Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 32

Tia Nguvu Imani Yako Katika Muumbaji

Tia Nguvu Imani Yako Katika Muumbaji

“Imani ni . . . uhakikisho wenye uko wazi wa mambo ya kweli yenye hayaonekane.”​—EBR. 11:1.

WIMBO 11 Uumbaji Unamusifu Mungu

KIFUPI YA HABARI *

1. Ulijifunza mambo gani kuhusu Muumbaji wetu?

KAMA ulikomala mu familia ya Mashahidi wa Yehova ni wazi kuwa ulijifunza juu ya Yehova ukiwa mutoto mudogo sana. Ulijifunza kama yeye njo Muumbaji, kama iko na utu wa muzuri, na kama iko na kusudi ya muzuri kwa ajili ya wanadamu.​—Mwa. 1:1; Mdo. 17:24-27.

2. Namna gani watu fulani wanaona wale wenye wanaamini kama kuko Muumbaji?

2 Lakini, watu wengi hawaamini kama Mungu iko na kama yeye njo Muumbaji wa kila kitu. Wanaamini kama uzima ulijitokeza wenyewe na kama ulianza kubadilika-badilika kuanzia mu vitu fulani vyenye kuishi vya kawaida mupaka kufikia mu aina zingine za vitu fulani vyenye kuishi vyenye kuwa ajabu zaidi. Watu fulani wenye wanaamini ile mambo ni watu wenye walisomaka sana. Wanaweza kusema kama sayansi ilishaonyesha kuwa mambo yenye Biblia inasema ni ya uongo na kama watu wenye hawakusoma sana, wenye hawana akili mingi ao wenye wanadanganywa kwa urahisi njo wanaamini kama kuko Muumbaji.

3. Juu ya nini ni jambo ya maana sana kutia nguvu imani yetu?

3 Mawazo ya watu fulani wenye kusoma sana inaweza kutufanya tukuwe na mashaka kama Yehova njo Muumbaji wetu mwenye upendo? Ile inategemea zaidi sana sababu zenye zinafanya tuamini kama Yehova njo Muumbaji. Tunaamini vile juu tu walituambia tuamini ao juu tulikamata wakati wa kuchunguza ushuhuda wenye kuonyesha kama kuko Muumbaji? (1 Ko. 3:12-15) Hata kama tulishafanya miaka ngapi na tuko Mashahidi wa Yehova, siye wote tunapaswa kuendelea kutia nguvu imani yetu. Kama tunafanya vile hatutadanganywa na “filozofia na udanganyifu wa bure,” wenye unafundishwa na watu wenye wanapinga Neno ya Mungu. (Kol. 2:8; Ebr. 11:6) Juu ya kutusaidia hii habari itazungumuzia (1) juu ya nini watu wengi hawaamini kama kuko Muumbaji, (2) namna gani unaweza kutia nguvu imani yako katika Yehova, Muumbaji wako na (3) namna gani unaweza kuendelea kutia nguvu imani yako.

JUU YA NINI WATU WENGI HAWAAMINI KAMA KUKO MUUMBAJI?

4. Kulingana na Waebrania 11:1 na maelezo ya chini, imani ya kweli inategemea nini?

4 Watu fulani wanawaza kama kukuwa na imani ni kuamini jambo fulani bila ushuhuda. Lakini, kulingana na Biblia ile haiko imani ya kweli. (Soma Waebrania 11:1 na maelezo ya chini.) Imani katika mambo ya kweli yenye haionekane, sawa vile Yehova, Yesu na Ufalme wa mbinguni inategemea uhakikisho wenye kusadikisha. (Ebr. 11:3) Mwanasayansi mumoja mwenye alifikia kuwa Shahidi anasema hivi: “Mambo yenye Mashahidi wa Yehova wanaamini iko na musingi fulani. Lakini hawapuuze mambo yenye sayansi inasema.”

