Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 29

Ufurahi juu ya Maendeleo Yako Mwenyewe!

Ufurahi juu ya Maendeleo Yako Mwenyewe!

‘Kila mutu . . . akuwe na sababu ya kufurahi juu yake yeye mwenyewe, na hapana kwa kujilinganisha na mutu mwingine.’​—GAL. 6:4.

WIMBO 34 Nitatembea kwa Uaminifu-Mushikamanifu

KIFUPI YA HABARI *

1. Juu ya nini Yehova hatulinganishake na wengine?

YEHOVA anapendaka muchanganyiko. Ile inaonekana waziwazi mu uumbaji wake wa ajabu, kutia ndani mwanadamu. Kila mutu iko tofauti na mwingine. Kwa hiyo, Yehova hatulinganishake na wengine. Anachunguza moyo wako, vile uko ndani kabisa. (1 Sa. 16:7) Anajua pia uwezo wako, uzaifu wako, na namna ulikomala. Na hakuombe ufanye mambo yenye inapita uwezo wako. Tunapaswa kumuiga Yehova kwa kujiona vile anatuonaka. Ile itafanya tukuwe na “akili ya muzuri,” na tuepuke kujiona kuwa wa maana sana ao kujiona kuwa wa bure sana.​—Ro. 12:3.

2. Juu ya nini haiko muzuri kujilinganisha na wengine?

2 Kusema kweli, tunaweza kujifunza mambo mingi kwa ndugu na dada wenye kupata matokeo ya muzuri mu mahubiri. (Ebr. 13:7) Ile inaweza kutusaidia kuona njia mbalimbali zenye tunaweza kutumia juu ya kupata matokeo ya muzuri zaidi mu mahubiri. (Flp. 3:17) Lakini kuko tofauti kati ya kuiga mufano muzuri wa mutu fulani na kujilinganisha naye. Kama tunajilinganisha na wengine, ile inaweza kufanya tukuwe na wivu, tuvunjike moyo, ao hata kujiona wa bure kabisa. Kama vile tuliona mu habari yenye ilitangulia, ni hatari sana kujaribu kushindana na wengine mu kutaniko. Kwa upendo, Yehova anatuambia hivi: “Kila mutu achunguze matendo yake mwenyewe, kisha atakuwa na sababu ya kufurahi juu yake yeye mwenyewe, na hapana kwa kujilinganisha na mutu mwingine.”​—Gal. 6:4.

3. Ulishafanya maendeleo gani ya kiroho yenye inakuletea furaha?

3 Yehova anapenda ufurahi juu ya maendeleo yako mwenyewe ya kiroho. Kwa mufano, kama ulishabatizwa, unapaswa kufurahi sana juu ulifikia ile muradi! Ni weye peke njo uliamua kubatizwa. Ni upendo wako kwa Yehova njo ulikuchochea kubatizwa. Waza kidogo juu ya maendeleo yenye ulishafanya tangu ubatizwe mupaka leo. Kwa mufano, umeanza kupenda sana kusoma na kujifunza Biblia? Sala zako zimekuwa za kutoka mu moyo zaidi kuliko zamani? (Zb. 141:2) Umekuwa na ufundi zaidi katika kuanzisha mazungumuzo mu mahubiri na katika kutumia vyombo vyetu vya mahubiri? Na kama uko na familia, Yehova amekusaidia ukuwe bwana muzuri zaidi, bibi muzuri zaidi, ao muzazi muzuri zaidi? Kuona maendeleo yenye ulishafanya mu mambo kama ile, kunapaswa kukuletea furaha sana.

4. Tutazungumuzia mambo gani mu hii habari?

4 Tunaweza kusaidia wengine wafurahi juu ya maendeleo ya kiroho yenye walishafanya. Tunaweza pia kuwasaidia wasikuwe wanajilinganisha na wengine. Mu hii habari, tutaona namna wazazi wanaweza kusaidia watoto wao, namna bibi na bwana wanaweza kusaidiana, na namna wazee na wengine wanaweza kusaidia ndugu na dada zao. Ku mwisho, tutazungumuzia kanuni fulani za Biblia zenye zinaweza kutusaidia kujiwekea miradi yenye tunaweza kufikia kulingana na uwezo na hali yetu.

