Ĩta kĩrĩ birĩa birĩ ndeene

Ĩta kĩrĩ birĩa birĩ ndeene

KĨTHOOMO GĨA KWIRITANA KĨA 9

Antũ Babeethĩ—Nĩatĩa Bũũmba Kũthithia Nĩkenda Bangĩ Babwĩtĩkia?

Antũ Babeethĩ—Nĩatĩa Bũũmba Kũthithia Nĩkenda Bangĩ Babwĩtĩkia?

“Kwĩna njũũrĩ ya antũ babeethĩ ta ĩme.” —ZAB. 110:3, NWT.

RWĨMBO 39 Jifanyie Jina Zuri Mbele za Mungu

MUHTASARI *

1. Atana ba baaba babeethĩ barĩ na ũũmbi bũrĩkũ?

NDUGU vijana, mnaweza kutimiza mengi. Wengi wenu mna nguvu na nishati nyingi. (Met. 20:29) Mnafanya mambo mengi ili kuwasaidia ndugu na dada zenu kutanikoni. Huenda mnatazamia kwa hamu wakati mtakapowekwa rasmi kuwa watumishi wa huduma. Hata hivyo, huenda mkahisi wengine wanaona kwamba mna umri mdogo sana au hamna uzoefu wa kutosha ili kukabidhiwa kazi muhimu. Hata ingawa nyinyi ni vijana, kuna mambo mnayoweza kufanya sasa ili wengine kutanikoni wawaamini na kuwaheshimu.

2. Nĩmbi tũkarĩĩria kĩthoomone gĩkĩ?

2 Katika makala hii, tutakazia fikira maisha ya Mfalme Daudi. Pia, tutapitia kwa ufupi matukio katika maisha ya Asa na Yehoshafati—wafalme wawili wa Yuda. Tutachunguza changamoto mbalimbali ambazo wanaume hao watatu walikabili, jinsi walivyotenda, na mambo ambayo ndugu vijana wanaweza kujifunza kutokana na mfano wao.

IRITANE KUUMANIA NA MŨNENE DAUDI

3. Nĩ njĩra ĩrĩkũ ĩmwe antũ babeethĩ boomba gũtetheeria antũ baakũrũ kĩũthũranone?

3 Alipokuwa kijana, Daudi alijifunza stadi ambazo wengine walizithamini. Ni wazi kwamba alikuwa mtu wa kiroho, na aliboresha ustadi wake akiwa mwanamuziki na alitumia kipawa hicho kumnufaisha Sauli, mfalme aliyewekwa rasmi na Mungu. (1 Sam. 16:16, 23) Enyi wanaume vijana, je, mna ustadi fulani ambao unaweza kuwanufaisha wengine kutanikoni? Wengi wenu mna ustadi fulani. Kwa mfano, huenda mmetambua kwamba baadhi ya ndugu na dada wenye umri mkubwa, wanathamini kuonyeshwa jinsi ya kutumia vizuri zaidi tablet zao na vifaa vingine vya kielektroni wanavyotumia kwa ajili ya kujifunza kibinafsi na mikutanoni. Ujuzi wenu wa kutumia vifaa hivyo unaweza kuwanufaisha sana ndugu na dada hao wenye umri mkubwa.

Daudi alithibitika kuwa mwenye kutegemeka alipokuwa akiwatunza kondoo wa baba yake, hata aliwalinda dhidi ya shambulizi la dubu (Tazama fungu la 4)

4. Ta Daudi, nĩ nkuma irĩkũ antũ babeethĩ boomba gũkũria? (Tega mbica karatacine ka mbere.)

4 Katika maisha yake ya kila siku, Daudi alithibitika kuwa mwenye kutegemeka. Kwa mfano, akiwa kijana, alifanya kazi kwa bidii ili kuwatunza kondoo wa baba yake. Huo ulikuja kuwa mgawo hatari. Baadaye, Daudi alimwambia hivi Mfalme Sauli: “Mimi mtumishi wako nimekuwa nikichunga kondoo wa baba yangu, na simba akaja, na pia dubu, na kila mmoja wao akamchukua kondoo kutoka kundini. Nilimfuata, nikamuua na kumwokoa kondoo kutoka kinywani mwake.” (1 Sam. 17:34, 35) Daudi alihisi kwamba alikuwa na wajibu wa kuwatunza kondoo hao, naye alipambana ili kuwalinda. Ndugu vijana wanaweza kumwiga Daudi kwa kutimiza kwa bidii mgawo wowote wanaopewa.

