Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 20

Endelea Kuwa na Mawazo ya Muzuri juu ya Mahubiri

Endelea Kuwa na Mawazo ya Muzuri juu ya Mahubiri

“Panda mbegu zako . . . na usiache mukono wako upumuzike.”​—MUH. 11:6.

WIMBO 70 Tutafute Wenye Kustahili

KIFUPI CHA HABARI *

Kisha Yesu kupanda mbinguni,wanafunzi wake wanahubiri kwa bidii katika Yerusalemu na pia katika miji ingine (Ona fungu la 1)

1. Yesu aliachia wafuasi wake mufano gani na walitenda namna gani? (Ona picha kwenye jalada.)

YESU aliendelea kuwa na mawazo ya muzuri juu ya kazi ya kuhubiri wakati alikuwa hapa ku dunia na alipenda wafuasi wake pia wakuwe na mawazo ya vile. (Yoh. 4:35, 36) Wakati walikuwa wangali na Yesu, wanafunzi wake walihubiri kwa bidii. (Lu. 10:1, 5-11, 17) Lakini kisha tu Yesu kukamatwa na kuuawa, wanafunzi wake walipoteza kwa muda fulani bidii yenye walikuwa nayo. (Yoh. 16:32) Wakati alifufuliwa, Yesu aliwatia moyo waedelee na kazi ya kuhubiri. Na kisha yeye kurudia mbinguni, wanafunzi wake walihubiri kwa bidii sana mupaka maadui wao wakaanza kusema hivi: “Muangalie! mumejaza Yerusalemu na mafundisho yenu.”​—Mdo. 5:28.

2. Namna gani Yehova amebariki kazi ya kuhubiri?

2 Yesu aliongoza Wakristo wa kwanza-kwanza mu kazi ya kuhubiri na Yehova aliwasaidia. Watu wengi walikubali ujumbe wao. Kwa mufano, kwenye Pentekoste mu 33 K.K.Y., watu 3 000 hivi walibatizwa. (Mdo. 2:41) Hesabu ya wanafunzi iliendelea kuongezeka sana. (Mdo. 6:7) Zaidi ya ile, Yesu alitabiri kama, kazi ya kuhubiri ingekuwa na matokeo ya muzuri sana mu siku za mwisho.​—Yoh. 14:12; Mdo. 1:8.

3-4. Juu ya nini inaweza kuwa nguvu kuhubiri fasi fulani, na ni mambo gani tutaona mu hii habari?

3 Siye wote tunajikazaka kuwa na mawazo ya muzuri juu ya kazi ya kuhubiri. Ni mwepesi kufanya vile mu inchi fulani. Juu ya nini? Juu watu wengi wanapenda kujifunza Biblia na ile inafanya wengine wachunge kidogo mupaka wapate Shahidi mwenye atawafundisha Biblia. Lakini mu inchi zingine wahubiri wako na magumu sana ya kuhubiri juu watu hawakuwake sana ku nyumba zao na wale wenye wako ku nyumba zao hawapendezwe sana na Biblia.

4 Kama uko unaishi fasi kwenye kuhubiri ni nguvu sana, mapendekezo yenye kuwa mu hii habari inaweza kukusaidia. Tutaona mambo yenye wahubiri fulani walifanya ili kuhubiria watu wengi zaidi. Na tutaona juu ya nini tunapaswa kuendelea kuwa na mawazo ya muzuri juu ya mahubiri, watu waitike ao wakatale.

UENDELEE KUWA NA MAWAZO YA MUZURI HATA KAMA NI NGUVU KUPATA WATU

5. Mashahidi wa Yehova wengi wanakutana na matatizo gani?

5 Mashahidi wengi wanaona kama inaendelea kuwa nguvu kuzungumuza na watu ku nyumba zao. Wahubiri fulani wanaishi mu maeneo yenye kuwa na nyumba zenye kulindwa sana, na zenye zinaweza kuwa na mulinzi mwenye haingize kila mutu bila ruhusa ya wenye-nyumba. Mu maeneo ingine ni mwepesi kwa wahubiri kuhubiri nyumba kwa nyumba lakini wanakuta tu watu kidogo ku nyumba. Na wengine wanahubiri fasi kwenye watu kidogo wanaishi. Wale wahubiri wanaenda kuhubiri mbali sana ili wapate tu mwenye-nyumba moja na pengine hatakuwa hata ku nyumba! Kama tuko tunahubiria mu maeneo ya vile hatupaswe kuvunjika moyo. Tunaweza kufanya nini juu tupiganishe hii matatizo na kuhubiria watu wengi zaidi?

