Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 31

Uko Tayari Kumungojea Yehova?

Uko Tayari Kumungojea Yehova?

“Nitaonyesha mutazamo wa kumungojea.”​—MIK. 7:7.

WIMBO 128 Vumilia Mupaka Mwisho

KIFUPI YA HABARI *

1-2. Ni mambo gani tutachunguza mu hii habari?

KAMA uko unachunga muzigo fulani wenye uko na kitu yako lakini haufike, unaweza kujisikia namna gani? Utakuwa na wasiwasi? Pengine utajisikia sawa vile Mezali 13:12 inasema: “Tazamio lenye kucheleweshwa linafanya moyo ugonjwe.” Lakini, tuseme nini kama unapata habari kuwa kuko sababu za muzuri zenye zinafanya ule muzigo usifike vile ulitazamia? Mu ile hali, utakuwa kabisa tayari kungojea na kuvumilia.

2 Mu hii habari, tutazungumuzia kanuni za Biblia zenye zinaweza kutusaidia kukomalisha na kuendelea kuonyesha “mutazamo wa kungojea.” (Mik. 7:7) Kisha, tutachunguza hali mbili zenye zinaomba tumungojee Yehova kwa uvumilivu ili atende. Na ku mwisho, tutachunguza mambo ya muzuri yenye Yehova ameahidi kuwafanyia wale wenye wako tayari kumungojea.

KANUNI ZA BIBLIA ZENYE ZINATUFUNDISHA UVUMILIVU

3. Mezali 13:11 inatufundisha nini?

3 Mufano moja wenye unaonyesha ulazima wa uvumilivu ni ule wenye kuwa mu Mezali 13:11. Inasema hivi: “Mali yenye kupatikana haraka itapunguka, lakini mali ya ule mwenye anaikusanya kidogo-kidogo itaongezeka.” Tunajifunza nini hapa? Mutu mwenye kuwa na hekima anafanyaka mambo kwa uangalifu, kwa uvumilivu, na anapataka matokeo ya muzuri.

4. Kanuni yenye kuwa mu Mezali 4:18 inaonyesha nini?

4 Mezali 4:18 inatuambia kama “njia ya wenye haki iko kama mwangaza wenye kungaa wa asubui wenye kungaa zaidi na zaidi mupaka muchana kamili.” Hii maneno inaonyesha waziwazi kama Yehova anasaidia watu wake waelewe kusudi yake hatua kwa hatua. Lakini, ile andiko inatusaidia pia kuelewa namna Mukristo anafanya mabadiliko mu maisha yake na namna anamukaribia Yehova zaidi. Inaomba wakati juu mutu afikie kumukaribia Yehova zaidi. Kama tunajifunza kwa uangalifu na kutumikisha mashauri yenye tunapata kupitia Neno ya Mungu na tengenezo yake, tutaendelea hatua kwa hatua kuwa na sifa sawa za Kristo. Tena tutamujua Mungu muzuri zaidi. Ona namna Yesu alizungumuzia ile jambo.

Sawa vile mumea unakomalaka hatua kwa hatua, ni vile pia na mutu mwenye anasikia na anakubali ujumbe wa Ufalme, anakomalaka kiroho hatua kwa hatua (Ona fungu ya 5)