5. Juu ya nini watu wengi wanaamini kama Mungu hakuumba viumbe vyote vyenye kuishi?

5 Pengine tunaweza kujiuliza, ‘Juu ya nini watu wengi wanaamini kama Mungu hakuumba viumbe vyote vyenye kuishi, ijapokuwa kuko ushuhuda wenye kusadikisha kama kuko Muumbaji?’ Kwa kifupi watu fulani hawayachunguzaka wao wenyewe ushuhuda wenye kuonyesha kama kuko Muumbaji. Robert, mwenye sasa ni Shahidi wa Yehova, anasema hivi: “Juu hakuna siku tulijifunzaka uumbaji ku masomo, nilikuwa hakika kama uumbaji haiko kweli. Lakini nilibadilisha mawazo yangu saa nilifikia miaka 20 hivi. Wakati niliongea na Mashahidi wa Yehova, walinisaidia kuelewa kama Biblia inaleta sababu zenye kusadikisha zenye zinaonyesha kama Mungu njo aliumba vitu vyote.” *​—Ona kisanduku “ Ujumbe kwa Wazazi.”

6. Juu ya nini watu fulani hawaamini kama kuko Muumbaji?

6 Watu fulani hawaamini kama kuko Muumbaji, juu wanasema kama wanaamini tu mambo yenye wanaweza kuona. Lakini wanaamini mambo yenye hawawezi hata kuona. Kwa mufano, wanaamini nguvu za uvutano juu wako na ushuhuda wenye kuonyesha kama ni ya kweli. Imani yenye Biblia inazungumuzia inatia ndani ushuhuda wa mambo ya “kweli yenye hayaonekane.” (Ebr. 11:1) Inaomba wakati na kujikaza sana ili kuchunguza ushuhuda, na watu wengi hawapendake kujikaza kufanya vile. Mutu mwenye hachunguze ushuhuda yeye mweyewe anaweza tu kufikia kusema kama hakuna Mungu.

7. Ni watu wote wenye kusoma njo wanakatalaka kama Mungu njo aliumbaka vitu vyote? Fasiria.

7 Kisha kuchunguza ushuhuda, wanasayansi fulani walifikia kuamini kama Mungu njo aliumbaka vitu vyote. * Sawa vile Robert, mwenye tulishataja, watu fulani wamesema kama hakuna Muumbaji juu tu hawakuwafundishaka mambo ya uumbaji ku université. Lakini, wanasayansi wengi wanafikia kumujua Yehova na kumupenda. Sawa vile wale wanasayansi, siye wote tunapaswa kutia nguvu imani yetu katika Mungu ikuwe tulisoma mingi ao hapana. Hakuna mutu mwenye anaweza kutufanyia ile.

NAMNA UNAWEZA KUTIA NGUVU IMANI YAKO KATIKA MUUMBAJI

8-9. (a) Tutazungumuzia ulizo gani? (b) Kujifunza kuhusu uumbaji kutakuletea faida gani?

8 Namna gani unaweza kutia nguvu imani yako katika Muumbaji? Tuzungumuzie basi njia ine.

9Ujifunze kuhusu uumbaji. Unaweza kutia nguvu imani yako katika Muumbaji kwa kuchunguza wanyama, mimea, na nyota. (Zb. 19:1; Isa. 40:26) Kadiri unajifunza mambo sawa ile ni vile utafikia kuwa hakika kama Yehova njo Muumbaji. Mara mingi, vichapo vyetu vinakuwaka na habari zenye zinafasiria mambo mbalimbali kuhusu uumbaji. Hata kama unaona kuwa ni nguvu kuelewa zile habari, usiepuka kuzisoma. Ujikaze kabisa kuzisoma na usikose kufungula site yetu ya jw.org ili kuangalia video za muzuri kuhusu uumbaji zenye tuliona ku mikusanyiko yetu ya eneo hivi karibuni.

