Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 34

Namna Gani Unaweza ‘Kuonja’ Wema wa Yehova?

Namna Gani Unaweza ‘Kuonja’ Wema wa Yehova?

“Muonje na muone kwamba Yehova ni mwema; mwenye furaha ni mutu mwenye anamukimbilia.”​—ZAB. 34:8.

WIMBO 117 Tukomalishe Sifa ya Wema

KIFUPI YA HABARI *

1-2. Kulingana na Zaburi 34:8, namna gani tunaweza kujifunza juu ya wema wa Yehova?

WAZIA wanakupatia chakula fulani, lakini hauyaikulaka hata siku moja. Ungependa kujua namna iko pengine kwa kuiona, kwa kusikia harufu, ao kwa kutaka kujua wanachangaka nini juu ya kuipika, ao unaweza kuuliza wengine kama wanaipendaka. Lakini, njia moja ya kujua kabisa kama utaipenda ni wakati unaionja weye peke.

2 Tunaweza kujifunza mambo fulani juu ya wema wa Yehova wakati tunasoma Biblia na vichapo vyetu, na wakati tunasikia wengine wanatufasiria namna Yehova aliwabariki. Lakini, tutaelewa muzuri kama Yehova ni mwema wakati siye wenyewe ‘tunaonja’ wema wake. (Soma Zaburi 34:8.) Tuone njia moja yenye tunaweza kufanya vile. Kwa mufano, tunapenda kuwa mu utumishi wa wakati wote, tunapaswa kufanya maisha yetu ikuwe mwepesi. Pengine tulishakasoma mara mingi ahadi ya Yesu yenye kuonyesha kama ikiwa tunatia faida za Ufalme pa nafasi ya kwanza, Yehova atatupatia mambo ingine yenye tuko nayo lazima kabisa, lakini pengine hatuyajioneakana siye wenyewe utimizo wa ile ahadi. (Mt. 6:33) Hata vile, juu tuko na imani katika ahadi ya Yesu, tunapunguza garama zetu, tunabadilisha kidogo programu yetu ya kazi ya kimwili, na tunakaza akili yetu juu ya utumishi. Wakati tunafanya vile, tutaona kabisa kama Yehova anahangaikia mahitaji yetu. ‘Tunaonja’ siye wenyewe wema wa Yehova.

3. Kulingana na Zaburi 16:1, 2, ni wa nani njo Yehova anaonyesha wema wake?

3 Yehova ni “mwema kwa wote,” hata kwa wale wenye hawamujue. (Zb. 145:9; Mt. 5:45) Lakini, ni mwema zaidi sana kwa wale wenye wanamupenda na kumutumikia kwa moyo wao wote. (Soma Zaburi 16:1, 2.) Tuone njia fulani zenye Yehova anatuonyesha wema wake, njia zenye zinatuletea faida.

4. Namna gani Yehova anaonyesha wema wake wale wenye wanaanza kuwa marafiki wake?

4 Kila wakati tunatumikisha mambo yenye tunajifunza kutoka kwa Yehova, tutaona matokeo ya muzuri mu maisha yetu. Kwa mufano, wakati tulijifunza kumuhusu na kuanza kumupenda, alitusaidia tuachane na mawazo na matendo yenye inamuchukiza. (Kol. 1:21) Na wakati tulitoa maisha yetu kwa Yehova na kubatizwa, tulijionea wema wake hata zaidi juu alitupatia zamiri safi na pendeleo ya kuwa marafiki wake.​—1 Pe. 3:21.