MAMBO WAZAZI NA WENYE WALISHAOANA WANAWEZA KUFANYA

Wazazi, muonyeshe kila mutoto wenu kama munaona mambo yenye anafanya kuwa ya maana sana (Ona fungu ya 5-6) *

5. Kulingana na Waefeso 6:4, wazazi wanapaswa kuepuka nini?

5 Wazazi wanapaswa kuwa waangalifu sana ili wasikuwe wanalinganisha watoto wao ao kuwaomba wafanye mambo yenye inapita uwezo wao. Kulinganisha-linganisha mutoto na mwingine ao kumuomba mambo yenye hawezi kufanya kunaweza kumuvunja moyo. (Soma Waefeso 6:4.) Dada Sachiko * anasema hivi: “Walimu wangu walitazamia nifanye muzuri zaidi kuliko wanafunzi wenzangu ku masomo. Tena, mama yangu alipenda nitumike muzuri sana ku masomo juu ya kutolea baba yangu mwenye haiko Shahidi na mwalimu wangu ushahidi muzuri. Alipenda niweze ma examens yote; lakini niliona kama ile haiwezekane. Hata kama kulishapita miaka mingi tangu nimalize masomo, wakati fulani najiulizaka kama niko namutolea kabisa Yehova yenye anastahili.”

6. Ni somo gani ya maana wazazi wanaweza kujifunza mu Zaburi 131:1, 2?

6 Somo moja ya maana yenye wazazi wanapata inapatikana mu Zaburi 131:1, 2. (Soma.) Mufalme Daudi alisema kama hakukuwa ‘anajitafutia mambo makubwa sana’ ao mambo yenye ilipita uwezo wake. Unyenyekevu na kiasi ‘vilimutuliza na kumunyamazisha.’ Maneno ya Daudi inaweza kufundisha wazazi nini? Wazazi wanapaswa kuwa wanyenyekevu na wenye kiasi mu mambo yenye wanatazamia juu yao wenyewe na mu mambo yenye wanatazamia kutoka kwa mutoto wao. Wazazi wanaweza kuonyesha mutoto wao kama iko wa maana, kwa kumusaidia aone uwezo na uzaifu wake wakati wako wanamusaidia ajiwekee miradi yenye anaweza kufikia. Dada Marina anasema hivi: “Hakuna siku mama yangu alikuwaka ananilinganisha na kaka zangu watatu ao na watoto wengine. Alinifundishaka kama kila mutu iko na uwezo wake, na iko wa maana sana ku macho ya Yehova. Ile ilinisaidia nisikuwe najilinganisha na wengine.”

7-8. Namna gani bwana anaweza kuonyesha kama anaheshimia bibi yake?

7 Bwana Mukristo anapaswa kumuheshimia bibi yake. (1 Pe. 3:7) Heshima inatia ndani kukazia akili watu wengine. Kwa mufano, bwana anaonyesha kama anaheshimia bibi yake kwa kumutendea mu njia yenye kuonyesha kama anamuona kuwa wa maana sana. Hapaswe kumuomba afanye mambo yenye kupita uwezo wake. Na hapaswe kumulinganisha na wanamuke wengine. Kama anafanya vile, ile inaweza kuwa na matokeo gani ya mubaya? Rosa iko na bwana mwenye haiko Shahidi. Mara mingi bwana yake anamulinganishaka na wanamuke wengine. Maneno ya makali ya bwana yake imefanya ajisikie mubaya na hata akuwe na mashaka kama kuko kabisa mutu mwenye anamupendaka. Rosa anasema hivi: “Kila mara, niko na lazima wanikumbushe kama Yehova ananiona kuwa wa maana.” Lakini bwana Mukristo anaheshimiaka bibi yake. Anajua kama namna iko anamutendea bibi yake inaweza kufanya akuwe na uhusiano wa muzuri pamoja naye na hata pamoja na Yehova. *

