Amila mo ibi abali

Amila mu gagabi

MAKALA JA FUNZO 33

Gupata Kutogule Katika Mapendeleu Gagubinaku

Gupata Kutogule Katika Mapendeleu Gagubinaku

“Kubi afazali mundu jutogulya mambu ambagu galinga miu gaki kuliku kuyumbayumba kukupwata tamaa yaki.”—MHU. 6:9.

NHAMBU 111 Sababu za Kuwa na Shangwe

MUHTASARI *

1.Aka ndugu na dada bingi bijitahidi kwi indela bo kuhenga gingi ngani katika utumishi guka Yehova?

 TUNA kazi nyingi zaidi za kufanya kadiri mfumo huu wa mambo unavyokaribia mwisho wake. (Mt. 24:14; Luka 10:2; 1 Pet. 5:2) Sote tunataka kumtumikia Yehova kwa uwezo wetu wote. Ndugu na dada wengi wanapanua huduma yao. Baadhi wanatamani kutumikia wakiwa mapainia. Wengine wanatamani kutumikia Betheli au kushiriki katika ujenzi wa majengo ya kitheokrasi. Na ndugu wengi wanajitahidi kustahili kufikia kuwa watumishi wa huduma au wazee. (1 Tim. 3:1, 8) Ni lazima Yehova awe anafurahi sana anapoona roho hiyo ya utayari miongoni mwa watu wake!—Zab. 110:3; Isa. 6:8.

2. Pangi tuhisi bo anangase tuhiki baazi jimalengu gitu gikiloho?

2 Hata hivyo, tunaweza kuanza kuvunjika moyo ikiwa muda mrefu umepita na bado hatujafikia baadhi ya malengo yetu ya kiroho. Au huenda tukavunjika moyo ikiwa kwa sababu ya umri au hali nyingine, hatuwezi kupata baadhi ya mapendeleo katika tengenezo la Yehova. (Met. 13:12) Hivyo ndivyo ilivyo kwa Melissa. * Angependa kutumikia Betheli au kuhudhuria Shule ya Waeneza Injili wa Ufalme lakini anasema hivi: “Nimepita kigezo cha umri. Hivyo kwangu mapendeleo hayo ni ndoto tu. Nyakati nyingine ninavunjika moyo.”

3. Pangi baazi jaka ndugu na dada bakaitajia kuhenga ki ilibistahilia mapendeleu fulane?

3 Baadhi ya ndugu na dada ni vijana na wana afya nzuri, lakini huenda wakahitaji muda wa kukomaa zaidi na kusitawisha sifa fulani kabla hawajastahili kupewa mapendeleo zaidi. Kwa upande mmoja, huenda wana akili, ni thabiti, na wana roho ya utayari; lakini kwa upande mwingine huenda wakahitaji kujifunza kuwa wenye subira zaidi, kufanya mambo kikamili zaidi, au kuwaheshimu wengine zaidi. Ikiwa utakazia fikira sifa zinazohitajika, unaweza kupata pendeleo la utumishi wakati ambapo hukulitarajia. Fikiria kisa cha Nick. Alipokuwa na umri wa miaka 20, alivunjika moyo sana kwa sababu hakupendekezwa kuwa mtumishi wa huduma. Anasema hivi: “Nilihisi kwamba lazima nina kasoro fulani.” Lakini Nick hakufa moyo. Alifanya yote aliyoweza kutanikoni na katika kazi ya kuhubiri. Leo, anatumikia akiwa mshiriki wa Halmashauri ya Tawi.

4. Ngisi tulongalya ki mu makala jenzeno?

4 Je, umevunjika moyo kwa sababu bado hujafikia malengo fulani ya kiroho? Ikiwa ndivyo, mweleze Yehova hangaiko lako. (Zab. 37:5-7) Pia, waombe akina ndugu wakomavu mapendekezo ya jinsi unavyoweza kuboresha utumishi wako kwa Mungu, kisha jitahidi kadiri unavyoweza kutumia ushauri wao. Kwa kufanya hivyo, huenda ukafaulu kupata pendeleo unalotamani au kufikia lengo lako. Lakini kama ilivyokuwa katika kisa cha Melissa, aliyetajwa awali, huenda kwa sasa huwezi kupata pendeleo hilo unalotamani. Utafanya nini? Unaweza kudumishaje shangwe yako? Ili kujibu swali hilo, makala hii itazungumzia (1) utafute wapi shangwe, (2) jinsi ya kuongeza shangwe yako, na (3) aina ya malengo unayoweza kujiwekea ambayo yataongeza shangwe yako.

