Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 30

Furahia Fasi Yako mu Familia ya Yehova

Furahia Fasi Yako mu Familia ya Yehova

“Ulimufanya kuwa mudogo kidogo kuliko wale wenye kuwa kama Mungu, na ulimuvalisha taji la utukufu na uzuri.”​—ZB. 8:5, maelezo ya chini.

WIMBO 123 Tutii Mupango wa Kiteokrasi

KIFUPI YA HABARI *

1. Pengine tunaweza kuwaza nini wakati tunafikiria vitu vyote vyenye Yehova aliumba?

WAKATI tunafikiria ukubwa wa ulimwengu wenye Yehova aliumba, pengine tunaweza kujisikia sawa vile mutunga-zaburi Daudi mwenye alisali kwa Yehova na kusema: “Wakati ninaona mbingu zako, kazi za vidole vyako, mwezi na nyota zenye umetayarisha, mwanadamu mwenye anaweza kufa ni nini ili umuweke katika akili, na mwana wa binadamu ili umuhangaikie?” (Zb. 8:3, 4) Kama Daudi, tunaweza kuona namna tuko kidogo wakati tunajilinganisha na vitu vyenye Yehova aliumba na kufikia hata kushangala kuona namna Yehova anatuhangaikia. Njo maana tutaona namna Yehova alihangaikia wanadamu wa kwanza, ni kusema, Adamu na Eva, lakini pia namna aliwafanya kuwa watu wa mu familia yake.

2. Yehova alikuwa na kusudi gani juu ya watoto wake wa kwanza hapa ku dunia?

2 Ni Adamu na Eva njo walikuwa watoto wa kwanza wa Yehova ku dunia, na Yehova alikuwa Baba yao mupendwa. Na aliwapatia kazi ya kufanya. Aliwaambia hivi: “Muzae na mukuwe wengi, mujaze dunia.” (Mwa. 1:28) Alipenda wazae na walinde dunia. Kama Adamu na Eva wangetii na kufanya mambo yenye Yehova aliwaomba wafanye, wao na wazao wao wangebakia mu familia ya Yehova milele.

3. Juu ya nini tunaweza kusema kama Yehova alipatia Adamu na Eva fasi ya muzuri mu familia yake?

3 Adamu na Eva walikuwa na fasi ya muzuri mu familia ya Yehova. Kama vile inaonyeshwa mu Zaburi 8:5 na maelezo ya chini, Daudi alisema hivi kuhusu namna Yehova aliumba mwanadamu: “Ulimufanya kuwa mudogo kidogo kuliko wale wenye kuwa kama Mungu, na ulimuvalisha taji la utukufu na uzuri.” Yehova hakuumba wanadamu na nguvu na akili ileile wala uwezo moja sawa vile malaika. (Zb. 103:20) Lakini, aliwavalisha taji la utukufu na uzuri. Waza kidogo juu ya ile! Yehova alipatia kabisa wazazi wetu wa kwanza maisha ya muzuri sana.

4. Ni nini njo ilipata Adamu na Eva juu hawakutii Yehova, na tutaona mambo gani mu hii habari?

 4 Jambo ya kuhuzunisha, Adamu na Eva walipoteza fasi yao mu familia ya Yehova juu hawakumutii. Ile ilileta matokeo ya mubaya sana kwa wazao wao, sawa vile tutaona mu hii habari. Lakini kusudi ya Yehova haijabadilika. Anapenda wanadamu wenye kumutii wakuwe watoto wake milele. Kwanza, tutaona namna Yehova ametuonyesha kama tuko wa maana sana kwake. Tutaona pia mambo tunaweza kufanya sasa ili kuonyesha kama tunapenda kuwa mu familia ya Mungu. Na ku mwisho, tutaona baraka zenye watu wa mu familia ya Yehova watapata ku dunia milele.