10. Leta mufano wenye unahakikisha kama kuko Muumbaji. (Waroma 1:20)

10 Wakati uko unajifunza kuhusu uumbaji utilie uangalifu ile unaweza kujifunza kuhusu Muumbaji wetu kupitia mambo fulani. (Soma Waroma 1:20.) Kwa mufano, jua inatutolea joto na mwangaza wenye uko wa lazima sana juu tuendelee kuishi hapa ku dunia. Lakini miale ao rayons fulani za jua inaweza kuwa hatari. Siye wanadamu tuko na lazima ya kulindwa na ile miale hatari. Na kusema kweli tunalindwa nayo. Namna gani? Dunia yetu inalindwa na ile yenye inaitwa gaze ya ozone. Ile gaze ya ozone inatulinda ili tusipatwe na miale hatari. Wakati ile miale hatari inakuwa nguvu zaidi, gaze ya ozone pia inaongezeka. Sasa hauone kama kunapaswa kuwa mutu mwenye kuwa nyuma ya ile yote, na kama anapaswa kuwa Muumbaji mwenye upendo na mwenye akili?

11. Ni wapi unaweza kupata habari zenye kutia nguvu imani katika uumbaji? (Ona kisanduku “ Vyombo Fulani Vya Kusaidia Kutia Nguvu Imani.”)

11 Unaweza kupata habari zenye kutia nguvu imani kuhusu uumbaji mu Fahirisi (Endekse) na kutafuta habari ku jw.org. Pengine unaweza kuanza na habari na video zenye kuwa ku sehemu “Kitu Hiki Kilijifanya Chenyewe?” Ni za mufupi-mufupi na zinaleta habari zenye kushangaza kuhusu wanyama na mimea. Ziko pia na mifano yenye kuonyesha namna wanasayansi wamejaribu kutengeneza vitu fulani kwa kuangalia uumbaji.

12. Ni mambo gani tunapaswa kukazia uangalifu wakati tuko tunajifunza Biblia?

12Ujifunze Biblia. Ku mwanzo, mwanasayansi mwenye tulishataja alikatala ile wazo yenye kusema kama kuko Muumbaji. Kisha wakati fulani alifikia kuamini kama kuko Muumbaji. Anasema hivi: “Imani yangu haikutegemea tu mambo yenye nilijifunza mu sayansi lakini ilitegemea pia mambo yenye nilijifunza mu Biblia.” Pengine tayari unajua muzuri mambo yenye Biblia inafundisha. Hata vile, ili kutia nguvu imani yako katika Muumbaji unapaswa kuendelea kujifunza Neno ya Mungu. (Yos. 1:8; Zb. 119:97) Fikiria maelezo ya kweli yenye Biblia inatoa juu ya matukio fulani. Kazia uangalifu unabii mbalimbali na namna Biblia inapatana. Kufanya vile, kutatia nguvu imani yako na kutakuhakikishia kama kuko Muumbaji mwenye upendo na hekima na kama ujumbe wenye kuwa mu Biblia ulitoka kwake. *​—2 Ti. 3:14; 2 Pe. 1:21.

13. Leta mufano moja wa hekima wenye kupatikana mu Neno ya Mungu?

13 Wakati uko unajifunza Neno ya Mungu, ona namna mashauri yenye kuwa ndani inaweza kukuletea faida. Kwa mufano, tangu zamani Biblia ilionya kama kupenda makuta ni hatari na inaweza kuleta “maumivu mengi.” (1 Ti. 6:9, 10; Mez 28:20; Mt. 6:24) Ile onyo inatuhusu pia leo? Kitabu moja inasema hivi: “Mara mingi watu wenye wanaamini kama kuwa na makuta njo jambo ya maana sana mu maisha, hawakuwake na furaha sana na wanakuwaka wenye kushuka moyo zaidi. Hata watu wenye wanapendaka kuwa na makuta mingi sana hakuwake na furaha sana na wanakuwaka na matatizo mingi ya afya.” (The Narcissism Epidemic) Kusema kweli, ile onyo ya Biblia kuhusu kupenda makuta ni ya muzuri sana! Unakumbuka kanuni zingine za Biblia zenye zimekusaidia? Kadiri tunapenda mashauri yenye kuwa mu Biblia, ni vile tutategemea hekima ya juu sana yenye Muumbaji wetu mwenye upendo anatutolea. (Yak. 1:5) Ile itafanya maisha yetu ikuwe ya muzuri zaidi.​—Isa. 48:17, 18.

