Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 36

Usamini Nguvu ya Vijana

Usamini Nguvu ya Vijana

“Utukufu wa vijana ni nguvu zao.”​—MEZ. 20:29.

WIMBO 88 Unijulishe Njia Zako

KIFUPI YA HABARI *

1. Ni muradi gani wa muzuri wenye tunaweza kujiwekea wakati tunazeeka?

 WAKATI tunazeeka, tunaweza kuanza kujiona kama hatuko tena wa maana sana kwa Yehova sawa zamani. Hata kama hatuna tena nguvu sawa vile wakati tulikuwa vijana, tunaweza kutumia hekima na uzoefu wenye tulipata ili kusaidia vijana wajue namna ya kutumia uwezo wao mu tengenezo ya Yehova na kukubali mapendeleo ingine ya utumishi. Ni saa vile muzee moja wa zamani alisemaka: “Wakati singeweza tena kufanya mengi zaidi juu ya uzee, nilikuwa mwenye shukrani sana juu kulikuwa ndugu vijana wenye kustahili wenye wangeweza kuendelea na kazi.”

2. Tutazungumuzia mambo gani mu hii habari?

2 Mu habari yenye ilitangulia, tulizungumuzia namna vijana wanapata faida wakati wanakuwa marafiki wa ndugu na dada wenye walishazeeka. Mu hii habari, tutaona namna gani sifa sawa vile unyenyekevu, kiasi, shukrani, na ukarimu inaweza kusaidia ndugu na dada wenye walishazeeka kutumika pamoja na vijana. Na ile ni baraka kabisa kwa kutaniko yote.

UKUWE MUNYENYEKEVU

3. Kulingana na Wafilipi 2:3, 4, unyenyekevu ni nini, na namna gani inaweza kusaidia Mukristo?

3 Ndugu na dada wenye walishazeeka wanapaswa kuwa wanyenyekevu wakati wanapenda kusaidia vijana. Mutu munyenyekevu anaona wengine kuwa wazuri zaidi kuliko yeye. (Soma Wafilipi 2:3, 4.) Ndugu na dada wenye walishazeeka wanapaswa kuelewa kama kuko njia mbalimbali ya kufanya mambo kulingana na Biblia na kulingana na kazi. Kwa hiyo, hawatazamie kama kila mutu atafanya mambo fulani kwa kutumia njia ileile yenye wao walikuwa wanatumia zamani. (Muh. 7:10) Wanaweza kusaidia vijana kwa kuwaambia mambo yenye walijifunza, lakini pia wanapaswa kujua kama “tamasha ya ulimwengu huu inabadilika” na kama inaweza kuwa muzuri kwao kujipatanisha na hali za mupya.​—1 Ko. 7:31.

Kwa ukarimu, wale wenye walishazeeka wanaambia wengine mambo wanajua na mambo yenye walikutana nayo (Ona fungu ya 4-5) *

4. Namna gani waangalizi wa mizunguko wanaonyesha mutazamo sawa ule wa Walawi?

4 Ndugu na dada wenye walishazeeka wenye ni wanyenyekevu, wanajua kama wakati wanazeeka hawawezi tena kufanya mengi sawa vile zamani. Kwa mufano, tufikirie waangalizi wetu wa mizunguko. Wakati wanaeneza miaka 70 wanawapatiaka migao ingine. Ile inaweza kuwa nguvu sana kwao. Walipenda sana pendeleo yenye walikuwa nayo ya kutumikia ndugu zao na wanaendelea kuipenda sana. Lakini wanaelewa kama ni muzuri zaidi kwa ndugu vijana kufanya ile kazi. Kwa kufanya vile, wanaonyesha kama wanaiga mutazamo wa Walawi wa Israeli ya zamani, wenye waliombwa kuacha kazi yao ya ku tabenakulo wakati walieneza miaka 50. Wale Walawi walikuwa wenye furaha hata kama waliwapatia mugao gani. Walifanya kwa bidii mambo yenye wangeweza kufanya na walisaidia vijana. (Hes. 8:25, 26) Leo, wakati waangalizi wa mizunguko wanakuwa na miaka 70 wanaacha kazi ya kutembelea makutaniko, lakini wanasaidia na kutia moyo kutaniko kwenye wanatumikia.