6. Namna gani wahubiri wanafanana na wavuvi?

6 Yesu alilinganisha kazi ya kuhubiri na kazi ya muvuvi. (Mk. 1:17) Wavuvi fulani wanaweza kufanya masiku mingi wako wanatafuta samaki lakini hawapate. Hata vile, hawaachake; wanabadilishaka njo wakati, fasi, na namna ya kuvua samaki. Na siye pia tunaweza kufanya mabadiliko fulani kuhusu kazi yetu ya kuhubiri. Tuone mapendekezo fulani.

Wakati uko unahubiri mu eneo kwenye watu hawapatikane sana ku nyumba, ujaribu kuwatafuta wakati ingine, fasi ingine, ao utumie njia zingine za kuhubiri ili kuwapata (Ona fungu la 7-10) *

7. Tunaweza kupata matokeo gani ya muzuri kama tunahubiria watu saa yenye wanaweza kupatikana?

7 Utafute watu saa yenye wanaweza kupatikana. Tunaweza kuhubiria watu wengi kama tunawatafuta saa yenye wanaweza kuwa kwao. Kwa kawaida, hakuna mutu analalaka fasi alienda, kila mutu anarudiaka kwake! Ndugu na dada wengi wanaona kama ni muzuri sana kuhubiri kisha midi ao mangaribi juu mu ile wakati ni mwepesi kupata watu wengi zaidi. Na zaidi ya ile, mu ile wakati wenye-nyumba wanaweza kuwa walishatulia na wako tayari kuongea na watu wengine. Ao pengine unaweza kufurahia hii pendekezo ya muzee mumoja mwenye kuitwa David. Anafasiria kama kisha kuhubiri kwa wakati fulani mu eneo moja, yeye na mwenzake walirudia ili kuhubiria wale wenye hawakukuta. Anasema hivi: “Kitu inanishangazaka ni wakati tunarudia na tunakuta watu wenye tulikosa.” *

Wakati uko unahubiri mu eneo kwenye watu hawapatikane sana ku nyumba, ujaribu kuwatafuta wakati ingine (Ona fungu la 7-8)

8. Namna gani tunaweza kutumikisha Muhubiri 11:6 mu kazi yetu ya kuhubiri?

8 Tunapaswa kuendelea kutafuta watu ku nyumba zao. Ile njo jambo tunajifunza mu andiko letu la musingi. (Soma Muhubiri 11:6.) David, mwenye tulishataja, hakuacha kutafuta watu ku nyumba zao. Ku nyumba moja alifikia kupata mwenye-nyumba kisha kumukosa mara mingi sana. Ule mwenye-nyumba alifurahia sana mazungumuzo ya Biblia na kisha alisema: “Nilishafanya miaka munane hivi na hakuna hata siku moja nilishakaona Shahidi wa Yehova ku mulango wangu.” David anaongezea hivi: “Nilifikia kuona kama watu wenye sikutake ku nyumba, siku nawakuta mara mingi wanafurahiaka ujumbe wetu.”

Wakati uko unahubiri mu eneo kwenye watu hawapatikane sana ku nyumba, ujaribu kuwatafuta fasi ingine (Ona fungu la 9)

9. Namna gani Mashahidi fulani wamefikia kuhubiria watu wenye ni nguvu kupata ku nyumba zao?

9 Ujaribu kutafuta watu fasi ingine. Juu ya kupata watu wenye ni nguvu kukuta ku nyumba, wahubiri fulani walibadilisha fasi kwenye walikuwa wanahubiria. Kwa mufano, kuhubiri mu barabara na kutumia prezantware kumesaidia sana kupata watu wenye wanaishi fasi kwenye hairuhusiwe kuhubiri nyumba kwa nyumba. Ile imesaidia sana Mashahidi wakutane na watu uso kwa uso. Tena, wahubiri wengi wameona kama mu soko, mu fasi zingine za biashara na mu fasi kwenye watu wanapitisha wakati wengi wanafurahiaka kuzungumuza na siye ao wanakuwaka wanakubali vichapo vyetu. Floiran, mwangalizi mumoja wa muzunguko wa inchi ya Bolivie, anasema hivi: “Tunaendaka ku soko na ku fasi zingine za biashara kati ya saa 7 na saa 9 (13:00–15:00) wakati wenye kuuzisha hawana wa clients mingi. Mara mingi tunakuwaka na mazungumuzo ya muzuri nao na hata tunaanzishaka mafunzo ya Biblia.”