5. Namna gani tunajionea wema wa Yehova mu mahubiri?

5 Tunaendelea kuona wema wa Yehova mu kazi ya kuhubiri. Unakuwaka mutu wa haya? Wengi kati ya Mashahidi wa Yehova wanakuwaka vile. Pengine mbele ukuwe Shahidi wa Yehova, haukuwaziaka hata siku moja kupiga hodi ku mulango ya mutu mwenye haujue na kuzungumuza naye juu ya Biblia. Lakini, leo, ilishakuwa kawaida yako kufanya vile. Zaidi ya ile, kwa musaada wa Yehova, umependa kazi ya kuhubiri! Umejionea musaada wa Yehova mu njia mbalimbali. Alikusaidia uendelee kuwa mutulivu wakati ulikutana na mupinzani mu mahubiri. Alikusaidia pia ukumbuke andiko yenye kufaa ili kuzungumuza na mutu mwenye kupendezwa. Tena, alikupatia nguvu ya kuendelea kuhubiri hata wakati ulikutana na watu wenye hawapendezwe.​—Yer. 20:7-9.

6. Namna gani mazoezi yenye Yehova anatutolea inaonyesha wema wake?

6 Yehova ametuonyesha tena wema wake wakati anatuzoeza kwa ajili ya mahubiri. (Yoh. 6:45) Ku mikutano yetu ya katikati ya juma, tunasikiliza maonyesho mbalimbali na tunatiwa moyo kuitumia mu mahubiri. Ku mwanzo, inaweza kuwa nguvu kidogo kutumia njia ya mupya ya kuhubiri, lakini wakati tunafanya vile, tunaweza kuona matokeo ya muzuri ya kutumia ile njia ya mupya mu eneo yetu. Tunatiwa pia moyo ku mikutano na ku mikusanyiko yetu ya eneo kutumia njia mbalimbali za kuhubiri zenye pengine tulikuwaka hatuyatumiaka. Ile pia, inaweza kutuletea wasiwasi, lakini wakati tunajaribu kufanya vile, Yehova atatubariki. Tuzungumuzie basi baraka fulani zenye tunaweza kupata wakati tunatumia njia mbalimbali za mupya ili kumupatia Yehova yetu yote, ijapokuwa hali zetu. Kisha, tutazungumuzia namna tunaweza kupanua utumishi wetu.

YEHOVA ANABARIKI WALE WENYE WANAMUTEGEMEA

7. Ni baraka gani tunapata wakati tunajikaza kupanua utumishi wetu?

7Tunamukaribia Yehova hata zaidi. Fikiria mufano wa muzee mumoja mwenye anaitwa Samuel, * mwenye iko anatumikia katika inchi ya Colombie pamoja na bibi yake. Huyu ndugu na bibi yake walifurahia kazi ya upainia mu kutaniko yao, lakini walipenda kupanua utumishi wao kwa kusaidia kutaniko ingine yenye ilikuwa na lazima kubwa. Juu ya kufikia ile muradi, walipaswa kuacha mambo fulani yenye walikuwa wanapenda. Samuel anasema hivi: “Tulitumikisha andiko ya Matayo 6:33 na tuliacha kuuza vitu vyenye hatukukuwa navyo lazima. Lakini jambo yenye ilikuwa nguvu sana ni kuacha nyumba yetu. Ilijengwa vile tulikuwa tulishapenda, na hatukujikopeshaka makuta juu ya kuijengesha.” Wakati walihamia mu kutaniko ya mupya, walikuwa na lazima ya makuta kidogo tu ili kuishi kuliko vile ilikuwa zamani. Samuel anasema tena hivi: “Tumeona namna gani Yehova iko anaongoza kila hatua yetu na namna iko anajibia sala zetu. Tunajua Yehova anafurahi sana na tunaona kama anatupenda mu njia yenye hatuyaonaka.” Je, na weye unaweza kupanua utumishi wako mu njia fulani? Kama ni vile, ukuwe hakika kama utamukaribia Yehova zaidi na yeye atakuhangakia.​—Zb. 18:25.

