Amila mo ibi abali

Amila mu gagabi

MAKALA JA FUNZO 26

Bo, Guwesa Kushiliki Nkasi ju Kuenga Wanafunze?

Bo, Guwesa Kushiliki Nkasi ju Kuenga Wanafunze?

“Mungu . . . jwachoche, nu kwapeke amu ni makili gu kuhenga.”​—FLP. 2:13, Tafsiri ya Ulimwengu Mpya.

NHAMBU 64 Kuyashiriki Mavuno kwa Furaha

MUHTASARI *

1. Yehova juguengi kike?

ULIKUJAJE kuwa Shahidi wa Yehova? Kwanza, ulisikia “habari njema”—labda kutoka kwa wazazi wako, mfanyakazi au mwanafunzi mwenzako, au kupitia kazi ya kuhubiri nyumba kwa nyumba. (Marko 13:10) Kisha, mtu fulani alitumia muda na jitihada nyingi kukufundisha Biblia. Kupitia funzo hilo, ulianza kumpenda Yehova na ulijifunza kwamba anakupenda wewe pia. Yehova alikuvuta katika kweli, na sasa ukiwa mwanafunzi wa Yesu Kristo, una tumaini la kuishi milele. (Yoh. 6:44) Bila shaka unamshukuru sana Yehova kwa kumchochea mtu fulani akufundishe kweli na kwa kukukubali kuwa mtumishi Wake.

2. Msitulongalya ki mu makala jenzeno?

2 Sasa kwa kuwa tunaijua kweli, tuna pendeleo la kuwasaidia wengine wajiunge nasi kwenye barabara ya uzima. Huenda ni rahisi kwetu kuhubiri nyumba kwa nyumba, lakini huenda tukaona kuwa vigumu kuanzisha na kuongoza mafunzo ya Biblia. Je, hivyo ndivyo unavyohisi? Ikiwa ndivyo, huenda baadhi ya mapendekezo katika makala hii yakakusaidia. Tutazungumzia mambo yanayotuchochea tushiriki katika kazi ya kufanya wanafunzi. Pia, tutachunguza jinsi tunavyoweza kushinda changamoto zinazoweza kutufanya tusite kuongoza funzo la Biblia. Kwanza, acheni tuchunguze kwa nini hatupaswi kuwa wahubiri tu, bali pia walimu wa habari njema.

YESU JUTUPEKYA AMLI TUUBILYA NU KUPUNDISA

3. Ndaba jaki tutenda kuhubili?

3 Yesu alipokuwa duniani aliwapa wafuasi wake amri yenye sehemu mbili. Kwanza, aliwaambia wahubiri habari njema za Ufalme, na aliwaonyesha jinsi ya kufanya hivyo. (Mt. 10:7; Luka 8:1) Kati ya mambo ambayo Yesu alifanya, ni kuwatayarisha wanafunzi wake ili wajue jinsi ya kutenda ikiwa watu wangeitikia vizuri au kukataa ujumbe wa Ufalme. (Luka 9:2-5) Pia, alitabiri kuhusu ukubwa wa kazi yao ya kuhubiri, akiwaambia kwamba wafuasi wake wangetoa “ushahidi kwa mataifa yote.” (Mt. 24:14; Mdo. 1:8) Haidhuru watu wangeitikia jinsi gani, wanafunzi wa Yesu walihitaji kuwaambia watu kuhusu Ufalme wa Mungu na mambo ambayo ungetimiza.

4. Kulengana na Mathayo 28:18-20, zaidi ju kuhubili kuusu Ufalme, jibi lasima tuenga ki senge?

4 Sehemu ya pili ya amri ya Yesu ni nini? Aliwaambia wafuasi wake wawafundishe watu wenye mwelekeo wa kuwa wanafunzi, kushika mambo yote aliyowaamuru. Je, kazi ya kuhubiri na kufundisha iliwahusu tu wanafunzi wa karne ya kwanza, kama baadhi ya watu wanavyodai? Hapana, Yesu alionyesha kwamba kazi hii muhimu ingeendelea hadi siku zetu, “mpaka umalizio wa mfumo wa mambo.” (Soma Mathayo 28:18-20.) Inaelekea Yesu alitoa amri hiyo alipowatokea wanafunzi wake zaidi ya 500. (1 Kor. 15:6) Na katika ufunuo aliompatia Yohana, Yesu alionyesha wazi kwamba wanafunzi wake wote wanatazamiwa wawasaidie wengine wajifunze kumhusu Yehova.—Ufu. 22:17.

