Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI JUU YA MAISHA YA WATU

“Nilijifunza Mambo Mingi Sana kwa Wengine!”

“Nilijifunza Mambo Mingi Sana kwa Wengine!”

NAKUMBUKA ilikuwa usiku moja, wakati miye na kikundi yetu ya maaskari Wafaransa, tulikuwa mu milima ya Algérie na ile wakati vita ilikuwa ilishakolea sana mu ile inchi. Nilikuwa nafanya ulinzi miye peke, na pembeni yangu kulikuwa saki zenye kujaa muchanga na nilikuwa na bunduki ya munene. Kisha kwa kushitukia, nikaanza kusikia makelele ya miguu yenye iko inakuya. Nikaanza kutetemeka sana. Nilikuwa tu njo ninaeneza miaka makumi mbili. Sikupenda kuuana ao kuuawa. Nikalalamika: “Nakufa! Mungu unisaidie!”

Ile hali ya kuogopesha yenye ilinifikiaka ile usiku ilifanya nianze kufikiri sana na nianze kutafuta kumujua Mungu. Lakini mbele niwafasirie kile kilitokea kisha pale, muache niwaelezee mambo yenye ilinifikiaka wakati nilikuwa mutoto yenye ilinipatiaka hamu ya kutaka kumujua Mungu.

MAMBO YENYE NILIJIFUNZA KWA BABA YANGU

Nilizaliwa mu 1937 mu muji wa Guesnain, wenye kuwa kaskazini mu inchi ya Ufaransa, kwenye watu wanazoea kuchimba minerais. Baba yangu alikuwa anachimba minerai yenye inaitwa charbon na alinifundisha ulazima wa kutumika sana. Baba yangu alipenda sana kufuatilia haki na miye niliiga mufano wake. Ile hali ya baba yangu ilimuchochea akuwe anatetea wachimbaji wengine wa minerais wenye walitumika mu hali za mubaya sana. Na ile ilifanya ajiunge na vikundi vyenye vilikuwa vinapigania haki ya wale wenye walikuwa wanachimba minerais. Tena, roho ilikuwa inamuluma sana wakati alikuwa anaona unafiki wa mapadri, kwenye tulikuwa tunaishi. Mapadri wengi walikuwa na maisha ya muzuri sana; lakini walikuwa wanaomba masikini wenye walikuwa wanachimba minerais wawapatie chakula na feza. Tabia ya wale mapadri ilimuhuzunisha sana baba, njo maana hakunifundisha jambo lolote juu ya dini. Kusema kweli, hakuna hata siku moja tulizungumuzaka kuhusu Mungu.

Vile nilikuwa nakomala, na miye nikaanza kuchukia ukosefu wa haki. Kitu moja yenye sikufurahia ni vile watu wengi walikuwa wanachukia sana wageni wenye walikuwa wanaishi mu inchi ya Ufaransa. Nilicheza kabumbu pamoja na watoto wa wamoja kati yao na nilifurahi sana kupitisha wakati pamoja nao. Tena, mama yangu hakukuwa Mufaransa, lakini alikuwa muzaliwa wa inchi ya Polandi. Nilipenda watu wa rangi mbalimbali ya ngozi waishi pamoja kwa amani na watendewe sawasawa.

NILIANZA KUFIKIRI SANA JUU YA MAISHA

Wakati nilikuwa ningali mu kazi ya jeshi

Niliingizwa mu kazi ya jeshi mu 1957. Na njo maana nikajikuta mu milima ya Algérie ile usiku, sawa vile nilifasiria ku mwanzo. Kisha kulalamika “Nakufa! Mungu unisaidie!” nikakutana uso kwa uso, hapana na adui askari, lakini na punda wa pori! Roho ikashuka! Vita na ile hali yenye ilinifikia, ilifanya nifikiri sana juu ya maisha. Nilijiuliza: Juu ya nini tuko tunaishi? Mungu anatuhangaikiaka kweli? Kuko siku kutakuwaka amani?

