Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 27

Tuige Uvumilivu wa Yehova

Tuige Uvumilivu wa Yehova

“Kupitia uvumilivu wenu mutaokoa uzima wenu.”​—LU. 21:19.

WIMBO 114 “Mukuwe na Uvumilivu”

KIFUPI YA HABARI *

1-2. Namna gani maneno ya Yehova yenye kuwa mu Isaya 65:16, 17 inatutia moyo tuendelee kuvumilia?

“USIACHE HATA KIDOGO!” njo ilikuwa kichwa ya programu ya mukusanyiko wa eneo wa 2017. Ile programu ilituonyesha namna tunaweza kuvumilia magumu yenye inatufikia. Kulishapita miaka ine tangu tulifuata ile mukusanyiko na tunaendelea kuvumilia magumu mu hii dunia.

2 Mu masiku yenye imepita umepata magumu gani? Kuko mutu wa familia yako ao rafiki yako mwenye amekufa? Uko na ugonjwa wa nguvu sana? Uko unateseka juu ya uzee? Ulipatwa na musiba wa asili, ulitendewa kwa jeuri, ao uko unateswa? Ao pengine uko unateseka juu ya ugonjwa kama vile Corona? Tunangojea kwa hamu wakati ile magumu yote itakuwa ya zamani, hatutaikumbuka na haitakuwaka tena!​—Soma Isaya 65:16, 17.

3. Tunapaswa kufanya nini sasa, na juu ya nini?

3 Maisha iko nguvu mu hii dunia, na pengine mu masiku yenye kuja tutapata magumu mingi sana. (Mt. 24:21) Kwa hiyo, tunapaswa kuendelea kutia nguvu uvumilivu wetu. Juu ya nini? Juu Yesu alisema: “Kupitia uvumilivu wenu mutaokoa uzima wenu.” (Lu. 21:19) Kufikiri kuhusu namna wengine wako wanavumilia magumu ya kufanana na yetu, kunaweza kutusaidia na siye tuendelee kuvumilia.

4. Juu ya nini tunasema kama Yehova ni mufano muzuri kabisa wa uvumilivu?

4 Ni nani mwenye kuwa mufano muzuri kabisa wa uvumilivu? Ni Yehova Mungu. Ile jibu inakushangaza? Pengine. Lakini kama unawaza muzuri, ile haitakushangaza. Ibilisi njo anatawala hii dunia na njo maana inayala magumu mingi. Hata kama Yehova iko na nguvu ya kumaliza ile magumu yote wakati wowote, iko anangojea wakati wenye kuja ili kufanya vile. (Ro. 9:22) Mungu wetu anaendelea kuvumilia mupaka wakati wenye ataharibu ulimwengu huu ufike. Tuone mambo kenda yenye Yehova iko anavumilia.

YEHOVA IKO ANAVUMILIA MAMBO GANI?

5. Namna gani jina ya Mungu imechafuliwa, na unajisikia namna gani kuhusu ile?

5 Kuchafuliwa kwa jina yake. Yehova anapenda jina yake, na anapenda kila mutu aiheshimie. (Isa. 42:8) Lakini jina yake imechafuliwa kwa miaka elfu sita hivi. (Zb. 74:10, 18, 23) Ile ilianza mu bustani ya Edeni wakati Ibilisi (maana yake “Musingiziaji”) alisema kama Mungu iko anaima Adamu na Eva kitu fulani yenye walikuwa nayo lazima ili wakuwe na furaha. (Mwa. 3:1-5) Tangu ile wakati, wamemusemea Yehova uongo kama iko anaima watu mambo yenye wako nayo lazima kabisa. Yesu alihuzunika juu jina ya Baba yake ilichafuliwa. Njo maana alifundisha wanafunzi wake wasali hivi: “Baba yetu mwenye kuwa mbinguni, jina lako litakaswe.”​—Mt. 6:9.

