Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 33

Furahia Mambo Unaweza Kufanya Kwa Ajili ya Yehova

Furahia Mambo Unaweza Kufanya Kwa Ajili ya Yehova

“Ni muzuri zaidi kufurahia mambo yenye macho yanaona kuliko mutu kuhangaikia tamaa zake.”​—MUH. 6:9.

WIMBO 111 Mambo Yenye Kufanya Tukuwe na Furaha

KIFUPI YA HABARI *

1. Namna gani wengi wako wanajikaza kufanya mengi zaidi mu tumishi wa Yehova?

 TUKO na kazi mingi ya kufanya kadiri mwisho unakuwa karibu. (Mt. 24:14; Lu. 10:2; 1 Pe. 5:2) Siye wote tunapenda kumutumikia Yehova kabisa kadiri tunaweza. Wengi wako wanapanua utumishi wao. Wamoja wako na muradi wa kuwa mapainia. Wengine wako na muradi wa kutumika ku Beteli ao mu kazi ya ujenzi. Na ndugu wengine wengi wako wanajikaza ili kufikia kuwa watumishi wa huduma ao wazee. (1 Ti. 3:1, 8) Yehova anapaswa kufurahi sana wakati anaona roho ya vile kati ya watu wake!​—Zb. 110:3; Isa. 6:8.

2. Tunaweza kujisikia namna gani kama hatufikie miradi fulani ya kiroho?

2 Inawezekana kuvunjika moyo kama wakati unapita na hatuyafikia miradi ya kiroho yenye tulijiwekea. Ao juu ya miaka yetu ao hali zingine inaweza kuwa nguvu kupata madaraka fulani, na ile inaweza kutuvunja moyo. (Mez. 13:12) Njo hali yenye ilimufikia Melissa. * Angependa kutumikia ku Beteli ao kuenda kusoma Masomo ya Waeneza-Injili wa Ufalme, lakini anasema hivi: “Miaka yangu ilishapita. Kwangu miye sasa, ile mapendeleo yote ni ndoto tu. Wakati fulani, ile inanivunjaka moyo.”

3. Watu fulani wanaweza kufanya nini ili wastahili kupata madaraka fulani mu utumishi wa Yehova?

3 Pengine itaomba vijana fulani wenye kuwa na afya ya muzuri wakomalishe sifa fulani mbele ya kupata madaraka ingine. Ku ngambo moja, wanaweza kuwa na akili, wanajua namna ya kukamata maamuzi haraka na wako tayari kutumika; lakini ku ngambo ingine, wako na lazima ya kujifunza kujua namna ya kuwa wavumilivu zaidi, namna ya kufanya kazi kwa uangalifu zaidi, na namna ya kuheshimia wengine zaidi. Wakati unajikaza kuonyesha sifa zenye zinaombwa, ndugu wanaweza kukupatia madaraka bila hata weye kutazamia. Ona mufano wa Nick. Wakati alikuwa na miaka 20, alivunjika moyo sana juu alikuwa hayakuwa mutumishi wa huduma. Alisema: “Nilianza kuona saa kuko kitu fulani hakiendeke kwangu.” Lakini Nick hakuvunjika moyo. Alifanya yake yote yenye aliweza mu kutaniko na mu kazi ya kuhubiri. Leo, Nick iko mushiriki wa Halmashauri moja ya Tawi.

4. Tutazungumuzia nini mu hii habari?

4 Ulishavunjika moyo juu hauyafikia muradi fulani wa kiroho? Kama ni vile, umumwangie Yehova moyo wako. (Zb. 37:5-7) Tena, uliza ndugu fulani wenye kukomaa ili wakupatie mapendekezo yenye itakusaidia kufanya utumishi wenye unamutolea Yehova ukuwe muzuri zaidi, na ujikaze ili kutumikisha mashauri yao. Kama unafanya vile, unaweza kupata ile pendeleo ao kufikia muradi wako. Lakini sawa vile mufano wa Melissa ulionyesha, pengine haiwezekane kwa sasa kufikia miradi fulani ya kiroho. Ni muradi gani? Namna gani unaweza kuchunga furaha yako? Juu ya kujibia ile ulizo, hii habari itazungumuzia (1) fasi kwenye unaweza kupata furaha, (2) namna ya kuongeza furaha yako, na (3) aina ya miradi yenye unaweza kujiwekea ili kuendelea kuwa na furaha.