GUTAPUTA KWA LAHA?

5. Ili tubya na laha tutakiwa kukasi fikila kike? (Mhubiri 6:9)

5 Kama Mhubiri 6:9 inavyoeleza, tunaweza kupata shangwe ikiwa tunaitafuta mahali sahihi. (Soma.) Mtu anayefurahia “mambo ambayo macho yanaona” anaridhika na kile alicho nacho, kama vile hali zake za sasa. Kinyume cha hilo, mtu anayetangatanga akifuatia tamaa zake anaendelea kutamani kitu ambacho hawezi kukipata. Hivyo, somo ni nini kwetu? Ili kupata shangwe, tunapaswa kukazia fikira kile tulicho nacho na kile ambacho kihalisi tunaweza kupata.

6. Ngisitusungasa nfanu bo, na ngisitukasila fikila kike?

6 Je, kwa kweli inawezekana kuridhika na vitu ambavyo tayari tunavyo? Isitoshe, kadiri muda unavyopita, kiasili sisi hutafuta changamoto mpya. Ndiyo, kwa kweli inawezekana kuridhika na vitu tulivyo navyo. Tunaweza kufurahia kile ambacho “macho yanaona,” si tu kukubaliana na hali. Tunaweza kufanyaje hivyo? Ili tupate jibu, acheni tuchunguze mfano wa Yesu wa talanta unaopatikana kwenye Mathayo 25:14-30. Tutakazia fikira mambo ambayo mfano huo unaweza kutufundisha kuhusu jinsi ya kupata na hata kuongeza shangwe yetu, katika baraka ambazo kwa sasa tunazo.

JINSI JU KUJONZUKE LAHA JAKU

7. Elasa ku ufupi nfanu guka Yesu gwa talanta.

7 Katika mfano wa talanta, mwanamume fulani alikuwa anaenda safarini. Kabla ya kuondoka, aliwaita watumwa wake na kuwakabidhi talanta ili wafanye biashara nazo. * Akifikiria uwezo wa kila mtumwa, mwanamume huyo alimpatia mtumwa mmoja talanta tano, mwingine talanta mbili, na mtumwa wa tatu talanta moja. Watumwa wawili wa kwanza walifanya kazi kwa bidii ili kupata pesa zaidi kwa ajili ya bwana wao. Hata hivyo, mtumwa wa tatu hakuzifanyia kazi pesa alizopewa na bwana wake na hivyo akamfukuza.

8. Ndabajaki mtumwa jwa kwanza katika nfanu gwa talanta jukawesa kuba na laha?

8 Ni lazima mtumwa wa kwanza alihisi ni pendeleo kubwa sana kukabidhiwa talanta tano na bwana wake. Hizo zilikuwa pesa nyingi sana, na ilionyesha jinsi bwana huyo alivyomtumaini mtumwa wake. Lakini vipi kuhusu mtumwa wa pili? Angeweza kuvunjika moyo kwa sababu hakupewa talanta nyingi kama mtumwa wa kwanza. Lakini alitendaje?

9. Yesu ngasejwapwaga ki kuusu mtumwa jwa pile? (Mathayo 25:22, 23)

9 Soma Mathayo 25:22, 23. Yesu hakusema kwamba mtumwa wa pili alikasirika na kuweka kinyongo kwa sababu alipewa talanta mbili tu. Na Yesu hakusema kwamba mtumwa huyo alilalamika hivi: ‘Yaani, amenipa hizi tu? Hata mimi nina uwezo sawa na yule mtumwa aliyepata talanta tano! Basi ikiwa bwana wangu hanithamini, ni bora nizifukie talanta hizi mbili na kufuatia mapendezi yangu mwenyewe.’