5. Ni mufano gani wenye Yesu alitoa ili kuonyesha kama inaomba wakati juu mutu afanye mabadiliko?

5 Yesu alitumia mufano moja ili kufasiria namna ujumbe wa Ufalme wenye tunahubiri unafanana na mbegu ya kidogo yenye inakomala polepole katika mioyo ya watu wenye kuwa tayari kusikiliza. Alisema: “Mbegu zinaota na zinakuwa za murefu​—lakini yeye [mupandaji] hajue zilifanya vile namna gani. Udongo wenyewe unazaa matunda hatua kwa hatua, kwanza jani, kisha suke, mwishowe mbegu kamili ndani ya suke.” (Mk. 4:27, 28) Yesu alipenda kusema nini? Alipenda tu kufasiria kama, sawa vile mumea unakomalaka hatua kwa hatua ni vile pia kwa mutu mwenye anakubali ujumbe wa Ufalme, anakomalaka kiroho hatua kwa hatua. Kwa mufano wakati wanafunzi wetu wa Biblia wanaanza kumukaribia Yehova zaidi ni vile tutaona mabadiliko ya muzuri yenye wanafanya. (Efe. 4:22-24) Lakini hatupaswe kusahau kama ni Yehova njo anafanya ile mbegu ya kidogo ikomale.​—1 Ko. 3:7.

6-7. Tunaweza kujifunza nini kuhusu namna Yehova aliumba dunia?

6 Mu mambo yote yenye Yehova anafanyaka anakamataka wakati wenye inaomba ili kutimiza kazi yake. Anafanyaka vile ili kuletea sifa jina yake na kusaidia wengine. Kwa mufano, fikiria namna Yehova alitayarisha dunia hatua kwa hatua kwa ajili ya wanadamu.

7 Kuhusu namna Yehova aliumba dunia, Biblia inaonyesha kama aliweka “vipimo vyake,” aliingiza “vikalio vyake,” na aliweka “jiwe lake la pembe.” (Yob. 38:5, 6) Alitumia hata wakati ili kuchunguza kazi yake. (Mwa. 1:10, 12) Fikiria namna malaika walijisikia wakati waliona kila kitu ya mupya yenye Yehova alikuwa ameumba. Walikuwa na furaha kabisa! Ile ilifanya waanze “kupandisha sauti za shangwe.” (Yob. 38:7) Namna Yehova aliumba dunia inatufundisha nini? Iliomba miaka ya mingi sana juu Yehova aumbe dunia, nyota na viumbe vyote vyenye kuishi, lakini wakati aliona mambo yote yenye alikuwa ameumba, alisema kama ‘ilikuwa muzuri sana.’​—Mwa. 1:31.

8. Ni mambo gani tutachunguza sasa?

8 Kama vile tumetoka kuona mu ile mifano, tumeona kanuni mbalimbali mu Biblia zenye zinatufundisha kama tunapaswa kuwa wavumilivu. Sasa, tuchunguze ni mu hali gani mbili tunapaswa kuwa tayari kumungojea Yehova.

NI WAKATI GANI TUKO NA LAZIMA YA KUMUNGOJEA YEHOVA?

9. Ni mu hali gani moja inaomba kumungojea Yehova?

9Tunaweza kumungojea Yehova ajibie sala zetu. Wakati tunamuomba Yehova atupatie nguvu ya kuvumilia magumu fulani ao atusaidie tuachane na jambo fulani yenye haimufurahishe, pengine tunaweza kujisikia sawa vile Yehova anakawia sana ili kujibia sala zetu. Juu ya nini Yehova hajibiake sala zote palepale?

10. Juu ya nini tunapaswa kungojea kwa uvumilivu Yehova ajibie sala zetu?

10 Yehova anasikilizaka kwa uangalifu sala zetu. (Zb. 65:2) Yehova anaona sala zetu kuwa ushuhuda wenye kuonyesha kama tuko na imani kwake. (Ebr. 11:6) Yehova anafurahi pia kuona namna tunajikaza ili kuishi kulingana na sala zetu, na wakati tunajikaza kufanya mapenzi yake. (1 Yo. 3:22) Kwa hiyo, wakati tunamuomba Yehova atusaidie tuache kufanya jambo fulani yenye haimupendeze, pengine tunapaswa kuwa wavumilivu na kufanya yote yenye tunaweza ili kubadilika. Yesu alitusaidia kuelewa kama, wakati fulani, pengine sala zetu haziwezi kujibiwa palepale. Alisema: “Muendelee kuomba, na mutapewa; muendelee kutafuta, na mutapata; muendelee kupiga hodi, na watawafungulia; kwa maana kila mutu mwenye anaomba anapewa, na kila mutu mwenye anatafuta anapata, na kila mutu mwenye anapiga hodi, watamufungulia.” (Mt. 7:7, 8) Wakati tunafuata hii shauri na “kudumu katika sala,” tunaweza kuwa hakika kama Baba yetu wa mbinguni atatusikiliza na atajibia sala zetu.​—Kol. 4:2.