6. Juu ya nini Yehova aliacha wakati ipite ili kuonyesha kama yeye njo iko na haki ya kutawala?

6 Kupingwa kwa mamlaka yake makubwa. Ni Yehova tu njo iko na haki ya kutawala mbingu na dunia, na namna yake ya kutawala njo ya muzuri zaidi. (Ufu. 4:11) Lakini Ibilisi alijaribu kudanganya malaika na watu kama Mungu hana ile haki. Iliomba wakati ili kuonyesha waziwazi kama Yehova njo iko na ile haki, na kama yeye njo Mutawala muzuri kabisa. Kwa hekima, Yehova ameacha watu wajiongoze wao wenyewe kwa wakati fulani ili wafikie kuona kama, hawataweza kujiongoza muzuri bila kumutii. (Yer. 10:23) Juu Yehova amevumilia, watu wote watafikia kujionea kama yeye njo iko na ile haki ya kuongoza wanadamu. Kwa hiyo, wote watajua kama ni Ufalme wa Yehova tu njo utaleta amani na usalama wa kweli ku dunia.

7. Nani njo waliasi Yehova, na atawatendea namna gani?

7 Uasi wa watoto wake fulani. Wakati Yehova aliumba malaika na wanadamu, walikuwa wakamilifu bila kasoro yoyote. Lakini malaika wake mumoja, ni kusema, Shetani (maana yake “Mupinzani”) alimupinga na akasadikisha watu wakamilifu, Adamu na Eva, wamupinge pia. Malaika na watu wengine pia walijiunga mu uasi wake. (Yud. 6) Tena, hata Waisraeli, watu wenye Mungu alichagula kuwa taifa yake, walimukatala na kuanza kuabudu miungu ya uongo. (Isa. 63:8, 10) Yehova alisalitiwa kabisa. Hata vile, iko anavumilia na anaendelea kuvumilia mupaka wakati ataharibu waasi wote. Ile itafanya watumishi washikamanifu wa Yehova, wenye wako wanavumilia pamoja naye, wakuwe na furaha!

8-9. Ni uongo gani unasemwa kuhusu Yehova, na tunaweza kufanya nini ili kuonyesha kama mambo yenye wako wanasema juu yake ni ya uongo?

8 Mambo ya uongo yenye Ibilisi anaendelea kusema juu yake. Shetani alisema kama Yobu na watumishi waaminifu wote hawamutumikie Yehova bure. (Yob. 1:8-11; 2:3-5) Ibilisi anaendelea kusema ule uongo kuhusu watu mupaka leo. (Ufu. 12:10) Tunaweza kuonyesha kama Shetani alisema uongo kwa kuendelea kuvumilia magumu na kubakia waaminifu kwa Yehova sababu tunamupenda. Kama vile alimubariki Yobu, atatubariki pia kama tunavumilia.​—Yak. 5:11.

9 Shetani anatumikisha viongozi wa dini ili kusema kama Yehova njo anatesaka watu. Wengine wanafikia hata kusema kama wakati watoto wanakufa, Mungu njo anawabeba juu iko na lazima ya malaika wengi mbinguni. Ile haimuheshimishe Mungu hata kidogo! Tunajua muzuri kama Yehova ni Baba mwenye upendo. Wakati tunapambana na ugonjwa wa nguvu ao wakati mutu fulani mwenye tunapendaka anakufa tusiseme kama ni kosa ya Mungu. Tunatumainia kama siku moja atatengeneza mambo yote. Tunaweza kuambia kila mutu mwenye anapenda kusikia kama Yehova ni Mungu wa upendo. Ile inamusaidia kujibia muzuri ule mwenye iko anamuchokoza.​—Mez. 27:11.

10. Zaburi 22:23, 24 inaonyesha nini juu ya Yehova?

10 Mateso ya watumishi wake wapendwa. Yehova ni Mungu wa huruma. Anasikiaka mubaya wakati tunalia juu ya mateso, ikuwe upinzani, magonjwa, ao kutokamilika kwetu. (Soma Zaburi 22:23, 24.) Yehova anajua maumivu yetu; anapenda kuimaliza na ataimaliza. (Linganisha na Kutoka 3:7, 8; Isaya 63:9.) Kuko siku “atapanguza kila chozi katika macho [yetu], na kifo hakitakuwa tena, wala maombolezo wala kilio wala maumivu havitakuwa tena.”​—Ufu. 21:4.

