Amila mo ibi abali

Amila mu gagabi

MAKALA JA LIFUNZU 35

Athaminia Akandugu na Dada Bitu Aaminifu Baabi na Umuli Nkolongu

Athaminia Akandugu na Dada Bitu Aaminifu Baabi na Umuli Nkolongu

“Ulia ndo litaji lu umalidadi.”​—MET. 16:31.

NHAMBU 138 Kichwa Chenye Mvi​—Taji la Uzuri

MUHTASARI *

1-2. (a) Kulengana na Methali 16:31, tupaswa kwabona bo, akandugu na dada bitu aaminifu baabi na umuli nkolongo? (b) Musitujibwa maswali bo, mu makala jenzeno?

HUENDA wageni wanaotembelea eneo la hifadhi katika jimbo la Arkansas, Marekani, wakaokota almasi zinazoonekana waziwazi ardhini. Hata hivyo, almasi hizo hazijakatwa, ziko katika muundo wake wa asili. Kwa sababu hiyo, huenda watu wengi wasitambue kwamba ni almasi, na hivyo kuzipita hazina hizo.

2 Kwa njia fulani, ndugu na dada zetu waaminifu wenye umri mkubwa ni kama almasi hizo; wao ni hazina zenye thamani. Neno la Mungu linazifananisha mvi zao na taji. (Soma Methali 16:31; 20:29) Hata hivyo, huenda tukakosa kuwakazia uangalifu ndugu na dada hao walio kama hazina. Vijana wanaotambua thamani ya wale wenye umri mkubwa, wanaweza kupata kitu chenye manufaa kuliko utajiri. Katika makala hii, tutajibu maswali matatu: Kwa nini Yehova anawaona ndugu na dada zetu wenye umri mkubwa kuwa hazina? Yehova amewapatia sehemu gani muhimu katika tengenezo lake? Tunaweza kufanya nini ili kunufaika kikamili kutokana na mfano wao?

NDABA JAKI YEHOVA JWABONA BAABI NA UMULI NKOLONGU KUBA AZINA?

3. Kulengana na Zaburi 92:12-15, ndaba jaki akandugu na dada bitu aaminifu bana umuli nkolongu abi na thamani kuka Yehova?

3 Ndugu na dada waaminifu wenye umri mkubwa ni wenye thamani machoni pa Yehova Mungu. Anawaona jinsi walivyo kikweli moyoni, anajua na kuthamini sifa zao za pekee. Yehova anathamini wenye umri mkubwa wanaposhiriki na vijana hekima ambayo wamejipatia kwa kumtumikia kwa uaminifu kwa miaka mingi. (Ayu. 12:12; Met. 1:1-4) Yehova pia anathamini uvumilivu wao. (Mal. 3:16) Walikabili matatizo mbalimbali maishani; hata hivyo imani yao katika Yehova haikuyumbishwa kamwe. Tumaini lao la wakati ujao ni jangavu zaidi kuliko walipojifunza kweli kwa mara ya kwanza. Na Yehova anawapenda kwa sababu wanaendelea kulitangaza jina lake “hata wakati wa uzeeni.”—Soma Zaburi 92:12-15.

4. Gabi mambu bo gagawesa kwafaliji akandugu na dada bitu baabi na umuli nkolongo?

4 Ikiwa umri wako umesonga, uwe na hakika kwamba Yehova anakumbuka kazi uliyofanya katika miaka iliyopita. (Ebr. 6:10) Kwa bidii, umetegemeza kazi ya kuhubiri, na hilo linamfurahisha Baba yetu wa mbinguni. Umevumilia majaribu—hata yenye kuvunja moyo sana—umetetea viwango vya uadilifu vya Biblia, umebeba majukumu mazito, na kuwazoeza wengine. Umefanya yote unayoweza ili kwenda sambamba na tengenezo la Yehova linalosonga kwa kasi sana. Umewategemeza na kuwatia moyo wengine walio katika utumishi wa wakati wote. Yehova anakupenda sana kwa kuwa wewe ni mshikamanifu. Anaahidi kwamba “hatawaacha washikamanifu wake”! (Zab. 37:28) Anakuhakikishia hivi: “Hata kichwa chako kikiwa na mvi nitaendelea kukubeba.” (Isa. 46:4) Hivyo, usifikie mkataa kwamba kwa sababu umri wako umesonga, hakuna unachotimiza katika tengenezo la Yehova. Bila shaka, unatimiza sehemu muhimu!