10. Mtumwa jwa pili juihengila ki talanta yake?

10 Kama mtumwa wa kwanza, mtumwa wa pili alichukua kwa uzito sana jukumu alilopewa na alifanya kazi kwa bidii ili kumtumikia bwana wake. Matokeo ni kwamba alipata talanta mbili zaidi. Mtumwa huyo alithawabishwa sana kwa sababu ya bidii na ustadi wake. Bwana wake hakushangilia tu, bali pia aliona kwamba mtumwa huyo alistahili kuongezewa majukumu hata zaidi!

11. Tuwesa kujonzuke bo talanta ito?

11 Vivyo hivyo, tunaweza kuongeza shangwe yetu kwa kuzama kabisa katika kazi yoyote ambayo tunapewa katika utumishi wa Yehova. ‘Jishughulishe sana’ na kazi ya kuhubiri na ujihusishe kikamili katika utendaji wa kutaniko. (Mdo. 18:5; Ebr. 10:24, 25) Hudhuria mikutano ukiwa umejitayarisha kutoa maelezo yenye kujenga kwenye habari mtakayozungumzia. Chukua kwa uzito migawo yote ya wanafunzi ambayo umepewa kwenye mkutano wa katikati ya juma. Ikiwa utaombwa kusaidia kazi fulani kutanikoni, fika kwa wakati na uwe mwenye kutegemeka. Usiuone mgawo wowote unaopewa kuwa si muhimu na kwamba huhitaji kutumia muda wako kuufanya. Jitahidi kuboresha ustadi wako. (Met. 22:29) Kadiri unavyozama kabisa katika utendaji na migawo yako ya kiroho, ndivyo utakavyofanya maendeleo haraka zaidi na shangwe yako itaongezeka zaidi. (Gal. 6:4) Pia, itakuwa rahisi zaidi kushangilia pamoja na wengine wanapopokea pendeleo ambalo unalitamani.—Rom. 12:15; Gal. 5:26.

12. Mashahidi abeli bahenga ki ilikujonzuke laha jabo?

12 Je, unamkumbuka Melissa, dada aliyesema kwamba alitamani kutumikia Betheli au kuhudhuria Shule ya Waeneza Injili wa Ufalme? Ingawa hawezi kutimiza malengo hayo, anasema hivi: “Ninajitahidi kuzama kabisa katika utumishi wangu wa upainia na kujitahidi kushiriki katika njia zote za kuhubiri. Kufanya hivyo kumeniletea shangwe kubwa.” Na Nick alikabilianaje na hali yake ya kuvunjika moyo wakati hakupendekezwa kuwa mtumishi wa huduma? Anasema hivi: “Nilikazia fikira mapendeleo niliyokuwa nayo, yaani, kushiriki katika huduma ya shambani na kutoa maelezo yenye kujenga kwenye mikutano. Pia, nilijaza fomu ya ombi la utumishi wa Betheli na nikaalikwa mwaka uliofuata.”

13. Gwipata matokeu bo ana gwilinga kabisa mumgau gwaku sajeno? (Mhubiri 2:24)

13 Ikiwa utazama kabisa katika mgawo wako wa sasa, je, utapata majukumu zaidi wakati ujao? Hilo linaweza kutokea, kama ilivyokuwa kwa Nick. Lakini isipotokea hivyo, kama ilivyokuwa kwa Melissa, bado unaweza kuongeza shangwe yako, nawe utaridhika sana na kufurahia yale unayotimiza. (Soma Mhubiri 2:24.) Zaidi ya hayo, bila shaka utapata shangwe nyingi ukijua kwamba jitihada zako zinamfurahisha Bwana wetu, Yesu Kristo.

