Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 9

Vijana—Munaweza Kufanya Nini juu Wengine Wawatumainie?

Vijana—Munaweza Kufanya Nini juu Wengine Wawatumainie?

“Uko na kikundi chako cha vijana kama vile matone ya umande.”​—ZB. 110:3.

WIMBO 39 Tujifanyie Jina ya Muzuri Mbele ya Mungu

KIFUPI CHA HABARI *

1. Tunajua nini juu ya ndugu zetu vijana?

NDUGU vijana, muko na mambo mingi ya kufanya mu kutaniko. (Mez. 20:29) Wengi kati yenu wako na uwezo na nguvu mingi. Munafanya mambo mingi ili kusaidia ndugu na dada zenu. Pengine unapenda kuwa mutumishi wa huduma, lakini wengine wanafikiri kuwa uko mutoto kidogo ao mutu mwenye hana uzoefu na kwa hiyo, hauwezi kupewa kazi fulani ya maana. Hata kama ungali mutoto kidogo, kuko mambo yenye unaweza kufanya leo ili ndugu na dada wa mu kutaniko wakuheshimie na kukutumainia.

2. Tutazungumuzia nini mu hii habari?

2 Mu hii habari tutazungumuzia maisha ya mufalme Daudi. Tutazungumuzia pia kwa kifupi mambo yenye ilitokea mu maisha ya wafalme wawili wa Yuda, ni kusema, Asa na Yehoshafati. Tutaona magumu yenye wale wanaume walipata, namna walitenda na mambo yenye vijana wanaweza kujifunza kupitia mifano yao.

UJIFUNZE KUPITIA MUFANO WA MUFALME DAUDI

3. Mu kutaniko, vijana wanaweza kufanya nini ili kusaidia ndugu na dada wenye kuzeeka?

3 Wakati alikuwa kijana, Daudi alijifunza ufundi mbalimbali wenye wengine waliona kuwa wa maana. Bila shaka, Daudi alikuwa mutu wa kiroho. Pia alijikaza sana ili kuwa mupiga-muziki muzuri na alitumia ule ufundi ili kusaidia Sauli, mufalme mwenye aliwekwa na Mungu. (1 Sa. 16:16, 23) Vijana, muko na ufundi fulani wenye munaweza kutumia ili kusaidia wengine mu kutaniko? Wengi kati yenu wako na ufundi fulani. Kwa mufano, ndugu na dada wenye kuzeeka wanafurahiaka sana wakati ndugu vijana wanawasaidia kujifunza namna ya kutumia tablete zao, na vyombo vingine vya kielektroniki ili kufanya funzo lao la kipekee na ili kuvitumia ku mikutano. Mambo yenye unajua juu ya vyombo vya kielektroniki inaweza kusaidia sana ndugu na dada wenye kuzeeka.

Daudi alikuwa mutu mwenye kutumainika na alilinda kondoo za baba yake wakati dubu aliwashambulia (Ona fungu la 4)

4. Kama Daudi, ndugu vijana wanapaswa kukomalisha sifa gani? (Ona picha ku jalada la gazeti hili.)

4 Mu maisha yake ya kila siku, Daudi alionyesha kama ni mutu mwenye kutumainika. Kwa mufano, wakati alikuwa kijana, alitumika kwa bidii ili kuchunga kondoo za baba yake. Ile kazi, ilitia maisha yake mu hatari. Daudi alifikia kumuambia Mufalme Sauli hivi: “Mutumishi wako amekuwa muchungaji wa kundi la baba yake, na simba akakuja, na pia dubu, na kila mumoja wao akabeba kondoo katika kundi. Nilimufuata na nikamupiga na kumuua na kumuokoa kondoo katika kinywa chake.” (1 Sa. 17:34, 35) Daudi alijua kama alipaswa kuhangaikia kondoo, na kwa uhodari, alipigana ili kuzilinda. Ndugu vijana wanaweza kuiga Daudi kwa kufanya kwa bidii kazi yoyote yenye wanapewa.