NAMNA YEHOVA ALITENDEA WATU KWA HESHIMA

Namna gani Yehova ametutendea kwa heshima? (Ona fungu ya 5-11) *

5. Juu Mungu alituumba na sifa sawa zake, namna gani tunaweza kuonyesha kama tunamutukuza?

5Yehova alituumba kwa mufano wake. (Mwa. 1:26, 27) Juu tuliumbwa kwa mufano wa Mungu, tunaweza kujifunza kuonyesha sifa zake za muzuri, kama vile, huruma, ushikamanifu, na haki. (Zb. 86:15; 145:17) Wakati tunaonyesha zile sifa, tunamutukuza Yehova na tunaonyesha kama tuko wenye shukrani kwake. (1 Pe. 1:14-16) Na wakati tunajiendesha mu njia yenye inamufurahisha Baba yetu wa mbinguni tutakuwa na furaha. Tena, juu tuko na sifa sawa za Yehova tunaweza kuwa aina ya watu wenye anapenda wakuwe mu familia yake.

6. Namna gani Yehova alitendea wanadamu kwa heshima wakati aliumba dunia?

6Yehova alitutayarishia fasi ya muzuri sana. Mbele aumbe mwanadamu wa kwanza, Yehova alitayarisha dunia kwa ajili ya wanadamu. (Yob. 38:4-6; Yer. 10:12) Juu Yehova ni mwema na mukarimu, aliumba vitu mingi vya muzuri juu tukuwe na furaha. (Zb. 104:14, 15, 24) Wakati fulani, aliwaza juu ya vitu vyenye aliumba na ‘akaona kwamba vilikuwa muzuri.’ (Mwa. 1:10, 12, 31) Wakati fulani alitendea wanadamu kwa heshima wakati aliwapatia “mamlaka juu ya” vitu vyote vya muzuri vyenye aliumba. (Zb. 8:6) Mungu anapenda wanadamu wakamilifu wachunge muzuri uumbaji wake milele na wafanye vile kwa furaha. Unakuwaka unamushukuru Yehova juu ya ile?

7. Namna gani Yoshua 24:15 inaonyesha kama mwanadamu iko na uhuru wa kuchagua?

7Yehova ametupatia uhuru wa kuchagua. Tunaweza kuchagua ni mambo gani tutafanya mu maisha. (Soma Yoshua 24:15.) Baba yetu mwenye upendo anafurahiaka wakati tunachagua kumutumikia. (Zb. 84:11; Mez. 27:11) Tunaweza kutumia muzuri uhuru wetu wa kuchagua ili kukamata maamuzi mingi ya muzuri. Tuone mufano moja wenye kuonyesha namna Yesu alitumia uhuru wake wa kuchagua.

8. Leta mufano wenye kuonyesha namna Yesu alitumia uwezo wake wa kuchagua.

8 Tunaweza kuiga mufano wa Yesu kwa kuchagua kutanguliza faida za wengine. Siku moja, wakati Yesu na mitume wake walikuwa wenye kuchoka sana, walienda fasi yenye kulikuwa kimya ili kupumuzika kwa wakati fulani. Lakini hawakupumuzika. Watu wengi waliwatangulia kwenye walikuwa na walikuwa tayari kusikiliza mafundisho ya Yesu. Kuliko kukasirika, Yesu aliwasikilia huruma. Sasa alifanya nini? “Akaanza kuwafundisha mambo mengi.” (Mk. 6:30-34) Tunaiga mufano wa Yesu saa yenye tunatumia wakati na nguvu yetu ili kusaidia wengine. Kufanya vile kunamutukuza Baba yetu wa mbinguni. (Mt. 5:14-16) Na tunaonyesha Yehova kama tunapenda kuwa mu familia yake.