5. Mufano wa Dan na Katie unakufundisha nini?

5 Fikiria mufano wa Dan, mwenye alikuwa mwangalizi wa muzunguko kwa miaka 23. Wakati Dan alieneza miaka 70, yeye na bibi yake Katie, walipewa mugao wa kuwa mapainia wa pekee. Nini njo iliwasaidia wafurahie mugao wao wa mupya? Dan anasema kama kwa sasa iko na mambo mingi sana ya kufanya kuliko zamani! Anaendelea kutimiza madaraka yake mu kutaniko, anasaidia ndugu wakuwe na sifa zenye zinaombwa ili kuwa mutumishi wa huduma, na anazoeza wengine kuhubiri mu miji mikubwa-mikubwa na mu gereza. Kama uko ndugu ao dada mwenye alishazeeka, ikuwe uko mu utumishi wa wakati wote ao hapana, unaweza kufanya mengi zaidi ili kusaidia wengine. Namna gani? Ufurahie mugao wako wa mupya, ujiwekee miradi ya mupya, na ukazie uangalifu mambo yenye unaweza kufanya na hapana mambo yenye hauwezi kufanya.

UKUWE MWENYE KIASI

6. Juu ya nini ni jambo ya hekima kuwa mwenye kiasi? Leta mufano.

6 Mutu mwenye kiasi anajuaka mipaka yake. (Mez. 11:2) Mutu mwenye kiasi hatazamie zaidi ya mambo anaweza kufanya. Ile inamusaidia aendelee kuwa na furaha na kuendelea kutumika kwa bidii. Tunaweza kulinganisha mutu mwenye kiasi na shofere mwenye kutembeza gari yenye kupanda kilima. Anapaswa kubadilisha mwendo wake juu apande kilima. Pengine atapunguza mwendo, lakini hatasimama. Vilevile, mutu mwenye kiasi anajua wakati gani inaomba “kubadilisha mwendo” juu aendelee kumutumikia Yehova na kusaidia wengine.​—Flp. 4:5.

7. Namna gani Barzilai alionyesha sifa ya kiasi?

7 Fikiria mufano wa Barzilai, mwenye alikuwa na miaka 80 wakati Mufalme Daudi alimuomba akuwe mushiriki wa makao yake ya kifalme. Juu Barzilai alikuwa mwenye kiasi alikatala ombi ya mufalme. Barzilai alijua kama hangeweza kufanya mengi zaidi kwa sababu ya miaka yake, njo maana aliomba kijana Kihamu aende fasi yake. (2 Sa. 19:35-37) Sawa vile Barzilai, ndugu wenye walishazeeka wanafurahia kupatia vijana wanaume nafasi ya kuendelea na kazi.

Yehova aliamua Sulemani njo ajenge hekalu. Mufalme Daudi alikubali ile uamuzi (Ona fungu ya 8)

8. Namna gani Mufalme Daudi alionyesha sifa ya kiasi wakati alipenda kujenga hekalu?

8 Mufalme Daudi pia alituachia mufano muzuri wa kiasi. Kwa moyo wake wote, alikuwa anapenda kumujengea Yehova hekalu. Lakini wakati Yehova alimuambia kama kijana Sulemani njo angefanya ile kazi, Daudi alikubali ile uamuzi na alifanya yake yote ili kutegemeza kazi ya ujenzi. (1 Ny. 17:4; 22:5) Daudi hakuwaza kama ni yeye tu njo angeweza kufanya muzuri ile kazi juu Sulemani alikuwa ‘mudogo na hakukuwa na uzoefu.’ (1 Ny. 29:1) Daudi alijua kama ujenzi wa hekalu ungewezekana juu ungetegemea baraka za Yehova na hapana miaka wala uzoefu wa wenye waliongoza ile kazi. Kama vile Daudi, leo, wale wenye walishazeeka wanaendelea kumutumikia Yehova kwa bidii hata kama mugao wao umebadilika. Na wanajua kama Yehova atabariki vijana wenye wako wanafanya kazi yenye wao walikuwa wanafanya.

9. Namna gani ndugu mumoja wa Halmashauri ya Tawi alionyesha sifa ya kiasi?

9 Mufano moja wa wakati wetu wa mutu fulani mwenye alionyesha sifa ya kiasi ni wa ndugu Shigeo. Mu 1976 wakati alieneza miaka 30, aliwekwa kuwa mushiriki wa Halmashauri ya Tawi. Mu 2004 aliwekwa kuwa muratibu wa Halmashauri ya Tawi. Kisha alifikia kutambua kama hakukuwa tena na uwezo sawa vile zamani na ilikuwa inakamata wakati mingi ili kutimiza kazi yake. Alisali juu ya ile hali na alifikiria faida ya kuwa na muratibu wa Halmashauri ya Tawi mwenye ni kijana. Hata kama haiko tena muratibu, Shigeo anaendelea kutumika pamoja na ndugu wa Halmashauri ya Tawi. Kama vile tumetoka kuona mu mufano wa Barzilai, Mufalme Daudi, na Shigeo, mutu munyenyekevu na mwenye kiasi atakaza akili yake juu ya nguvu yenye vijana wako nayo hapana juu ya kukosa uzoefu kwa vijana. Atawaona hapana sawa vile washindani wake lakini sawa vile wafanyakazi wenzake.​—Mez. 20:29.