5. Kulingana na Zaburi 25:14, ni jambo gani la maana sana lenye ndugu vijana wanaweza kufanya?

5 Wakati Daudi alikuwa kijana, alifanya urafiki wa karibu sana pamoja na Yehova. Ule urafiki wenye Daudi alikuwa nao pamoja na Yehova, ulikuwa wa maana sana kuliko uhodari wake na ufundi wake wa kupiga chombo cha muziki. Yehova alikuwa Mungu wa Daudi, lakini pia alikuwa rafiki yake wa karibu sana. (Soma Zaburi 25:14.) Ndugu vijana, jambo la maana sana lenye munaweza kufanya ni kutia nguvu urafiki wenu pamoja na Baba yenu wa mbinguni. Mukifanya vile, munaweza kupata mapendeleo ingine mu kutaniko.

6. Ni mawazo gani yenye haifae yenye watu walikuwa nayo juu ya Daudi?

6 Watu walikuwa na mawazo yenye haifae juu ya Daudi. Na ile ni tatizo lenye Daudi alipaswa kupiganisha. Kwa mufano, wakati Daudi alijitolea ili kupigana na Goliati, Mufalme Sauli alijaribu kumuzuia kwa kusema hivi: “Wewe ni kijana tu.” (1 Sa. 17:31-33) Mbele ya pale, ndugu ya Daudi alisema bila sababu kama Daudi hakamate mambo kwa uzito. (1 Sa. 17:26-30) Lakini, Yehova hakumuona Daudi kuwa mutoto kidogo ao mutu mwenye hakamate mambo kwa uzito. Alijua Daudi muzuri. Na Daudi aliweza kumuua Goliati juu alimutegemea rafiki yake Yehova.​—1 Sa. 17:45, 48-51.

7. Tunaweza kujifunza nini kupitia habari moja ya Daudi?

7 Tunaweza kujifunza nini kupitia mambo yenye Daudi alikutana nayo? Tumejifunza kama tunapaswa kuwa wavumilivu. Inaomba wakati ili wale wenye walikuwa wanakuona kuwa mutoto kidogo waanze kukuona kama kijana mwenye kukomaa. Lakini ukuwe hakika kama Yehova haone tu namna unaonekana kwa inje. Anakujua muzuri na anajua mambo yenye unaweza kufanya. (1 Sa. 16:7) Utie nguvu urafiki wako pamoja na Mungu. Daudi alifanya vile kwa kuangalia sana vitu vyenye Yehova aliumba. Daudi alifikiri sana juu ya mambo yenye vile vitu vilimufundisha juu ya Muumbaji. (Zb. 8:3, 4; 139:14; Ro. 1:20) Pia unaweza kumuomba Yehova akupatie nguvu yenye uko nayo lazima. Kwa mufano, kuko wanafunzi wenzako wenye wanakuchekeleaka juu uko Shahidi wa Yehova? Kama ni vile, usali kwa Yehova akusaidie uvumilie ile hali. Na utumikishe mashauri yenye kuwa mu Neno lake na mu vichapo na video zetu zenye kutegemea Biblia. Kila mara wakati unaona Yehova anakusaidia kuvumilia hali fulani, utakuwa na imani kama atakusaidia mu hali zingine. Zaidi ya ile, wengine watakutumainia wakati wataona namna unamutumainia Yehova.

Kwa unyenyekevu, ndugu vijana wanaweza kusaidia wengine mu njia mingi (Ona fungu la 8-9)

8-9. Ni nini ilimusaidia Daudi angojee kwa uvumilivu mbele akuwe mufalme? Na ndugu vijana wanaweza kujifunza nini kupitia mufano wake?