9. Wazazi wanapaswa kuchunga nini mu akili yao?

9Yehova alipatia watu uwezo wa kuwa na watoto na daraka ya kuwafundisha wamupende na kumutumikia. Kama uko muzazi, uko mwenye shukrani juu ya hii zawadi ya muzuri sana? Hata kama Yehova alipatia malaika uwezo mingi, tusisahau kama malaika hawana uwezo wa kuwa na watoto. Kama wanachunga ile wazo mu akili, wazazi watasamini daraka ya maana sana yenye wako nayo, ni kusema, kukomalisha watoto wao “katika nizamu na maonyo ya Yehova.” (Efe. 6:4; Kum. 6:5-7; Zb. 127:3) Ili kusaidia wazazi, tengenezo ya Mungu inatoa vyombo mbalimbali vyenye kutegemea Biblia, kama vile vichapo, video, muziki na mambo ingine yenye kuwa ku site yetu. Kusema kweli, Baba yetu wa mbinguni na mwana wake wanapenda vijana sana. (Lu. 18:15-17) Wakati wazazi wanamutegemea Yehova na wanafanya yao yote ili kuhangaikia watoto wao, ile inamufurahisha Yehova. Wanasaidia pia watoto wao kuwa mu familia ya Yehova milele!

10-11. Mupango wa bei ya ukombozi wenye Yehova alikamata unatuwezesha kupata nini?

10Yehova alitoa mwana wake mupendwa juu tuweze tena kuwa mu familia yake. Sawa vile tuliona mu  fungu ya ine, Adamu na Eva walipoteza fasi yao na ya watoto wao mu familia ya Yehova. (Ro. 5:12) Adamu na Eva walikosa kutii kimakusudi njo maana Mungu aliwatosha mu familia yake. Sasa tuseme nini juu ya watoto wao? Kwa upendo, Yehova alikamata mupango ili watoto wao wenye kumutii wakuwe mu familia yake. Alifanya vile kupitia zabihu yenye Mwana wake muzaliwa-pekee, Yesu Kristo, alitoa. (Yoh. 3:16; Ro. 5:19) Ile zabihu ya Yesu imefanya watu 144 000 waaminifu wakuwe watoto wa Mungu.​—Ro. 8:15-17; Ufu. 14:1.

11 Pia, mamilioni ya waaminifu wengine wako wanafanya mapenzi ya Yehova. Wako na tumaini ya kuwa mu familia yake kisha jaribu ya mwisho ku mwisho wa miaka 1 000. (Zb. 25:14; Ro. 8:20, 21) Juu wako na ile tumaini, kuanzia sasa wanamuita Yehova, Muumbaji wao, “Baba.” (Mt. 6:9) Wale wenye watafufuliwa watakuwa pia na pendeleo ya kujifunza mambo yenye Yehova anapenda wafanye. Wale wenye watamutii watafikia pia kuwa mu familia ya Yehova.

12. Ni ulizo gani tutajibia sasa?

12 Kama vile tuliona, Yehova ametendea watu kwa heshima. Tayari amefanya watiwa-mafuta kuwa wana wake, na amepatia wale wa “kundi kubwa la watu” tumaini ya kuwa watoto wake mu dunia mupya. (Ufu. 7:9) Tunaweza kufanya nini tangu leo ili kuonyesha kama tunapenda kuwa mu familia ya Yehova milele?

UMUONYESHE YEHOVA KAMA UNAPENDA KUWA MU FAMILIA YAKE

13. Tunaweza kufanya nini juu tukuwe mu familia ya Mungu? (Marko 12:30)

13Uonyeshe kama unamupenda Yehova kwa kumutumikia kwa moyo wako wote. (Soma Marko 12:30.) Kati ya zawadi za muzuri zenye Mungu ametupatia, pengine moja kati ya zawadi za mukubwa ni uwezo wa kumuabudu. Tunaonyesha kama tunamupenda Yehova kwa ‘kushika amri zake.’ (1 Yo. 5:3) Moja kati ya amri zenye Yehova anapenda tutii ni ile yenye Yesu alitupatia, ni kusema, kufanya wanafunzi na kuwabatiza. (Mt. 28:19) Tena, Yesu alituamuru kupendana. (Yoh. 13:35) Yehova atafanya wale wenye kumutii wakuwe mu familia ya waabudu wake.​—Zb. 15:1, 2.

