Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 38

Ukuwe Karibu na Familia Yako ya Kiroho

Ukuwe Karibu na Familia Yako ya Kiroho

“Ninapanda kuenda kwa Baba yangu na Baba yenu.”​—YOH. 20:17.

WIMBO 3 Nguvu Yangu, Tumaini Yangu, Ninakutegemea

KIFUPI YA HABARI *

1. Wanadamu waaminifu wanaweza kuwa na uhusiano gani pamoja na Yehova?

 MU FAMILIA ya waabudu wa Yehova muko pia Yesu, mwenye ni “muzaliwa wa kwanza wa viumbe vyote,” na malaika wengi. (Kol. 1:15; Zb. 103:20) Wakati Yesu alikuwa hapa ku dunia, alionyesha kama wanadamu waaminifu wanaweza kumuona Yehova kuwa Baba yao. Wakati alikuwa anazungumuza na wanafunzi wake, Yesu alimutaja Yehova kuwa “Baba yangu na Baba yenu.” (Yoh. 20:17) Na wakati tunajitoa kwa Yehova na kubatizwa, tunakuwa mu familia yenye upendo ya ndugu na dada.​—Mk. 10:29, 30.

2. Ni mambo gani tutaona mu hii habari?

2 Ni nguvu kwa watu fulani kuona Yehova kuwa Baba mwenye upendo. Pengine wengine hawajue namna ya kuonyesha ndugu na dada zao kama wanawapenda. Mu hii habari tutaona namna Yesu anatusaidia kuona Yehova kama Baba mwenye upendo, Baba mwenye tunaweza kukaribia. Tutaona pia njia mbalimbali zenye tunaweza kumuiga Yehova mu namna yenye tunatendea ndugu na dada zetu.

YEHOVA ANAPENDA UMUKARIBIE

3. Namna gani sala ya mufano inafanya tumukaribie Yehova?

3 Yehova ni Baba mwenye upendo. Yesu anapenda tumuone Yehova vile yeye anamuona, ni kusema, sawa muzazi muchangamufu, mwenye upendo na mwenye tunaweza kukaribia kwa urahisi, hapana sawa mutu mubaya mwenye kulazimisha watu mambo ya kufanya. Ile inaonekana wazi mu namna Yesu alifundisha wanafunzi wake kusali. Alianza na sala ya mufano kwa kutumia maneno: “Baba yetu.” (Mt. 6:9) Pengine Yesu angetuambia tumuite Yehova “Mweza-Yote,” “Muumbaji,” ao “Mufalme wa umilele.” Na ile haiko mubaya juu ni majina yenye Biblia inatumia na yenye inamufaa. (Mwa. 49:25; Isa. 40:28; 1 Ti. 1:17) Lakini Yesu alituambia tumuite Yehova “Baba.”

4. Tunajua namna gani kama Yehova anapenda tumukaribie?

4 Ni nguvu kwako kumuona Yehova kama Baba mwenye upendo? Kwa watu fulani ni nguvu. Kama baba yetu hakukuwa anatutendea muzuri, pengine inaweza kuwa nguvu kukubali kama kuko baba mwenye anaweza kutupenda. Ni jambo yenye kufariji sana kujua kama Yehova anaelewa kabisa namna tunajisikia! Anapenda kutukaribia. Njo maana Neno yake inatuambia hivi: “Mumukaribie Mungu, naye atawakaribia ninyi.” (Yak. 4:8) Yehova anatupenda na anasema kama atakuwa Baba wa muzuri zaidi mwenye hatuyapataka.