5. Kulengana na 1 Wakorintho 3:6-9, Paulo jwaboa nfanu bo gogulangi uusianu gogubi kati ju kuhubili nu kupundisa?

5 Mtume Paulo alilinganisha kazi ya kufanya wanafunzi na kupanda mmea ili kuonyesha kwamba ni lazima tufanye mengi zaidi ya kupanda tu mbegu. Aliwakumbusha hivi Wakorintho: “Mimi nilipanda, Apolo akatia maji . . . Ninyi ni shamba la Mungu linalolimwa.” (Soma 1 Wakorintho 3:6-9.) Tukiwa wafanyakazi katika “shamba la Mungu,” hatupandi tu mbegu, bali pia tunazitia maji na kukagua kwa ukawaida maendeleo ya mimea yetu. (Yoh. 4:35) Na wakati huohuo, tunatambua kwamba ni Mungu anayefanya mbegu hizo zikue.

6. Kasi ju kupundisa jiusisha kike?

6 Tunawatafuta wale walio na “mwelekeo unaofaa kwa ajili ya uzima wa milele.” (Mdo. 13:48) Ili kuwasaidia watu hao wawe wanafunzi wa Kristo, ni lazima tuwasaidie (1) kuelewa, (2) kukubali, na (3) kufanyia kazi mambo wanayojifunza katika Biblia. (Yoh. 17:3; Kol. 2:6, 7; 1 The. 2:13) Wote kutanikoni wanaweza kuwasaidia wanafunzi wa Biblia kwa kuweka mfano mzuri wa kuwaonyesha wapya upendo, na kuwafanya wahisi wakiwa wamekaribishwa wanapohudhuria mikutano. (Yoh. 13:35) Huenda anayeongoza funzo la Biblia akahitaji pia kutumia muda na jitihada nyingi ili kumsaidia mwanafunzi apindue imani na mazoea yaliyo kama “ngome zenye nguvu.” (2 Kor. 10:4, 5) Huenda ikachukua miezi mingi kumsaidia mtu afanye mabadiliko hayo ili mwishowe afikie hatua ya ubatizo. Lakini jitihada hizo si za bure.

UPALANI GUTUCHOCHE KUENGA WANAFUNZI

7. Ki sesutuchoche kushiliki nkasi ju kuhubili nu kuenga wanafunzi?

7 Kwa nini tunashiriki katika kazi ya kuhubiri na kufanya wanafunzi? Kwanza, ni kwa sababu tunampenda Yehova. Unapofanya yote unayoweza ili kutii amri ya kuhubiri na kufanya wanafunzi, unaonyesha upendo wako kwa Mungu. (1 Yoh. 5:3) Fikiria hili: Upendo wako kwa Yehova tayari umekuchochea kuhubiri nyumba kwa nyumba. Je, ilikuwa rahisi kutii amri hiyo? Huenda hapana. Je, ulikuwa na wasiwasi ulipoenda kuhubiri nyumba kwa nyumba kwa mara ya kwanza? Bila shaka! Lakini ulijua kwamba hii ni kazi ambayo Yesu anataka uifanye, nawe ulitii amri hiyo. Na labda baada ya muda kupita, imekuwa rahisi zaidi kwako kushiriki katika kazi ya kuhubiri. Lakini namna gani kuhusu kuongoza funzo la Biblia? Je, wazo tu la kuongoza funzo la Biblia hukupa wasiwasi? Huenda. Hata hivyo, ukimwomba Yehova akusaidie ushinde wasiwasi wako na kupata ujasiri wa kuongoza funzo la Biblia, anaweza kukusaidia uimarishe tamaa yako ya kufanya wanafunzi.