Kisha wakati fulani nikaenda kutembelea wazazi wangu, na kule nikakutana na Shahidi moja wa Yehova. Alinipatia La Sainte Bible, Biblia ya Kikatoliki ya luga ya Kifaransa. Nilianza kuisoma wakati nilirudia Algérie. Andiko moja yenye ilinigusa sana ni Ufunuo 21:3, 4, yenye inasema: “Hema ya Mungu iko pamoja na wanadamu . . . Na atapanguza kila chozi katika macho yao, na kifo hakitakuwa tena, wala maombolezo wala kilio wala maumivu havitakuwa tena.” * Ile maneno ilinishangaza sana. Nilijiuliza hivi: ‘Hii maneno ni ya kweli kabisa?’ Ile wakati sikukuwa najua hata kitu fulani juu ya Mungu wala Biblia.

Kisha kuacha kazi ya jeshi mu 1959, nilikutana na François, mwenye alikuwa Shahidi wa Yehova. Alinifundisha kweli mingi za Bibila. Kwa mufano, alinionyesha mu Biblia jina la pekee la Mungu, Yehova. (Zb. 83:18) François alinifasiria pia kama Yehova ataleta haki ku dunia, atageuza dunia hii ikuwe paradiso, na atatimiza maneno yenye kuwa mu Ufunuo 21:3, 4.

Ile mafundisho ilikuwa inaeleweka kabisa, na iligusa moyo wangu. Lakini nilikasirikia pia mapadri na nilipenda kuonyesha waziwazi kama mafundisho yenye walikuwa wanafundisha haikukuwa mu Biblia! Inaonekana mawazo ya baba yangu ilikuwa ingali mu damu. Nilipenda kufanya kitu fulani bila kukawia!

François na mashahidi wengine, wenye walikuwa sasa marafiki wangu, walinisaidia nijue namna ya kuzuia kasirani yangu. Walinifasiria kama, siye Wakristo, kazi yetu haiko kuhukumu watu lakini ni kuwapatia tumaini kupitia habari njema ya Ufalme wa Mungu. Njo kazi yenye Yesu alifanya na njo kazi yenye alipatia wafuasi wake wafanye. (Mat. 24:14; Lu. 4:43) Nilipaswa pia kujifunza namna ya kuzungumuza na watu kwa upole na busara hata kama sikukubaliana na mambo yenye wanaamini. Biblia inasema hivi: “Mutumwa wa Bwana hana lazima ya kupigana, lakini anapaswa kuwa mupole kwa wote.”​—2 Ti. 2:24.

Nilifanya mabadiliko yenye iliomba nifanye na nikabatizwa na kuwa Shahidi wa Yehova mu 1959, ku mukusanyiko wa muzunguko. Kule nikakutana na dada mwenye anaitwa Angèle, mwenye alinivutia sana. Nilianza kutembelea kutaniko kwenye alikuwa anahuzuria, na kisha tukaoana mu 1960. Kusema kweli, ni mwanamuke muzuri sana, bibi kabisa, zawadi kutoka kwa Yehova.​—Mez. 19:14.

Siku tulifunga ndoa

NILIJIFUNZA MAMBO MINGI KWA WANAUME WENYE HEKIMA NA WENYE UZOEFU

Mu miaka mingi yenye imepita, nimejifunza mambo ya maana sana kwa ndugu wenye hekima na wenye uzoefu. Ya kwanza kupita yote yenye nimejifunza ni hii: kama unapenda kutimiza mugao fulani wenye kuwa nguvu, ni muzuri ukuwe munyenyeku na utumikishe maneno yenye kuwa mu Mezali 15:22, yenye inasema: “Mambo yanatimizwa kupitia washauri wengi.”

Katika kazi ya muzunguko mu Ufaransa, mu 1965

Mu 1964, nilianza kujionea na macho yangu namna gani ile maneno ni ya kweli kabisa. Mu ile mwaka, nikakuwa mwangalizi wa muzunguko. Nilikuwa natembelea makutaniko juu ya kutia moyo ndugu na dada na kuwajenga kiroho. Lakini, nilikuwa tu na miaka 27 na sikukuwa na uzoefu kabisa. Njo maana nilikuwa nafanya makosa sana. Lakini ile makosa ilinifundisha mambo mingi. Zaidi ya yote, nilijifunza mambo ingine ya muzuri sana kwa “washauri” wenye kuwa na uzoefu.