5. Kulingana na Luka 10:22, namna gani Yesu anaweza kutusaidia tumukaribie Yehova?

5 Yesu anaweza kutusaidia tumukaribie Yehova. Juu anamujua Yehova muzuri na juu anaiga sifa zake kwa ukamili, njo maana alisema: “Kila mutu mwenye ameniona mimi amemuona Baba pia.” (Yoh. 14:9) Sawa vile kaka mukubwa, Yesu anatufundisha namna tunaweza kuheshimia na kumutii Baba yetu, namna tunaweza kuepuka kufanya mambo yenye inamuchukiza na namna tunaweza kukubaliwa naye. Lakini namna ya Yesu ya kuishi wakati alikuwa hapa ku dunia inatusaidia zaidi sana kuelewa kama Yehova ni Mungu mwema na mwenye upendo. (Soma Luka 10:22.) Tufikirie basi mifano fulani.

Akiwa Baba mwenye upendo, Yehova alitia nguvu mwana wake kupitia malaika (Ona fungu ya 6) *

6. Leta mifano yenye kuonyesha namna Yehova alisikiliza sala za Yesu.

6 Yehova anasikilizaka watoto wake. Fikiria namna Yehova alisikiliza muzaliwa wake wa kwanza. Kusema kweli, Yehova alisikiliza sala mingi zenye Yesu alitoa wakati alikuwa hapa ku dunia. (Lu. 5:16) Alisikia Yesu akisali kuhusu maamuzi ya maana sana yenye alipaswa kukamata, sawa vile wakati alichagua mitume wake 12. (Lu. 6:12, 13) Yehova alisikiliza pia sala ya Yesu wakati alikuwa na mahangaiko. Mbele asalitiwe na Yuda, Yesu alisali kwa Baba yake kuhusu mambo yenye ingemufikia. Yehova hakusikiliza tu sala ya Yesu lakini pia alimutumia malaika ili kumutia nguvu.​—Lu. 22:41-44.

7. Tunajisikia namna gani wakati tunajua kama Yehova anasikilizaka sala zetu?

7 Leo, Yehova anaendelea kusikiliza sala za watumishi wake na anajibia zile sala kwa wakati wenye kufaa na mu njia ya muzuri zaidi. (Zb. 116:1, 2) Fikiria dada moja wa Inchi ya India, mwenye alijionea ile. Alikuwa na mahangaiko mingi sana yenye ilikuwa inamusumbua na alisali sana kwa Yehova kuhusu ile tatizo. Anasema hivi: “Programu ya JW Télédiffusion ya Mwezi wa 5, 2019 yenye ilizungumuzia namna ya kupambana na woga na mahangaiko ilifika wakati yenye nilikuwa nayo lazima. Ilikuwa kabisa Jibu ya sala zangu.”

8. Ni mu njia gani Yehova alionyesha kama anamupenda Yesu?

8 Yehova anatupenda na anatuhangaikia sawa vile alimupendaka Yesu na kumuhangaikia wakati alikuwa hapa ku dunia. (Yoh. 5:20) Alimusaidia Yesu aendelee kutia nguvu imani yake, alimutia moyo wakati alikuwa na mahangaiko na alihakikisha kama Yesu iko na mambo yote yenye alikuwa nayo lazima ili kuishi. Na Yehova alimuambia mwana wake kama anamupenda na kama anamukubali. (Mt. 3:16, 17) Yesu hakukuwa anajisikia kuwa yeye peke juu siku zote alikuwa anategemea Baba yake wa mbinguni mwenye upendo.​—Yoh. 8:16.

9. Tunajua namna gani kama Yehova anatupenda?

9 Kama Yesu, siye wote tumejionea upendo wa Yehova mu njia mingi. Waza kidogo: Yehova alituvuta kwake na alitupatia familia ya kiroho yenye kuwa na upendo na umoja juu tufurahi na anatutegemeza wakati tuko na mahangaiko. (Yoh. 6:44) Tena, Yehova anatutolea chakula ya kiroho ili kutia nguvu imani yetu. Na hata anatusaidia tukuwe na mambo yote yenye tuko nayo lazima ili kuishi. (Mt. 6:31, 32) Wakati tunafikiri sana juu ya namna Yehova anatupenda ile inafanya tumupende tena zaidi.