8. Maelezo ya Ivan na Viktoria inakufundisha nini?

8Tunapata furaha mu utumishi wetu. Ona maelezo ya Ivan na bibi yake Viktoria, wenye ni mapainia katika inchi ya Kirghizstan. Walijikaza juu maisha yao ikuwe mwepesi ili wajitolee mu mugao wowote, kutia ndani kazi ya ujenzi. Ivan anasema hivi: “Tulijitoa kabisa mu kila mugao, hata kama ku mwisho wa siku tulikuwa tulishachoka sana, tulikuwa na amani ya moyo na wenye kutosheka, sababu tulikuwa tumetumia nguvu yetu kwa ajili ya kazi ya Ufalme. Tena, tulipata furaha kubwa sana sababu tulipata marafiki wengi, na kuko mambo mingi ya muzuri yenye tulionaka yenye hatuwezi kusahau.”​—Mk. 10:29, 30.

9. Dada moja mwenye kuwa na magumu amefanya nini ili kupanua utumishi wake, na ile imekuwa na matokeo gani?

9 Tunapata furaha mu utumishi wa Yehova hata kama tuko na magumu. Kwa mufano, Mirreh, dada mujane wa Afrika ya mangaribi, mwenye alishazeeka, alikuwaka doktere. Lakini wakati alieneza miaka ya kuacha kutumika, aliacha ile kazi na akakuwa painia. Mirreh iko na magonjwa ya mubaya sana yenye inafanya ikuwe nguvu kwake kutembea muzuri, na kwa hiyo, iko na uwezo wa kupitisha tu saa moja mu mahubiri ya nyumba kwa nyumba. Lakini anaweza kupitisha saa mingi mu mahubiri ya mahali pa watu wengi. Iko na marudio mingi na mafunzo mingi ya Biblia. Anazungumuzaka na wamoja kati yao ku telefone. Ni nini ilimuchochea Mirreh ajitoe zaidi mu kazi ya Yehova? Yeye peke anasema hivi: “Moyo wangu unajaa upendo kwa ajili ya Yehova na Kristo Yesu. Na mara mingi namuomba Yehova anisaidie nifanye yote yenye ninaweza mu utumishi wake.”​—Mt. 22:36, 37.

10. Kulingana na 1 Petro 5:10, wale wenye wanajitoa zaidi mu kazi ya Yehova wanapata nini kutoka kwake?

10Tunapata mazoezi ingine kutoka kwa Yehova. Kenny, painia mumoja mwenye kutumikia mu Maurice, aliona ile kuwa kweli. Wakati alijifunza kweli, aliacha université, akabatizwa, na akaanza utumishi wa wakati wote. Anasema hivi: “Nilijikaza kabisa kuishi kulingana na maneno ya nabii Isaya, mwenye alisema: ‘Mimi huyu! Unitume mimi!’” (Isa. 6:8) Kenny alitumika mu kazi mingi za ujenzi, na alisaidia pia kutafsiri vichapo vyetu mu luga yake ya kizalikio. Kenny anasema hivi: “Nilipata mazoezi yenye ilinisaidia nikuwe na ufundi wenye nilikuwa nao lazima ili kutimiza migao yangu.” Lakini alijifunza mambo mingi zaidi ya kujua namna ya kufanya ile kazi. Anaongezea hivi: “Nilijifunza pia mambo ya nguvu yenye singeweza kufanya, na nilijifunza pia kuhusu sifa zenye nilipaswa kukomalisha juu nifikie kuwa mutumishi muzuri zaidi wa Yehova.” (Soma 1 Petro 5:10.) Pengine na weye unaweza kufanya mabadiliko juu uone namna Yehova anaweza kukuzoeza mu njia mingi zaidi, hauone vile?

Wanahubiri mu eneo yenye kuwa na lazima kubwa sana ya wahubiri wa Ufalme; dada moja kijana iko anasaidia mu kazi ya kujenga Jumba la Ufalme; bwana fulani na bibi yake wenye walishazeeka wako wanahubiri kupitia telefone. Wote wanapata furaha sana mu utumishi wao (Ona fungu ya 11)

11. Ni mambo gani yenye dada fulani wa Korea ya Kusini walifanya ili kuhubiri, na ile ilikuwa na matokeo gani? (Ona picha kwenye jalada.)