MUNGU JWAPEKI BAABI NA UMULI NKOLONGU SEHEMU MUHIMU MULITENGENEZU LAKI

5. Baabi na umuli nkolongu bala apaswa kukomboka lijambu bole?

5 Ndugu na dada wenye umri mkubwa wana mengi ya kushiriki pamoja na wengine. Ingawa huenda hawana nguvu walizokuwa nazo zamani, wana uzoefu mwingi ambao wamejipatia kwa miaka mingi. Yehova anaweza kuendelea kuwatumia katika njia mbalimbali, kama tutakavyoona kwenye mifano ifuatayo ya wakati uliopita na ya sasa.

6-7. Boa mifanu ja bandu baabi na umuli nkolongu babalogo Mmbibilia ambabu babalikiwa kwa ndaba jutumishi gwabu nkamulani.

6 Katika Biblia tunaweza kupata mifano mizuri ya watu waaminifu ambao walimtumikia Yehova kwa bidii umri wao ulipokuwa umesonga. Kwa mfano, Musa alikuwa na umri wa miaka 80 alipoanza kutumikia akiwa nabii wa Yehova na mwakilishi wa taifa la Israeli. Inaelekea Yehova bado alikuwa akimtumia Danieli akiwa msemaji Wake, nabii huyo alipokuwa na umri wa zaidi ya miaka 90. Na inaelekea mtume Yohana alikuwa na umri wa zaidi ya miaka 90 alipoongozwa na roho ya Mungu kuandika kitabu cha Ufunuo.

7 Watu wengine wengi waaminifu hawakuwa maarufu au hawakujulikana sana, na huenda wangeweza kupuuzwa kirahisi na watu. Hata hivyo, Yehova aliwaona na kuwathawabisha kwa ushikamanifu wao. Kwa mfano, mwanamume ‘mwadilifu na aliyemwogopa Mungu’ Simeoni, anatajwa kwa kifupi sana katika Biblia, lakini Yehova alimjua na kumpa pendeleo la kumwona mtoto Yesu na kutoa unabii kuhusu mtoto huyo na mama yake. (Luka 2:22, 25-35) Mfikirie pia Ana aliyekuwa nabii wa kike na mjane. Alikuwa na umri wa miaka 84, lakini “hakukosa kamwe hekaluni.” Yehova alimbariki kwa sababu alienda hekaluni kwa ukawaida, naye alimruhusu amwone mtoto Yesu. Simeoni na Ana walikuwa wenye thamani machoni pa Yehova.​—Luka 2:36-38.

8-9. Akadada ajani aendale kuba nunsangu bo, mulitengenezu lika Yehova?

8 Katika nyakati zetu, ndugu na dada wengi waaminifu wenye umri mkubwa wanawawekea mfano bora vijana. Fikiria mfano wa Dada Lois Didur. Alikuwa na umri wa miaka 21 alipoanza kutumikia akiwa painia wa pekee nchini Kanada. Baadaye, yeye na John, mume wake, walitumikia katika kazi ya kuzungukia makutaniko kwa miaka mingi. Kisha, walitumikia katika Betheli ya Kanada kwa zaidi ya miaka 20. Lois alipokuwa na umri wa miaka 58, walialikwa wakatumikie nchini Ukrainia. Wangefanyaje? Je, wangefikia mkataa kwamba umri wao ulikuwa umesonga sana hivi kwamba hawawezi kwenda kutumikia katika nchi nyingine? Walikubali mgawo huo, na John aliwekwa rasmi kutumikia akiwa mshiriki wa Halmashauri ya Tawi huko. Miaka saba baadaye, John alipokufa, Lois aliamua kubaki katika mgawo wake. Sasa, akiwa na umri wa miaka 81, Lois bado anaendelea kutumikia kwa bidii na anapendwa sana na familia ya Betheli ya Ukrainia.

9 Akina dada wajane kama Lois, huenda wasikaziwe sana uangalifu kama ilivyokuwa wakati waume zao walipokuwa hai; hata hivyo kuwa wajane hakupunguzi thamani yao. Yehova anawathamini sana akina dada waliowaunga mkono waume zao kwa miaka mingi na ambao sasa wanaendelea kuonyesha bidii ileile. (1 Tim. 5:3) Pia, wanawatia moyo sana vijana.