8 Tuzungumuzie hali ingine yenye Daudi alikutana nayo. Kisha kutiwa mafuta ili akuwe mufalme, Daudi alipaswa kungojea miaka mingi mbele aanze kutawala juu ya Yuda. (1 Sa. 16:13; 2 Sa. 2:3, 4) Ni nini ilimusaidia Daudi angojee kwa uvumilivu mu ile kipindi? Kuliko kuvunjika moyo sana, Daudi alikaza akili juu ya mambo yenye angeweza kufanya. Kwa mufano, wakati alikuwa mukimbizi mu eneo la Wafilisti, Daudi alitumia ile nafasi ili kupigana na maadui wa taifa la Israeli. Kwa kufanya vile, alilinda mipaka ya eneo la Yuda.​—1 Sa. 27:1-12.

9 Mufano wa Daudi unaweza kufundisha nini ndugu vijana? Tumia nafasi zenye uko nazo ili kusaidia wengine. Fikiria mufano wa ndugu mumoja mwenye kuitwa Ricardo. * Wakati alikuwa mudogo, alipenda kuwa painia wa kawaida. Lakini wazee walimuambia kama hakukuwa tayari. Kuliko kuvunjika moyo ao kukasirika, Ricardo alianza kuhubiri sana. Anasema hivi: “Wakati nakumbuka hali yangu ya zamani, natambua kama nilikuwa na lazima ya kufanya maendeleo. Nilijikaza kurudilia watu wote wenye walipendezwa na nilijitayarisha mbele ya kuwarudilia. Nilifikia hata kuongoza funzo langu la kwanza la Biblia. Kadiri nilihubiri zaidi ni vile wasiwasi wangu uliendelea kupunguka.” Leo, Ricardo ni painia wa kawaida mwenye kupata matokeo ya muzuri na ni mutumishi wa huduma.

10. Daudi alifanya nini wakati fulani mbele ya kukamata uamuzi wa maana?

10 Tufikirie hali ingine yenye Daudi alikutana nayo mu maisha yake. Wakati yeye na watu wake walikuwa wakimbizi, waliacha familia zao na kuenda kupigana vita. Wakati watu wake walikuwa ku vita, maadui fulani walifika ku nyumba zao na wakakamata familia zao mateka. Daudi angewaza kama juu iko na uzoefu mu mambo ya vita, angeweza tu kufanya mupango fulani ili kuokoa wale wenye walikamatwa mateka. Kuliko kufanya vile, Daudi alitafuta muongozo wa Yehova. Kwa musaada wa kuhani mwenye kuitwa Abiatari, Daudi alimuuliza Yehova hivi: “Je nifuatilie kikundi hiki cha wanyanganyi?” Yehova alimuambia Daudi kama anapaswa kuenda na alimuhakikishia kama atawakomboa. (1 Sa. 30:7-10) Hii habari inaweza kukufundisha nini?

Ndugu vijana wanapaswa kutafuta mashauri kwa wazee (Ona fungu la 11)

11. Unaweza kufanya nini mbele ya kukamata maamuzi?

11 Omba wengine mashauri mbele ya kukamata maamuzi. Omba pia wazazi wako mashauri. Tena, unaweza kupata mashauri ya muzuri wakati unazungumuza na wazee wenye kuwa na uzoefu. Yehova anatumainia wale wanaume wenye wamewekwa, wewe pia unaweza kufanya vile. Yehova anawaona kuwa “zawadi” kwa kutaniko. (Efe. 4:8) Wakati unaiga imani yao na kusikiliza mashauri yao ya hekima, utapata faida. Tuone sasa mambo yenye habari ya Mufalme Asa inaweza kutufundisha.