5. Kũringana na Zaburi 25:14, nĩ ũntũ bũrĩkũ bwa gĩtũmi nkũrũki antũ babeethĩ boomba kũthithia?

5 Kijana Daudi alisitawisha uhusiano wa kibinafsi na wa karibu pamoja na Yehova. Uhusiano huo ulikuwa muhimu zaidi kuliko ujasiri ambao Daudi alikuwa nao au ustadi wake wa kupiga kinanda. Yehova hakuwa tu Mungu wa Daudi, bali pia alikuwa Rafiki yake—Rafiki yake wa karibu. (Soma Zaburi 25:14.) Enyi ndugu vijana, jambo muhimu zaidi mnaloweza kufanya ni kuimarisha uhusiano wenu pamoja na Baba yenu wa mbinguni, na mnapofanya hivyo huenda mkapata mapendeleo zaidi.

6. Nĩ mwonere jũrĩkũ jũmũthũũku bamwe baarĩ naju jwegie Daudi?

6 Daudi alihitaji kushinda maoni yasiyofaa ambayo wengine walikuwa nayo kumhusu. Kwa mfano, Daudi alipojitolea kwenda kupigana na Goliathi, Mfalme Sauli alijaribu kumvunja moyo akisema: “Wewe ni mvulana tu.” (1 Sam. 17:31-33) Awali, ndugu yake mkubwa alimshutumu kuwa hachukui majukumu yake kwa uzito. (1 Sam. 17:26-30) Hata hivyo, Yehova hakumwona Daudi kama mvulana tu ambaye hajakomaa au asiyechukua majukumu yake kwa uzito. Alimjua vizuri kijana huyo. Na alipomtegemea Yehova Rafiki yake, ili kupata nguvu, Daudi alimuua Goliathi.—1 Sam. 17:45, 48-51.

7. Nĩmbi ũũmba kwiritana kuumania na mantũ ja Daudi?

7 Tunaweza kujifunza nini kutokana na kisa cha Daudi? Tunajifunza kwamba tunahitaji kuwa na subira. Huenda ikachukua muda kwa wale ambao wamekujua tangu ukiwa mtoto kuanza kukuona kama kijana mkomavu. Hata hivyo, unaweza kuwa na hakika kwamba Yehova hakazii tu jinsi unavyoonekana kwa nje. Anakujua vizuri na anajua mambo unayoweza kufanya. (1 Sam. 16:7) Imarisha uhusiano wako na Mungu. Daudi alifanya hivyo kwa kuchunguza vitu ambavyo Yehova ameumba. Daudi alifikiria kwa kina mambo ambayo vitu hivyo vinafunua kumhusu Muumba. (Zab. 8:3, 4; 139:14; Rom. 1:20) Jambo lingine unaloweza kufanya ni kumwomba Yehova akupe nguvu unazohitaji. Kwa mfano, je, baadhi ya wanafunzi wenzako wanakudhihaki kwa sababu wewe ni Shahidi wa Yehova? Ikiwa ndivyo, sali kwa Yehova ili akusaidie kukabiliana na changamoto hiyo. Na utumie ushauri hususa unaopata kwenye Neno lake na katika video na machapisho yetu yanayotegemea Biblia. Kila mara unapoona jinsi Yehova anavyokusaidia kukabiliana na changamoto fulani, uhakika wako kwake utaongezeka. Zaidi ya hilo, kadiri wengine wanavyoona jinsi unavyomtegemea Yehova, ndivyo watakavyokuamini zaidi.

Kwa unyenyekevu, ndugu vijana wanaweza kuwasaidia wengine kwa njia nyingi (Tazama fungu la 8 na 9)

8-9. Nĩmbi yateetherie Daudi kwĩthĩrwa na weteeri mwanka rĩrĩa ambĩrĩrie gũtumĩka arĩ Mũnene, na nĩmbi atana ba baaba babeethĩ boomba kwiritana kuumania na ngerekano yawe?