Wakati uko unahubiri mu eneo kwenye watu hawapatikane sana ku nyumba, ujaribu kuwatafuta ao utumie njia zingine za kuhubiri ili kuwapata (Ona fungu la 10)

10. Ni njia gani unaweza kutumia ili kuhubiria watu?

10 Ujaribu kutumia njia ingine ili kupata watu. Waza umejaribu kutembelea mutu fulani mara kwa mara lakini bila kumupata. Umejaribu hata kubadilisha saa juu tu umupate, lakini wapi. Unawaza kuko njia zingine zenye unaweza kutumia ili kumupata? Katarína, anasema hivi: “Naandikiaka barua wale wenye sikutake ku nyumba. Nawaandikiaka mambo yenye ningewaambia kama ningewakuta.” Unaelewa wazo yenye kuwa hapa? Ujaribu kutumia njia yoyote ili kuhubiria kila mutu mu eneo lenu.

ENDELEA KUWA NA MAWAZO YA MUZURI HATA KAMA WATU HAWAPENDEZWE

11. Juu ya nini watu fulani hawapendezwe na ujumbe wetu?

11 Watu fulani hawapendezwe na ujumbe wetu. Wanaona kama hawana lazima ya Mungu wala Biblia. Hawamuamini Mungu juu wako wanaona mateso mingi mu dunia. Wanakatala Biblia juu wanaona kama viongozi wengi wa dini ni wanafiki, hawaishi kupatana na mambo yenye iko mu Biblia. Wengine wanahangaikia zaidi kazi zao, familia, mambo yao ya kipekee, na hawaone namna gani Biblia inaweza kusaidia. Namna gani tunaweza kuchunga furaha yetu wakati tunahubiria watu wenye hawapendezwe kabisa na Biblia?

12. Namna gani kutumikisha maneno yenye kuwa mu Wafilipi 2:4 kunaweza kutusaidia mu kazi ya kuhubiri?

12 Uonyeshe kama unahangaikia wengine. Watu wengi wenye ku mwanzo hawakukuwa wanapendezwa na habari njema walifikia kuipenda kisha, juu muhubiri fulani aliwaonyesha kabisa kama anawahangaikia. (Soma Wafilipi 2:4.) Kwa mufano, David, mwenye tulishataja, anasema hivi: “Kama mutu fulani anasema kama hawapendezwe, tunatia kwanza pembeni mambo ya Biblia na mambo ya vichapo na kisha tunamuambia: ‘Nilipenda kujua juu ya nini unawaza vile.’” Watu wanaonaka kama tunawahangaikia. Wanaweza kusahau mambo yenye tuliwaambia, lakini pengine hawawezi kusahau namna tulifanya wajisikie. Pengine mwenye-nyumba hawezi kutuachia wakati tuseme, lakini tunaweza kuonyesha kama tunamuhangaikia kupitia namna yetu ya kutenda na pia kupitia ishara za uso.

13. Unaweza kufanya nini ili ujumbe wako ufurahishe zaidi mwenye-nyumba?

13 Tunaonyesha kama tunahangaikia watu wakati tunabadilisha namna yetu ya kusema ili ujumbe wetu upatane na hali ya mwenye-nyumba na ili aufurahie. Kwa mufano, kuko alama fulani zenye zinakuonyesha kama mu hii nyumba muko watoto? Wazazi wanaweza kufurahia sana mashauri ya Biblia kuhusu namna ya kukomalisha watoto na namna ya kuwa na maisha ya familia yenye furaha. Unaona kufuli za mingi ku mulango? Unaweza kuamua kuzungumuza juu ya jeuri na namna ile inafanya watu waogope sana leo. Pengine mwenye-nyumba anaweza kufurahia kujua kama kuko siku ile hali itaisha. Ikuwe ni hali gani, usaidie kabisa wale wenye wanapenda kujua namna mashauri ya Biblia inaweza kuwasaidia. Katarína, mwenye tulishataja, anasema hivi: “Siwezi kusahau namna Biblia imenisaidia mu maisha yangu.” Matokeo inakuwa gani? Katarína anaamini kabisa mambo yenye iko anasema, na watu wenye iko anazungumuza nao wanaona vile.