11 Hata watu wenye wamekuwa Mashahidi na imepita miaka mingi, wako pia na lazima ya mazoezi wakati wanajiingiza mu aina ingine ya utumishi. Wakati wa Coronavirus, wazee wa kutaniko fulani yenye kuwa mu inchi ya Korea ya Kusini, waliandika hivi: “Ndugu na dada fulani wenye, ku mwanzo, waliwaza kama hawangeweza kuhubiri juu ya afya yao, kwa sasa wanafanya vile kupitia vidéoconférence. Dada watatu wenye kuwa na miaka 80 hivi walijifunza teknolojia ya sasa na walianza kuhubiri karibu kila siku.” (Zb. 92:14, 15) Ungependa kupanua utumishi wako na kuonja wema wa Yehova hata zaidi? Fikiria mambo fulani yenye unaweza kufanya ili kufikia ile muradi.

NAMNA UNAWEZA KUJITOA ZAIDI MU KAZI YA YEHOVA

12. Yehova anaahidi nini wale wenye wanamutegemea?

12Ujifunze kumutegemea Yehova. Anaahidi kutumwangia baraka wakati tunamutegemea na wakati tunamutolea yetu yote. (Mal. 3:10) Dada Fabiola, mwenye anaishi Colombie, aliona namna Yehova alimutimizia ile ahadi. Alipenda kuwa painia wa kawaida kisha kubatizwa. Lakini alipaswa kutumika sana ili kutegemeza bwana yake na watoto wao watatu. Wakati alieneza miaka ya kuacha kazi, alisali sana kwa Yehova ili amusaidie. Anasema hivi: “Kwa kawaida, watu wanachungaka masiku mingi sana mbele waanze kupata makuta yenye wanapatiaka mutu mwenye anaacha kazi juu ya uzee, lakini miye nilianza kupokea ile makuta kisha mwezi moja tu. Ilikuwa sawa vile muujiza!” Kisha miezi mbili alikuwa painia. Kwa sasa iko na miaka 70 hivi na amekuwa painia kwa zaidi ya miaka 20. Mu ile kipindi, alisaidia watu munane mupaka kubatizwa. Anasema hivi: “Hata kama wakati fulani najisikia kuwa muzaifu, Yehova ananisaidia kila siku niendelee na kazi yangu ya upainia.”

Namna gani Abrahamu na Sara, Yakobo, na makuhani wenye walivuka Muto Yordani walionyesha kama walimutegemea Yehova? (Ona fungu ya 13)

13-14. Ni mifano gani inaweza kutusaidia tumutegemee Yehova na tujitoe zaidi mu kazi yake?

13Ujifunze kupitia mifano ya wale wenye walimutegemea Yehova. Biblia iko na mifano mingi ya watu wenye walijitoa sana mu utumishi wa Yehova. Mu mifano mingi, wale watumishi wa Yehova walipaswa kufanya jambo fulani mbele wapate baraka za pekee kutoka kwake. Kwa mufano, ni kisha tu Abrahamu kuacha nyumba yake​—“hata kama hakujua mahali alikuwa anaenda”​—njo Yehova alimubariki. (Ebr. 11:8) Na ni kisha tu Yakobo kupigana na malaika njo alipata baraka ya pekee sana. (Mwa. 32:24-30) Wakati Waisraeli walikuwa karibu kuingia katika Inchi ya Ahadi, siku moja wakafika ku Muto Yordani. Lakini, waliweza kuvuka ile Muto Yordani yenye kujaa sana maji kisha tu makuhani kuingiza miguu yao katika ile muto.​—Yos. 3:14-16.

