumishi wake na kama atawasaidia hata kama wako mu magumu gani. Hii habari inaonyesha nini unaweza kufanya ili habari zenye uko unasoma mu funzo lako la Biblia zikuletee faida.

^ fu. 2 Ile mambo ine yenye tumetaja iko kati ya mambo ingine mingi yenye unaweza kutumia. Mambo ingine yenye unaweza kutumia ili kujifunza Biblia inapatikana mu kitabu Musaada wa Kutafuta Habari kwa Ajili ya Mashahidi wa Yehova kwenye kichwa “Biblia” chini ya kichwa kidogo “Kusoma na Kuelewa Biblia.”

^ fu. 14 Musisome hii maandiko wakati wa funzo la Munara wa Mulinzi mu kutaniko.

^ fu. 22 Ona sehemu “Tuige Imani Yao​—Wanaume na Wanamuke Wenye Kuzungumuziwa mu Biblia” yenye kuwa ku jw.org. (Fungua MAFUNDISHO YA BIBLIA > IMANI KATIKA MUNGU.)