UKUWE MWENYE SHUKRANI

10. Ni mutazamo gani wale wenye walishazeeka wako nayo kuhusu vijana mu kutaniko?

10 Ndugu na dada wenye walishazeeka wanaona vijana kuwa zawadi kutoka kwa Yehova na wako wenye shukrani juu ya mambo yenye vijana wanafanya. Wakati nguvu yao inakuwa kidogo, wale wenye walishazeeka wako wenye shukrani kuona vile kuko wale wenye kuwa na nguvu ya ujana na wenye wako na uwezo wa kutumikia kutaniko.

11. Namna gani Rutu 4:13-16 inaonyesha baraka yenye mutu mwenye alishazeeka anaweza kupata kwa sababu anakubali musaada wa vijana?

11 Mufano wa Naomi wenye kuzungumuziwa mu Biblia ni mufano muzuri sana wa mutu muzee mwenye alikubali kwa furaha musaada wa kijana moja. Kwanza, Naomi alimuomba Rutu, binti-mukwe wake, arudie kwa watu wake. Lakini wakati Rutu alisema kama hatamuacha Naomi arudie yeye peke Betlehemu, Naomi alikubali musaada wa Rutu. (Rut. 1:7, 8, 18) Na ile iliwaletea baraka sana wote wawili! (Soma Rutu 4:13-16.) Unyenyekevu unaweza kuchochea wale wenye walishazeeka wafuate mufano wa Naomi.

12. Namna gani mutume Paulo alionyesha shukrani yake?

12 Mutume Paulo alikuwa mwenye shukrani sana kwa musaada wenye alipata. Kwa mufano, alishukuru Wakristo wa Filipi juu walimutumia musaada fulani wa kimwili. (Flp. 4:16) Alionyesha pia shukrani yake kwa Timoteo juu alimutegemeza. (Flp. 2:19-22) Na Paulo alimushukuru Mungu kwa ajili ya wale wote wenye walikuja kumutia moyo wakati alikuwa anapelekwa Roma na iko mufungwa. (Mdo. 28:15) Paulo alikuwa mutu mwenye bidii sana, mwenye alisafiri makilometre mingi ili kuhubiri na kutia moyo makutaniko. Lakini alikuwa munyenyekevu na alikubali musaada wa ndugu na dada zake.

13. Namna gani wale wenye walishazeeka wanaweza kuonyesha shukrani yao kwa vijana?

13 Nyie ndugu na dada wenye mulishazeeka, munaweza kuonyesha shukrani yenu kwa vijana katika kutaniko mu njia mbalimbali. Kama wanapenda kuwasaidia, kwa mufano, juu ya transport, kuuza vitu fulani, ao juu ya mambo ingine ya kimwili yenye muko nayo lazima, mukuwe tayari kukubali musaada wao. Muone ile musaada kuwa alama yenye kuonyesha kama Yehova anawapenda. Munaweza kushangaa sababu uhusiano wenu pamoja na vijana unaweza kuwa nguvu sana. Kila mara, muonyeshe kama munapendezwa na maendeleo ya kiroho ya vijana wenu wapendwa, na muwaambie kama munafurahi sana kuona vile wako wanafanya mengi zaidi mu kutaniko. Na mukuwe tayari kupitisha wakati pamoja nao, lakini pia mukuwe tayari kuwafasiria mambo fulani yenye mulijionea mu maisha yenu. Wakati munafanya vile, ‘munajionyesha kuwa wenye shukrani’ kwa Yehova kwa ajili ya vijana wenye alivuta katika kutaniko.​—Kol. 3:15; Yoh. 6:44; 1 Te. 5:18.

UKUWE MUKARIMU

14. Namna gani Mufalme Daudi alionyesha ukarimu wake?

14 Katika mufano wa Mufalme Daudi tunapata sifa ingine ya maana sana yenye wale wenye walishazeeka wanapaswa kuonyesha: Ukarimu. Daudi alitoa makuta mingi na vitu mingi ya bei ili kutegemeza kazi ya ujenzi wa hekalu. (1 Ny. 22:11-16; 29:3, 4) Alifanya vile hata kama kwa kiasi fulani, sifa ingemuendea mutoto yake Sulemani. Kama hatuna tena uwezo wa kushiriki mu kazi ya ujenzi, tunaweza kuendelea kutegemeza ile kazi kupitia michango yetu, kulingana na uwezo wetu. Na tunaweza pia kusaidia vijana wapate faida kabisa kwa kuwaambia mambo fulani yenye tulijionea mu maisha yetu.