14 Unaweza pia kujifunza kupitia mifano ya Mashahidi wa wakati wetu wenye wanamutegemea Yehova na wenye wamejitoa ili kufanya mambo mengi zaidi katika kazi yake. Kwa mufano, ndugu Payton na bibi yake, Diana, walifurahia kusoma habari kuhusu ndugu na dada wenye walipanua utumishi wao, sawa vile wale wenye kuzungumuziwa mu sehemu “Walijitoa kwa Kujipendea.” * Payton anasema hivi: “Wakati tulisoma zile habari, tulijisikia sawa vile tulikuwa tunaona mutu fulani mwenye alikuwa anakula chakula ya butamu sana. Kadiri tuliendelea kuangalia, ni vile tulipenda ‘kuonja na kuona kama Yehova ni mwema.’” Ku mwisho, Payton na Diana wakahamia fasi kwenye kulikuwa lazima kubwa ya wahubiri. Ulishakasoma zile habari? Na ulishakaangalia video Wanahubiri Katika Eneo la Mbali​—Australia na Kuhubiri Katika Eneo la Mbali​—Ireland zenye kuwa ku jw.org? Ile yote inaweza kukusaidia kujua njia mbalimbali zenye unaweza kutumia juu ya kupanua utumishi wako.

15. Namna gani marafiki wazuri wanaweza kutusaidia?

15Chagula marafiki wazuri. Inakuwaka mwepesi kukula chakula yenye hatuyakulaka pamoja na watu wenye wanaizoea. Vilevile, kama tunapitisha wakati pamoja na wale wenye wanatia Yehova pa nafasi ya kwanza mu maisha yao, ile pia inaweza kutuchochea kutafuta njia mbalimbali za kupanua utumishi wetu. Ndugu Kent na bibi yake Veronica waliona ile kuwa kweli. Kent anasema hivi: “Marafiki wetu na familia yetu walitutia moyo tujaribu aina ingine ya utumishi. Tulitambua kama, wakati tunakuwa marafiki pamoja na wale wenye wanatanguliza faida za Ufalme pa nafasi ya kwanza, ile inatuchochea na siye kujaribu kufanya jambo fulani ya mupya.” Kwa sasa, Kent na Veronica wako mapainia wa pekee mu inchi ya Serbia.

16. Kama vile mufano wa Yesu wenye kuwa mu Luka 12:16-21 unaonyesha, juu ya nini tunapaswa kuwa tayari kuacha mambo fulani ili kufanya kazi ya Yehova?

16Ukuwe tayari kuacha mambo fulani ili kufanya kazi ya Yehova. Hatulazimike kuacha kila kitu juu tu ya kumufurahisha Yehova. (Muh. 5:19, 20) Lakini, kama hatupende kufanya mengi zaidi mu kazi ya Yehova juu tu hatupende kuacha mambo fulani yenye tunapendaka, tunaweza kufanya kosa sawa ya mutu mwenye Yesu alizungumuzia mu mufano wake. Ule mutu alitumika sana juu apate vitu mingi vya muzuri bila kuhangaikia mambo ya Mungu. (Soma Luka 12:16-21.) Ndugu Christian, mwenye anaishi mu inchi ya Ufaransa, anasema hivi: “Sikukuwa namupatia Yehova nguvu na wakati wangu. Ilikuwa pia vile kwa familia yangu.” Yeye na bibi yake waliamua kufanya kazi ya upainia. Lakini juu wafikie ile muradi, walipaswa kuacha kazi zao. Ili kupata makuta kidogo ya kuwasaidia kuishi, walianza kufanya kazi ya kusafisha nyumba ao biro, na walijifunza namna ya kutosheka na kidogo yenye walikuwa wanapata. Kufanya vile, kuliwaletea baraka gani? Christian anasema hivi: “Sasa tunafurahia kazi ya mahubiri na kuona vile mafunzo yetu ya Biblia na pia marudio yetu wako wanajifunza juu ya Yehova.”