14. Kulingana na Mezali 27:17, namna gani ndugu na dada wanaweza kusaidiana mu mahubiri?

14 Ukubali musaada wa wengine. Paulo alimufundisha Timoteo ufundi wake wa kuhubiri na kufundisha na alimutia moyo afundishe wengine pia namnna ya kufanya vile. (1 Ko. 4:17) Sawa vile Timoteo, na siye pia tunaweza kujifunza mambo fulani kupitia uzoefu wa ndugu na dada mu kutaniko. (Soma Mezali 27:17.) Fikiria mufano wa ndugu mwenye kuitwa Shawn. Wakati fulani alifanya kazi ya upainia katika eneo lenye watu wengi walifurahia kuwa mu dini yao. Namna gani aliendelea kuchunga furaha yake? Anasema hivi: “Wakati wowote wenye iliwezekana, nilihubiri pamoja na ndugu ao dada fulani. Wakati tulitoka ku mulango moja ili kuenda ku mulango ingine, tulitumia ile wakati ili kusaidiana kukomalisha ufundi wetu wa kufundisha. Kwa mufano, tulizungumuzia mambo yenye mwenye-nyumba alisema na namna tulimujibia. Kisha tulizungumuzia namna tunaweza kufanya wakati ingine ikiwa mwenye-nyumba anasema mambo ya kufanana na ile.”

15. Juu ya nini sala ni ya maana sana mu kazi yetu ya kuhubiri?

15 Usali kwa Yehova ili akusaidie. Umuombe Yehova akusaidie kila wakati unahubiri, juu bila musaada wa roho yake takatifu hakuna mwenye anaweza kutimiza jambo lolote. (Zb. 127:1; Lu. 11:13) Wakati unamuomba Yehova akusaidie, umuambie mambo waziwazi. Kwa mufano, umuombe Yehova akuongoze kwa kila mutu mwenye anapenda kujifunza juu yake na mwenye iko tayari kusikiliza. Kisha utende kulingana na sala yako kwa kuhubiria kila mutu mwenye unakutana naye.

16. Juu ya nini kuwa na funzo la kipekee kutatusaidia sana mu kazi yetu ya kuhubiri?

16 Utafute wakati wa kufanya funzo la kipekee. Neno la Mungu linasema hivi: “Mujihakikishie ninyi wenyewe mapenzi ya Mungu yenye kuwa mema na yenye kukubalika na makamilifu.” (Ro. 12:2) Wakati tunajifunza Biblia tunafikia kumujua Yehova Mungu muzuri zaidi, ile itatusaidia wakati tunazungumuza na watu kumuhusu. Wataona kabisa kama tunaamini mambo yenye tuko tunasema. Katarína, mwenye tulishataja, anasema hivi: “Kumepita wakati kidogo, nilitambua kama nilikuwa na lazima ya kutia nguvu imani yangu katika mafundisho fulani ya musingi ya Biblia. Njo maana, nilijifunza kwa uangalifu mambo yenye kuonyesha kama kuko Muumbaji, kama kweli Biblia ni Neno la Mungu, na kama leo Mungu iko na tengenezo lenye linamuakilisha.” Katarína anasema kama funzo lake la kipekee lilimusaidia atie nguvu imani yake na liliongeza furaha yake mu mahubiri.

JUU YA NINI TUENDELEE KUWA NA MAWAZO YA MUZURI KUHUSU KAZI YETU YA KUHUBIRI

17. Juu ya nini Yesu aliendelea kuwa na mawazo ya muzuri kuhusu utumishi wake?

17 Yesu aliendelea kuwa na mawazo ya muzuri na aliendelea kuhubiri hata kama watu fulani hawakupenda kusikiliza ujumbe wake. Juu ya nini? Alijua kama watu walikuwa na lazima ya kujifunza kweli, na alipenda kusaidia watu wengi kadiri inawezekana. Alijua pia kama watu fulani wangekatala ujumbe wake ku mwanzo lakini wangefikia kuukubali. Fikiria mambo yenye ilimufikia Yesu mu familia yake. Katika utumishi wake wenye ulifanya miaka tatu na nusu hakuna hata ndugu yake mumoja mwenye alifikia kuwa mwanafunzi wake. (Yoh. 7:5) Lakini kisha ufufuo wake, walifikia kuwa Wakristo.​—Mdo. 1:14.