8. Kulengana na Marko 6:34, lijambu bo lengi leliwesa kutuchoche twapundisa bange?

8 Pili, upendo kwa jirani zetu unatuchochea tuwafundishe kweli. Pindi moja, Yesu na wanafunzi wake walikuwa wamechoka baada ya kuhubiri kwa muda mrefu sana. Walihitaji mahali ambapo wangepumzika, lakini umati mkubwa wa watu ukawafuata. Yesu aliwasikitikia watu hao na kuanza kuwafundisha “mambo mengi.” (Soma Marko 6:34.) Pindi hiyo, Yesu alijitoa sana licha ya kwamba alikuwa amechoka. Kwa nini? Yesu alijiweka katika hali ya watu hao. Aliona jinsi walivyokuwa wakiteseka—jinsi walivyohitaji tumaini—naye alitaka kuwasaidia. Leo, watu wana hali hiyohiyo. Usipotoshwe na jinsi wanavyoonekana kwa nje. Wao ni kama kondoo wanaotanga-tanga, bila kuwa na mchungaji wa kuwaongoza. Mtume Paulo aliwafafanua watu hao kuwa wasio na Mungu na hawana tumaini. (Efe 2:12) Wako kwenye “barabara inayoongoza kwenye uharibifu”! (Mt. 7:13) Tunapofikiria hali ya kiroho ya watu walio katika eneo letu, sifa ya upendo na huruma zitatuchochea tuwasaidie. Na njia bora tunayoweza kuwasaidia ni kwa kuwapendekezea wajifunze Biblia pamoja nasi.

9. Kulengana na Wafilipi 2:13, Yehova juwesa kugujangati bole?

9 Huenda unasita kuanzisha funzo la Biblia kwa sababu unatambua kwamba utahitaji kutumia muda mwingi kutayarisha na kuongoza funzo hilo. Ikiwa unahisi hivyo, mweleze Yehova hisia zako. Mwombe akusaidie kusitawisha tamaa ya kutafuta na kuongoza funzo la Biblia. (Soma Wafilipi 2:13.) Mtume Yohana alituhakikishia kwamba Mungu atajibu sala zinazopatana na mapenzi Yake. (1 Yoh. 5:14, 15) Hivyo, unaweza kuwa na hakika kwamba Yehova atakusaidia usitawishe tamaa ya kushiriki katika kazi ya kufanya wanafunzi.

KUSHINDA CHANGAMOTU JENGI

10-11. Tosa ndaba jaki tuwesa kusita kuongoza lifunzu la Bibilia?

10 Tunachukua kwa uzito amri ya kufundisha hata ingawa tunakabili changamoto ambazo huenda zikatuzuia kufanya yote tunayotaka kutimiza katika kazi ya kufanya wanafunzi. Acheni tuchunguze baadhi ya changamoto hizo na jinsi tunavyoweza kuzishinda.

11 Huenda tukahisi hali zetu zinatuzuia kutimiza yote ambayo tungependa kufanya. Kwa mfano, baadhi ya wahubiri wana umri mkubwa au wana matatizo ya afya. Je, unapitia hali kama hizo? Ikiwa ndivyo, fikiria jambo moja ambalo tumejifunza kutokana na janga la COVID-19. Tumejionea kwamba tunaweza kuongoza mafunzo ya Biblia yanayofanya maendeleo kwa kutumia simu na vifaa vingine vya kielektroni! Hivyo, unaweza kuanzisha na kuongoza funzo la Biblia ukiwa nyumbani kwako. Kuna faida nyingine pia. Baadhi ya watu wangependa kujifunza Biblia lakini hawapatikani muda ambao kwa kawaida ndugu zetu wametenga kwa ajili ya kuhubiri. Hata hivyo, watu hao wanaweza kupatikana asubuhi na mapema au usiku. Je, uko tayari kutumia wakati huo ili kuongoza mafunzo hayo? Yesu alimfundisha Nikodemo usiku, wakati ambao Nikodemo alipendelea.—Yoh. 3:1, 2.