10. Tony jutubeki mfanu bo bola?

10 Ndugu na dada wengi wenye umri mkubwa wanaoishi kwenye nyumba za kuwatunza wazee-wazee ni hazina za kiroho pia. Kwa mfano, ndugu anayeitwa Tony kwa sasa anaishi katika nyumba hizo. Alibatizwa katika jimbo la Pennsylvania, Marekani, Agosti 1942, akiwa na umri wa 20. Muda mfupi baada ya kubatizwa, alifungwa gerezani kwa miaka miwili na nusu kwa sababu ya suala la kutounga mkono upande wowote. Yeye pamoja na Hilda, mke wake, waliwalea watoto wao wawili katika kweli. Katika miaka iliyopita, Tony alitumikia katika makutaniko matatu akiwa mwangalizi msimamizi (sasa mratibu wa baraza la wazee) na pia alitumikia akiwa mwangalizi wa kusanyiko la mzunguko. Aliongoza mikutano na mafunzo ya Biblia kwenye gereza la jimbo. Sasa, Tony ana umri wa miaka 98, lakini hayuko tayari kupunguza bidii yake ya kumtumikia Yehova. Anaendelea kufanya yote anayoweza ili kumtumikia Yehova, na anafanya kazi kwa ukaribu na kutaniko lake!

11. Tuwesa kulangi bo, kwamba twathamini baatama munyumba yakwatunza azee-azee?

11 Tunaweza kuonyeshaje kwamba tunawaheshimu ndugu na dada zetu wenye umri mkubwa wanaoishi kwenye nyumba za kuwatunza wazee-wazee? Wazee wa kutaniko wanaweza kuwahusisha katika utendaji wa kutaniko kadiri inavyowezekana. Tunaweza kuwaonyesha upendezi wa kibinafsi kwa kuwatembelea au kuzungumza nao kupitia video. Tunataka kuwaonyesha upendezi wa pekee ndugu na dada zetu wenye umri mkubwa ambao huenda wanaishi kwenye nyumba za kuwatunza wazee-wazee ambazo ziko mbali na kutaniko lao la nyumbani. Tunahitaji kuwa makini, ili tusiwasahau ndugu na dada hao. Huenda isiwe rahisi kwa baadhi yao kuzungumzia mambo waliyofanya maishani, au huenda wakafikiri kwamba si jambo linalofaa. Lakini tutanufaika sana ikiwa tutatumia muda kuwauliza maswali na kuwasikiliza wanapotueleza kuhusu mambo waliyofurahia katika tengenezo la Yehova.

12. Tuwesa kupata ki mulikutaniku litu twabete?

12 Huenda tukashangazwa kujua kwamba tuna mifano ya pekee ya ndugu na dada waaminifu wenye umri mkubwa katika kutaniko letu wenyewe. Dada anayeitwa Harriette alimtumikia Yehova kwa uaminifu kwa miaka mingi katika kutaniko lake la nyumbani huko New Jersey, Marekani. Kisha, alihama ili akaishi na binti yake. Akina ndugu katika kutaniko lake jipya walijitahidi kumjua zaidi, na wakagundua kuwa walikuwa wamepata hazina. Aliwatia moyo kwa kuwasimulia mambo aliyojionea katika utumishi wa shambani alipojifunza kweli katika miaka ya 1920. Wakati huo, sikuzote alibeba mswaki alipoenda kuhubiri—kwa sababu angeweza kukamatwa na kuwekwa mahabusu kwa kipindi fulani cha wakati. Isitoshe, mwaka wa 1933, mara mbili, alikamatwa na kuwekwa mahabusu kwa kipindi cha juma moja. Wakati huo, mume wake ambaye si Shahidi na aliyemuunga mkono, aliwatunza watoto wao watatu wadogo. Hapana shaka kwamba ndugu na dada waaminifu wenye umri mkubwa kama Harriette wanastahili kuthaminiwa!

13. Tuliboliki ki kuhusu sehemu ambaju baabi na umuli nkolongu atimisa mulitengenezu lika Yehova?

13 Ndugu na dada zetu wenye umri mkubwa wanatimiza sehemu muhimu katika tengenezo la Yehova. Wamejionea jinsi ambavyo Yehova amelibariki tengenezo Lake kwa njia nyingi mbalimbali, na jinsi alivyowabariki wao kibinafsi. Wamejifunza masomo muhimu kutokana na makosa yao wenyewe. Waone kama “chemchemi ya hekima,” na ujifunze kutokana na uzoefu wao. (Met. 18:4) Ikiwa utatumia muda wako kuwafahamu vizuri, imani yako inaweza kuimarishwa na utajifunza mambo mengi kutoka kwao.