UTENDEE FAMILIA YAKO YA KIROHO KAMA VILE YEHOVA

10. Namna Yehova anatendea ndugu na dada zetu inaweza kutufundisha nini?

10 Yehova anapenda ndugu na dada zetu. Lakini, kila mara haikuwake mwepesi kwetu kupenda ndugu na dada zetu na kuonyesha kama tunawapenda. Tena, wakati fulani inaweza kuwa nguvu kufanya vile, juu hatuna desturi moja na hatukukomalia fasi moja. Na siye wote tunafanyaka makosa yenye kukasirisha ao kuhuzunisha wengine. Lakini, siye wote tunaweza kutia nguvu upendo wenye tuko nao mu familia yetu ya kiroho. Namna gani? Kwa kuonyesha upendo ndugu na dada zetu sawa vile Baba yetu Yehova. (Efe. 5:1, 2; 1 Yo. 4:19) Tuone basi mambo yenye tunaweza kujifunza kupitia mufano wa Yehova.

11. Namna gani Yesu aliiga “huruma nyingi” ya Yehova?

11 Yehova anaonyesha “huruma nyingi.” (Lu. 1:78) Mutu mwenye kuwa na huruma anajisikiaka mubaya wakati anaona wengine wanateseka, anatafutaka njia mbalimbali ili kusaidia na kufariji wengine. Namna Yesu alitendea watu ilionyesha kama aliiga huruma wa Yehova. (Yoh. 5:19) Siku fulani wakati aliona watu wengi, Yesu “akawasikilia huruma, kwa sababu walikuwa wamechunwa ngozi na kutupwa huku na huku kama kondoo wenye hawana muchungaji.” (Mt. 9:36) Yesu hakusikilia tu watu huruma lakini alifanya jambo fulani ili kuwasaidia. Aliponyesha wagonjwa na kusaidia wale wenye kuteseka na wenye “kulemewa na mizigo.”​—Mt. 11:28-30; 14:14.

Uige huruma na ukarimu wa Yehova kuelekea ndugu na dada zako (Ona fungu ya 12-14) *

12. Namna gani tunaweza kuonyesha kama tunasikilia wengine huruma? Leta mufano.

12 Kama tunafikiria magumu yenye ndugu na dada zetu wako nayo, ile itafanya tuwasikilie huruma na kuwasaidia. Kwa mufano, dada fulani anaweza kuwa na matatizo ya nguvu sana ya afya. Hazungumuzie juu ya ile tatizo yake, lakini pengine anaweza kufurahi kuona mutu fulani anamusaidia. Iko na uwezo wa kupatia familia yake mambo yenye wako nayo lazima? Je, tunaweza kumusaidia kupika chakula ao kumusaidia kusafisha nyumba yake? Pengine ndugu fulani hana kazi tena. Tunaweza pengine kumupatia makuta kidogo, bila hata kumuambia kama siye njo tulimupatia na kumusaidia mupaka vile atapata kazi ingine.

13-14. Namna gani tunaweza kuonyesha kama tuko wakarimu sawa vile Yehova?

13 Yehova ni mukarimu. (Mt. 5:45) Hatupaswe kungojea wakati ndugu na dada zetu watatuomba tuwasaidie njo tuwasikilie huruma. Kama vile Yehova tunapaswa kuwa tayari kuwasaidia mbele watuambie. Yehova anatutolea jua kila siku bila hata siye kumuomba na kila mutu anapata faida kupitia ile jua, haiko tu wale wenye wanamushukuru! Hauone kama wakati Yehova anatutimizia mahitaji yetu ile inaonyesha kama anatupenda? Tunamupenda Yehova sana juu ni mwema na mukarimu!