12. Gabi mambu bo gagawesa kutujangati kujiamini ngani na kuba twaka mwalimu bina matokeo?

12 Huenda tukatilia shaka uwezo wetu wa kuongoza funzo la Biblia. Labda tunahisi kwamba tunahitaji kuwa na ujuzi au ustadi zaidi wa kufundisha kabla ya kujifunza Biblia na mtu. Ikiwa unahisi hivyo, fikiria mambo matatu yanayoweza kukusaidia ujiamini zaidi. Kwanza, Yehova anaona kwamba unastahili kuwafundisha wengine. (2 Kor. 3:5) Pili, Yesu, aliye na “mamlaka yote mbinguni na duniani,” amekuamuru uwafundishe wengine. (Mt. 28:18) Tatu, unaweza kupata msaada kutoka kwa wengine. Yesu alitegemea mambo ambayo Baba yake alimfundisha aseme, nawe unaweza kufanya vivyo hivyo. (Yoh. 8:28; 12:49) Zaidi ya hayo, unaweza kumwomba mwangalizi wako wa kikundi cha utumishi, painia, au mhubiri mwenye uzoefu akusaidie kuanzisha na kuongoza funzo la Biblia. Njia moja inayoweza kukusaidia ujiamini zaidi ni kushiriki kwenye funzo la Biblia linaloongozwa na mmoja kati ya wahubiri hao.

13. Ndabajaki tuitaji kuba tayali kuyobale indela inyai yu kupundisa?

13 Huenda tukaona kuwa changamoto kuzoea mbinu na vifaa vipya. Kwa sasa, njia tunayotumia kuongoza mafunzo ya Biblia imebadilika. Kitabu chetu cha msingi cha kujifunza pamoja na watu, Furahia Maisha Milele!, kinahitaji tujitayarishe kwa ajili ya funzo na kuliongoza kwa njia tofauti na tulivyokuwa tukifanya wakati uliopita. Tunasoma mafungu machache zaidi na funzo linaongozwa kwa njia ya mazungumzo zaidi. Tunapofundisha tunatumia zaidi video, habari zinazopatikana kwenye tovuti yetu, na JW Library®. Ikiwa huna uzoefu wa kutumia vifaa hivyo, zungumza na mtu anayeweza kukufundisha jinsi ya kuvitumia. Tukiwa wanadamu tunapenda kufanya mambo kwa njia tuliyozoea. Si rahisi kwetu kuzoea njia mpya za kufanya mambo. Lakini kwa msaada wa Yehova na msaada wa wengine, utakuja kuzoea njia hizo na hata utafurahia zaidi kujifunza na watu. Painia mmoja alisema kwamba njia hii ya kujifunza “inamburudisha mwanafunzi na mwalimu.”

14. Tupaswa kukomboka ki patuhubili mulieneu ambalu bandu ngase pendezwa nu ujumbi gwitu, na 1 Wakorintho 3:6, 7 lutujege mwoju jinsi bole?

14 Huenda tunaishi kwenye eneo ambalo si rahisi kuanzisha mafunzo ya Biblia. Huenda watu wakaonekana hawapendezwi na ujumbe wetu au hata kuupinga. Ni nini kinachoweza kutusaidia tuwe na mtazamo unaofaa tunapokuwa kwenye eneo kama hilo? Kumbuka kwamba hali za watu zinaweza kubadilika haraka katika ulimwengu huu wenye misukosuko, na watu hao ambao wakati fulani hawakupendezwa, huenda wakaanza kutambua uhitaji wao wa kiroho. (Mt. 5:3) Baadhi ya watu ambao wakati uliopita walikataa machapisho yetu, baadaye walikubali funzo la Biblia. Pia, tunajua kwamba Yehova ndiye Bwana wa mavuno. (Mt. 9:38) Anataka tuendelee kupanda na kutia maji, lakini Yeye ndiye anayekuza. (1 Kor. 3:6, 7) Inatia moyo sana kukumbuka kwamba hata ikiwa hatuwezi kuongoza funzo la Biblia kwa sasa, Yehova atatuthawabisha kwa msingi wa jitihada zetu, na si matokeo! *