Tunaendelea kusali kwa imani kwa Yehova, wakati tuko tunamungojea atende (Ona fungu ya 11) *

11. Namna gani Waebrania 4:16 inaweza kutusaidia wakati tunaona kama sala zetu zinakawia kujibiwa?

11 Hata kama, pengine tunaweza kuona kama sala zetu zinakawia na hazijibiwe, Yehova anatuahidi kuwa atajibia sala zetu “kwa wakati wenye kufaa.” (Soma Waebrania 4:16.) Njo maana hatupaswe kumulaumu Yehova, wakati jambo fulani yenye tulikuwa natazamia itimie kwa uharaka haitimie. Kwa mufano, watu wengi wamesali kwa miaka mingi juu Mungu alete Ufalme wake wenye utamaliza magumu yote. Hata Yesu alituambia kama tunapaswa kusali juu ya ile. (Mt. 6:10) Itakuwa kukosa akili kama mutu fulani anaacha imani yake kwa Mungu iregee juu tu mwisho haukufika kama vile wanadamu walitazamia! (Hab. 2:3; Mt. 24:44) Lakini, ni jambo ya hekima kuendelea kumungojea Yehova na kusali kwake, tukiwa na imani. Mwisho utafika kwa wakati wenye kufaa, juu Yehova alishapanga “siku na saa” yenye mwisho utafika. Na ile siku, njo itakuwaka siku ya muzuri zaidi kuliko zote.​—Mt. 24:36; 2 Pe. 3:15.

Mufano wa Yosefu unatufundisha nini kuhusu uvumilivu? (Ona fungu ya 12-14)

12. Ni wakati gani, inaweza kuwa nguvu zaidi kuonyesha uvumilivu ?

12Tunaweza kuwa na lazima ya uvumilivu wakati tunatendewa mu njia yenye haiko ya haki. Mara mingi, watu mu hii dunia, wanatendea wengine mubaya juu tu wako na rangi ingine ya ngozi, ni wa kabila ingine, ni wa inchi ingine ao juu tu ni wanaume ao wanamuke. Wengine wanatendewa mubaya juu tu wako na ulemavu fulani, ikuwe wa kimwili ao wa kiakili. Mashahidi wa Yehova wengi wametendewa kwa njia yenye haiko ya haki juu tu ya imani yao. Wakati tunatendewa mu njia ya vile, ni muzuri tusisahau hii maneno ya Yesu: “Ule mwenye atavumilia mupaka mwisho ataokolewa.” (Mt. 24:13) Lakini, unaweza kufanya nini ukisikia kama mutu fulani mu kutaniko alifanya kosa nzito? Kisha wazee kujulishwa, je, utaacha ile mambo ku mikono yao na kuendelea kuwangojea kwa uvumilivu ili washugulikie ile hali mu njia yenye inapatana na mapenzi ya Yehova ? Wazee wanaweza kufanya nini kama mutu fulani anafanya zambi nzito?