UJIFUNZE KUPITIA MUFANO WA MUFALME ASA

12. Mufalme Asa alikuwa na sifa gani wakati alianza kutawala?

12 Wakati alikuwa kijana, Mufalme Asa alikuwa na sifa ya unyenyekevu na uhodari. Kwa mufano, kisha baba yake Abiya kufa, Asa alianza kutawala. Na akaanza kuondoa mu inchi ibada ya sanamu. Pia, “aliambia Yuda wamutafute Yehova Mungu wa mababu zao na washike Sheria na amri.” (2 Ny. 14:1-7) Na wakati Zera Mwetiopia alishambulia Yuda pamoja na maaskari wake 1 000 000, kwa hekima, Asa alimuomba Yehova musaada. Alisema hivi: “Ee Yehova, haiko shida kwako ikuwe wale wenye unasaidia ni wengi ao hawana nguvu. Utusaidie, Ee Yehova Mungu wetu, kwa maana tunakutegemea wewe.” Hii maneno ya muzuri yenye Asa alisema, inaonyesha kuwa Asa alikuwa na imani yenye nguvu kama Yehova iko na uwezo wa kumuokoa na kuokoa watu wake. Asa alimutumainia Yehova, Baba yake wa mbinguni, na “Yehova akashinda Waetiopia.”​—2 Ny. 14:8-12.

13. Ni nini ilifikia kumupata Asa, na juu ya nini?

13 Bila shaka, kupigana na kikundi cha maaskari 1 000 000 ilikuwa jambo la kuogopesha sana, lakini Asa alipata ushindi juu alimutumainia Yehova. Lakini, jambo la kuhuzunisha, wakati Asa alipata tatizo lingine lenye haliko la kuogopesha sana, Asa hakumutumainia Yehova. Wakati Baasha, mufalme muovu wa Israeli alimuogopesha, Asa alienda kuomba mufalme wa Siria musaada. Ule uamuzi ulileta matokeo ya mubaya! Kupitia nabii Hanani, Yehova alimuambia Asa hivi: “Kwa sababu ulimutegemea mufalme wa Siria na haukumutegemea Yehova Mungu wako, jeshi la mufalme wa Siria limeponyoka kutoka katika mukono wako.” Kwa kweli, kuanzia pale, Asa alikuwa anapigana vita kila mara. (2 Ny. 16:7, 9; 1 Fa. 15:32) Ile habari inatufundisha nini?

14. Namna gani unaweza kuonyesha kama unamutumainia Yehova? Na kulingana na 1 Timoteo 4:12, ile itakuletea matokeo gani?

14 Uendelee kuwa munyenyekevu na uendelee kumutumainia Yehova. Wakati ulibatizwa, ulionyesha kama uko na imani yenye nguvu na ulimutumainia sana Yehova. Na Yehova alifurahi sana na akakupatia pendeleo la kuwa mu familia yake. Jambo lenye unapaswa kufanya sasa ni kuendelea kumutumainia Yehova. Inaweza kuonekana mwepesi kumutumainia Yehova wakati unapaswa kukamata maamuzi ya maana sana. Lakini utafanya nini wakati wa kukamata maamuzi ingine? Ni jambo la maana sana umutumainie Yehova wakati unakamata maamuzi, hata kama inahusu mambo ya kujifurahisha, kazi ya kimwili na miradi yenye unajiwekea. Usitegemee hekima yako mwenyewe. Kuliko kufanya vile, tafuta kanuni za Biblia zenye zinahusu hali yako na kisha utumikishe muongozo wenye umepata. (Mez. 3:5, 6) Kama unafanya vile, utamufurahisha Yehova na ndugu na dada mu kutaniko watakuheshimia.​—Soma 1 Timoteo 4:12.

UJIFUNZE KUPITIA MUFANO WA MUFALME YEHOSHAFATI

15. Kulingana na 2 Mambo ya Nyakati 18:1-3; 19:2, ni makosa gani yenye Mufalme Yehoshafati alifanya?

15 Bila shaka, kama sisi wote, vijana ninyi pia hamukamilike. Na wakati fulani mutafanya makosa. Lakini, ile haipaswe kuwazuia kufanya yote yenye munaweza mu utumishi wa Yehova. Fikiria mufano wa Mufalme Yehoshafati. Alikuwa na sifa mingi za muzuri. Wakati alikuwa kijana, “alimutafuta Mungu wa baba yake na kufuata amri yake.” Pia, alituma wakubwa waende mu miji yote ya Yuda ili kufundisha watu juu ya Yehova. (2 Ny. 17:4, 7) Lakini, hata kama alikuwa na nia ya muzuri, wakati fulani, Yehoshafati alikamata maamuzi ya mubaya. Na siku moja, Yehova alitumia mutumishi wake fulani ili kumushauria Yehoshafati kuhusu uamuzi wa mubaya wenye alikamata. (Soma 2 Mambo ya Nyakati 18:1-3; 19:2.) Habari yake inaweza kutufundisha nini?