Nakumbuka mambo fulani yenye ilinifikia wakati nilikuwa ningali tu mwangalizi wa mupya. Kisha kutembelea kutaniko moja mu muji wa Paris, ndugu mumoja mwenye kukomaa kiroho aliniuliza kama naweza kuongea naye. Nikamuambia: “Ndiyo, ni sawa.”

Akaniuliza: “Louis, unawaza doktere anatunzaka njo mugonjwa ao mutu mwenye iko na afya ya muzuri?”

Nikamuambia: “Mugonjwa.”

Akasema: “Njo vile. Lakini naona kama weye uko napitisha wakati sana na ndugu wenye wako wakomavu kiroho, sawa vile mwangalizi wa kutaniko. Mu kutaniko yetu, muko ndugu na dada wengi wenye walishavunjika moyo, wengine ni wapya, na wengine wako na haya. Watafurahia sana kama unapitisha wakati pamoja nao na hata kama unaenda kuwatembelea kwao na kula nao.”

Shauri ya ule ndugu ilikuwa ya muzuri sana. Upendo wenye alikuwa nao kwa ajili ya kondoo wa Yehova ulinigusa sana. Njo maana, hata kama haikukuwa mwepesi kukubali kama nilifanya kosa, bila kukawia nilianza kutumikisha mambo alisema. Nakuwaka namushukuru sana Yehova kwa kutupatia ndugu wengi sawa ule.

Mu 1969 na 1973, niliwekwa ili kusimamia departema yenye ilishugulikia mambo ya chakula ku mikusanyiko mbili ya kimataifa katika Colombes, kule Paris. Ku mukusanyiko wa 1973, kulikuwa watu 60 000 hivi wenye walipaswa kula chakula kwa siku tano! Niliishiwa kabisa. Lakini pale tena, niliona faida ya kutumikisha maneno yenye kuwa mu Mezali 15:22, ni kusema, kuomba shauri kwa wenye hekima. Niliomba mashauri kwa ndugu wenye kukomaa kiroho wenye walikuwa na uzoefu mu mambo yenye inahusu chakula. Kati ya wale ndugu kulikuwa wale wenye walikuwa wanafanya kazi ya kuua na kuuzisha nyama, wengine walikuwa walimaji wa mboga za majani, wengine walikuwa wapika-chakula, na wengine walizoea mambo ya kuuza vitu. Siye wote pamoja tuliweza kufanya ile kazi ya nguvu sana.

Mu 1973, miye na bibi yangu tulialikwa ili kutumikia ku Beteli ya Ufaransa. Mugao wangu wa kwanza ulikuwa nguvu sana. Kazi yangu ilipaswa kuwa kupelekea vichapo ndugu na dada wa inchi ya Cameroun, yenye kuwa mu Afrika, kwenye kazi yetu ilikuwa ilishakatazwa kati ya 1970 na 1993. Pale tena, niliishiwa kabisa. Pengine kisha kutambua hali yangu, ndugu mumoja mwenye alikuwa anasimamia kazi mu Ufaransa, alinitia moyo na akaniambia: “Ndugu zetu wa Cameroun wako na lazima ya chakula ya kiroho. Acha tuwasaidie waikule!” Na ni vile tulifanya.

Ku mukutano moja wa pekee mu Nigeria pamoja na Mashahidi wa Yehova wa Cameroun, mu 1973

Nilisafiri sana mu inchi zenye zilikuwa pembeni-pembeni ya Cameroun ili kukutana na wazee wenye walitoka Cameroun. Wale ndugu wenye uhodari na wenye hekima walikuwa wananisaidia kila mara ili kutumia ndugu zetu wa Cameroun vichapo. Yehova alibariki bidii yetu. Kwa kweli, kwa muda wa miaka 20, ndugu zetu mu ile inchi hawakukosa hata siku moja Munara wa Mulinzi na kichapo Utumishi Wetu wa Ufalme, yenye ilikuwa inatolewa kila mwezi.