13. Kushugulikia mambo kwa kufuata muongozo wa Yehova, inatia ndani nini?

13 Wakati wazee wanapata habari kama mutu fulani alifanya zambi nzito,wanakuwaka wanatafuta “hekima yenye inatoka juu” katika sala, ili Yehova awasaidie waelewe ile hali mu namna yenye yeye anaielewa. (Yak. 3:17) Kusudi yao ni kusaidia ‘kurudisha mutenda-zambi kutoka kwenye kosa yake,’ kama inawezekana. (Yak. 5:19, 20) Tena, wanafanya yote yenye wanaweza ili kulinda kutaniko na kufariji wale wenye kuumizwa. (2 Ko. 1:3, 4) Wakati wako wanashugulikia zambi nzito, wazee wanapaswa kuelewa kwanza nini njo ilitokea, na ile inaomba wakati. Kisha wanasali, wanatoa mashauri yenye inatoka mu Maandiko na kutoa nizamu kwa “kiasi chenye kufaa.” (Yer. 30:11) Wazee wanaepuka kuchelewesha mambo, lakini, hawakamatake uamuzi haraka-haraka. Wakati wazee wanashugulikia mambo muzuri kwa kufuata muongozo wa Yehova, ile inaletea kutaniko faida. Hata kama wazee walishugulikia mambo mu njia ya muzuri, wale wenye walipatwa na matendo ya mubaya ya mutenda-zambi, wanaweza kuendelea tu kuhuzunika. Kama ile njo hali yenye uko nayo, unaweza kufanya nini ili kupunguza huzuni yako?

14. Ni mufano gani wenye kuwa mu Biblia wenye unaweza kukusaidia wakati Mukristo mwenzako anakukwaza?

14 Ulishakaumizwa sana na mutu fulani, hata Mukristo mwenzako? Unaweza kupata mifano ya muzuri sana mu Biblia yenye inaonyesha namna unaweza kuendelea kumungojea Yehova ili atengeneze mambo. Kwa mufano, hata kama Yosefu alitendewa mubaya na ndugu zake, hakuacha ile imufanye akuwe mutu wa kukasirika-kasirika. Kuliko kufanya vile, alikaza akili yake juu ya utumishi wake kwa Yehova, mwenye alimubariki sana juu ya uvumilivu wake. (Mwa. 39:21) Kisha wakati fulani, Yosefu alisamehe wale wenye walimukoseaka, na aliona namna Yehova alimubariki. (Mwa. 45:5) Sawa vile Yosefu, tunafarijiwa wakati tunamukaribia Yehova na tunaacha mambo ya mubaya yenye walitutendea mu mikono yake.​—Zb. 7:17; 73:28.

15. Ni nini ilisaidia dada moja avumilie ukosefu wa haki na akuwe na amani?

15 Kwa kweli, haiko kila aina ya ukosefu wa haki njo iko sawa ile yenye Yosefu alipataka. Lakini, hata kutendewa mubaya mu njia fulani, kunaweza kufanya tuhuzunike. Wakati kuko tatizo fulani kati yetu na mutu mwingine, hata mwenye haiko mutumishi wa Yehova, tunaweza kupata faida kubwa kama tunatumikisha kanuni za Biblia. (Flp. 2:3, 4) Fikiria mufano wenye kufuata. Dada moja alikwazika sana wakati alivumbula kama mufanyakazi mwenzake alikuwa anasema mambo yenye haiko ya muzuri juu yake kwa wengine. Kuliko kutenda haraka-haraka, dada yetu alikamata wakati na kufikiri sana juu ya mufano wa Yesu. Wakati Yesu alitukanwa, hakujibu kwa matukano. (1 Pe. 2:21, 23) Akiwa na ile mu akili, aliamua kutofanya jambo yoyote juu ya ile. Kisha wakati fulani, alipata habari kama ule mufanyakazi mwenzake alikuwa anahangaishwa sana na magonjwa. Kisha, dada akaelewa sasa kama ni ile hali njo ilifanya ule mufanyakazi mwenzake akuwe anasema vile. Njo maana, dada yetu alifurahi sana sababu alionyesha uvumilivu na ku mwisho alipata amani.

16. Ni nini inaweza kukufariji wakati uko unavumilia ukosefu wa haki? (1 Petro 3:12)

16 Kama uko unateseka kwa sababu ya ukosefu wa haki ao juu ya sababu ingine, kumbuka kama Yehova iko karibu na wale “wenye kuvunjika moyo.” (Zb. 34:18) Anakupenda sababu unaonyesha uvumilivu na unamutupia muzigo wako. (Zb. 55:22) Yeye njo muamuzi wa dunia. Anaona mambo yote yenye inatupata. (Soma 1 Petro 3:12.) Wakati uko unapambana na magumu yenye hauwezi kumaliza, je, uko tayari kumungojea Yehova?