NI WAPI TUNAWEZA KUPATA FURAHA?

5. Juu tukuwe na furaha, tunapaswa kukazia akili yetu ku mambo gani? (Muhubiri 6:9)

5 Muhubiri 6:9 (Soma.) inaonyesha mambo yenye inaweza kutusaidia tupate furaha. Mutu mwenye anafurahia “mambo yenye macho yanaona” anapendaka mambo yenye iko nayo, kama vile hali yake ya sasa. Lakini mutu mwenye anahangaikia tamaa zake anaendeleaka kupenda mambo yenye hawezi kupata. Kwa hiyo, tunajifunza nini hapa? Juu tukuwe na furaha, tunapaswa kukazia akili yetu ku mambo yenye tuko nayo na mambo yenye tunaweza kuwa na uwezo wa kupata.

6. Tutazungumuzia mufano gani sasa, na ni mambo gani tutajifunza kupitia ile mufano?

6 Inawezekana kabisa kutosheka na mambo yenye tayari uko nayo? Watu wengi wanawaza kama haiwezekane, juu tunapendaka kujifunza namna ya kufanya mambo ingine ya mupya. Lakini, inawezekana. Tunaweza kabisa kufurahia mambo yenye tayari tuko nayo. Namna gani tunaweza kufanya vile? Juu tuweze kufanya vile, tuchunguze basi mufano wa Yesu wa talanta, wenye kupatikana mu Matayo 25:14-30. Tutajifunza kuhusu namna tunaweza kuwa na furaha na hata kukuwa na furaha zaidi mu hali yetu ya sasa.

NAMNA UNAWEZA KUONGEZA FURAHA YAKO

7. Fasiri kwa kifupi mufano wa Yesu kuhusu talanta.

7 Mu ile mufano, mwanaume mumoja alikuwa tayari kuenda mu safari. Mbele aende, aliita watumwa wake na alipatia kila mumoja wao talanta ili kufanya nayo biashara. * Juu ule mwanaume alijua kama watumwa wake walikuwa na uwezo tofauti, njo maana alipatia talanta tano mutumwa mumoja, talanta mbili mwingine, na wa tatu talanta moja. Wale watumwa mbili wa kwanza walifanya biashara na zile talanta na wakapata faida. Lakini ule mutumwa wa tatu hakufanya jambo yoyote na ile talanta yenye walimupatia, na bwana wake wa kazi akamufukuza.

8. Juu ya nini mutumwa wa kwanza katika mufano alipaswa kuwa na furaha?

8 Mutumwa wa kwanza alipaswa kufurahi sana juu bwana wake alimupatia talanta tano. Ile ilikuwa makuta mingi sana, na ilionyesha kama bwana wake alimutumainia sana! Lakini tuseme nini juu ya mutumwa wa pili? Pengine angevunjika moyo juu hakupata talanta mingi sawa vile ule mutumwa wa kwanza. Lakini alifanya nini?

Ni mambo gani tunaweza kujifunza kupitia mufano wa ule mutumwa wa pili mwenye Yesu alizungumuzia? (1) Alipokea talanta mbili kutoka kwa bwana wake. (2) Alitumika sana ili kupata makuta zaidi kwa ajili ya bwaa wake. (3) Alipata talanta mbili zingine (Ona fungu ya 9-11)

9. Ni mambo gani Yesu hakusema kuhusu mutumwa wa pili? (Matayo 25:22, 23)

9 Soma Matayo 25:22, 23. Yesu hakusema kama mutumwa wa pili alikasirika na kuweka kinyongo juu tu alipata talanta mbili. Na Yesu hakusema kama ule mutumwa alinungunika kwa kusema hivi: ‘Hii njo yote yenye miye napata? Juu ya nini? Niko pia na uwezo sawa ule mutumwa mwingine mwenye alipata talanta tano! Kama bwana wangu hapendezwe na miye, acha tu kumbe na miye nizike hizi talanta mbili na nifanye mambo yangu.’