17. Ni nini inaweza kutuzuia kujaribu kufanya jambo fulani ya mupya mu utumishi wetu?

17Ukuwe tayari kujaribu aina mupya za utumishi. (Mdo. 17:16, 17; 20:20, 21) Dada Shirley, mwenye ni painia mu inchi ya Amerika, alipaswa kufanya mabadiliko fulani mu kipindi ya Coronavirus. Ku mwanzo, alikuwa na mashaka kidogo kuhusu kuanza kuhubiri kupitia telefone. Lakini, wakati alipata mazoezi saa yenye mwangalizi wa muzunguko alitembelea kutaniko yao, akaanza kuhubiri kwa ukawaida kupitia telefone. Anasema hivi: “Ku mwanzo, niliogopa, lakini sasa nafurahia kuhubiri kupitia telefone. Tuko tunahubiria watu wengi zaidi leo kuliko vile tulikuwa tunafanya kupitia mahubiri ya nyumba kwa nyumba!”

18. Nini inaweza kutusaidia kupambana na magumu wakati tuko tunajaribu kupanua utumishi wetu?

18Ujiwekee muradi na ujikaze kuifikia. Wakati tuko na magumu, tunasali ili kupata musaada na kufikiri sana kuhusu namna tunaweza kupambana nayo. (Mez. 3:21) Sonia, mwenye ni painia wa kawaida mu kikundi fulani ya luga ya Kiromani mu Ulaya, anasema hivi: “Napendaka kuandika miradi yangu ku karatasi na kuiweka fasi kwenye naweza kuiona mbiombio. Ku meza yangu, kuko muchoro wenye kuonyesha barabara mbili zenye kupeleka fasi mbili tofauti. Wakati inaomba nikamate uamuzi fulani, naangalia zile barabara mbili na kuona kama ile uamuzi itanisaidia kufikia muradi wangu ao hapana.” Sonia anajikazaka kuwa na mawazo ya muzuri juu ya magumu yenye anapambana nayo. Anasema tena hivi: “Kila hali ya mupya inaweza kuwa sawa vile ukuta wenye kunizuia ao sawa vile kilalo yenye kunisaidia​—inategemea tu namna miye niko naona ile hali.”

19. Tunapaswa kuazimia kufanya nini?

19 Yehova iko anatubariki mu njia mbalimbali. Tunaonyesha kama tunasamini zile baraka kwa kufanya yetu yote ili kumuletea sifa. (Ebr. 13:15) Kwa mufano, tunaweza kufanya vile kwa kutafuta njia za mupya ili kupanua utumishi wetu, na ile itafanya Yehova atubariki hata zaidi. Tuazimie basi kila siku kutafuta njia za mupya ili ‘kuonja na kuona kama Yehova ni mwema.’ Kisha tutakuwa kama Yesu, mwenye alisemaka: “Chakula changu ni kufanya mapenzi ya ule mwenye alinituma na kumaliza kazi yake.”​—Yoh. 4:34.

WIMBO 80 Uonje na Uone Vile Yehova Ni Mwema

^ fu. 5 Yehova njo Chanzo cha wema. Anapatia kila mutu mambo ya muzuri, hata watu wabaya. Lakini, anapenda zaidi sana kufanyia waabudu wake waaminifu mambo ya muzuri. Mu hii habari, tutaona namna Yehova anaonyesha watumishi wake wema wake. Tena, tutaona namna wale wenye wanapanua utumishi wao wanajionea wema wa Yehova mu njia ya pekee kabisa.

^ fu. 7 Majina fulani imebadilishwa.

^ fu. 14 Zile habari zilikuwaka zinatolewa mu Munara wa Mulinzi, lakini sasa zinatolewa ku jw.org. Fungua sehemu HABARI JUU YETU > USHUHUDA WA MASHAHIDI WA YEHOVA > KUFIKIA MIRADI YA KIROHO.