BARAKA ZA MILELE KWA WALE WENYE WANAMUNGOJEA YEHOVA

17. Ni ahadi gani yenye Yehova ametupatia yenye kuwa mu Isaya 30:18?

17 Kupitia Ufalme wake, hivi karibuni, Baba yetu wa mbinguni atatubariki. Isaya 30:18 inasema hivi: “Yehova anawangojea kwa uvumilivu ili awaonyeshe wema, na atasimama ili kuwaonyesha rehema. Kwa maana Yehova ni Mungu wa haki. Wenye furaha ni wale wote wenye wanaendelea kumungojea.” Wale wote wenye wanaendelea kumungojea Yehova watapata baraka mingi, sasa na mu dunia mupya yenye kuja.

18. Ni baraka gani ziko zinatuchunga?

18 Wakati watu wa Mungu watakuwa mu dunia mupya, hawatakuwa tena wanapambana na mahangaiko na magumu yenye wako nayo leo. Ukosefu wa haki hautakuwa tena wala maumivu. (Ufu. 21:4) Hatutakuwa tena na wasiwasi juu ya mambo yenye tuko nayo lazima, sababu kila mutu atakuwa tayari na kila kitu yenye iko nayo lazima. (Zb. 72:16; Isa. 54:13) Ile itakuwa baraka kabisa, hauone vile?

19. Namna gani Yehova iko anatutayarisha tangu sasa hatua kwa hatua?

19 Tangu sasa, Yehova iko anatutayarisha ili tuishi chini ya utawala wake, kwa kutusaidia tushinde tabia za mubaya na pia kwa kukomalisha sifa zenye zinamupendeza. Njo maana, usivunjike moyo na usiache hata kidogo kumutumikia Yehova. Mambo ya muzuri zaidi iko mbele yetu! Wakati wenye kuja wa muzuri sana uko unatuchunga. Kwa hiyo basi, tuendelee kuwa tayari kumungojea Yehova kwa uvumilivu wakati anaendelea kutimiza mambo yenye alituahidi!

WIMBO 118 ‘Unipatie Imani Zaidi’

^ fu. 5 Ulishakasikia mutumishi fulani wa Yehova mwenye alishakawia sana mu tengenezo anasema, ‘Sikuwaziaka kama ningezeeka mu hii dunia muovu ya Shetani!’ Siye wote tunapenda Yehova amalize magumu yote yenye kuwa mu hii dunia, zaidi sana mu hii kipindi ya mubaya. Lakini tunapaswa kujifunza kuwa wavumilivu. Mu hii habari, tutachunguza kanuni fulani za Biblia zenye zitatusaidia kuendelea kuwa na mutazamo wa kungojea. Tutaona pia hali mbili, zenye zinaomba tuendelee kumungojea Yehova kwa uvumilivu. Na ku mwisho, tutaona mambo ya muzuri yenye Yehova ameahidi kuwafanyia wale wenye wako tayari kumungojea.

^ fu. 56 MAFASIRIO YA PICHA: Tangu wakati alikuwa mutoto, dada mumoja iko na zoezi ya kusali kwa Yehova. Wakati alikuwa mudogo, wazazi wake walimufundisha namna ya kusali. Na wakati alikuwa kijana, alianza kufanya kazi ya upainia na kila mara alikuwa anaomba Yehova abariki utumishi wake. Kisha miaka fulani, wakati bwana yake aligonjwa, alisali sana kwa Yehova ili amupatie nguvu yenye iko nayo lazima juu ya kuvumilia ile hali. Leo, iko mujane, lakini anadumu katika sala, na iko hakika kama Baba yake wa mbinguni Yehova atajibia sala zake, sawa vile alijibia sala zake mu maisha yake.