14. Namna gani tunaweza kuonyesha wengine upendo? (Matayo 9:36-38; Waroma 12:10)

14Uonyeshe wengine upendo. Upendo njo sifa kubwa zaidi ya Yehova. (1 Yo. 4:8) Yehova alituonyesha upendo wake mbele hata siye tumujue. (1 Yo. 4:9, 10) Tunamuiga wakati tunaonyesha wengine upendo. (Efe. 5:1) Njia moja ya muzuri zaidi yenye tunaweza kuonyesha watu upendo ni kuwasaidia wajifunze juu ya Yehova hivi kungali wakati. (Soma Matayo 9:36-38.) Wakati tunafanya vile, tunawatolea nafasi ya kuwa mu familia ya Mungu. Kisha mutu kubatizwa, tunapaswa kuendelea kumupenda na kumuheshimia. (1 Yo. 4:20, 21) Tunaweza kufanya vile namna gani? Njia moja, ni kuwa hakika kama iko na nia za muzuri. Kwa mufano, kama hatuelewe juu ya nini alifanya jambo fulani, hatutamuwazia kama aliifanya juu tu ya sababu fulani ya mubaya. Lakini, tutamuheshimia na kumuona kuwa wa muzuri zaidi kuliko siye.​—Soma Waroma 12:10; Flp. 2:3.

15. Ni nani njo tunapaswa kuonyesha huruma na wema?

15Utendee watu wote kwa huruma na wema. Kama tunapenda kuwa mu familia ya Yehova milele, tunapaswa kutumikisha Neno yake mu maisha yetu. Kwa mufano, Yesu alifundisha kama tunapaswa kuonyesha watu wote huruma na wema, hata maadui wetu. (Lu. 6:32-36) Pengine tunaweza kuona ni nguvu kufanya vile wakati fulani. Kama ni vile, tunapaswa kujifunza kuwaza na kutenda kama Yesu. Wakati tunafanya yetu yote juu ya kutii Yehova na kumuiga Yesu, tunaonyesha Baba yetu wa mbinguni kama tunapenda kuwa mu familia yake milele.

16. Namna gani tunaweza kulinda sifa ya muzuri ya familia ya Yehova?

16Ulinde sifa ya muzuri ya familia ya Yehova. Mu familia ya kawaida, kwa ujumla mudogo anakuwaka anaiga ndugu yake mukubwa. Kama ule ndugu mukubwa anatumikisha kanuni za Biblia mu maisha yake, atamuwekea mudogo yake mufano muzuri. Lakini, kama ule ndugu mukubwa anaanza kufanya mambo ya mubaya, mudogo yake pia anaweza kufuata mufano wake wa mubaya. Ni vile pia mu familia ya Yehova. Kama Mukristo fulani mwenye alikuwa muaminifu anakuwa muasi-imani ao anachagua kuwa na mwenendo mubaya, wengine wanaweza kumuiga. Wale wenye wanafanya vile, wanaharibisha sifa ya muzuri ya familia ya waabudu wa Yehova. (1 Te. 4:3-8) Tunapaswa kuepuka kufuata mifano ya mubaya na hatupaswe kuruhusu kitu fulani iharibishe uhusiano wetu pamoja na Baba yetu wa mbinguni mwenye upendo.