Wakati miye na Angèle tulitembelea inchi ya Nigeria tukiwa pamoja na waangalizi wa mizunguko na bibi zao wenye walitoka Cameroun, mu 1977

NILIJIFUNZA MAMBO MINGI SANA KWA BIBI YANGU MUPENDWA

Tangu siku tulianza kujuana, niliona kama Angèle alikuwa na sifa mingi za kiroho. Na wakati tulioana zile sifa zilionekana tena wazi zaidi. Mangaribi ya siku yenye tulifunga ndoa, aliniomba nitoe sala juu ya kumuomba Yehova atusaidie tumutumikie kulingana na uwezo wetu, tukiwa bibi na bwana. Yehova alijibia ile sala.

Angèle alinisaidia pia nimutegemee zaidi Yehova. Muache niwafasirie mufano fulani: Mu 1973 tulialikwa ili kutumika ku Beteli. Ku mwanzo nilikuwa na mashaka juu nilipenda sana kazi ya muzunguko. Lakini Angèle alinikumbusha kama tulimutolea Yehova maisha yetu. Sasa juu ya nini hatungefanya mambo yenye tengenezo lake lilituomba tufanye? (Ebr. 13:17) Ningesema tena nini! Kwa hiyo, tukaenda ku Beteli. Kuishi na Angèle muda wa miaka yote hii, kumenisaidia kuona kama ni dada mwenye kuwa na hekima na usawaziko, na mwenye anamupenda kabisa Yehova. Zile sifa zimetia nguvu ndoa yetu na zimetusaidia kukamata maamuzi ya muzuri.

Miye na Angèle mu bustani ya Beteli ya Ufaransa

Hata kama tulishazeeka, Angèle anaendelea kunitegemeza kabisa, ni bibi muzuri kweli. Kwa mufano, juu ya kusoma masomo fulani ya kiteokrasi, yenye mingi kati ya ile masomo inafanyiwa mu Kiingereza, miye na Angèle tulifanya yetu yote ili kujua muzuri luga ya Kiingereza. Ile ilifanya tuhamie mu kutaniko la luga la Kiingereza hata kama ile wakati tulikuwa na miaka 70 hivi. Juu niko mushiriki wa Halmashauri ya Tawi ya Ufaransa, kujifunza luga ingine haiko mwepesi. Lakini Angèle na miye tumesaidiana sana. Leo tuko na miaka 80 hivi, na tunaendelea kutayarisha mikutano mu Kiingereza na mu Kifaransa. Tunajikaza pia ili kuhubiri na kukusanyika pamoja na kutaniko letu. Yehova amebariki bidii yetu ya kujifunza Kiingereza.

Mu 2017, tulipata baraka moja ya pekee. Miye na Angèle tulipata pendeleo la kuenda kusoma masomo ya Washiriki wa Halmashauri za Tawi na Bibi Zao, yenye ilifanywa kule New York, ku Mahali pa Elimu ya Watchtower katika Patterson.

Yehova njo Mufundishaji Mukubwa. (Isa. 30:20) Njo maana hatushangae kuona watu wake, ikuwe wazee ao vijana, wako wanapata elimu ya muzuri sana! (Kum. 4:5-8) Kwa kweli, nimeona kama vijana wenye wanamusikiliza Yehova na wenye wanasikiliza ndugu na dada wenye kuwa na uzoefu wanafanya maendeleo ya muzuri sana ya kiroho na wanakuwa watumishi waaminifu kabisa wa Yehova. Mezali 9:9 inatukumbusha hivi: “Patia mwenye hekima, na atakuwa mwenye hekima zaidi. Fundisha mwenye haki, na elimu yake itaongezeka.”

Wakati fulani, nakumbukaka mambo yenye ilinifikiaka ile usiku wakati tulikuwa mu milima ya Algérie, kumepita sasa miaka 60 hivi. Ile usiku, sikukuwa nawazia hata kidogo mambo ya muzuri yenye ilikuwa inanichunga. Nilijifunza mambo mingi sana kwa wengine! Miye na Angèle tumeona namna gani Yehova amebariki sana maisha yetu. Njo maana tunaazimia kuendelea kujifunza mambo mingi kuhusu Baba yetu wa mbinguni na kujifunza mambo mingi kwa ndugu na dada wenye hekima na wenye uzoefu, wenye wanamupenda Yehova.

^ fu. 11 Biblia Tafsiri ya Ulimwengu Mupya.