10. Ule mutumwa wa pili alifanya nini na talanta zake?

10 Kama vile mutumwa wa kwanza, mutumwa wa pili alikamata kwa uzito daraka yenye alipewa na alimutumikia bwana wake kwa bidii sana. Ile ilifanya apate talanta zingine mbili. Bidii na ufundi ya ule mutumwa ilimuletea baraka kabisa. Bwana wake alipendezwa naye na alimuona kuwa mutu mwenye kutumainika na akamupatia madaraka mingi zaidi!

11. Namna gani tunaweza kuongeza furaha yetu?

11 Vilevile, tunaweza kuongeza furaha yetu kwa kujikaza kufanya mambo yote yenye wametupatia kufanya mu utumishi wa Yehova. ‘Uhangaikie sana’ kazi ya kuhubiri, na ujikaze kutumika sana pamoja na kutaniko. (Mdo. 18:5; Ebr. 10:24, 25) Ujitayarishe muzuri kwa ajili ya mikutano juu utoe maelezo yenye kutia moyo. Ukamate kwa uzito migao yote yenye uko nayo ku mukutano wa katikati ya juma. Kama unaombwa kusaidia mu kazi fulani mu kutaniko, ukuwe tayari kuifanya kwa wakati. Usiwaze kama kazi yenye unapewa haiko ya maana sana na kama haiko lazima upitishe wakati wako juu ya kuifanya. Ujikaze kukomalisha ufundi wako. (Mez. 22:29) Kadiri unajikaza kumutumikia Yehova, ni vile urafiki wako pamoja naye utaongezeka na ni vile utakuwa na furaha. (Gal. 6:4) Itakuwa pia mwepesi kwako kufurahi pamoja na wengine wakati wanapata madaraka yenye pengine ungependa kupata.​—Ro. 12:15; Gal. 5:26.

12. Ni mambo gani ilisaidia Melissa na Nick wakuwe na furaha zaidi?

12 Unakumbuka Melissa, dada mwenye alieleza hamu yenye alikuwa nayo ya kutumika ku Beteli ao ya kusoma Masomo ya Waeneza-Injili wa Ufalme? Hata kama haikuwezekana kwake kutimiza ile miradi, anasema hivi: “Nilijikaza sana mu kazi yangu ya upainia na kutumia njia mbalimbali ya kuhubiri. Ile iliniletea furaha mingi sana.” Na namna gani Nick alipambana na hali ya kuvunjika moyo wakati hakuwekwa kuwa mutumishi wa huduma? Anasema hivi: “Nilikazia akili mambo yenye ningeweza kufanya, kama vile kuhubiri na kutoa maelezo ku mikutano. Nilijaza pia fomu ya kutumikia ku Beteli na nilikubaliwa mwaka wenye kufuata.”

13. Ni matokeo gani utapata kama unajitolea mu mugao wenye uko nao kwa sasa? (Muhubiri 2:24)

13 Kama unajitoa sana mu mugao wenye uko nao kwa sasa, ile itafanya upate madaraka ingine mu wakati wenye kuja? Inawezekana, kama vile ilimufikia Nick. Lakini kama haupate, sawa vile Melissa, furaha yako itaendelea kuongezeka, na utatosheka juu ya mambo yenye unamufanyia Yehova. (Soma Muhubiri 2:24.) Zaidi ya ile, utakuwa na furaha ya kujua kama bidii yako inamupendeza Bwana wetu, Yesu Kristo.

MIRADI YENYE INAONGEZA FURAHA YETU

14. Ni mambo gani hatupaswe kusahau kuhusu miradi yetu ya kiroho?

14 Kama tuko tunajitoa mu migao yenye tuko nayo kwa sasa, ile inaonyesha kama hatupaswe kujikaza kufanya mengi zaidi? Hapana! Tunaweza na tupaswa kujitilia miradi ya kiroho yenye itatusaidia tukuwe wahubiri na walimu wazuri na kutegemeza pia ndugu na dada zetu. Tutafikia ile miradi wakati tunasaidia kwa hekima na kwa kiasi wengine kuliko kukaza akili juu yetu wenyewe.​—Mez. 11:2; Mdo. 20:35.