Ndugu vijana wenye wanafanya kazi kwa bidii na wenye kutumainiwa wanajifanyia jina la muzuri (Ona fungu la 16)

16. Mufano wa Rajeev unaweza kukufundisha nini?

16 Ukubali na utumikishe mashauri yenye unapata. Pengine, kama vile vijana wengi, ni nguvu kwako kujua mambo yenye unapaswa kutia pa nafasi ya kwanza. Lakini, usivunjike moyo. Fikiria mufano wa ndugu mumoja kijana mwenye kuitwa Rajeev. Rajeev anafikiria maisha yake wakati alikuwa na miaka kati ya 13 na 19. Anasema hivi: “Wakati fulani sikujua nifanye nini mu maisha yangu. Kama vile vijana wengine, nilipenda sana michezo na mambo ya kujifurahisha kuliko kuenda ku mikutano ao kuhubiri.” Ni nini njo ilimusaidia? Muzee mumoja alimupatia mashauri fulani. Rajeev anasema hivi: “Alinisaidia kufikiri juu ya kanuni yenye kuwa mu 1 Timoteo 4:8.” Kwa unyenyekevu, Rajeev alikubali mashauri na akafikiria mambo yenye ilikuwa ya maana sana mu maisha yake. Anasema hivi: “Niliamua kutia miradi ya kiroho pa nafasi ya kwanza.” Ile ilileta matokeo gani? Rajeev anafasiria hivi: “Miaka fulani kisha kupata ile mashauri, niliwekwa kuwa mutumishi wa huduma.”

MUMUFURAHISHE BABA YENU WA MBINGUNI

17. Ndugu na dada wenye kuzeeka wanajisikia namna gani juu ya ndugu vijana wenye kumutumikia Yehova?

17 Ndugu vijana, mujue kama ndugu na dada wenye kuzeeka wanawaona kuwa wa maana wakati munamutumikia Yehova pamoja nao “bega kwa bega”! (Sef. 3:9) Wanafurahi sana wakati munafanya kwa bidii kazi yenye munapewa. Wanawapenda sana.​—1 Yo. 2:14.

18. Kulingana na Mezali 27:11, Yehova anajisikiaka namna gani juu ya ndugu vijana wenye kumutumikia?

18 Ndugu vijana, musisahau hata kidogo kama Yehova anawapenda na anawatumainia. Yehova alitabiri kama mu siku za mwisho, kutakuwa jeshi la vijana wenye watajitoa kwa kujipendea. (Zb. 110:1-3) Yehova anajua kama munamupenda na kama munapenda kumutumikia kwa uwezo wenu wote. Kwa hiyo, mukuwe wavumilivu na muvumilie wengine. Wakati munafanya makosa, mukubali mazoezi na muongozo wenye munapata na muione kuwa inatoka kwa Yehova. (Ebr. 12:6) Mufanye kwa bidii kazi yoyote yenye munapewa. Na zaidi ya yote, mumufurahishe Baba yenu wa mbinguni mu mambo yote yenye munafanya.​—Soma Mezali 27:11.

WIMBO 135 Yehova Anakuomba “Ukuwe na Hekima”

^ fu. 5 Ndugu vijana wenye kukomaa kiroho, wanapenda kumutumikia Yehova mu njia zingine mbalimbali. Juu wastahili kuwa watumishi wa huduma, wanapaswa kufanya mambo fulani juu ndugu na dada mu kutaniko wawaheshimie na waendelee kuwaheshimia. Sasa ni mambo gani ndugu vijana wanaweza kufanya juu wengine wawaheshimie?

^ fu. 9 Majina fulani imebadilishwa.