8 Fikiria changamoto nyingine ambayo Daudi alikabili. Baada ya kutiwa mafuta kuwa mfalme, Daudi alihitaji kusubiri kwa miaka mingi kabla ya kuanza kutawala rasmi akiwa mfalme wa Yuda. (1 Sam. 16:13; 2 Sam. 2:3, 4) Ni nini kilichomsaidia kungojea kwa subira katika kipindi hicho? Badala ya kuruhusu hisia za kuvunjika moyo zimzuie kutenda, Daudi alikazia fikira mambo ambayo angeweza kufanya. Kwa mfano, alipokuwa akiishi akiwa mkimbizi katika eneo la Wafilisti, Daudi alitumia fursa hiyo kupigana na maadui wa Waisraeli. Kwa kufanya hivyo, alilinda mipaka ya eneo la Yuda.—1 Sam. 27:1-12.

9 Ndugu vijana wanaweza kujifunza nini kutokana na kielelezo cha Daudi? Tumieni fursa mlizo nazo kuwatumikia ndugu zenu. Fikiria kisa cha ndugu anayeitwa Ricardo. * Tangu alipokuwa na umri wa miaka 10 hivi, alikuwa na ndoto ya kutumikia akiwa painia wa kawaida. Lakini wazee walimwambia kwamba hakuwa tayari. Badala ya kufa moyo au kukasirika, Ricardo aliongeza wakati aliotumia katika huduma. Anasema hivi: “Ninapokumbuka wakati uliopita, ninatambua kwamba nilihitaji kufanya maendeleo. Na nikazia fikira kufuatia upendezi wowote niliopata katika huduma na kuwa na ziara za kurudia zenye matokeo. Hata niliongoza funzo langu la kwanza la Biblia. Kadiri nilivyopata uzoefu, ndivyo nilivyojiamini zaidi.” Sasa Ricardo anatumikia akiwa painia wa kawaida mwenye matokeo na pia mtumishi wa huduma.

10. Ĩgiita rĩmwe, nĩatĩa Daudi athithĩrie mbere ya atua matua ja gĩtũmi?

10 Fikiria jambo lingine lililotukia katika maisha ya Daudi. Pindi fulani Daudi na wanaume wake walipokuwa katika eneo la Wafilisti wakimkimbia Sauli, waliacha familia zao na kwenda kupigana vita. Wanaume hao walipokuwa wameondoka, maadui walivamia nyumba zao na kuteka familia zao. Daudi angeweza kufikia mkataa kwamba kwa kuwa alikuwa shujaa wa vita mwenye uzoefu, angeweza kupanga kirahisi mkakati wa kuwakomboa mateka. Badala ya kufanya hivyo, Daudi alitafuta mwongozo kutoka kwa Yehova. Kwa msaada wa kuhani aliyeitwa Abiathari, Daudi alimuuliza hivi Yehova: “Je, nilifuatie kundi hili la wavamizi?” Yehova alimwambia Daudi alipaswa kufanya hivyo na akamhakikishia kwamba angefanikiwa. (1 Sam. 30:7-10) Unaweza kujifunza nini kutokana na kisa hicho?

Ndugu vijana wanapaswa kutafuta ushauri wa wazee wa kutaniko (Tazama fungu la 11)

11. Nĩatĩa ũũmba kũthithia mbere ya ũtua matua?

11 Tafuta ushauri kabla ya kufanya maamuzi. Waulize wazazi wako. Unaweza pia kupata ushauri mzuri kwa kuzungumza na mzee wa kutaniko mwenye uzoefu. Yehova anawatumaini wanaume hao waliowekwa rasmi, nawe unaweza kufanya vivyo hivyo pia. Yehova anawaona kuwa “zawadi” kwa kutaniko. (Efe. 4:8) Utanufaika kwa kuiga imani yao na kwa kusikiliza mapendekezo yenye hekima wanayokupa. Sasa acheni tuchunguze mambo tunayoweza kujifunza kutoka kwa Mfalme Asa.