15. Ni zawadi gani za muzuri sana zenye mutume Paulo alipatia Timoteo?

15 Kuhusu ukarimu, muache tufikirie mufano wenye mutume Paulo alituachia. Aliomba Timoteo amusindikize mu kazi ya umisionere, na kwa ukarimu wote, Paulo alionyesha Timoteo namna ya kuhubiri na namna ya kufundisha. (Mdo. 16:1-3) Mazoezi ya Paulo ilimusaidia Timoteo akuwe na matokeo ya muzuri mu kazi ya kutangaza habari njema. (1 Ko. 4:17) Timoteo alitumia njia zilezile za Paulo ili kuzoeza wengine.

16. Juu ya nini Shigeo alizoeza wengine?

16 Leo, wale wenye walishazeeka hawawaze kama wakizoeza vijana ili wafanye kazi yenye walikuwa wanafanya zamani, ile itafanya wao wasikuwe tena wa maana mu kutaniko. Kwa mufano, kwa miaka mingi, Shigeo, mwenye tulishataja, alizoeza ndugu vijana wa Halmashauri ya Tawi. Alifanya vile juu ya kutegemeza kazi ya Ufalme mu inchi kwenye iko anatumikia. Ile ilifanya, kisha wakati fulani, ndugu mwingine kijana mwenye alizoezwa muzuri akamate nafasi yake na akuwe muratibu wa Halmashauri ya Tawi. Shigeo anaendelea kutumika mu Halmashauri ya Tawi kisha kufanya zaidi ya miaka 45 ndani, na anaendelea kusaidia ndugu vijana wenye kuwa mu ile halmashauri. Ni baraka sana kwa watumishi wa Mungu kuwa na watu sawa ule!

17. Kulingana na Luka 6:38, ni jambo gani ndugu ao dada mwenye alishazeeka anaweza kupatia wengine?

17 Nyie ndugu na dada wenye walishazeeka muko ushuhuda wenye kuwa wazi, wenye kuonyesha kama kumutumikia Yehova kwa uaminifu na kuendelea kuonyesha imani katika yeye, njo maisha ya muzuri sana kuliko yote. Kupitia mufano wenu, munaonyesha kama kujifunza kanuni za Biblia na kuzitumikisha mu maisha yenu kumewaletea baraka mingi. Munajua vile mambo ilikuwa inafanywa zamani, lakini muliona pia ulazima wa kujipatanisha na mabadiliko mbalimbali. Hata nyie, ndugu na dada wenye walishazeeka wenye mulibatizwa hivi karibuni, muko pia na mambo mingi ya kutoa; munaweza kufasiria wengine furaha yenye mulipata kwa kujifunza kumujua Yehova mu miaka yenu ya uzee-uzee. Vijana watafurahi sana kusikia habari zenu za muzuri na mambo ingine yenye mulijifunza. Kama ‘munazoea kupatia watu’ kwa kuwafasiria mambo yenye mulijionea, Yehova atawabariki sana.​—Soma Luka 6:38.

18. Namna gani wale wenye walishazeeka na vijana wanaweza kusaidiana?

18 Wakati nyie, wenye mulishazeeka na vijana, munakuwa marafiki mutakuwa tayari kutegemezana. (Ro. 1:12) Kila mumoja wenu iko na jambo fulani ya maana yenye mwingine hana. Wale wenye walishazeeka wako na hekima na uzoefu wenye walipata mu maisha yao yote. Lakini vijana wao, wako na nguvu sana. Wakati vijana na wale wenye walishazeeka wako marafiki, wanamuletea sifa Baba yetu wa mbinguni mwenye upendo na wako baraka kwa kutaniko yote.

WIMBO 90 Tutiane Moyo

^ fu. 5 Ni baraka kabisa kuwa na vijana wanaume na wanamuke mu makutaniko yetu wenye wanajikaza kutegemeza tengenezo ya Yehova. Hata kama wako na desturi mbalimbali, ndugu na dada wenye walishazeeka wenye kuwa mu kutaniko, wanaweza kusaidia vijana watumie kabisa nguvu yao mu utumishi wa Yehova.

^ fu. 55 MAFASIRIO YA PICHA: Wakati mwangalizi wa muzunguko alieneza miaka 70, yeye na bibi yake walipata mugao mupya. Uzoefu wenye walipata unawasaidia kuzoeza wengine mu kutaniko yao.