14. Funzo ya Biblia inafunua nini kuhusu Yehova?

14Ujifunze Biblia na kusudi ya kufikia kumujua Yehova zaidi. (Yoh. 17:3) Wakati unajifunza Biblia utajua mambo mingi kuhusu utu na sifa za Yehova​—zile sifa ni zilezile zenye ulipata wakati ulikuwa unajifunza kuhusu uumbaji. Kujifunza kuhusu sifa za Yehova kutatuhakikishia kama Yehova anakuwaka kabisa. (Kut. 34:6, 7; Zb. 145:8, 9) Kadiri unajifunza kuhusu Yehova muzuri zaidi ni vile utakuwa na imani ya nguvu zaidi katika yeye na urafiki wako pamoja naye utakuwa nguvu zaidi.

15. Ni faida gani utapata kama unaambia wengine imani yako?

15Uambie wengine juu ya imani yako. Kama unafanya vile imani yako itakuwa nguvu sana. Lakini tuseme nini kama mutu fulani mwenye uko unahubiria anakuuliza ulizo, ili kujua kama Mungu anakuwaka ao hapana na pengine haujue umujibie nini? Jaribu kutafuta jibu ya Biblia mu vichapo vyetu na kisha uongee naye. (1 Pe. 3:15) Tena, unaweza kuomba musaada kwa Shahidi mwenzako mwenye kuwa na uzoefu zaidi. Ikuwe ule mutu anakubali majibu ya Biblia ao hapana utakuwa umepata faida juu ulitafuta habari. Imani yako itakuwa nguvu zaidi. Ile itafanya usiamini fundisho ya wale wenye wanaonekana kuwa na hekima ao wenye walisomaka sana, wenye wanasema kama hakuna Muumbaji.

ENDELEA KUTIA NGUVU IMANI YAKO!

16. Ni nini inaweza kutokea kama hatuendelee kutia nguvu imani yetu?

16 Hata kama tulishamutumikia Yehova masiku ngapi, tunapaswa kuendelea kutia nguvu imani yetu. Juu ya nini? Ni juu kama hatuko waangalifu imani yetu inaweza kuregea. Tusisahau kama, imani inatia ndani uhakikisho wa mambo ya kweli yenye hayaonekane. Ni mwepesi kusahau mambo yenye hatuwezi kuona. Njo maana Paulo alisema kama kukosa imani ni “zambi yenye kutuzuia kwa wepesi.” (Ebr. 12:1) Sasa, tunaweza kufanya nini juu tusiangukie mu ile mutego?​—2 Te. 1:3.

17. Tuko na lazima ya nini juu ya kuendelea kuwa na imani ya nguvu?

17 Kwanza, umuombe Yehova akupatie roho yake takatifu na ufanye vile mara mingi. Juu ya nini? Juu imani ni sehemu ya tunda la roho. (Gal. 5:22, 23) Hatuwezi kuendelea kutia nguvu imani yetu katika Muumbaji bila musaada wa roho yake takatifu. Tukiendelea kumuomba Yehova roho yake takatifu atatupatia. (Lu. 11:13) Kwa mufano, tunaweza hata kumuambia hivi: “Utupatie imani zaidi.”​—Lu. 17:5.