15. Ni miradi gani fulani yenye inaweza kuongeza ku furaha yako?

15 Ni miradi gani unaweza kujiwekea? Umuombe Yehova akusaidie ujue ni miradi gani unaweza kufikia. (Mez. 16:3; Yak. 1:5) Unaweza kufikia moja kati ya miradi  yenye ilitajwa mu fungu ya kwanza ya hii habari, ni kusema, kufikia kuwa painia musaidizi ao wa kawaida, kutumika ku Beteli, ao kusaidia mu kazi ya ujenzi? Ao pengine unaweza kujifunza luga ya mupya juu ya kuhubiri habari njema ao hata kuhubiri mu eneo ya kigeni. Unaweza kujifunza mengi zaidi kuhusu ile miradi kwa kusoma sura ya 10 ya kitabu Tengenezo Yenye Kufanya Mapenzi ya Yehova na kwa kuzungumuza na wazee wa kutaniko yenu. * Wakati unajikaza kufikia ile miradi, maendeleo yako itakuwa wazi na furaha yako itaongezeka.

16. Unaweza kufanya nini kama hauwezi kufikia muradi fulani kwa sasa?

16 Lakini, tusema nini kama hauwezi kufikia moja kati ya miradi yenye tumetoka kuona? Siri ni kutafuta muradi ingine yenye unaweza kufikia. Fikiria kwa mufano hii yenye tunataka kuona sasa.

Ni muradi gani unaweza kufikia? (Ona fungu ya 17) *

17. Kulingana na 1 Timoteo 4:13, 15, ndugu anaweza kufanya nini juu afikie kuwa mwalimu muzuri zaidi?

17 Soma 1Timoteo 4:13, 15. Kama uko ndugu mwenye alishabatizwa, pengine unaweza kujikaza kufikia kuwa musemaji muzuri na mwalimu muzuri. Juu ya nini? Ni juu ‘utazama’ katika kusoma, kusema, na kufundisha muzuri na ile itasaidia wale wenye wanakusikiliza. Ujitilie muradi wa kujifunza na kutumikisha kila somo ya broshua Fanya Bidii Katika Kusoma na Kufundisha. Ujifunze somo moja, kisha ufanye mazoezi ku nyumba, na upime kutumikisha mambo yenye umejifunza wakati unatoa hotuba. Omba mashauri kwa mushauri musaidizi ao kwa wazee wengine “wenye wanafanya kazi kwa bidii katika kusema na kufundisha.” * (1 Ti. 5:17) Kazia kwa uangalifu namna ya kutumikisha somo yenye kuwa mu ile broshua lakini pia namna ya kusaidia wasikilizaji wako watie nguvu imani yao ao uwachochee watumikishe mambo yenye wanajifunza. Wakati unafanya vile, utaongeza furaha yako na yao pia.

Ni muradi gani unaweza kufikia? (Ona fungu ya 18) *

18. Ni nini inaweza kutusaidia kufikia miradi yenye tulijiwekea kuhusu kazi ya kuhubiri?

18 Siye wote tuko na daraka ya kuhubiri na ya kufanya wanafunzi. (Mt. 28:19, 20; Ro. 10:14) Utafurahia kupata ufundi zaidi mu hii kazi ya maana? Ujiwekee miradi fulani yenye kuwa wazi wakati uko unajifunza na kutumikisha mambo yenye umepata mu broshua Kufundisha. Unaweza pia kupata mashauri ingine mu Buku la Mukutano​—Utumishi na Maisha ya Mukristo na mu video zenye kuonyesha namna ya kuanzisha mazungumuzo, zenye tunaonaka ku mukutano wa katikati ya juma. Tumia mawazo mbalimbali yenye utapata na uone ni ya wapi inaweza kufaa. Kwa kufuata ile mashauri mbalimbali, bila shaka utapata furaha kubwa sana ya kuwa muhubiri mwenye ufundi kabisa.​—2 Ti. 4:5.