8 Bwana mwenye anaheshimia bibi yake, anajikazaka kumusifu, anaonyeshaka kama anamupenda, na anamupongezaka. (Mez. 31:28) Njo vile bwana ya Katerina, mwenye tulizungumuzia mu habari yenye ilitangulia, alimusaidia bibi yake apiganishe ile hali ya kujiona kuwa wa bure. Wakati alikuwa angali mutoto, bibi yake alionwa kuwa wa bure na mama yake, mwenye mara mingi alikuwa anamulinganisha na watoto wengine wanamuke, kutia ndani marafiki wake. Ile ilifanya Katerina aanze kujilinganisha na wengine hata wakati alifikia kuwa Shahidi wa Yehova! Lakini bwana yake Mukristo, alimusaidia kupiganisha ile hali na kujikaza kuwa na mawazo yenye kusawazika juu yake mwenyewe. Katerina anasema hivi: “Bwana yangu ananipendaka, ananipongezaka juu ya mambo ya muzuri yenye ninafanyaka, na anakuwaka anasali juu yangu. Tena, ananikumbushaka sifa za muzuri za Yehova na kurekebisha mawazo yangu ya mubaya.”

MAMBO YENYE WAZEE NA WENGINE WANAWEZA KUFANYA

9-10. Namna gani wazee fulani wenye upendo walisaidia dada moja apiganishe muelekeo wa kujilinganisha na wengine?

9 Namna gani wazee wanaweza kusaidia wale wenye wako na muelekeo wa kujilinganisha na wengine? Ona mufano wa dada Hanuni, mwenye hakukuwa anapongezwa sana, wakati alikuwa angali mutoto. Anasema hivi: “Nilikuwa mutu wa haya na niliona kama watoto wengine walikuwa wa maana zaidi kunishinda. Kwa hiyo, nilianza kujilinganisha na wengine tangu wakati nilikuwa mutoto.” Hata wakati alifikia kuwa Shahidi wa Yehova, Hanuni alikuwa anajilinganisha tu na wengine. Ile ilifanya ajione kuwa mutu wa bure kabisa mu kutaniko. Lakini sasa iko painia mwenye furaha. Nini njo ilimusaidia abadilishe mawazo yake?

10 Hanuni anasema kama wazee wenye upendo njo walimusaidia. Walionyesha kama wanamutumainia na walikuwa wanamupongeza juu ya uaminifu wake. Anaandika hivi: “Wakati fulani wazee walikuwa wananiomba nitie moyo dada fulani wenye walikuwa na lazima ya musaada. Ile migao ilifanya nijione kuwa wa maana. Nakumbuka namna wazee walinishukuru juu nilitia moyo dada fulani vijana. Kisha wakanisomea 1 Watesalonike 1:2, 3. Ile ilinigusa sana! Kupitia zaidi sana wale wachungaji wazuri, leo niko najiona kuwa wa maana mu tengenezo ya Yehova.”

11. Namna gani tunaweza kusaidia wale wenye “kupondwa” kama vile Isaya 57:15 inaonyesha?

11 Soma Isaya 57:15. Yehova anahangaikia sana wale wenye “kupondwa.” Siye wote, hapana tu wazee, tunaweza kutia moyo wale ndugu na dada. Njia moja ya kufanya vile, ni kuonyesha kama tunawahangaikia kabisa. Yehova anapenda tuonyeshe kondoo zake, wenye anapenda sana, upendo wake. (Mez. 19:17) Tunaweza pia kusaidia ndugu na dada zetu kwa kuwa wanyenyekevu na wenye kiasi. Hatupendi kujionyesha juu tusifanye wengine wakuwe na wivu. Lakini, tunatumia njo uwezo na ujuzi wetu ili kutiana moyo.​—1 Pe. 4:10, 11.

Wanafunzi wa Yesu walikuwa karibu sana naye juu hakuna siku Yesu alijionyesha kama iko muzuri zaidi kuwashinda. Alifurahia kuwa pamoja na rafiki zake (Ona habari ya kujifunza ya 29, fungu ya 12)

12. Juu ya nini watu wanyenyekevu walipenda kuwa na Yesu? (Ona picha kwenye jalada.)

12 Tunaweza kujifunza namna ya kutendea wengine muzuri zaidi kwa kuchunguza namna Yesu alitendea wafuasi wake. Hakuna mwanadamu mwenye alikuwaka sawa yeye. Lakini, alikuwa “mwenye tabia ya upole na munyenyekevu katika moyo.” (Mt. 11:28-30) Hakujionyesha kama iko na akili na kama anajua mambo mingi sana. Alifundisha watu kwa kutumia maneno ya mwepesi na mifano yenye kuvutia yenye iligusa mioyo ya watu wanyenyekevu. (Lu. 10:21) Tofauti na viongozi wa dini wenye kiburi, hakuna siku Yesu alifanya watu wajione kuwa wa bure ku macho ya Mungu. (Yoh. 6:37) Kuliko kufanya vile, alitendea watu wa kawaida kwa heshima.