14 Ndugu na dada zetu wengi wanamuiga Yehova kwa kuonyesha wengine ukarimu. Kwa mufano, mu 2013 kulikuwa upepo mukali sana wenye unaitwa Haiyan wenye uliharibisha vitu mingi mu Ufilipino. Ndugu na dada wengi walipoteza nyumba zao na vitu vyao. Lakini ndugu na dada wa mu dunia yote waliwategemeza. Wengi walitoa michango na waliwasaidia kutengeneza na kujenga upya nyumba zao 750 hivi, ile kazi yote haikueneza hata mwaka moja! Mu kipindi ya Coronavirus, Mashahidi wa Yehova walitumika sana ili kutegemeza ndugu na dada zao. Wakati tuko tayari kutegemeza watu wa familia yetu ya kiroho tunaonyesha kama tunawapenda.

15-16. Kulingana na Luka 6:36, ni mu njia gani moja ya maana tunaweza kumuiga Baba yetu wa mbinguni?

15 Yehova ni mwenye rehema na mwenye kusamehe. (Soma Luka 6:36.) Kila siku tunajionea rehema ya Baba yetu wa mbinguni. (Zb. 103:10-14) Wafuasi wa Yesu hawakukuwa wakamilifu lakini Yesu aliwaonyesha rehema na alikuwa tayari kuwasamehe. Alikuwa hata tayari kutoa uzima wake juu zambi zetu zisamehewe. (1 Yo. 2:1, 2) Musamaha na rehema yenye Yehova na Yesu wanatuonyesha inafanya tuwakaribie, hauone vile?

16 Tunaweza kutia nguvu upendo wenye tuko nao mu familia yetu ya kiroho, wakati tuko tayari ‘kusameheana kwa kupenda.’ (Efe. 4:32) Kusema kweli, kusamehe wengine inaweza kuwa nguvu sana wakati fulani, lakini tunapaswa kujikaza. Habari moja ya gazeti Munara wa Mulinzi yenye kuwa na kichwa “Tuwe Tayari Kusameheana” ilisaidia dada moja. * Anasema hivi: “Kujifunza ile habari kulinisaidia kuelewa kama, kusamehe wengine kunaweza kuwa na matokeo ya muzuri juu yangu. Ile habari ilionyesha kama wakati uko tayari kusamehe wengine ile haimaanishe kama unakubaliana na mambo ya mubaya yenye walikutendea ao unapunguza uzito wa matokeo ya kosa yenye walikutendea. Lakini kusamehe kunamaanisha kuepuka kuchunga kinyongo na kuendelea kuwa na amani ya moyo.” Wakati tunasamehe ndugu na dada zetu kwa kupenda, tunaonyesha kama tunawapenda na tunaonyesha kama tunaiga Baba yetu Yehova.

FURAHIA PENDELEO YA KUWA MU FAMILIA YA YEHOVA

Vijana na wenye walishazeeka wanaonyesha upendo ndugu na dada zao (Ona fungu ya 17) *

17. Kulingana na Matayo 5:16, namna gani tunaweza kumuletea Baba yetu wa mbinguni utukufu?

17 Ni pendeleo kubwa sana kuwa mu familia yenye upendo ya ndugu na dada wa mu dunia yote. Tunapenda kadiri inawezekana watu wengi wajiunge na siye ili kumuabudu Yehova. Tukiwa na ile mu akili, hatupaswe kufanya jambo yoyote yenye inaweza kufanya watu wakuwe na mawazo ya mubaya juu ya Yehova ao juu ya watu wake. Njo maana tunapaswa kujiendesha mu njia yenye itafanya watu wakubali habari njema.​—Soma Matayo 5:16.

18. Ni mambo gani inaweza kutusaidia kutoa ushahidi bila woga?

18 Wakati fulani, watu fulani wanaweza kusema mambo ya mubaya ao hata kututesa juu tunamutii Baba yetu wa mbinguni. Tunaweza kufanya nini kama tunaogopa kuambia wengine mambo yenye tunaamini? Tunapaswa kumutegemea Yehova na mwana wake ili kupata musaada. Yesu alihakikishia wanafunzi wake kama hawapaswe kuhangaika juu ya namna ya kusema na mambo watasema. Juu ya nini? Yesu alisema kama: “Kwa sababu mutapewa mambo ya kusema saa hiyo; kwa maana wenye kusema haiko ninyi tu, lakini ni roho ya Baba yenu ndiyo inasema kupitia ninyi.”​—Mt. 10:19, 20.