IRITANE KUUMANIA NA MŨNENE ASA

12. Nĩ nkuma irĩkũ Mũnene Asa arĩ nacio rĩrĩa ambĩrĩrie kwathana?

12 Alipokuwa kijana, Mfalme Asa alikuwa mnyenyekevu na jasiri. Kwa mfano, aliporithi ufalme kutoka kwa Abiya, baba yake, alianzisha kampeni dhidi ya ibada ya sanamu. Pia, “aliwaambia watu wa Yuda wamtafute Yehova Mungu wa mababu zao na kushika Sheria na amri.” (2 Nya. 14:1-7) Na Zera Mwethiopia alipovamia Yuda akiwa na wanajeshi 1,000,000, kwa hekima Asa alimgeukia Yehova ili kuomba msaada, akisema: “Ee Yehova, haijalishi kwako ikiwa wale unaowasaidia ni wengi au hawana nguvu. Tusaidie, Ee Yehova Mungu wetu, kwa maana tunakutegemea wewe.” Maneno hayo mazuri sana yanaonyesha jinsi ambavyo Asa alikuwa na uhakika katika uwezo wa Yehova wa kumwokoa yeye na watu wake. Asa alimtumaini Baba yake wa mbinguni, na “Yehova akawashinda Waethiopia.”—2 Nya. 14:8-12.

13. Nĩ ũntũ bũrĩkũ nyumene bwagwatĩre Asa, na nĩkĩ?

13 Bila shaka, utakubali kwamba kukabili jeshi lenye askari 1,000,000 ilikuwa changamoto kubwa—changamoto ambayo Asa alifanikiwa kuishinda. Hata hivyo, kwa kusikitisha, Asa alipokabili changamoto nyingine iliyokuwa ndogo kuliko hiyo, hakumtafuta Yehova. Alipotishwa na Baasha, mfalme mwovu wa Israeli, Asa alimgeukia mfalme wa Siria ili kutafuta msaada. Uamuzi huo ulikuwa na matokeo mabaya sana! Kupitia nabii Hanani, Yehova alimwambia hivi Asa: “Kwa sababu ulimtegemea mfalme wa Siria nawe hukumtegemea Yehova Mungu wako, jeshi la mfalme wa Siria limeponyoka kutoka mikononi mwako.” Isitoshe, tangu wakati huo na kuendelea Asa alikuwa akipigana vita kwa ukawaida. (2 Nya. 16:7, 9; 1 Fal. 15:32) Tunajifunza nini?

14. Nĩatĩa ũũmba kwĩrĩgĩĩra Jehova, na kũringana na 1 Timotheo 4:12, gũkeethĩrwa na maumĩĩra jarĩkũ?

14 Endelea kuwa mnyenyekevu na kumtumaini Yehova. Ulipobatizwa, ulionyesha imani kubwa na ulionyesha kwamba unamtumaini Yehova. Na Yehova alifurahi kukukabidhi pendeleo la kuwa miongoni mwa washiriki wa familia yake. Jambo kuu sasa ni kuendelea kumtegemea Yehova. Huenda ikaonekana kuwa rahisi kumtegemea Yehova unapofanya maamuzi mazito maishani, lakini vipi kuhusu nyakati nyingine? Ni muhimu sana kumtumaini Yehova unapofanya maamuzi, hata yale yanayohusu burudani, kazi ya kimwili, na malengo yako maishani! Usitegemee hekima yako mwenyewe. Badala yake, tafuta kanuni za Biblia zinazohusu hali yako, kisha utende kulingana na mwongozo uliopata. (Met. 3:5, 6) Ukifanya hivyo, utamfanya Yehova afurahi na utajipatia heshima kutoka kwa wengine kutanikoni.—Soma 1 Timotheo 4:12.

IRITANE KUUMANIA NA MŨNENE JEHOSHAFATU

15. Ja ũrĩa ĩandĩko rĩa 2 Mantu ja Karaja 18:1-3; 19:2 ĩkwonania, Mũnene Jehoshafatu athithĩrie maatia jarĩkũ?

15 Bila shaka, kama tu sisi sote, wewe pia si mkamilifu, na nyakati nyingine utakosea. Hata hivyo, jambo hilo halipaswi kukuzuia kufanya yote unayoweza katika utumishi wa Yehova. Fikiria mfano wa Mfalme Yehoshafati. Alikuwa na sifa nyingi nzuri. Alipokuwa kijana, “alimtafuta Mungu wa baba yake na kufuata amri yake.” Zaidi ya hayo, aliwatuma wakuu wazunguke majiji ya Yuda ili kuwafundisha watu kumhusu Yehova. (2 Nya. 17:4, 7) Ingawa Yehoshafati alikuwa mnyoofu, nyakati nyingine alifanya maamuzi mabaya. Kwa sababu ya uamuzi fulani mbaya, Yehoshafati alipewa shauri na mmoja wa wawakilishi wa Yehova. (Soma 2 Mambo ya Nyakati 18:1-3; 19:2.) Unaweza kujifunza nini kutokana simulizi hilo?