Ni muradi gani unaweza kufikia? (Ona fungu ya 19) *

19. Namna gani unaweza kukomalisha sifa zenye zinamupendeza Mungu?

19 Haupaswe kusahau muradi moja wa maana sana kuliko miradi yote yenye unaweza kujiwekea, ni kusema, kukomalisha sifa zenye zinamupendeza Mungu. (Gal. 5:22, 23; Kol. 3:12; 2 Pe. 1:5-8) Namna gani unaweza kufikia ile muradi? Waza kwa mufano, unapenda kufanya imani yako ikuwe nguvu zaidi. Unaweza kusoma habari mbalimbali zenye kuwa katika vichapo vyetu, vyenye vinatoa mashauri ya muzuri kuhusu namna ya kutia nguvu imani yako. Bila shaka, utapata faida wakati unaangalia sehemu mbalimbali za JW Télédiffusion zenye zinafasiria namna ndugu na dada zetu walionyesha imani mu magumu mbalimbali. Kisha, unaweza kuona ni mu njia gani unaweza kuiga imani yao mu maisha yako.

20. Namna gani tunaweza kuongeza furaha yetu na kujisikia kuwa hatuvunjike moyo sana?

20 Bila shaka, siye wote tungependa kufanya mengi zaidi kwa ajili ya Yehova kuliko vile tunaweza kufanya sasa. Lakini mu dunia mupya, tutaweza kumutumikia Yehova kwa ukamili. Kwa sasa, tukijikaza kufanya yetu yote yenye tunaweza kufanya, tunaweza kuongeza furaha yetu na hatutajisikia sana kuwa wenye kuvunjika mouyo. Ya maana zaidi, tutaletea utukufu na sifa Yehova, “Mungu [wetu] mwenye furaha.” (1 Ti. 1:11) Muache basi kila mumoja wetu afurahie mambo anaweza kufanya kwa ajili ya Yehova!

WIMBO 82 “Muache Mwangaza Wenu Uangaze”

^ fu. 5 Tunamupenda Yehova sana, na tunapenda kufanya yote yenye tunaweza mu utumishi wake. Ile inaweza kutuchochea kupanua utumishi wetu ao kufanya yote yenye tunaweza ili kupata madaraka zaidi mu kutaniko. Lakini tuseme nini hata kama tunafanya yetu yote lakini hatufikie miradi fulani? Ni nini inaweza kutusaidia kuendelea kutumikia Yehova kwa bidii na kuchunga furaha yetu? Jibu tunaipata mu mufano wa talanta wenye Yesu alileta.

^ fu. 2 Majina fulani imebadilishwa.

^ fu. 7 MAFASIRIO YA MANENO FULANI: Talanta moja ililingana na mushahara wa miaka 20 hivi wa mufanyakazi wa kawaida.

^ fu. 15 Ndugu wenye walishabatizwa wanatiwa moyo kutimiza sifa zenye zinaombwa ili kuwa watumishi wa huduma ao wazee. Ili kupata maelezo zaidi kuhusu sifa zenye zinaombwa, ona sura ya 5 na ya 6 ya kitabu Tengenezo Yenye Kufanya Mapenzi ya Yehova.

^ fu. 17 MAFASIRIO YA MANENO FULANI: Mushauri musaidizi ni muzee mwenye amepewa mugao wa kupatia wazee na watumishi wa huduma mashauri fulani, kama ni lazima, kuhusiana na migao ya kufundisha ao kusoma katika kutaniko.

^ fu. 64 MAFASIRIO YA PICHA: Juu afikie kuwa mwalimu muzuri zaidi, ndugu moja iko anatafuta habari mu vichapo vyetu.

^ fu. 66 MAFASIRIO YA PICHA: Kisha kujiwekea muradi wa kuanza kuhubiri wakati wowote, dada moja anatolea mwanamuke fulani karte ya jw.org.

^ fu. 68 MAFASIRIO YA PICHA: Sifa zenye zinamupendeza Mungu zinachochea dada moja aletea mwenzake moja Shahidi zawadi bila hata ule mwenzake kutazamia.