13. Ni mu njia gani wema na upendo wa Yesu ilionekana mu namna alitendea wanafunzi?

13 Wema na upendo wa Yesu ilionekana mu namna alitendea wanafunzi wake. Alijua kama walikuwa na uwezo na hali mbalimbali. Kwa hiyo, haingewezekana wakuwe na madaraka ileile, na haingewezekana wapate matokeo ileile mu mahubiri. Alisamini bidii yenye kila mumoja wao alifanya. Tunaona ile jambo mu mufano wa talanta wenye Yesu alileta. Mu ile mufano, bwana alipatia kila mutumwa kazi “kulingana na uwezo wake mwenyewe.” Mumoja kati ya wale watumwa wazuri alipata faida zaidi kuliko mwingine. Lakini bwana aliwapongeza wote wawili kwa kutumia maneno ileile: “Umefanya muzuri, mutumwa mwema na muaminifu!”​—Mt. 25:14-23.

14. Namna gani tunaweza kuonyesha kama tunamuiga Yesu mu namna tunatendea wengine?

14 Yesu anatutendeaka kwa wema na upendo. Anajua muzuri kama uwezo na hali zetu ziko tofauti, na anafurahi kuona tunafanya yetu yote. Tunafanya muzuri sana wakati tunatendea wengine sawa vile Yesu alikuwa anafanya. Hatuwezi kupenda muabudu mwenzetu ajisikie kuwa wa bure ao apate haya juu hawezi kufanya mambo mingi sawa vile wengine. Kuliko kufanya vile, muache tutafute kila nafasi yenye inajitokeza ili kupongeza ndugu na dada kwa yote yenye wako wanafanya ili kumutumikia Yehova.

UJIWEKEE MIRADI YENYE UNAWEZA KUFIKIA

Pata furaha kwa kujiwekea miradi yenye unaweza kufikia (Ona fungu ya 15-16) *

15-16. Dada moja alipata faida gani juu alijiwekea miradi yenye angeweza kufikia?

15 Wakati tuko na miradi ya kiroho, maisha yetu inakuwa na kusudi na inakuwa na maana. Siri ni kujiwekea miradi kulingana na uwezo na hali zetu, hapana kufuata miradi ya wengine. Ile itatusaidia tusihuzunike ao kuvunjika moyo bure. (Lu. 14:28) Tuone mufano wa dada moja painia mwenye kuitwa Midori.

16 Baba ya Midori, mwenye haiko Shahidi, alikuwa anamufanya ajione kuwa wa bure wakati alikuwa angali mutoto kwa kumulinganisha na wadogo wake na wanafunzi wenzake. Midori anasema hivi: “Nilijiona wa bure kabisa.” Lakini wakati alikuwa mutu muzima, akaanza kuwa na mawazo ya muzuri juu yake mwenyewe. Anasema: “Ninasomaka Biblia kila siku, juu ile inanisaidiaka kuwa na amani ya moyo na kujisikia kuwa Yehova ananipenda.” Tena, alijiwekea miradi yenye angeweza kufikia, na alisali kwa Yehova juu amusaidie afikie ile miradi. Matokeo? Midori aliweza kufurahi juu ya maendeleo yake ya kiroho.

ENDELEA KUMUTUMIKIA YEHOVA KWA UWEZO WAKO WOTE

17. Namna gani tunaweza ‘kuendelea kufanywa upya katika mutazamo wenye unatawala akili yetu,’ na ile itatuletea faida gani?