11. Yehova anajisikiaka namna gani kuhusu wanaume na wanamuke waaminifu wenye walishakufa?

11 Kifo ya marafiki wake. Yehova anajisikiaka namna gani kuhusu wanaume na wanamuke waaminifu wenye walishakufa? Anatamani kuwaona tena! (Yob. 14:15) Wazia namna Yehova iko anamukumbuka sana rafiki yake Abrahamu! (Yak. 2:23) Halafu Musa, mwenye alikuwa anaongea naye “uso kwa uso”? (Kut. 33:11) Na wazia namna Yehova anangojea kwa hamu kusikia tena Daudi na waandikaji wengine wa zaburi wako wanaimba nyimbo za muzuri sana za sifa! (Zb. 104:33) Hata kama wale marafiki wa Mungu walishakufa, Yehova hawasahau hata kidogo. (Isa. 49:15) Anakumbuka kila kitu juu ya utu wao. Biblia inasema kama, “kwa maoni yake wote ni wazima.” (Lu. 20:38, maelezo ya chini) Siku moja, atawafufua, na atakuwa anasikiliza tena sala zao za kutoka ku moyo, na kukubali ibada yao. Kama ulishapoteza mupendwa wako katika kifo, hii mawazo inaweza kukufariji na kukutia nguvu.

12. Nini njo inamuhuzunisha Yehova zaidi sana mu hizi siku za mwisho?

12 Kuona watu wabaya wako wanatesa wengine. Wakati uasi ulianza mu Edeni, Yehova alijua kama hali zingekuwa mubaya sana mbele mambo ikuwe muzuri. Yehova anachukia uovu, ukosefu wa haki, na jeuri yenye iko mu dunia leo. Sikuzote anahangaikiaka zaidi sana wale wenye kuwa zaifu, sawa vile watu wenye hawana mutu wa kuwatetea, mayatima, na wajane. (Zek. 7:9, 10) Yehova anahuzunikaka zaidi sana, wakati anaona watumishi wake waaminifu wako wanateswa na kufungwa. Ukuwe hakika kama, anapenda wale wote wenye kuvumilia pamoja naye.

13. Namna gani mwenendo wa wanadamu umeharibika, na Mungu atafanya nini juu ya ile?

13 Kuharibika kwa mwenendo wa wanadamu. Shetani anapenda watu wenye waliumbwa kwa mufano wa Mungu wafanye matendo ya mubaya. Wakati Mungu ‘aliona kwamba uovu wa mwanadamu ulikuwa mwingi’ katika siku za Noa, “Yehova akasikitika kwamba alikuwa ameumba wanadamu kwenye dunia, na akaumia katika moyo wake.” (Mwa. 6:5, 6, maelezo ya chini, 11) Tangu ile wakati, mambo imekuwa muzuri? Hapana! Ibilisi anafurahi sana wakati anaona kama uasherati wa kila namna unaongezeka, ikuwe ngono kati ya wanaume na wanamuke na ngono kati ya wanaume na wanaume na ile ya wanamuke na wanamuke! (Efe. 4:18, 19) Wakati Shetani anaangusha muabudu wa Yehova katika zambi, anafurahiaka hata zaidi. Wakati uvumilivu wa Yehova utafika mwisho, ataonyesha kama anachukia sana mwenendo muchafu kwa kuharibu watu wote wenye kuwa na ile mwenendo wenye hawapendi kubadilika.

14. Namna gani watu wako wanaharibu dunia yenye Yehova aliumba?

14 Kuharibiwa kwa dunia. Mwanadamu ‘hamutawale tu mwanadamu mwenzake ili kumuumiza’ lakini iko pia anaharibu dunia na wanyama wenye Yehova alimupatia achunge. (Muh. 8:9; Mwa. 1:28) Wanasayansi fulani, walishasema kama mambo yenye mwanadamu iko anafanya inaweza kupoteza kabisa zingine espese * milioni moja za wanyama mu miaka kidogo yenye iko inakuja. Njo maana hatushangale kuona kama watu wako na wasiwasi juu ya mazingira! Lakini tunamushukuru Yehova juu alishaahidi kama ‘ataharibu wale wenye wanaharibu dunia’ na ataigeuza yote kuwa paradiso.​—Ufu. 11:18; Isa. 35:1.

MAMBO YENYE UVUMILIVU WA YEHOVA UNATUFUNDISHA

15-16. Ni nini njo inapaswa kutuchochea kuendelea kuvumilia pamoja na Yehova? Leta mufano.