19. Leta mufano wa mutu moja mwenye alihubiri kwa uhodari.

19 Fikiria mufano wa Robert. Wakati fulani, saa yenye alikuwa angali mwanafunzi wa Biblia na hakukuwa na ujuzi mingi wa Biblia, siku moja alijikuta mbele ya tribinali fulani ya kijeshi mu Afrika ya Kusini. Bila kuogopa alifasiria waziwazi ile tribinali kama hakupenda kujiingiza mu mambo ya politike juu alipenda ndugu zake Wakristo. Alifurahia sana fasi yenye alikuwa nayo mu famila yetu ya kiroho! Juge akamuuliza hivi: “Ndugu zako ni nani?” Robert hakukuwa anatazamia ile ulizo, lakini mara moja andiko ya ile siku ilikuya mu akili yake. Ilikuwa Matayo 12:50 yenye inasema: “Kila mutu mwenye anafanya mapenzi ya Baba yangu mwenye kuwa mbinguni, huyo ndiye ndugu yangu, dada yangu, na mama yangu.” Hata kama Robert alikuwa tu angali anajifunza Biblia, roho ya Yehova ilimusaidia ajibie ile ulizo na pia ajibie maulizo ingine yenye hakukuwa anatazamia. Yehova alipaswa kufurahi sana kumuona Robert anatetea imani yake! Na Yehova anafurahi sana kama tunaendelea kumutegemea ili kutoa ushahidi ijapokuwa hali za nguvu zenye tunaweza kujikuta ndani.

20. Tunapaswa kuazimia kufanya nini? (Yoh. 17:11, 15)

20 Tuko wenye shukrani sana kuwa mu familia hii ya kiroho ya ndugu na dada wa mu dunia yote. Tuko na Baba muzuri sana lakini pia ndugu na dada wazuri wenye wanatupenda. Kila mara tunapaswa kuwa wenye shukrani juu ya ile. Shetani na watu wake wenye kumuunga mukono wenye kutuchukia wanajaribu kutufanya tukuwe na mashaka kama Yehova anatupenda na wanajaribu pia kuvunja umoja wenye tuko nao. Hata vile Yesu alisali kwa ajili yetu, alimuomba Baba yake aendelee kutulinda juu familia yetu iendelee kuwa na umoja. (Soma Yohana 17:11, 15.) Yehova iko anajibia ile sala. Sawa vile Yesu, hatuna mashaka kwamba Baba yetu wa mbinguni anatupenda na kama atatusaidia. Kwa hiyo basi, tuazimie kuwa karibu zaidi na familia yetu ya kiroho.

WIMBO 99 Ndugu na Dada Wote

^ fu. 5 Tuko na pendeleo kubwa sana ya kuwa kati ya familia ya ndugu na dada wenye kupendana. Siye wote tunapenda kutia nguvu upendo wenye tuko nao kati yetu. Tunaweza kufanya vile namna gani? Kwa kuiga namna Baba yetu mwenye upendo anatutendea na kwa kufuata mufano wa Yesu na wa ndugu na dada zetu.

^ fu. 57 MAFASIRIO YA PICHA: Yehova alituma malaika wake ili kumutia nguvu Yesu wakati alikuwa mu bustani ya Getsemane.

^ fu. 59 MAFASIRIO YA PICHA: Mu kipindi ya Coronavirus, wengi walitumika sana ili kutayarisha na kugawia ndugu zetu chakula.

^ fu. 61 MAFASIRIO YA PICHA: Mama moja iko anasaidia mutoto wake mwanamuke mwenye iko anatuma barua ya kutia moyo ndugu moja mwenye kuwa mu gereza.