MALENGU GAGUTUJONZUKE LAHA

14. Pakuusu malengu gitu gikiloho tutakiwa kukomboka kike?

14 Je, kukazia fikira mgawo wetu wa sasa kunamaanisha kwamba tunapaswa kuacha kutafuta njia za kupanua utumishi wetu kwa Yehova? La hasha! Tunaweza na tunapaswa kujiwekea malengo ya kiroho yanayoweza kutusaidia kuendelea kujitahidi kuwa na matokeo zaidi katika huduma, na kuwasaidia ndugu na dada zetu. Tutafaulu kufikia malengo hayo ikiwa kwa hekima na kiasi tutakazia fikira kuwatumikia wengine badala ya kujifikiria sisi wenyewe.—Met. 11:2; Mdo. 20:35.

15. Gabi malengu bo gagijonzukya laha jako?

15 Unaweza kujiwekea malengo gani? Mwombe Yehova akusaidie kutambua malengo ambayo kihalisi unaweza kutimiza. (Met. 16:3; Yak. 1:5) Je, unaweza kujitahidi kufikia mojawapo ya malengo yaliyotajwa katika  fungu la kwanza la makala hii, yaani, kufanya upainia msaidizi au upainia wa kawaida, kutumikia Betheli au kushiriki katika miradi ya ujenzi? Au unaweza kujifunza lugha mpya ili ushiriki kueneza habari njema au hata kwenda kuhubiri katika eneo lingine la kigeni. Unaweza kujifunza yale yanayohusika kwa kusoma sura ya 10 ya kitabu Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova na kwa kuzungumza na wazee katika kutaniko lako. * Unapojitahidi kufikia malengo hayo, maendeleo yako yataonekana wazi na shangwe yako itaongezeka.

16. Guwesa kuhenga ki ana kwa sajenu ngakuwesa kuiki lilengu fulani ususa?

16 Lakini vipi ikiwa kwa sasa huwezi kufikia mojawapo ya malengo yaliyotajwa katika makala hii? Jambo muhimu ni kujiwekea lengo lingine ambalo unaweza kulifikia. Fikiria malengo yafuatayo.

17. Kulengana na 1 Timotheo 4:13, 15,ndugu juwesa kuhenga ki ilijubya mwalimu jwa sapi ngane?

17 Soma 1 Timotheo 4:13, 15. Ikiwa wewe ni ndugu aliyebatizwa, unaweza kuboresha uwezo wako wa kuwa msemaji na mwalimu mzuri. Kwa nini? Kwa sababu unapojitahidi ‘kuzama’ kabisa katika kuwa msomaji, msemaji, na mwalimu mzuri utakuwa baraka kwa wale wanaokusikiliza. Jitahidi kujiwekea lengo la kujifunza na kutumia kila somo linalozungumziwa kwenye broshua Boresha Uwezo Wako wa Kusoma na Kufundisha. Jifunze somo moja baada ya lingine, fanya mazoezi kwa bidii nyumbani, na ujitahidi kutumia masomo hayo katika migawo unayopewa. Omba mapendekezo kutoka kwa mshauri msaidizi au wazee wengine “wanaofanya kazi kwa bidii katika kusema na kufundisha.” * (1 Tim. 5:17) Usikazie fikira tu kuelewa mbinu inayofafanuliwa, bali pia wasaidie wasikilizaji wako waimarishe imani yao au uwachochee watende kulingana na yale wanayojifunza. Kwa kufanya hivyo, utaongeza shangwe yako na yao pia.

18. Ki sekiwesa kutujangati kuhiki malengu gitu pakuusu uduma jukushamba?

18 Sisi sote tuna mgawo wa kufundisha na kufanya wanafunzi. (Mt. 28:19, 20; Rom. 10:14) Je, ungependa kuboresha ustadi wako katika kazi hii muhimu sana? Jiwekee malengo hususa unapojifunza na kutumia mambo unayosoma katika broshua Kufundisha. Unaweza kupata mapendekezo mengine kutoka kwenye Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha ya Kikristo na video za mapendekezo ya kuanzisha mazungumzo zinazoonyeshwa kwenye mikutano ya katikati ya juma. Jaribu mapendekezo mbalimbali ili kupata linalokufaa zaidi. Ukifuata mapendekezo hayo, kwa hakika utapata shangwe isiyoweza kulinganishwa na chochote ya kuwa mhudumu Mkristo mwenye ustadi.—2 Tim. 4:5.