Ndugu vijana wenye bidii na wanaotegemeka hujipatia sifa nzuri (Tazama fungu la 16)

16. Nĩmbi ũũmba kwiritana kuumania na ũtũũro bwa Rajeev?

16 Kubali na utumie shauri. Labda, kama vijana wengi, si rahisi kwako kutanguliza utumishi wa Yehova maishani mwako. Lakini usivunjike moyo. Fikiria kisa cha ndugu kijana anayeitwa Rajeev. Akirejelea kipindi alipokuwa na umri wa miaka kati ya 13 na 19, Rajeev anasema hivi: “Nyakati nyingine sikujua nilichotaka kufanya maishani. Kama vijana wengine wengi, nilipendezwa zaidi na michezo na kufurahia maisha kuliko kwenda kwenye mikutano au kwenda katika huduma.” Ni nini kilichomsaidia Rajeev? Mzee wa kutaniko mwenye kujali alimpa shauri. Rajeev anasema hivi: “Alinisaidia kutafakari kuhusu kanuni inayopatikana kwenye 1 Timotheo 4:8.” Rajeev alipokea shauri hilo kwa unyenyekevu na kutathmini upya mambo aliyotanguliza maishani. Anasema hivi: “Niliamua kutanguliza malengo ya kiroho maishani.” Matokeo yakawaje? Rajeev anaeleza hivi: “Miaka michache baada ya kupata shauri hilo, nilistahili kutumikia nikiwa mtumishi wa huduma.”

GWĨRIA BAABA WAKU WA ĨGŨRŨ

17. Antũ baakũrũ nĩatĩa baigagua bwegie atana ba baaba babeethĩ barĩa bagũtumĩkĩra Jehova?

17 Ndugu na dada wenye umri mkubwa wanawathamini sana ninyi ndugu vijana mnaomtumikia Yehova “bega kwa bega” pamoja nao! (Sef. 3:9) Wanapenda jinsi mnavyofanya kazi mnazopewa kwa bidii, kwa nguvu, na kwa shauku. Mmepata kibali machoni pao.—1 Yoh. 2:14.

18. Ja ũrĩa Njuno 27:11 ĩkwonania, nĩatĩa Jehova aigagua rĩrĩa atana ba baaba babeethĩ bakũmũtumĩkĩra?

18 Enyi ndugu vijana, msisahau kamwe kwamba Yehova anawapenda na kuwatumaini. Alitabiri kwamba katika siku za mwisho, kungekuwa na jeshi la vijana ambao wangejitoa kwa hiari. (Zab. 110:1-3) Anajua kwamba mnampenda na mnataka kumtumikia kwa uwezo wenu wote. Hivyo, waonyeshe wengine subira, na uwe na subira kujielekea. Unapokosea, kubali mazoezi na nidhamu unayopata, na uione kuwa inatoka kwa Yehova. (Ebr. 12:6) Timiza kwa bidii mgawo wowote unaopewa. Na zaidi ya yote, katika kila jambo unalotenda, mfanye Baba yako wa mbinguni akuonee fahari.—Soma Methali 27:11.

RWĨMBO 135 Mwaliko Wenye Upendo wa Yehova: “Uwe na Hekima, Mwanangu”

^ gic. 5 Kadiri ndugu vijana wanavyokomaa kiroho, ndivyo ambavyo wangependa kumtumikia Yehova zaidi. Ili wastahili kuwa watumishi wa huduma, wanahitaji kujipatia heshima kutoka kwa wengine kutanikoni na kuidumisha. Ndugu vijana wanaweza kufanya nini ili wajipatie heshima kutoka kwa wengine?

^ gic. 9 Baadhi ya majina yamebadilishwa.