18. Kulingana na Zaburi 1:2, 3, siye wote tuko na pendeleo gani?

18 Tena, ukuwe unajifunza Neno ya Mungu kwa ukawaida. (Soma Zaburi 1:2, 3.) Wakati ile zaburi ilitungwa ni Waisraeli kidogo tu njo walikuwa na kopi ya Sheria yote ya Mungu yenye kuandikwa. Lakini, mufalme na makuhani walikuwa na kopi, na ku mwisho wa kila miaka saba mipango ilikamatwa ili “wanaume, wanamuke, watoto,” na wakaaji wageni wenye walikuwa mu Israeli wasikilize usomaji wa Sheria ya Mungu. (Kum. 31:10-12) Mu wakati ya Yesu, ni watu kidogo tu njo walikuwa na vitabu vya kukunjwa vya Maandiko na pia mu masinagogi. Tofauti na ile, leo watu wengi wanaweza kupata Neno ya Mungu. Ile ni pendeleo. Namna gani tunaweza kuonyesha kama tunasamini ile pendeleo?

19. Tunapaswa kufanya nini juu imani yetu iendelee kuwa nguvu?

19 Tunaonyesha kama tunasamini ile pendeleo kwa kusoma Neno ya Mungu kwa ukawaida. Tunapaswa kupanga wakati wetu muzuri ili kusoma na kujifunza Biblia, hapana tu kuisoma saa yenye tunajisikia tuko na wakati. Wakati tunaendelea kuheshimia programu yetu ya kujifunza Biblia ile inaweza kufanya imani yetu iendelee kuwa nguvu.

20. Tunapaswa kuazimia kufanya nini?

20 Tofauti na “wenye hekima na wenye elimu” wa hii dunia, siye imani yetu inategemea Neno ya Mungu. (Mt. 11:25, 26) Kwa kujifunza ile kitabu takatifu, tunaelewa sababu zenye kufanya hali mu dunia ikuwe mubaya na nini Yehova anapanga kufanya wakati wenye kuja. Kwa hiyo basi, tuazimie kuendelea kutia nguvu imani yetu na kusaidia watu wengi kadiri inawezekana ili nao wakuwe na imani katika Muumbaji wetu. (1 Ti. 2:3, 4) Na tuendelee pia kuchunga kwa furaha wakati yenye kila kiumbe yenye kuwa na uzima hapa ku dunia kitamusifu Yehova na kusema maneno yenye kuwa mu Ufunuo 4:11: “Unastahili, Yehova Mungu wetu, kupokea utukufu . . . kwa sababu uliumba vitu vyote.”

WIMBO 2 Jina Yako Ni Yehova

^ fu. 5 Biblia inafundisha kabisa kama Yehova Mungu njo Muumbaji. Lakini watu wengi hawaamini vile. Wanasema kama mambo yote ilijitokeza. Mambo yote yenye wanasema itafanya tukuwe na mashaka kuwa Yehova ni Muumbaji wa kila kitu? Hapana. Hatutakuwa na mashaka ikiwa tunatia nguvu imani yetu katika Mungu na katika Biblia. Hii habari itafasiria namna tunaweza kufanya vile.

^ fu. 5 Ku masomo ya mingi, walimu hawafundishe hata kama Mungu njo aliumbaka vitu vyote. Walimu fulani wanasema kama, kufundisha mambo ya vile kunavunja uhuru wa dini wa wanafunzi.

^ fu. 7 Maelezo ya watu zaidi ya 60 wenye walisoma sana, kutia ndani wanasayansi wenye wanaamini uumbaji, inapatikana mu Fahirisi (Endekse). Ona sehemu “Sayansi,” chini ya kichwa “wanasayansi wanaoamini uumbaji.” Maelezo fulani kati ya ile inaweza pia kupatikana mu Musaada wa Kutafuta Habari kwa Ajili ya Mashahidi wa Yehova. Ona sehemu “Sayansi na Teknolojia,” chini ya kichwa “‘Sehemu ya Kuuliza Maulizo’ (ya Amuka!).”

^ fu. 12 Kwa mufano, ona habari “Je, Sayansi Inapatana na Biblia?” yenye kuwa mu Gazeti Amuka! ya Mwezi wa 2, 2011 na habari “Yale Anayotabiri Yehova Yanatimia,” yenye kuwa mu Munara wa Mulinzi wa Tarehe 1 Mwezi wa 1, 2008.