PATA SHANGWI JU KUENGA WANAFUNZI

15. Yehova juisi bo mundu ejujetake kulibola Bibilia nu kuenga kulengana na mambu gajulibolike?

15 Yehova hushangilia mtu anapokubali kweli za Biblia na kushiriki na wengine kweli hizo. (Met. 23:15, 16) Kwa kweli, lazima Yehova anafurahi sana anapoona watu wake wakihubiri na kufundisha kwa bidii! Kwa mfano, licha ya janga la COVID-19, katika kipindi cha mwaka wa utumishi wa 2020, mafunzo 7,705,765 yaliongozwa, ambayo yaliwasaidia watu 241,994 kujiweka wakfu kwa Yehova na kubatizwa. Wanafunzi hao wapya wa Kristo nao pia wataongoza mafunzo ya Biblia na kufanya wanafunzi zaidi. (Luka 6:40) Bila shaka, tunamfanya Yehova afurahi tunaposhiriki katika kazi ya kufanya wanafunzi.

16. Tuwesa kulibeke lilengu bo lasape?

16 Kufanya wanafunzi ni kazi ngumu, lakini kwa msaada wa Yehova tunaweza kutimiza sehemu yetu katika kuwafundisha wapya wampende Baba yetu wa mbinguni. Je, tunaweza kujiwekea lengo la kuanzisha na kuongoza angalau funzo moja la Biblia? Huenda tukashangazwa na matokeo tunayopata tunapotumia kila fursa inayofaa, kuwauliza wale tunaokutana nao ikiwa wangependa kujifunza Biblia pamoja nasi. Tunaweza kuwa na hakika kwamba Yehova atabariki jitihada zetu.

17. Twiisia bo ana twiwesa kuongoza lifunzu la Bibilia?

17 Tuna pendeleo kubwa sana la kuhubiri na pia kuwafundisha wengine kweli! Kazi hiyo inatupatia furaha ya kweli. Mtume Paulo aliyewasaidia watu wengi katika Thesalonike kuwa wanafunzi, alieleza hisia zake hivi: “Ni nini tumaini letu au shangwe au taji la furaha mbele ya Bwana wetu Yesu wakati wa kuwapo kwake? Je, kwa kweli si ninyi? Kwa kweli ninyi ndio utukufu na shangwe yetu.” (1 The. 2:19, 20; Mdo. 17:1-4) Wengi leo wanahisi vivyo hivyo. Dada anayeitwa Stéphanie, ambaye pamoja na mume wake wamewasaidia watu wengi kufikia hatua ya ubatizo anasema hivi: “Hakuna shangwe kubwa kuliko ile ya kuwasaidia watu wajiweke wakfu kwa Yehova.”

NHAMBU 57 Kuwahubiria Watu wa Namna Zote

^ ekichweka 5 Yehova hajatupatia tu pendeleo la kuwahubiria wengine, bali pia la kuwafundisha mambo yote ambayo Yesu aliamuru. Ni nini kinachotuchochea tutake kuwafundisha wengine? Tunapata changamoto gani katika kazi ya kuhubiri na kufanya wanafunzi? Na tunaweza kushindaje changamoto hizo? Makala hii itajibu maswali hayo.

^ ekichweka 14 Kwa maelezo zaidi kuhusu sehemu tunayotimiza katika kazi ya kufanya wanafunzi, tazama makala “Mkiwa Kutaniko, Wasaidieni Wanafunzi wa Biblia Wafikie Hatua ya Ubatizo,” iliyochapiswa katika gazeti la Mnara wa Mlinzi la Machi 2021.

^ ekichweka 53 MAELEZO YA PICHA: Ona mabadiliko ambayo mtu anaweza kufanya kwa kujifunza Biblia: Mwanzoni maisha ya mwanamume huyo yanaonekana hayana kusudi, ametengwa mbali na Yehova. Kisha Mashahidi wanakutana naye wanapohubiri, naye anakubali funzo la Biblia. Mambo anayofundishwa yanamwongoza kwenye wakfu na ubatizo. Baada ya muda, yeye pia anashiriki katika kazi ya kufanya wanafunzi. Mwishowe, wote wanafurahia maisha katika Paradiso.