NUFAIKA KIKAMILI KUBOKANA NUMFANU GWA BAABI NA UMULI NKOLONGU

14. Liandiku la Kumbukumbu la Torati 32:7 lajege mwoju akakombu ahenga kike?

14 Chukua hatua ya kwanza kuzungumza na ndugu na dada wenye umri mkubwa. (Soma Kumbukumbu la Torati 32:7.) Ni kweli kwamba huenda macho yao hayaoni vizuri, wanatembea taratibu, na huenda wanazungumza kwa sauti ndogo, hata hivyo wao ni vijana moyoni, na wamejifanyia “jina zuri” pamoja na Yehova. (Mhu. 7:1) Kumbuka sababu inayomfanya Yehova awathamini. Endelea kuwaonyesha heshima. Uwe kama Elisha. Elisha alisisitiza kukaa karibu na Eliya katika siku yao ya mwisho kuwa pamoja. Mara tatu Elisha alisema hivi: “Sitakuacha.”—2 Fal. 2:2, 4, 6.

15. Tuwesa kwalaluki maswali bo, akandugu na dada bitu baabi na umuli nkolongo?

15 Waonyeshe upendezi wa kibinafsi ndugu na dada wenye umri mkubwa kwa kuwauliza maswali kwa fadhili ili kuyateka mawazo yao. (Met. 1:5; 20:5; 1 Tim. 5:1, 2) Waulize maswali kama vile: “Ulipokuwa kijana ni nini kilichokusadikisha kwamba umeipata kweli?” “Mambo uliyopitia maishani yamekusaidiaje kumkaribia zaidi Yehova?” “Je, ungesema siri ya kuendelea kuwa mwenye furaha katika utumishi wa Yehova ni nini?” (1 Tim. 6:6-8) Kisha wasikilize wanapokusimulia mambo hayo.

16. Baabi na umuli nkolongu nakakombu anufaika bo, paalonge pamwa?

16 Ndugu au dada mwenye umri mkubwa anapozungumza pamoja na kijana, wote hunufaika. (Rom. 1:12) Enyi vijana, mazungumzo hayo yatawasaidia kuongeza uthamini wenu kuelekea jinsi Yehova anavyowatunza watumishi wake waaminifu, na ndugu au dada mwenye umri mkubwa atahisi anaheshimiwa. Atafurahia kukusimulia kuhusu baraka alizopokea kutoka kwa Yehova.

17. Ndaba jaki tuwesa kupwaga kwamba uzuli gwaka ndugu na dada baabi na umuli nkolongu guendale kujonzukeka kadili miaka ejipeta?

17 Kwa kawaida, uzuri wa nje hufifia kadiri umri unavyosonga, lakini wale ambao ni washikamanifu kwa Yehova wanaendelea kuwa wazuri hata zaidi machoni pake kadiri miaka inavyosonga. (1 The. 1:2, 3) Kwa nini hilo ni kweli? Kwa sababu kwa miaka mingi, wameruhusu roho ya Yehova iwafinyange na kuwasaidia wasitawishe sifa nzuri. Kadiri tunavyowajua, kuwaheshimu, na kujifunza zaidi kutoka kwa ndugu na dada hao wenye thamani, ndivyo tutakavyowaona kuwa hazina yenye thamani sana!

18. Twilongalya ki mumakala jejipwata?

18 Kutaniko haliwi tu imara zaidi wakati vijana wanapowathamini wenye umri mkubwa, bali pia wakati wenye umri mkubwa wanapowathamini vijana. Katika makala inayofuata, tutazungumzia jinsi wale wenye umri mkubwa wanavyoweza kuonyesha kwamba wanawathamini vijana kutanikoni.

NHAMBU 144 Kaza Macho Kwenye Zawadi!

^ ekichweka 5 Ndugu na dada zetu waaminifu wenye umri mkubwa ni kama hazina zenye thamani. Makala hii itatutia moyo tuongeze uthamini wetu kwao na itazungumzia jinsi tunavyoweza kunufaika kikamili kutokana na hekima na uzoefu wao. Pia, makala hii itawahakikishia wale wenye umri mkubwa kwamba wana sehemu muhimu katika tengenezo la Mungu.