Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Mutume Paulo alimaanisha nini wakati alisema: “Kupitia sheria nilikufa kuelekea sheria”?​—Gal. 2:19.

Paulo aliandika: “Kupitia sheria nilikufa kuelekea sheria, ili nikuwe muzima kuelekea Mungu.”​—Gal. 2:19.

Maneno yenye Paulo aliandika ilipatana na wazo kubwa yenye alipenda ndugu na dada wenye kuwa mu makutaniko mbalimbali yenye kuwa Galatia kule Roma waelewe. Wakristo fulani kule walichochewa na walimu wa uongo. Wale wanaume walikuwa wanafundisha kama juu mutu apate wokovu alipaswa kufuata mambo yenye Sheria ya Musa ilisema, zaidi sana kutahiriwa. Lakini, Paulo alijua kama Mungu hakuomba tena waamini watahiriwe. Njo maana alifikiri mu njia yenye kusadikisha na kuonyesha kama ile mafundisho ilikuwa ya uongo, na alitia nguvu imani ya ndugu na dada katika zabihu ya bei ya ukombozi ya Yesu.​—Gal. 2:4; 5:2.

Biblia inaonyesha waziwazi kama wakati mutu anakufa, hajue tena kitu ao hakuna kitu kinaweza kumusumbua. (Muh. 9:5) Wakati Paulo alisema: “Nilikufa kuelekea sheria,” alimaanisha kama Sheria ya Musa haikukuwa tena na uwezo wowote juu yake. Lakini, Paulo alikuwa hakika kama kupitia imani yake katika bei ya ukombozi, ‘alifikia kuwa muzima kuelekea Mungu.’

Ile badiliko ilimupata Paulo “kupitia sheria.” Namna gani? Yeye mwenyewe alifasiria mbele kama “mutu anatangazwa kuwa mwenye haki, hapana kupitia matendo ya sheria, lakini kupitia tu imani katika Yesu Kristo.” (Gal. 2:16) Kwa kweli, Sheria ilitimiza jambo moja ya maana sana. Paulo alifasiria Wagalatia hivi: “Iliongezwa ili kufanya makosa yakuwe wazi, mupaka uzao ufike wenye ulikuwa umepewa ahadi.” (Gal. 3:19) Ndiyo, Sheria ilionyesha waziwazi kama wanadamu wenye hawakamilike ao watenda-zambi hawawezi kushika Sheria yenye kuwa kamilifu na kama walikuwa na lazima ya zabihu yenye kuwa kamilifu. Kwa hiyo, Sheria iliongoza watu kwa “uzao,” ni kusema, Kristo. Wakati mutu anaonyesha imani katika Yesu Kristo, anatangazwa kuwa mwenye haki mbele ya Mungu. (Gal. 3:24) Paulo alifikia ku ile wazo juu kupitia Sheria alifikia kumukubali Yesu na kutia imani katika yeye. Kwa hiyo, Paulo ‘alikufa kuelekea sheria’ na alifikia ‘kuwa muzima kuelekea Mungu.’ Sheria haikukuwa tena na uwezo juu yake, lakini Mungu, ndiyo.

Paulo alizungumuzia wazo yenye kufanana na ile mu barua yenye aliandikia Waroma. Aliwaambia hivi: “Ndugu zangu, ninyi pia mulifanywa kuwa wafu kuhusiana na Sheria kupitia mwili wa Kristo . . . sasa tumefunguliwa kutoka katika Sheria, kwa sababu tumekufa kuhusiana na kile chenye kilituzuia.” (Ro. 7:4, 6) Hii andiko na ile ya Wagalatia 2:19, inaonyesha kama Paulo hakukuwa anazungumuzia kufa kama mutenda-zambi mwenye alihukumiwa chini ya Sheria. Lakini, alikuwa anazungumuzia kuwekwa huru. Sheria haikukuwa na uwezo wowote juu yake ao juu ya wengine sawa yeye. Waliwekwa huru kupitia imani katika bei ya ukombozi ya Kristo.