17. Tunapaswa kuepuka mawazo ya namna gani na juu ya nini?

17Umutegemee Yehova hapana vitu vya kimwili. Yehova anatuahidi kama atatupatia chakula, manguo, na fasi ya kulala, kama tunatafuta kwanza Ufalme wake na kuishi kulingana na kanuni zake za haki. (Zb. 55:22; Mt. 6:33) Kama tunaweka ile mu akili, tutaepuka kuwaza kama, vitu vya kimwili vyenye ulimwengu unatutolea njo vinaweza kutulinda na kutuletea furaha ya kudumu. Tunajua kama njia moja tu ya kupata amani ya kweli ni kufanya mapenzi ya Yehova. (Flp. 4:6, 7) Hata kama tuko na uwezo wa kuuza vitu mingi, tunapaswa kujiuliza kabisa kama tuko na wakati na nguvu ya kuvihangaikia. Je, unahangaikiaka sana vitu vya kimwili mupaka inakuwa nguvu kwako kuachana navyo? Tunapaswa kukumbuka kama Mungu alitupatia kazi ya kufanya mu familia yake. Ile inamaanisha kama, hatupaswe kuacha jambo yoyote itukengeushe. Kusema kweli, hatupende kuwa sawa vile kijana moja mwenye alipoteza pendeleo ya kumutumikia Yehova na ya kufanywa kuwa mwana wake, juu tu hakupenda kuachana na vitu vyake vya kimwili!​—Mk. 10:17-22.

MAMBO YENYE WATOTO WA YEHOVA WATAFURAHIA MILELE

18. Ni pendeleo gani kubwa na baraka gani watu watiifu watafurahia milele?

18 Watu watiifu watapata pendeleo kubwa sana ya kumupenda na kumuabudu Yehova milele! Wale wenye kuwa na tumaini ya kuishi ku dunia, watakuwa na furaha ya kutunza dunia yenye Yehova aliumbaka juu ikuwe makao yao milele. Hivi karibuni Ufalme wa Mungu utafanya dunia na kila kitu yenye kuwa ndani ipendeze tena. Yesu atatosha magumu yote yenye tumepata juu tu Adamu na Eva waliamua kutoka mu familia ya Yehova. Yehova atafufua mamilioni ya watu na atawapatia nafasi ya kuishi milele wakiwa na afya kamilifu mu dunia yenye imefanywa kuwa paradiso. (Lu. 23:42, 43) Wakati wanadamu wenye kumutumikia Yehova watakuwa wakamilifu, wote wenye kuwa hapa ku dunia watakuwa na “taji la utukufu na uzuri” wenye Daudi alizungumuziaka.​—Zb. 8:5.

19. Ni nini hatupaswe kusahau?

19 Kama uko kati ya “kundi kubwa la watu,” uko na tumaini ya muzuri sana. Mungu anakupenda na anapenda uendelee kuwa mu familia yake. Kwa hiyo, fanya yote yenye unaweza ili kumupendeza. Usisahau hata siku moja ahadi za Mungu. Furahia pendeleo ya kumuabudu Baba yetu wa mbinguni na tumaini yako ya kumusifu milele!

WIMBO 107 Tuonyeshe Upendo Kama Mungu

^ fu. 5 Juu familia ikuwe na furaha, kila mutu anapaswa kujua mambo yenye anatazamiwa kufanya na anapaswa kusaidia watu wengine wa familia. Baba anaongoza kwa upendo familia, mama anamutegemeza, na watoto wanajitiisha kwa wazazi wao. Ni vile pia kuhusu familia ya Yehova. Mungu wetu iko na kusudi fulani juu yetu, na kama tunaishi kulingana na ile kusudi tutakuwa mu familia yake milele.

^ fu. 55 MAFASIRIO YA PICHA: Kuumbwa kwa mufano wa Mungu kunachochea bibi na bwana fulani waonyeshane upendo na huruma na pia waionyeshe watoto wao wanaume. Wale bibi na bwana wanamupenda Yehova. Zawadi ya kuwa na watoto inawapatia nafasi ya kuwasaidia watoto wao wamupende Yehova na kumutumikia. Wazazi wanatumia video juu ya kuwafasiria sababu ilifanya Yehova atoe Yesu kuwa bei ya ukombozi. Tena wanawafundisha kama, katika paradiso tutatunza dunia na wanyama milele.