17 Mawazo ya mubaya haiwezi kuisha mu siku moja. Yehova anatuamuru hivi: “Munapaswa kuendelea kufanywa upya katika mutazamo wenye unatawala akili yenu.” (Efe. 4:23, 24) Juu tufikie kufanya vile, tunapaswa kusali, kujifunza Biblia, na kufikiri sana. Uendelee kufanya ile mambo tatu, na kisha umuombe Yehova akupatie nguvu. Roho yake takatifu itakusaidia kushinda muelekeo wowote wa kutaka kujilinganisha na wengine. Tena, Yehova atakusaidia utambue wakati wivu na kiburi vinaanza kuingia mu moyo wako, na atakusaidia uvitoshe haraka.

18. Namna gani maneno yenye kuwa mu 2 Mambo ya Nyakati 6:29, 30 inatufariji?

18 Soma 2 Mambo ya Nyakati 6:29, 30. Yehova anajua moyo wetu. Anajua pia vita yenye tuko tunafanya ili kupiganisha roho ya ulimwengu na uzaifu wetu. Wakati Yehova anaona namna tuko tunafanya yetu yote ili kupiganisha ile mambo, anaendelea kutupenda zaidi.

19. Ni mufano gani Yehova anatumia ili tuelewe namna anatupenda?

19 Juu ya kutusaidia kuelewa namna anatupenda, Yehova anazungumuzia uhusiano wenye unakuwaka kati ya mama na mutoto. (Isa. 49:15) Fikiria mufano wa mama mwenye anaitwa Rachel. Anasema hivi: “Mutoto yangu Stephanie alizaliwa mbele miezi ienee. Wakati nilimuona mara ya kwanza, alionekana wa kidogo sana, na mwenye kuwa na lazima ya musaada. Lakini munganga aliniruhusu nikuwe namubeba kila siku mu ile mwezi ya kwanza yenye alikuwa anapata matunzo. Ile ilifanya miye na mutoto yangu tukuwe marafiki sana. Leo iko na miaka sita na iko wa kidogo tofauti na watoto wa miaka yake. Namupendaka sana juu iko anapiganisha sana juu aishi, na ameniletea furaha ya mingi sana mu maisha yangu!” Inatia moyo sana kujua kama Yehova naye anatupendaka sana wakati anaona vile tuko tunapigana sana ili kuendelea kumutumikia kwa nafsi yetu yote!

20. Juu uko mutumishi mwenye alishajitoa kwa Yehova, uko na sababu gani ya kuendelea kufurahi?

20 Juu uko mutumishi wa Yehova, ujue kama uko wa maana sana mu familia yake, na hakuna mwingine sawa weye. Yehova hakukuvuta kwake juu ulikuwa wa muzuri zaidi kuliko majirani wako. Alikuvuta kwake juu aliona moyo wako, aliona kama uko mutu mupole na uko tayari kukubali mafundisho yake na kubadilika. (Zb. 25:9) Ukuwe hakika kama anasamini sana wakati unamutumikia kwa uwezo wako wote. Uvumilivu wako na uaminifu wako ni ushuhuda wenye kuonyesha kama uko na “moyo muzuri na mwema.” (Lu. 8:15) Kwa hiyo, endelea kumutumikia Yehova kwa uwezo wako wote. Ile itakupatia sababu ya muzuri ya kufurahi “juu [yako] mwenyewe.”

WIMBO 38 Atakupatia Nguvu

^ fu. 5 Yehova hatulinganishake na wengine. Lakini, wamoja kati yetu wanaweza kujilinganisha na wengine na kujiona kuwa wa bure kabisa. Mu hii habari, tutaona juu ya nini ni mubaya sana kujilinganisha na wengine. Tutaona pia namna tunaweza kusaidia watu wa familia yetu na watu wengine mu kutaniko wajione sawa vile Yehova anawaona.

^ fu. 5 Majina fulani imebadilishwa.

^ fu. 7 Hata kama hii mawazo inakazia sana bwana, kanuni mingi zenye kuzungumuziwa zinahusu pia bibi.

^ fu. 58 MAFASIRIO YA PICHA: Wakati wa ibada ya familia, wazazi wanaonyesha kama wanafurahia kitu yenye kila mutoto alifanya ili kutia mu safina ya Noa.

^ fu. 62 MAFASIRIO YA PICHA: Mama moja mwenye iko nakomalisha mutoto yake mudogo yeye peke, iko anafanya mipango ili kuwa painia musaidizi, na anafurahi juu amefikia ile muradi.