19. Guwesa kustawisha bo sifa Ikikristo?

19 Unapofikiria kujiwekea malengo, usisahau mojawapo ya mambo muhimu zaidi, yaani, kusitawisha sifa za Kikristo. (Gal. 5:22, 23; Kol. 3:12; 2 Pet. 1:5-8) Unaweza kufanya nini ili kufikia lengo hilo? Kwa mfano, tuseme unataka kuimarisha imani yako. Huenda ukasoma makala mbalimbali katika machapisho yetu zilizo na mapendekezo ya jinsi ya kuimarisha imani yako. Bila shaka, utanufaika kwa kutazama video za JW Broadcasting® zinazoonyesha jinsi ambavyo akina ndugu na dada wameonyesha imani ya pekee walipokabiliana na majaribu mbalimbali. Kisha, fikiria njia ambazo unaweza kuiga imani yao katika maisha yako.

20. Tuwesa kujonzuke bo laha jitu nu kupungusa hisia jukutunyuka mwojo?

20 Bila shaka, sisi sote tunatamani tungeweza kufanya mengi zaidi kwa ajili ya Yehova kuliko tunavyofanya sasa. Katika ulimwengu mpya wa Mungu, tutaweza kumtumikia kikamili. Kwa sasa, tunapotumia vizuri fursa zozote tulizo nazo za kumtumikia Yehova, tunaweza kuongeza shangwe yetu na kupunguza hisia zozote za kuvunjika moyo. Jambo muhimu hata zaidi, tutamletea sifa na utukufu Yehova, ‘Mungu wetu mwenye furaha.’ (1 Tim. 1:11) Hivyo, acheni tupate shangwe katika mapendeleo tuliyo nayo!

NHAMBU 82 “Acheni Nuru Yenu Iangaze”

^ ekichweka 5 Tunampenda sana Yehova na tunataka kufanya yote tunayoweza katika utumishi wake. Tukiwa na hilo akilini, huenda tukachochewa kupanua huduma yetu au kujitahidi kustahili kufikia mapendeleo zaidi kutanikoni. Lakini vipi ikiwa licha ya jitihada zetu zote, hatuwezi kufikia baadhi ya malengo yetu? Tunaweza kuendeleaje kuwa na mengi ya kufanya katika utumishi wa Yehova na kudumisha shangwe yetu? Tunapata jibu katika mfano wa Yesu wa talanta.

^ ekichweka 2 Baadhi ya majina yamebadilishwa.

^ ekichweka 7 UFAFANUZI WA MANENO: Talanta moja ilikuwa inalingana na mshahara wa miaka 20 wa mfanyakazi wa kawaida.

^ ekichweka 15 Akina ndugu waliobatizwa wanatiwa moyo wajitahidi kustahili kuwa watumishi wa huduma na wazee. Ili upate habari zaidi kuhusu sifa za kustahili, tazama sura ya 5 na 6 ya kitabu Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova.

^ ekichweka 17 UFAFANUZI WA MANENO: Mshauri msaidizi ni mzee aliyepewa mgawo wa kuwapa shauri la faraghani ikihitajika, wazee na watumishi wa huduma kuhusiana na migawo yoyote ya ufundishaji wanayoshughulikia kutanikoni.

^ ekichweka 64 MAELEZO YA PICHA: Ili kufikia lengo lake la kuwa mwalimu mzuri zaidi, ndugu huyu anafanya utafiti kwenye machapisho yetu.

^ ekichweka 66 MAELEZO YA PICHA: Baada ya kujiwekea lengo la kufanya mahubiri yasiyo rasmi, dada yetu anampatia kadi ya mawasiliano mhudumu aliyemhudumia.

^ ekichweka 68 MAELEZO YA PICHA: Akichochewa na tamaa ya kuonyesha sifa za Kikristo, dada yetu anampatia mwabudu mwenzake zawadi ambayo hakuitarajia.