15 Fikiria magumu yote yenye Baba yetu wa mbinguni amevumilia kwa miaka mingi sana. (Ona kisanduku “ Mambo Yenye Yehova Iko Anavumilia.”) Kama Yehova angependa, angeharibu huu ulimwengu muovu wakati wowote. Lakini uvumilivu wenye ameonyesha umetusaidia sana! Juu tuelewe tufikirie hii mufano: Wazia munganga anaambia bibi na bwana fulani kama mutoto wao atazaliwa na ulemavu fulani wa nguvu sana, hatakuwa na afya ya muzuri, na atakufa na angali mudogo. Lakini wazazi wanafurahi wakati mutoto anazaliwa hata kama itakuwa nguvu kumuhangaikia. Juu wanapenda sana mutoto wao, ile inawafanya wavumilie na kufanya yao yote ili kumutunza ili aendelee kuishi.

16 Vilevile, watoto wote wa Adamu na Eva wanazaliwaka na zambi. Hata vile, Yehova anawapenda na kuwahangaikia. (1 Yo. 4:19) Na tofauti na wazazi wenye tulizungumuzia mu mufano wetu, Yehova yeye anaweza kufanya jambo fulani kuhusu ile hali. Alishapanga siku yenye atamaliza magumu yote yenye iko inatesa wanadamu. (Mt. 24:36) Hauone kama upendo wake unapaswa kutuchochea kuendelea kuvumilia pamoja naye?

17. Namna gani mambo yenye kutajwa mu Waebrania 12:2, 3 yenye ilimufikia Yesu, inaweza kutupatia nguvu ya kuendelea kuvumilia?

17 Yehova anatuwekea mufano mukamilifu wa uvumilivu. Yesu aliweza kabisa kuiga uvumilivu wa Baba yake. Wakati alikuwa mwanadamu, Yesu alivumilia maneno makali, haya, na maumivu ku muti wa mateso kwa ajili yetu. (Soma Waebrania 12:2, 3.) Bila shaka, uvumilivu wa Yehova ulimupatia Yesu nguvu ya kuvumilia. Ule uvumilivu unaweza pia kutupatia nguvu.

18. Namna gani 2 Petro 3:9 inatusaidia kuelewa mambo yenye uvumilivu wa Yehova uko unatimiza?

18 Soma 2 Petro 3:9. Yehova anajua wakati muzuri kabisa wa kuharibu huu ulimwengu muovu. Uvumilivu wake umesaidia kukusanya kundi kubwa la watu, ni kusema mamilioni ya watu wenye kumuabudu na kumusifu. Wote wako na furaha juu Yehova amevumilia mupaka wafikie kuzaliwa, wajifunze kumupenda, na kutoa maisha yao kwake. Itaonekana wazi kama Yehova alifanya muzuri kwa kuamua kuvumilia, wakati atabariki mamilioni ya watu wenye watakuwa wamevumilia mupaka mwisho.

19. Tunapaswa kuazimia kufanya nini, na tutapata baraka gani?

19 Yehova ametufundisha kuvumilia kwa furaha. Hata kama Shetani ameleta maumivu na mateso mingi, Yehova anaendelea kuwa “Mungu mwenye furaha.” (1 Ti. 1:11) Na siye pia tunaweza kuendelea kuwa wenye furaha wakati tuko tunachunga kwa uvumilivu Yehova atakase jina yake, atetee mamlaka yake makubwa, amalize uovu wote, na atoshe magumu yetu yote. Tuazimie basi kuendelea kuvumilia, na tupate faraja kwa kujua kama Baba yetu wa mbinguni naye iko anavumilia. Kama tunafanya vile, hii maneno itakuwa ya kweli kabisa kwa kila mumoja wetu: “Mwenye furaha ni mutu mwenye anaendelea kuvumilia jaribu, kwa sababu akiisha kukubaliwa atapokea taji la uzima, lenye Yehova aliahidi wale wenye wanaendelea kumupenda.”​—Yak. 1:12.

WIMBO 139 Wazia Uko mu Dunia Mupya

^ fu. 5 Siye wote tuko na magumu mbalimbali. Lakini, kwa sasa, hatuna uwezo wa kumaliza magumu mingi; njo maana tunapaswa tu kuvumilia. Lakini haiko siye peke njo tuko navumilia. Yehova pia iko anavumilia mambo mingi. Mu hii habari, tutaona mambo kenda kati ya mambo yenye Yehova iko anavumilia. Tutaona pia mambo yenye uvumilivu wa Yehova umetimiza na namna tunaweza kupata faida kupitia mufano wake.

^ fu. 14 Neno “espese” iko tofauti na neno “aina” yenye Biblia inatumia. Aina inahusu vikundi vikubwa vya viumbe vyenye uzima.