18. Juu ya nini tunaendelea kuhubiri?

18 Kusema kweli, hatujue ni nani mwenye anaweza kufikia kuwa mutumishi wa Yehova. Kwa watu fulani inaomba wakati mingi ili wajifunze kweli. Hata wale wenye hawapende kutusikiliza wanaweza kuona kama tuko na mwenendo wa muzuri na mawazo ya muzuri, na pengine ile inaweza kuwafanya “wamutukuze Mungu.”​—1 Pe. 2:12.

19. Kulingana na 1 Wakorinto 3:6, 7, tunapaswa kukumbuka nini?

19 Hata kama tunapanda na kutia maji, tunapaswa kukumbuka kama Mungu njo anakomalishaka. (Soma 1 Wakorinto 3:6, 7.) Ndugu Getahun, mwenye anatumikia Etiopia, anasema hivi: “Kwa zaidi ya miaka 20, ni miye tu njo nilikuwa Shahidi wa Yehova mu eneo kwenye niliishi. Lakini sasa kuko wahubiri 14. Wahubiri 13 walibatizwa, kutia ndani bibi yangu na watoto wangu watatu. Ku mikutano tunakuwaka watu 32 hivi.” Getahun anafurahi juu aliendelea kuhubiri na aliendelea kuvumilia ili Yehova avute wale wenye moyo muzuri mu tengenenzo Lake!​—Yoh. 6:44.

20. Ni mu njia gani kazi yetu ya kuhubiri inafanana na kazi ya kuokoa watu?

20 Yehova anaona watu wote kuwa wa maana sana. Anatupatia pendeleo la kutumika pamoja na Mwana wake ili kukusanya watu kutoka mu mataifa yote mbele mwisho ufike. (Hag. 2:7) Kazi yetu ya kuhubiri inafanana na kazi ya kuokoa. Na tuko sawa vile kikundi ya watu wenye kuokoa wale wenye kuwa mu mashua yenye ilishazama. Hata kama wote hawatapata watu wa kuokoa, lakini wote watakuwa wamefanya kazi ya maana sana. Ni vile pia na kazi yetu ya kuhubiri. Hatujue ni watu wangapi wenye wataokoka mu ulimwengu wa Shetani. Lakini Yehova anaweza kutumikisha mutu yeyote kati yetu ili kuwasaidia. Andreas, mwenye kuishi Bolivie, anasema hivi: “Najua kama wakati mutu anajifunza kweli na anafikia kubatizwa ni juu watu wengi walitumika pamoja ili kumusaidia.” Tuendelee basi kuwa na mawazo ya vile kuhusu kazi yetu ya kuhubiri. Tukifanya vile Yehova atatubariki, na kazi yetu ya kuhubiri itatuletea furaha mingi.

WIMBO 66 Tuhubiri Habari Njema

^ fu. 5 Namna gani tunaweza kuendelea kuwa na mawazo ya muzuri juu ya mahubiri hata kama watu wenye tunapenda kuhubiria hawako ku nyumba ao hawapendezwe na ujumbe wetu? Hii habari itatupatia mapendekezo yenye itatusaidia kuwa na mawazo ya muzuri juu ya mahubiri.

^ fu. 7 Wakati wahubiri wanatumia njia mbalimbali ili kuhubiri, kama vile inaonyeshwa mu hii habari, wanapaswa kuheshimia sheria za inchi kuhusu kutunza habari za watu.

^ fu. 60 MAELEZO YA PICHA: (kuanzia juu mupaka chini): Bibi na bwana wako wanahubiri fasi kwenye ni nguvu kupata watu. Mwenye-nyumba wa kwanza iko ku kazi yake, wa pili iko ku hopitali, na wa tatu iko anauza vitu. Walimupata wa kwanza wakati walimutembelea mangaribi ya ile siku. Walipata wa pili wakati walikuwa wanahubiri ku prezantware pembeni ya ile hopitali. Na walipata mwenye-nyumba wa tatu wakati walimuita ku telefone.